Mlitika
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 457
- 260
Fursa aliyoipewa na watanzania ya kuwa rais wa taifa Ndugu Ben imempa heshima kubwa na kwa mila za kiafrika yeye ni kama baba kwa watanzania wote. Anayo haki ya kuheshimiwa na watanzania wana wajibu wa kumheshimu na halipashwi kuwepo jambo la kumfanya asigane na watanzania.
Nionavyo mimi kitendo cha raisi mstaafu kujihusisha na siasa za majukwaani tena katika kada za chini kama majimbo hasa katika mazingira ya siasa za kibongo kunamweka katika mazingira ya kusigana na watanzania maana wako huru kutofautiana kifikra na mtazamo. Mbaya zaidi Mr. Ben mwenyewe hana diplomasia ya kikampeni; yaani ana ubabe fulani hivyi akiwa jukwaani.
Matokeo yake ndo kama tulichoshuhudia Arumeru. Mzee wa heshima kubwa kama yeye kuanza kukashifiwa na hata kutukanwa na watoto wadogo majukwaani na katika mitandao. Anasababisha laana ya bure kwa watoto wanaoshindwa kuzuia kishawishi cha kumkashifu na kumtukana baba yao! Kwa CCM kubwagwa Ben amevuna aibu kubwa kuliko Sumari! Jambo hili halina faida kwa nchi na linabomoa heshima yake Mr. Clean. He should only be called to intervene on serious issues of national or international interest.
Samahani Mr. Ben, ni mtazamo tu. Ila siyo siri, unajiaibisha bure!
Nionavyo mimi kitendo cha raisi mstaafu kujihusisha na siasa za majukwaani tena katika kada za chini kama majimbo hasa katika mazingira ya siasa za kibongo kunamweka katika mazingira ya kusigana na watanzania maana wako huru kutofautiana kifikra na mtazamo. Mbaya zaidi Mr. Ben mwenyewe hana diplomasia ya kikampeni; yaani ana ubabe fulani hivyi akiwa jukwaani.
Matokeo yake ndo kama tulichoshuhudia Arumeru. Mzee wa heshima kubwa kama yeye kuanza kukashifiwa na hata kutukanwa na watoto wadogo majukwaani na katika mitandao. Anasababisha laana ya bure kwa watoto wanaoshindwa kuzuia kishawishi cha kumkashifu na kumtukana baba yao! Kwa CCM kubwagwa Ben amevuna aibu kubwa kuliko Sumari! Jambo hili halina faida kwa nchi na linabomoa heshima yake Mr. Clean. He should only be called to intervene on serious issues of national or international interest.
Samahani Mr. Ben, ni mtazamo tu. Ila siyo siri, unajiaibisha bure!