Mkapa umejifunza nini Arumeru?

Mlitika

JF-Expert Member
Mar 23, 2012
457
260
Fursa aliyoipewa na watanzania ya kuwa rais wa taifa Ndugu Ben imempa heshima kubwa na kwa mila za kiafrika yeye ni kama “baba” kwa watanzania wote. Anayo haki ya kuheshimiwa na watanzania wana wajibu wa kumheshimu na halipashwi kuwepo jambo la kumfanya asigane na watanzania.

Nionavyo mimi kitendo cha raisi mstaafu kujihusisha na siasa za majukwaani tena katika kada za chini kama majimbo hasa katika mazingira ya siasa za kibongo kunamweka katika mazingira ya kusigana na watanzania maana wako huru kutofautiana kifikra na mtazamo. Mbaya zaidi Mr. Ben mwenyewe hana diplomasia ya kikampeni; yaani ana ubabe fulani hivyi akiwa jukwaani.

Matokeo yake ndo kama tulichoshuhudia Arumeru. Mzee wa heshima kubwa kama yeye kuanza kukashifiwa na hata kutukanwa na watoto wadogo majukwaani na katika mitandao. Anasababisha laana ya bure kwa watoto wanaoshindwa kuzuia kishawishi cha kumkashifu na kumtukana baba yao! Kwa CCM kubwagwa Ben amevuna aibu kubwa kuliko Sumari! Jambo hili halina faida kwa nchi na linabomoa heshima yake Mr. Clean. He should only be called to intervene on serious issues of national or international interest.

Samahani Mr. Ben, ni mtazamo tu. Ila siyo siri, unajiaibisha bure!
 
"La kuvunda halina ubani". Sasa kama chama kimeoza unafikiri uheshimiwa utatibu hali. Watanzania hawaangalii anyepiga kampeni ana cheo gani. Ikumbukwe, migogoro ya ardhi huko Arumeru ilisababishwa na Mh Mkapa ya kuuza ardhi kwa wageni akitumia mwavuli wa uwekezaji
 
"La kuvunda halina ubani". Sasa kama chama kimeoza unafikiri uheshimiwa utatibu hali. Watanzania hawaangalii anyepiga kampeni ana cheo gani. Ikumbukwe, migogoro ya ardhi huko Arumeru ilisababishwa na Mh Mkapa ya kuuza ardhi kwa wageni akitumia mwavuli wa uwekezaji

Kwenda kwake Arumeru alikwenda kuwazidishia hasira Wameru na amesaidia kuangushwa kwa CCM na yeye kuvuna aibu na matusi!

CCM IS DESPERATE!​
 
Fursa aliyoipewa na watanzania ya kuwa rais wa taifa Ndugu Ben imempa heshima kubwa na kwa mila za kiafrika yeye ni kama “baba” kwa watanzania wote. Anayo haki ya kuheshimiwa na watanzania wana wajibu wa kumheshimu na halipashwi kuwepo jambo la kumfanya asigane na watanzania.

Nionavyo mimi kitendo cha raisi mstaafu kujihusisha na siasa za majukwaani tena katika kada za chini kama majimbo hasa katika mazingira ya siasa za kibongo kunamweka katika mazingira ya kusigana na watanzania maana wako huru kutofautiana kifikra na mtazamo. Mbaya zaidi Mr. Ben mwenyewe hana diplomasia ya kikampeni; yaani ana ubabe fulani hivyi akiwa jukwaani.

Matokeo yake ndo kama tulichoshuhudia Arumeru. Mzee wa heshima kubwa kama yeye kuanza kukashifiwa na hata kutukanwa na watoto wadogo majukwaani na katika mitandao. Anasababisha laana ya bure kwa watoto wanaoshindwa kuzuia kishawishi cha kumkashifu na kumtukana baba yao! Kwa CCM kubwagwa Ben amevuna aibu kubwa kuliko Sumari! Jambo hili halina faida kwa nchi na linabomoa heshima yake Mr. Clean. He should only be called to intervene on serious issues of national or international interest.

Samahani Mr. Ben, ni mtazamo tu. Ila siyo siri, unajiaibisha bure!


Safi sana. Natamani angeisoma hii
 
Mlitika,

You are absolutely right. Kama majimboni wanamtumia hadi ex-president kukampenia watoto wadogo, sasa ikifika 2015 kwenye kampeni za urais si CCM watamleta OBAMA na viongozi wote wa G7??
 
Nafikiri atakua amejifunza kwamba:
1. Siasa haibakwi
2. Mfiwa hafutwi machozi kwa kupewa ubunge
3. Kustaafu uraisi na kuendelea kuishi kwa gharamba za walipa kodi hatakiwi tena kurudi kwenye siasa za majukwaani
 
Fursa aliyoipewa na watanzania ya kuwa rais wa taifa Ndugu Ben imempa heshima kubwa na kwa mila za kiafrika yeye ni kama "baba" kwa watanzania wote. Anayo haki ya kuheshimiwa na watanzania wana wajibu wa kumheshimu na halipashwi kuwepo jambo la kumfanya asigane na watanzania.

Nionavyo mimi kitendo cha raisi mstaafu kujihusisha na siasa za majukwaani tena katika kada za chini kama majimbo hasa katika mazingira ya siasa za kibongo kunamweka katika mazingira ya kusigana na watanzania maana wako huru kutofautiana kifikra na mtazamo. Mbaya zaidi Mr. Ben mwenyewe hana diplomasia ya kikampeni; yaani ana ubabe fulani hivyi akiwa jukwaani.

Matokeo yake ndo kama tulichoshuhudia Arumeru. Mzee wa heshima kubwa kama yeye kuanza kukashifiwa na hata kutukanwa na watoto wadogo majukwaani na katika mitandao. Anasababisha laana ya bure kwa watoto wanaoshindwa kuzuia kishawishi cha kumkashifu na kumtukana baba yao! Kwa CCM kubwagwa Ben amevuna aibu kubwa kuliko Sumari! Jambo hili halina faida kwa nchi na linabomoa heshima yake Mr. Clean. He should only be called to intervene on serious issues of national or international interest.

Samahani Mr. Ben, ni mtazamo tu. Ila siyo siri, unajiaibisha bure!

Ukweli ni kwamba hawajifunzi kutokana na matukio kama hayo, hususani BWM. Imagine energy iliyotumika na CCM (Ikishirikiana na Serikali yake) kutafuta jimbo kama ingetumika kutatua tatizo moja tu hapo (Say Ardhi) Arumeru Mashariki tungekuwa mbali sana kimaendeleo.
 
ukweli ni kwamba hawajifunzi kutokana na matukio kama hayo, hususani bwm. Imagine energy iliyotumika na ccm (ikishirikiana na serikali yake) kutafuta jimbo kama ingetumika kutatua tatizo moja tu hapo (say ardhi) arumeru mashariki tungekuwa mbali sana kimaendeleo.

nasikia ccm wamempa hiyo km adhabu kwa kutumbukiza nchi kwenye lindi la mikashfa ya ufisadi. Aliambiwa asipopanda majukwaani watamshitaki kwa ufisadi wake wa kujiuzia kiwira.
 
Mkapa alilazimishwa tu kwenda Arumeru ndio maana hata siku ya uzinduzi ilibadilishwa. Hatahivyo viongozi wa CCM huwa hawana desturi ya kujifunza kutokana na matukio wapowapo tu
 
Mkapa alilazimishwa tu kwenda Arumeru ndio maana hata siku ya uzinduzi ilibadilishwa. Hatahivyo viongozi wa CCM huwa hawana desturi ya kujifunza kutokana na matukio wapowapo tu

Mzee Mkapa anatakiwa kusoma alama za nyakati, alitakiwa apumzike maana heshima aliyonayo na madhambi aliyofanya wakati akiwa madarakani RADAR, EPA, UBINAFISISHAJI nk vitaibuliwa upyaaaaaa, pumzika mzee BEN kama walivyowapumzisheni kwenye NEC
 
Mzee Mkapa anatakiwa kusoma alama za nyakati, alitakiwa apumzike maana heshima aliyonayo na madhambi aliyofanya wakati akiwa madarakani RADAR, EPA, UBINAFISISHAJI nk vitaibuliwa upyaaaaaa, pumzika mzee BEN kama walivyowapumzisheni kwenye NEC
Ecxactly! Anapashwa atambue kuwa kuitwa akatoe msaada majukwaani ni kejeli kwake hasa baada ya kuambiwa kwenye NEC hawataki kumwona. Kwama kweli wanautahamini msaada wa busara zake basi sehemu ya maana ilikuwa kwenye NEC.
 
Fursa aliyoipewa na watanzania ya kuwa rais wa taifa Ndugu Ben imempa heshima kubwa na kwa mila za kiafrika yeye ni kama "baba" kwa watanzania wote. Anayo haki ya kuheshimiwa na watanzania wana wajibu wa kumheshimu na halipashwi kuwepo jambo la kumfanya asigane na watanzania.

Nionavyo mimi kitendo cha raisi mstaafu kujihusisha na siasa za majukwaani tena katika kada za chini kama majimbo hasa katika mazingira ya siasa za kibongo kunamweka katika mazingira ya kusigana na watanzania maana wako huru kutofautiana kifikra na mtazamo. Mbaya zaidi Mr. Ben mwenyewe hana diplomasia ya kikampeni; yaani ana ubabe fulani hivyi akiwa jukwaani.

Matokeo yake ndo kama tulichoshuhudia Arumeru. Mzee wa heshima kubwa kama yeye kuanza kukashifiwa na hata kutukanwa na watoto wadogo majukwaani na katika mitandao. Anasababisha laana ya bure kwa watoto wanaoshindwa kuzuia kishawishi cha kumkashifu na kumtukana baba yao! Kwa CCM kubwagwa Ben amevuna aibu kubwa kuliko Sumari! Jambo hili halina faida kwa nchi na linabomoa heshima yake Mr. Clean. He should only be called to intervene on serious issues of national or international interest.

Samahani Mr. Ben, ni mtazamo tu. Ila siyo siri, unajiaibisha bure!
Well said Mlitika. Napigia mstari ushauri wako kwa bwna Ben. Nyongeza kidogo ni hii:

  1. BWM anatakiwa kujua kuwa "wenye CCM" wa wakati huu ni maadui zake nambari one na wala siyo kisiri siri bali wazi wazi. Wameanzisha na kuratibu kwa makusudi propaganda nyingi dhidi yake za kumchafua na kufunika yote aliyoifanyia nchi hii wakati wake (pamoja na mapungufu ambayo hayawezi kukosekana). Anapofumba macho na kuvimba kichwa wanapokuja kumwomba akasaidie wapate ulaji anawapa nafasi wajione wajanja sana na wazidi kumkebehi. Mbona alikataa wazi wazi kuzunguka kumnadi JK 2005? Ujasiri huo anaukosaje sasa?
  2. Kwa upande wa pili fundisho linawageukia wataka madaraka wanaotapatapa (CCM). Ingawa walimchafua kwa makusudi bado waliamini watu wengi nje na ndani ya nchi wanamheshimu sana BWM na ndiyo maana wanarudi kumwangukia awape tafu wakimhakikishia kuwa "Watanzania wanakuheshimu sana na wanakuskiliza mzee". Sasa wajue kuwa huo si mtaji tena; watanzania washafunguka akili na machi na HAWADANGANYIKI hata umlete Obama au nani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom