Geeque
JF-Expert Member
- Aug 17, 2007
- 936
- 316
Aliyekuwa Rais wa awamu ya tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Benjamin William Mkapa na Waziri Mkuu mstaafu katika serikali ya awamu ya nne Mh. Edward Ngoyayi Lowassa wamekamatwa na kufikishwa katika mahakama ya kisutu leo hii asubuhi wakihusishwa na makosa ya kutumia madaraka yao vibaya na ulaji wa rushwa. Kukamatwa kwa viongozi hao waastafu kumewashtua wananchi wengi ambao hawakutegemea viongozi hao wangeweza kufikishwa mahakamani. Hadi tunaingia mitamboni kesi yao ilikuwa bado inasikilizwa, habari zaidi na picha zitaletwa hivi punde.