Mpitagwa
JF-Expert Member
- Feb 10, 2012
- 2,339
- 1,119
Ama kweli dunia hii ni ndogo sana, juzi na jana pale chuo kikuu kwenye tamasha la kigoda cha Mwl. Nyerere, wote wawili walihudhuria, kwakuwa na mie nilikuwepo nilisoma macho ya mkapa na kuona anahamu ya kuongea na Ulimwengu. Ikatokea wakagonga na kusalimia kiaina hiyo juzi, Jana Nkrumah pale baada ya Mkapa kuongea, ukafika muda wa wachangiaji akasimama Ulimwengu watu wakajua sasa hapa atawasha moto. Alivyomshule yule jamaa akasoma mawazo ya watu akachangia ile hoja kisomi bila kumgusia Mkapa, na hoja yake ikumkuna sana Mkapa binafsi pamoja na watu wengine na kuendelea kumtesa Mkapa moyoni. Kwani alidhihilisha uelewa wake wa tabia za watu zinavyoathiriwa na madalaka. Ikumbukwe kuwa walikuwa ni vijana wa Nyerere kwa muda mrefu wote wawili lakini Mkapa akiwa madarakani alitangaza kuwa Ulimwengu si raia. Na sasa uamuzi huo wa serikali yake unamtesa sana Mkapa kisaikolojia.