JOB SEEKER
Senior Member
- Aug 1, 2011
- 145
- 33
WIKI hii nzima nimeitumia kuwaza lakini sikupata majibu ya
kuniridhisha. Wazo langu kuu ni nani ndani ya Chama cha Mapinduzi
(CCM), alipanga na kuidhinisha wazee wawili yaani Rais mstaafu
Benjamin Mkapa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano wa
jamii), Stephen Wassira, waende kumpigia kampeni mgombea wa
chama hicho jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari?
Pasipo kumng'unya maneno kama walilazimishwa kwenda huko basi
aliyewalazimisha na alaaniwe kwa ubabe huo na kama
walijipendekeza wao bila kujali kuwa zama zao zimepita na kukubali
kwenda kujipaka matope, basi aibu yao ya chama chao dhaifu.
Niliwahi kuandika huko nyuma nikisema kuwa CCM ni dhaifu lakini
watu hawaichukii kwa hilo bali kwa matendo ya baadhi ya viongozi
wao wanaofikia maamuzi pasipo kujali madhara yake na mustakabali
wa chama mbeleni.
Ni aibu kubwa sana kwa chama kikongwe chenye umri wa miaka 35
na makada chungu nzima, kumtegemea rais mstaafu kwenda
kuwazindulia na kuwafanyia kampeni ya kugombea nafasi ndogo ya
ubunge.
Nilivyosikia Halmashauri Kuu ya CCM mwaka jana ikimteua mzee
huyo kuzindua kampeni katika Jimbo la Igunga, nilipigwa butwaa
nikidhani pengine ni hadaa ya kuwababaisha wapinzani wao lakini
mwisho wa siku nikajua Mkapa atakuwepo pale kama mwalikwa tu
na mshauri wa wenzake.
Lakini Mkapa alipopanda jukwaani mara mbili Igunga kwa kufungua
na kufunga kampeni za CCM, niliamini kuwa chama hicho sasa basi,
kama hakiwezi kuwatumia makada wake wasafi kimatendo na hoja
kuomba ubunge hadi wakimbilie kwa Rais mstaafu na magamba
mengine basi ni hatari.
Sasa Mkapa amenogewa jukwaa, akaona ni sehemu ya kupitishia
mashambulizi yake kwa kujibu tuhuma zilizoelekezwa kwake miaka
mingi lakini akawa kimya kuzijibu na kujijengea heshima ya kaulimbiu
yake ya uwazi na ukweli.
Badala yake mzee wetu anadhani Watanzania wa leo ni wale wa
miaka 10 iliyopita, kumbe hawa hawadanganyiki tena, hawaogopi
mikwara yake, wanataka kujua aliwezaje kufanya biashara kwa
kutumia rasilimali zao akiwa Ikulu.
Mzee Mkapa bila kutambua hilo na kwa ushauri dhaifu wa chama
chake legelege akakubali kudanganyika kwenda Arumeru kumnadi
Sioi ili atumie mwanya huo kuendelea kufunika ukweli wa tuhuma za
ufisadi zinazomkabili.
Hata hivyo, kwa udhaifu wa hoja, akajikuta ameishiwa maneno ya
kuwapumbaza wananchi wa Arumeru na badala yake shetani
akampitia akaamua kuikashifu familia ya Baba wa Taifa hayati
Mwalimu Julius Nyerere.
Ni Mkapa huyu huyu aliyejitapa kwenye mazishi ya Nyerere mwaka
1999 kule Butiama kuwa yeye, CCM na serikali wangemuenzi muasisi
huyo kwa kila jinsi, lakini akageuka muasi wa kudai kwamba Mbunge
wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA) si mmoja wa
wanafamilia ya Nyerere.
Haijulikani shetani huyo alitokea wapi hadi Mkapa kuacha kumnadi
Sioi na kurukia kumshambulia mbunge huyo kijana ambaye anajua
fika ni mtoto wa mdogo wake Nyerere, Kiboko Nyerere, akidai si
mmoja wa wanafamilia.
Akaenda mbele na kujinasibu kuwa Nyerere alimtambulisha wana
ndugu wote kwa muda waliofanya kazi naye lakini Vincent hayumo.
Hivi ni kweli Mkapa alikuwa akifanya kazi ya kukariri wanafamilia wa
Nyerere kujua nani anazaliwa, ameolewa, ameoana na nani?
Yeye ndoa yake iko safi, familia aliyonayo haina kasoro hadi apate
muda wa kuhama hoja ya kampeni na kurukia kumdhalilisha hayati
Baba wa Taifa kwa kumzushia uongo? Na hata kama ingekuwa ni
kweli, Vincent si mmoja wa wanafamilia ya Nyerere, watu wa
Arumeru ilikuwa inawasaidia nini?
Lakini kama wasemavyo wahenga kuwa siku za mwizi ni arobaini au
muosha huoshwa, Mkapa alipata aibu ya mwaka baada ya mtoto wa
Nyerere, Madaraka Nyerere, kukanusha uongo wake na kukiri kuwa
Vincent ni mwanafamilia wao akiwa mtoto wa baba mdogo wao.
Hapa utapima mwenyewe, kuwa hiyo ndiyo CCM ambayo tegemeo
lao ni Mkapa anayekosa hoja jukwaaani na kuamua kusema uongo
pasipo kujali kuwa wananchi wanataka kufahamu mengi na ya msingi
kutoka kwake.
Kwa mantiki kama hiyo, unadhani nani anaweza kuisemea CCM ili
watu waelewe kuwa chama bado ni makini ikiwa vijana wamewekwa
kando na kufanywa mtaji wa kutumika kurubuniwa kufanikisha
ushindi wa hila na ghiriba?
Kama kawaida CCM bila kukaa chini na kutathmini aibu na madhara
aliyowaletea Mkapa, wakakurupuka na kumpeleka mkongwe
mwingine, Waziri Wassira huko Arumeru kunusuru jahazi.
CCM ama kwa kutojua kuwa enzi za Wassira zimeisha na amechoka
hadi anapigwa picha akiwa ameuchapa usingizi bungeni,
walimpandisha jukwaani, naye kama Mkapa akatumia muda wote
kulidhalisha Kanisa Katoliki na Katibu Mkuu wa CHADEMA badala ya
kumnadi Sioi.
Wassira kwa makusudi aliwadanganya wananchi wa Arumeru kuwa
Dk. Willibrod Slaa alifukuzwa upadri baada ya kuiba fedha za ujio wa
Papa Yohane Paul II, alipokuja nchini mwaka 1990, wakati huo
akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).
Lakini kama ilivyo kwenye maandiko matakatifu kuwa Mungu
hamfichi mnafiki, siku moja baada ya uongo huo wa kumdhalilisha
Dk. Slaa na kanisa kwa ujumla, Rais wa TEC, Askofu Mkuu Juda
Thaddeus Ruwa'ichi, alimjibu akimtaka kutoa ushahidi kuthibitisha
kama kweli.Ruwai'chi ambaye pia ni Askofu wa Jimbo Kuu la
Mwanza, alisema Wassira athibitishe tuhuma zake kwani kanisa hilo
halijawahi kumtuhumu Dk. Slaa kwa tuhuma za wizi.Kanisa
halijawahi kumshutumu Dk. Slaa kuhusu madai hayo (ya Wassira).
Kama Wassira ameyatoa kwenye mkutano wa hadhara, njia sahihi
ya kupata ukweli ni yeye kutupa ushahidi wa vielelezo kuthibitisha
madai yake, alisema Ruwaichi.Kwa mwendo huu wa wakongwe wa
CCM kuamua kujivua nguo hadharani kwa kusema uongo, nini hatima
ya chama hicho mbeleni, je, vijana na watoto wajao wanaweza
kujifunza nini katika maadili ya viongozi ikiwa watu wenyewe ni
kama hawa wanaosema lolote linalowajia mdomoni.Safu hii ya Fikra
Mpya katika kutafakari, imekuja na njia nyepesi kwa wale
wanaoiwaza CCM kwa sasa kuwa wachukue kanuni hii ya hesabu;
Mkapa+Wassira=CCM dhaifu, kama huamini tupe hoja yako maana
hawa ndio walikuwa tegemeo huko Arumeru Mashariki wakaishia
kuwadhalilisha watu na taasisi za imani za dini. Tafakari
kuniridhisha. Wazo langu kuu ni nani ndani ya Chama cha Mapinduzi
(CCM), alipanga na kuidhinisha wazee wawili yaani Rais mstaafu
Benjamin Mkapa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano wa
jamii), Stephen Wassira, waende kumpigia kampeni mgombea wa
chama hicho jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari?
Pasipo kumng'unya maneno kama walilazimishwa kwenda huko basi
aliyewalazimisha na alaaniwe kwa ubabe huo na kama
walijipendekeza wao bila kujali kuwa zama zao zimepita na kukubali
kwenda kujipaka matope, basi aibu yao ya chama chao dhaifu.
Niliwahi kuandika huko nyuma nikisema kuwa CCM ni dhaifu lakini
watu hawaichukii kwa hilo bali kwa matendo ya baadhi ya viongozi
wao wanaofikia maamuzi pasipo kujali madhara yake na mustakabali
wa chama mbeleni.
Ni aibu kubwa sana kwa chama kikongwe chenye umri wa miaka 35
na makada chungu nzima, kumtegemea rais mstaafu kwenda
kuwazindulia na kuwafanyia kampeni ya kugombea nafasi ndogo ya
ubunge.
Nilivyosikia Halmashauri Kuu ya CCM mwaka jana ikimteua mzee
huyo kuzindua kampeni katika Jimbo la Igunga, nilipigwa butwaa
nikidhani pengine ni hadaa ya kuwababaisha wapinzani wao lakini
mwisho wa siku nikajua Mkapa atakuwepo pale kama mwalikwa tu
na mshauri wa wenzake.
Lakini Mkapa alipopanda jukwaani mara mbili Igunga kwa kufungua
na kufunga kampeni za CCM, niliamini kuwa chama hicho sasa basi,
kama hakiwezi kuwatumia makada wake wasafi kimatendo na hoja
kuomba ubunge hadi wakimbilie kwa Rais mstaafu na magamba
mengine basi ni hatari.
Sasa Mkapa amenogewa jukwaa, akaona ni sehemu ya kupitishia
mashambulizi yake kwa kujibu tuhuma zilizoelekezwa kwake miaka
mingi lakini akawa kimya kuzijibu na kujijengea heshima ya kaulimbiu
yake ya uwazi na ukweli.
Badala yake mzee wetu anadhani Watanzania wa leo ni wale wa
miaka 10 iliyopita, kumbe hawa hawadanganyiki tena, hawaogopi
mikwara yake, wanataka kujua aliwezaje kufanya biashara kwa
kutumia rasilimali zao akiwa Ikulu.
Mzee Mkapa bila kutambua hilo na kwa ushauri dhaifu wa chama
chake legelege akakubali kudanganyika kwenda Arumeru kumnadi
Sioi ili atumie mwanya huo kuendelea kufunika ukweli wa tuhuma za
ufisadi zinazomkabili.
Hata hivyo, kwa udhaifu wa hoja, akajikuta ameishiwa maneno ya
kuwapumbaza wananchi wa Arumeru na badala yake shetani
akampitia akaamua kuikashifu familia ya Baba wa Taifa hayati
Mwalimu Julius Nyerere.
Ni Mkapa huyu huyu aliyejitapa kwenye mazishi ya Nyerere mwaka
1999 kule Butiama kuwa yeye, CCM na serikali wangemuenzi muasisi
huyo kwa kila jinsi, lakini akageuka muasi wa kudai kwamba Mbunge
wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA) si mmoja wa
wanafamilia ya Nyerere.
Haijulikani shetani huyo alitokea wapi hadi Mkapa kuacha kumnadi
Sioi na kurukia kumshambulia mbunge huyo kijana ambaye anajua
fika ni mtoto wa mdogo wake Nyerere, Kiboko Nyerere, akidai si
mmoja wa wanafamilia.
Akaenda mbele na kujinasibu kuwa Nyerere alimtambulisha wana
ndugu wote kwa muda waliofanya kazi naye lakini Vincent hayumo.
Hivi ni kweli Mkapa alikuwa akifanya kazi ya kukariri wanafamilia wa
Nyerere kujua nani anazaliwa, ameolewa, ameoana na nani?
Yeye ndoa yake iko safi, familia aliyonayo haina kasoro hadi apate
muda wa kuhama hoja ya kampeni na kurukia kumdhalilisha hayati
Baba wa Taifa kwa kumzushia uongo? Na hata kama ingekuwa ni
kweli, Vincent si mmoja wa wanafamilia ya Nyerere, watu wa
Arumeru ilikuwa inawasaidia nini?
Lakini kama wasemavyo wahenga kuwa siku za mwizi ni arobaini au
muosha huoshwa, Mkapa alipata aibu ya mwaka baada ya mtoto wa
Nyerere, Madaraka Nyerere, kukanusha uongo wake na kukiri kuwa
Vincent ni mwanafamilia wao akiwa mtoto wa baba mdogo wao.
Hapa utapima mwenyewe, kuwa hiyo ndiyo CCM ambayo tegemeo
lao ni Mkapa anayekosa hoja jukwaaani na kuamua kusema uongo
pasipo kujali kuwa wananchi wanataka kufahamu mengi na ya msingi
kutoka kwake.
Kwa mantiki kama hiyo, unadhani nani anaweza kuisemea CCM ili
watu waelewe kuwa chama bado ni makini ikiwa vijana wamewekwa
kando na kufanywa mtaji wa kutumika kurubuniwa kufanikisha
ushindi wa hila na ghiriba?
Kama kawaida CCM bila kukaa chini na kutathmini aibu na madhara
aliyowaletea Mkapa, wakakurupuka na kumpeleka mkongwe
mwingine, Waziri Wassira huko Arumeru kunusuru jahazi.
CCM ama kwa kutojua kuwa enzi za Wassira zimeisha na amechoka
hadi anapigwa picha akiwa ameuchapa usingizi bungeni,
walimpandisha jukwaani, naye kama Mkapa akatumia muda wote
kulidhalisha Kanisa Katoliki na Katibu Mkuu wa CHADEMA badala ya
kumnadi Sioi.
Wassira kwa makusudi aliwadanganya wananchi wa Arumeru kuwa
Dk. Willibrod Slaa alifukuzwa upadri baada ya kuiba fedha za ujio wa
Papa Yohane Paul II, alipokuja nchini mwaka 1990, wakati huo
akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).
Lakini kama ilivyo kwenye maandiko matakatifu kuwa Mungu
hamfichi mnafiki, siku moja baada ya uongo huo wa kumdhalilisha
Dk. Slaa na kanisa kwa ujumla, Rais wa TEC, Askofu Mkuu Juda
Thaddeus Ruwa'ichi, alimjibu akimtaka kutoa ushahidi kuthibitisha
kama kweli.Ruwai'chi ambaye pia ni Askofu wa Jimbo Kuu la
Mwanza, alisema Wassira athibitishe tuhuma zake kwani kanisa hilo
halijawahi kumtuhumu Dk. Slaa kwa tuhuma za wizi.Kanisa
halijawahi kumshutumu Dk. Slaa kuhusu madai hayo (ya Wassira).
Kama Wassira ameyatoa kwenye mkutano wa hadhara, njia sahihi
ya kupata ukweli ni yeye kutupa ushahidi wa vielelezo kuthibitisha
madai yake, alisema Ruwaichi.Kwa mwendo huu wa wakongwe wa
CCM kuamua kujivua nguo hadharani kwa kusema uongo, nini hatima
ya chama hicho mbeleni, je, vijana na watoto wajao wanaweza
kujifunza nini katika maadili ya viongozi ikiwa watu wenyewe ni
kama hawa wanaosema lolote linalowajia mdomoni.Safu hii ya Fikra
Mpya katika kutafakari, imekuja na njia nyepesi kwa wale
wanaoiwaza CCM kwa sasa kuwa wachukue kanuni hii ya hesabu;
Mkapa+Wassira=CCM dhaifu, kama huamini tupe hoja yako maana
hawa ndio walikuwa tegemeo huko Arumeru Mashariki wakaishia
kuwadhalilisha watu na taasisi za imani za dini. Tafakari