Mkapa: tume tangazeni matokeo CCM imeshinda muuwaache waende mahakamani

kama ccm na serikali yake wamechoka na amani na utulivu wa nchi hii wajaribu kucheza na matokeo ya Arumeru! hakuna atakayekwenda mahakamani mahakama tutakuwa ni sisi wenyewe tunechoka Arusha mjini mlisababisha tukakesha siku zaiidii ya tatu safari hii hatukeshi hata nusu saa,. tupo tayari kwa lolote iba kura popote sio Arusha man!!
 
Tatizo la Mkapa ni genetic zake kwa asilimia 100% ni za Kibandido, na aziwezi kumbadili kwa kuwa kazaliwa
Tanzania. Msukumo wa kutenda mabaya kwake ni asilimia 99% na kuyaacha mazuri katika asilimia 1%
maovu yanayotendwa na hao mabandido ndio yaliyo kichwani mwake, mseme mpindukie huyo abadiliki atabakia
hivyo hivyo kuwa jambazi. Kipindi cha haki kikifika yeye awe wa kwanza katika milango ya sheria.
 
dr mkapa ni mtu makin sana hawezi kuwa na myopia vision kama weewe.mwandishi wa thread hii muongo ,maana ametoa mfano wa amosi makala kupitishwa kwa nguvu, makala amekuwa mbunge mwaka 2010 wakati mkapa ame retire 2005 ! Wapi na wspi?

umakini wake ndio ule wa kusema vicent nyerere hana uhusiano wowote kiukoo na baba wa taifa mwl. Nyerere?
 
BWM ni miongoni mwa viongozi bora barani AFRIKA,chuki zenu weka kapuuuuuuuuuuuuuuni a.k.a trashhhhhhhhhhhhhhhhhout.Kusema Vicent Nyerere si mtoto wa Mwl. JK Nyerere alikuwa sahihi.Japo kuwa ni ndugu yake ! Hilo suala limegeuzwa kama ni kosa kwa MKAPA ambaye amefanya mambo mengi makubwa na yanaonekana.Mfano barabara na madaraja yamejengwa kwa wingi wakati wa utawala wake.Tuhuma ambazo azithibitishwa si vizuri kuzitumia kuwachafua viongozi wastaafu.
Watanzania kama wewe mkiendelea kulala hivi hakutakuwa na chembe ya mabadiliko nchi hii......Mkapa kujenga mabarabara na madaraja ni kutekeleza wajibu wake.....hizo ndizo kazi alizotakiwa asimamie kama kiongozi....wala huitaji kumshukuru kwa hilo....ni sehemu ya kazi yake....lini watanzania mtaacha hii kasumba ya kuomba serikali iwatimizie wajibu wake???unajua kwanini unalipa kodi wewe??..inasikitisha sana haki zenu Tz mnaziona kama fadhila.....sasa ulitegemea MKapa afanye nini kama rais kama si kukujengea barabara na madaraja??......aliekudanganya Mkapa ni rais bora africa ni nani???marais bora africa wanajulikana na Mkapa hayumo(wala JK)....hizi porojo watanzania zitawamaliza...By the way, Mkapa akiwa hai atajitahidi awezavyo kukandamiza upinzani....anajua wapinzani wakichukua nchi yeye Mkapa lazima ataishia jela....analijua hilo fika.....sishangai kumsikia Mkapa hapendi upinzani tz....heri yake Mkapa ni pale tu ccm itakapoendelea kukaa madarakani kwani ataendelea kulindwa na watawala wa ccm...Mkapa anajua tu pindi wapinzani wakichukua nchi hana chake tena...zaidi ya kunyea debe...hili analijua fika na halikwepeki....labda afe.......
 
Jana Dr. Slaa amedai kuwa ktk vikao vya siri vya ccm anekaririwa rais mstaafu BWM akiishinikiza tune ya uchaguzi kuitangaza ccm imeshinda uchaguzi wa Arumeru hata kama wameshindwa kwa sababu wataenda mahakamani na kesi itafia huko.

Napata picha kuwa ccm ni wezi, wanyang'anyi na wauwaji mbinu kama hii ndio iliyompa ubunge Makala baada ya mkapa kumtishia maisha mbunge wa cdm aliyekuwa ameshinda Mvomero baada ya kushindwa kumhonga

Tusikubali ushenzi huu cz wanajua fika tume na mahakama ni wateule wa mwenyekiti wao

Na hapa ndio napata shida na Chadema, CCM wana capitalize katika upole na upenda amani wenu. Mtu mwenye akili timamu hawezi kupanga kuiba kwa jeuri. Sasa CCM imeshawageuza Chadema wajinga. Walijaribu 2010 wananchi wote walisimama na Chadema na ushindi ukapatikana katika sehemu nyingi. Wakaja CCM na wizi wao wakachelewesha matokeo katika kila jimbo CHADEMA ilikoshinda kisha wakayabadadili. Wananchi wakaja juu hadi kieleweke. Baadaye kwa nguvu ya FFU NA JESHI matokeo yakatangazwa. Viongozi wakuu wa Chadema kwa kutopenda shari wakapotea kabisa katika scenes na hawakusema lolote. Taifa lilingoja Dr Slaa atamke ili watu wasimama naye, ikiwa kimya. Labdal kweli alitumia busara kuepusha mauaji KARAGWE walikuwa tayari, SHINYANGA, KIBAHA n.k n.k Sasa tangu hapo CCM wameshajua CHADEMA waoga, ukitaja damu kumwagika wanakimbia. Sasa ona wanayosema juu ya Arumeru. Mcheso huu utaendelea mpaka lini na wapi? Kuna lolote Chadema mwaweza kufanya kurudisha moyo wa wanannchi waliokuwa tayari kupoteza maisha kwa mustakabali wa nchi yao na watoto wao?
 
Dr mkapa ni mtu makin sana hawezi kuwa na myopia vision kama weewe.mwandishi wa thread hii muongo ,maana ametoa mfano wa amosi makala kupitishwa kwa nguvu, makala amekuwa mbunge mwaka 2010 wakati mkapa ame retire 2005 ! Wapi na wspi?

Ongezea hii -mkapa kastaafu 2005 sawa je huko arumeru anasalisha msikiti?au? Je kama ungeambiwa kuwa alichangia ushindi pale igunga je ungeendelea kuuliza hilo swali?
 
Hakuna atakayeenda mahakamani !
Kwani Tunisia walienda mahakamani ?

Mmmh! Ikishaanza haitoishia hapo! Itaendelea! Haichagui! Haina macho! Isikie tu hivo hivo, angalia tu hivohivo visegment vilivyo editiwa cnn! BASI. God forbid!
 
Mkapa ni kapa kweli amani ya nchi na utulivu kwake ni msamiati,tatizo hajafikishwa the Hague kujibu mashitaka ya mauaji ya halaiki ya watu huko Pemba na sehemu zingine nchini mwetu.Kwa kuwa anadhani Watanzania ni watu wa kubeep aendelee kubeep ndipo ataona jeuri na nguvu ya umma,na kwa kuwa mchuma janga hulia na wakwao nafikiri wakati sasa umefika wa kulia na kusaga meno.Zamani tulidhani kipara ni ishara za ukomavu na uelewa wa mambo kumbe kweli ule usemi wa akili ni nywele sasa unajidhihirisha wazi
 
nafikiri kama haya ni ya kweli ni aibu sana kwa huyo mzee. hivi wana arumeru wakipelekewa bungeni mwakilishi ambaye hawakumtaka mkapa ananufaika na nini? nini maana ya uchaguzi sasa. I think it a shame to mkapa na tanzania kwa ujumla. huu wizi wa kura can only happen to tanzania and few countries. jamani tusikubali na wizi huu
si ni FISI HARD chochote anaweza fanya:A S 13:
 
Duuuh mzEe kwa kuunga Makala alimuacha yule dogo kwa kura 25elf sasa hapo kaibiwaje unafikiri kwa makalio wewe

Ukiongeza vituo vya wapiga kura 55 waweza kumzidi mpinzani hata kwa kura 50000 kwa majimbo yenye watu wengi!!!!!
 
Naisubiria ipite sheria ya kwamba wastaafu wanaojihusisha na siasa walipwe na vyama vyao wasiendelee kulipwa kama wastaafu wa taifa , mfano Mkapa asilipwe kama rais mstaafu bali alipwe na ccm anayoitumikia
 
Nimempenda sana Mkapa kwani ameturahisishia ushindi Arumeru, CCM endeeleni kumtuma kwenye Campaign zote zijazo.

Viva Mkapa!
 
Achaneni na Mkapa aliye jaa siasa za kizamani za matusi, visasi, ubabe.
 
Mkapa safi sn. Nadhani anaichangia vizuri ccm kupitia mgodi aliojiuzia kifisadi kwa bei chee. Na amepewa km adhabu na ccm kuwa lazima aende kwenye kampeni la sivyo ccm na serikali yake watampeleka court kwa kujimilikisha kampuni.
Kweli ndio maana mkapa alisema watz wavivu wa kufikiri
 
Back
Top Bottom