Mkapa hamuelewi Kikwete!

The Fixer

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
1,365
583

Ndugu zangu wana JF !
Mkapa hamuelewi Kikwete, unaweza ukaona ni kama mchezo flani wa kuigiza lakini ukweli ni kwamba yanaendelea huko nyuma ya pazia ni mazito kuliko yale ambayo tunayaona na kuyasikia hata pale Habari maelezo na hali ni ya kutoaminiana hadi leo hii !

Wakati Rais Kikwete, Anaingia madarakani si kwamba alikuwa mgeni na serikali aliyokuwa anaifanyia kazi na ambayo angekuwa ndio kiongozi wake muda ule alipoingia rasmi kama Rais wa nchi, Hakuwa mgeni alikuwa anayaelewa mambo ya kifisadi yote yaliyokuwa yanaendelea hata kama naye atakuwa ni mmoja wa wahusika kama ambavyo mnyororo unavyoonyesha ! Ili kuendelea na Serikali yake safi na kutoa mambo yote ya kifisadi ambayo Watu wake wa karibu walikuwa wanamweleza kuhusu Mkapa na kama mlivyokuwa mnajua kuwa Kikwete hakua chaguo la Mkapa basi aliamua kuunda kikundi chake cha siri ambacho kilianika mambo yote ya Mkapa na kumletea kila Data za Mkapa na Kikwete akaa nazo !

Katika hali ambayo hata mwenyewe Mkapa alishangaa ni pale ,Alipomuita yule Mama Anna Mkapa siku moja pale Ikulu na kumuonyesha utitiri wa malimbikizo ya mali ambayo yule Mama pamoja ama kwa kutumia cheo cha Mumewe Mkapa aliamua kutumia kila njia na kuikamua nchi ,Ikiwa ni pamoja na sakata zima la makabidhiano la TASAF ! Baada ya Mama Anna Mkapa kukataa kuiacha pale Ikulu ,Kikwete alituma Jamaa wake waifuatilie na kuifumua kwa kuifanyia "ODITING" ya nguvu hadi walipogundua kuwa yule Mama alikwisha kuumaliza ule Mfuko na masurufu yake !

Alipomuita alimuonyesha kila kitu kuhusu TASAF, na yule Mama wa watu akabaki hana la kusema ,kwani aliombwa tu aendelee na safari zake na kumuachia jamaa afikirie namna ya kufanya ! Aliyomuonyesha yalimtoa yule Mama jasho Achilia yale Magorofa ya Kariakoo aliyonayo, wala ile hotel ya Lamada aliyojinyakulia pale Ilala karibu na Msimbazi center, Alionyeshwa ubadhirifu wote alioufanya kwa kutumia cheo cha Mumewe kama Rais.
 
Anacho kuwa hamuelewi ni kuwa mbona jamaa anajua Data zangu zote na kazifuatilia mwanzo hadi mwisho ila amekaa kimya tu !
Ananifikiriaje ?
 
Hivi mimi ndio sielewi au mwandishi wa Hoja ndiye simuelewi.

TASAF na mama Mkapa wapi na Wapi...

Au Mwandishi alikuwa anamaanisha mfuko wa frusa sawa kwa wote uliokuwa unaongozwa na mama Anna Mkapa.
 
Ndugu zangu wana JF !
Mkapa hamuelewi Kikwete, unaweza ukaona ni kama mchezo flani wa kuigiza lakini ukweli ni kwamba yanaendelea huko nyuma ya pazia ni mazito kuliko yale ambayo tunayaona na kuyasikia hata pale Habari maelezo na hali ni ya kutoaminiana hadi leo hii !

Wakati Rais Kikwete, Anaingia madarakani si kwamba alikuwa mgeni na serikali aliyokuwa anaifanyia kazi na ambayo angekuwa ndio kiongozi wake muda ule alipoingia rasmi kama Rais wa nchi, Hakuwa mgeni alikuwa anayaelewa mambo ya kifisadi yote yaliyokuwa yanaendelea hata kama naye atakuwa ni mmoja wa wahusika kama ambavyo mnyororo unavyoonyesha ! Ili kuendelea na Serikali yake safi na kutoa mambo yote ya kifisadi ambayo Watu wake wa karibu walikuwa wanamweleza kuhusu Mkapa na kama mlivyokuwa mnajua kuwa Kikwete hakua chaguo la Mkapa basi aliamua kuunda kikundi chake cha siri ambacho kilianika mambo yote ya Mkapa na kumletea kila Data za Mkapa na Kikwete akaa nazo !

Katika hali ambayo hata mwenyewe Mkapa alishangaa ni pale ,Alipomuita yule Mama Anna Mkapa siku moja pale Ikulu na kumuonyesha utitiri wa malimbikizo ya mali ambayo yule Mama pamoja ama kwa kutumia cheo cha Mumewe Mkapa aliamua kutumia kila njia na kuikamua nchi ,Ikiwa ni pamoja na sakata zima la makabidhiano la TASAF ! Baada ya Mama Anna Mkapa kukataa kuiacha pale Ikulu ,Kikwete alituma Jamaa wake waifuatilie na kuifumua kwa kuifanyia "ODITING" ya nguvu hadi walipogundua kuwa yule Mama alikwisha kuumaliza ule Mfuko na masurufu yake !

Alipomuita alimuonyesha kila kitu kuhusu TASAF, na yule Mama wa watu akabaki hana la kusema ,kwani aliombwa tu aendelee na safari zake na kumuachia jamaa afikirie namna ya kufanya ! Aliyomuonyesha yalimtoa yule Mama jasho Achilia yale Magorofa ya Kariakoo aliyonayo, wala ile hotel ya Lamada aliyojinyakulia pale Ilala karibu na Msimbazi center, Alionyeshwa ubadhirifu wote alioufanya kwa kutumia cheo cha Mumewe kama Rais.


Huu ni uongo mtupu na uzushi usio na maana. Mods thread hii inamaliza bytes tu hapa.
 
Hivi mimi ndio sielewi au mwandishi wa Hoja ndiye simuelewi.

TASAF na mama Mkapa wapi na Wapi...

Au Mwandishi alikuwa anamaanisha mfuko wa frusa sawa kwa wote uliokuwa unaongozwa na mama Anna Mkapa.

Mama Mkapa na TASAF! Haya makubwa, hata mimi yameniacha hoi. kama ni sifa ya kubreak news hapa umeipata. hebu tupe mchapo kamili jinsi huyo mama wa kiraracha alivyoshiki kuifilisi TASAF ambayo sasa inadunda katika awamu yake ya pili ikimwaga mahela huko vijijini!!!!!
 
JF. Hapa kuna moto unawaka chinichini.
Lakini Kikwete naye anaangalia mbali, muda wake wa urais utakapoisha hajui atafuata nani maana tutaweza tukaifanya Tanzania kuwa Zambia.
Yetu Macho na Masikio
 
I dont see the meaning of this thread!!! What are you trying portray? Usitudanganye kwamba Mkapa na Kikwete hawaelewani/wanatafutana. In this world of tanzanian politics that cannot happen within CCM.
 
"Lisemwalo lipo kama halipo linakuja".... Wahenga
Lakini kwa kweli itakuwa ni ajabu ya chura kupaka poda.
 
kitila big up ,,nimekupongeza ila unakumbuka mwosha huoshwa,,nilikushauri siku moja kwenye mada moja waache watu wajadili wawe huru swala la mtoto wa kikwete na wenzake umeona leo ""MUOSHWA HUOSHWA""
 
mie nadhani wadau saa ingine tuwe tunafikiri na kutafuta hoja zenye mtiririko unaoeleweka la sivyo itakua JF ni mtandao wa Udaku kama Manumba alivyouita...but kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake kwa upande wangu hapa samahani bosi sijakusoma wala kukuelewa endapo una uhakika na unachokisema au umetoa habari kijiweni kwako ukaikimbiza hapa??? anyway kile la kheri kama una lengo zuri ila sijakuelewa
 
Back
Top Bottom