Mkapa amkaanga Kikwete

Jamani kama JK kweli hana Chuki binafsi kwanini hasi deal na Radar issue, Kagoda, Meremeta etc?? apo ndo tutajua hafanyi mchezo na rushwa sasa ili la Mahalu sidhani kama anajenga anachotaka maybe ni kweli lakini anaitaji another 4 or 5 high profile cases! am just saying...
 
Kama kuna fitina na hila lzm kati ya JK na BWM kuna mwenye nayo zaidi kati ya hao wawili:

Maswali
1. Je ni kweli hilo jengo la ubalozi lilinunuliwa kwa bei halali ya soko?
2. Imekuwaje Jk kakubali serikali yake ifungue kesi dhidi ya jambo ambalo yeye mwenyewe alishawahi kutolea ufafanuzi bungeni? (rejea hansard)
3.Kam BWM anatoa ushahidi kutetea uamuzi ulifanywa na serikali yake wakati huo hii ni kuisafisha serikali yake,kumwokoa rafiki yake Mahalu(kama huo urafiki upo) au ni kumwumbua Jk?
4. Prof Mahalu ni mwajiriwa taasisi ya serikali bagamoyo(jina sikumbuki),kwa hiyo unaweza kuwa mshitakiwa na ukawa mwajiriwa wa serikali hiyo hiyo?
 
Kiongozi, unachozungumza ni kitu ambacho kweli kabisa na ndivyo mambo yanavyotakiwa kuwa.
Binafsi hili la kesi ya Mahalu naona kama maluweluwe tu.
Kuna ukakasi katika hili suala, nipingane na wewe kitu kimoja sio sahihi kwamba tunaweza kumuita Jk shujaa kwa hili, vile vile Mkapa!
Kama akweli Jk ni shujaa, kuna masuala mengi sana yanayofilisi nchi pamoja na ufisadi uliokubuu pia utendaji wa "kishkaji" wa utawala ameenda nayo mbali kiasi gani?
Jk kufikia ushujaa katika suala hili, angelifanya kama muendelezo wa kupigania hayo niliyoyasema.
Sasa Prof Mahalu anabeba ujiko wa "kuonewa huruma" sababu inaleta picha ya "Dr Msabaha na kisa cha bangusiro".... kondoo wa kafara.
Haiwezekani katika dimbwi la mfumo ulijivuruga katika ufisadi wa kupindukia mbele ya serikali iliyokoma kusimamia masuala muhimu na matatizo ya msingi ya WATU na ubunifu leo hii tumuone Rais wake ni shujaa kwa kukapeleka mahakamani kaprofessa kamoja kalikokuwa balozi huko nje, Mkuu Mbopo hii ni sawa???
Je mifumo ya balozi zetu ipoje? Tunauhakika hayajatokea kama haya ya Mahalu huko kwingine? Nini kinafanyika? Kuna maslahi ya nani?
Hata Mahalu akifungwa na hata kunyongwa na kupigwa risasi, katika namna yetu ya usimamizi wa mambo kwa ilivyosasa ni kazi bure na bado itaonekana ni uonevu tu.
Kwa ninavyowafahamu JK ( kama Rais wangu wa miaka 6) na Mkapa (kama rais wangu mstaafu) katika utendaji wao, kwa hili kila mtu kati ya hao mabwana wawili anamaslahi yake wala hamna maslahi ya taifa hapo, tusidanganyane.

Mimi nafikiri wewe ume-widen scope ya discussion na kwa namna hiyo huwezi kupata sense ya tunachuzungumza. Issue hapa ni whether Mahalu ameonewa au la kwa kumfungulia mashtaka. Kati ya wote waliotoa utetezi kwa Mahalu kwa kutumia hoja yao hiyo hawajaonyesha kwamba (a) kuna bifu kati ya Rais na Mahalu; (b) kwamba wizi huo haujafanyika na wala Mahalu hajahusika; (c) kwamba mashitaka hayo yamchochewa na chuki tu aliyonayo rais dhidi ya Mahalu. Lakini kilichojitokeza hapa ni kwamba eti kwa sababu Mkapa anakwenda kutoa ushahidi mahakamani, basi Mahalu ameshinda kesi na kwamba yeye Mahalu ameonewa.

Huu ni mtazamo finyu na hupati sababu yoyote ya kufikia conclusion hiyo zaidi ya chuki ambayo watu wanayo dhidi ya rais. Mahalu ana kesi ya kujibu and it doesn't matter who he brings as a witness lakini kudhani kwamba ushahidi wa Mkapa ndiyo ukweli wa mambo ni kutokuelewa mambo kwa hali ya juu kwa sababu kama inadhaniwa kwamba Mkapa ni msafi basi wangeangalia jinsi watu wote aliokuwa amewaamini wakati wa utawala wake walivyozalisha makashfa. Muangalie Ballali, Mramba, Yona, Mgonja, Mahalu, Kitine, Kigoda na wengine wengi na yuko tayari kuwatetea wote hao.

Mimi nafikiri tumejikita kudhani kwamba mafisadi ni wale tu waliotajwa Mwembe yanga na Tabora na kwamba wale ambao wanachukuliwa hatua kivingine basi hao si mafisadi bali ni maadui wa JK ambao ana bifu nao. Much as kuna safari ndefu katika kuchukua hatua dhidi ya hao waliotajwa, lakini ukweli ni kwamba hatua hizi zinatia moyo. Kwa mwenendo huu ni wazi kwamba very soon tutaambiwa kwamba hata Yona, Mramba na Mgonja tutaambiwa wanaonewa. This is unfair to the war against corruption.
 
Huhitaji akili nyingi kujua nani ni mkurupukaji kati yetu. Kama ulifuatilia kesi ile vizuri utajua kwamba kinachofanyika sasa hivi ni kuinyonga haki na dhana ya kwamba wakubwa hawastahili kwenda jela! Kama ungekuwepo pale IFM (mimi nilikuwepo)wakati wa video evidence ambayo Marando aliipinga sana (bila mafanikio) ungejua kwamba nchi hii ilipaswa kugeuka kuwa China kwa muda na kumtia adabu Mahalu. Yule muuzaji wa jengo lile alionyesha kushangazwa na Tanzania kuwa na maofisa ambao wanalazimisha kutengeneza mikataba miwili tean mmoja ambao una-inflate bei ya mauzo na huku Mahalu akikiri wazi kwamba alitaka kujipatia kitu. Na kwa nini ilielekezwa fedha hizo za malipo ziingie kwenye akaunti binafsi ya Mahalu. Fungua macho! Usiingie kwenye mkumbo wa watu ambao wana chuki binafsi na rais na kubeza hata yale ambayo yanafanyika kuwasaidia watanzania. Kwa mwenendo huu hakika kuna haja ya kutangaza wazi kwamba kila aliye na dhamana ya mali au rasilimali za umma sasa ajichukulie tu! Hivi mnadhani Mahalu ni malaika? Ulizeni mtaambiwa. Jiulize kwa nini imechukua miaka hataki kujitetea kama hana hatia na ana utetezi wa nguvu? Hivi tutabadilika lini na kuweka maslahi ya taifa mbele? Kama Kikwete ni mtu wa bifu basi angemwadhibu Prof. Mwandosya. Mbona wanapiga kazi pamoja tena bila matatizo? Acheni kulishwa sumu na huku mnachekelea!

huwa namshusha hadhi sana mtu anayeongeza chumvi kwenye argument ili aweze kuonekana mbele ya watu kashinda. Inaskitisha zaidi chumvi yenyewe inapokua so low & obvious kama misrepresentation ya public scene ambayo kwa vyovyote vile baadhi ya watu unaojaribu kujikweza mbele yao watakua walishuhudia
 
You are better than this! Yaani badala ya nyie kushangazwa na kitendo cha Mkapa kujishushia hadhi yake kwa sababu tu ya urafiki, sasa mnamshutumu Kikwete kwa kufanya kitu ambacho asingefanya mngemlaumu. Sisi wengine tunajua kabisa juhudi ambazo Mkapa alizifanya kuhakikisha kwamba Mahalu hashitakiwi kwa sababu tu ya urafiki wao. Lakini ukweli ni kwamba ushahidi uliotolewa mahakamani umemuumbua Mahalu na ndiyo Maana Marando na wenzake walihaha sana kukimbia kila mahakama ili Mahalu asijitetee wakati tayayri kuna uamuzi wa kwamba ana kesi ya kujibu.

Hii affidavit ya Mkapa ilikuwa itumike kuombe Nolle Prosequi lakini Mkurugenzi wa Mashitaka alipokataa ndo sasa wakaamua kuitoa hadharani ili kutafuta public sympathy, na huyu Marando akawa anatamba kwamba sasa wanaandika barua ya kuomba Kikwete akatoe ushahidi halafu wai-leak kwenye press na kweli wakafanya hivyo. Hivi mpaka hapo hamuoni kwamba kuna tatizo hapa. Tena wanaofanya hivyo ndiyo wale wanaojifanya kupambana na ufisadi (Marando akiwa Chadema) na huku akifanya mambo ambayo mengine ni kinyume na maadili ya taaluma yake. Nchi hii ni ya ajabu sana. Mtu akiwa mwizi wa mali ya umma watu wanamuona kama shujaa na kumpongeza. Hivi kuna nini cha kupongeza hapa wakati profesa mzima wa sheria anafanya forgery ya wazi na ya kitoto ili kukomba hazina ya nchi? Halafu nyie hao hao mnapigia kelele ufisadi mwingine wakati huu wa Mahalu mnauchekea!

mbona wahusika wa mabilioni ya EPA wanadunda wanapelekeshwa kina maranda hao kagoda wako wapi, meremeta, deep green mbona wanapeta so akamuona mahalu ndo mnyonge amuangushie jumba bovu au? angekuwa na nia ya kweli angeanza na wale mabig fish otherwise si tunaona ni visasi tu anachagua mafisadi wa kushtaki
 
@Mbopo & W.J Malecela nimewapa sana kwa maelezo yenu, but inabidi mkumbuke kunamengi tunayajua yaliyo jificha kipindi Prof. akiwa Italy na Kikwete akiwa Waziri wa mambo ya Nje, usifanye kulaumu wachangia mada na Will kuweka msisitizo. Hii isue, jamani kuambo mengi sana ambayo yametokea kwy deal hii na Mm nina some document nitazi scan apa JF soon, nadhani kwa sasa naofia usalama wangu but kama ninaweza ku prove sitapata madhara yeyote nitazi release. mtaona jinsi Mkuu alivyo weka sign mwenye na kukubaliana na iyo contract akiwa kama Waziri mwenye dhamana ya Malizetu zote zilizo nje ya Nchi.
 
Sisi wanyonge Atuwezi kuchangia bali tunashukuru kwa yote, Yetu Macho tusubiri mwisho wake.
 
Kwani Jk akiwa waziri wa mambo ya nje ndio kusema mabalozi wote wanamtumikia yeye?.. balozi huchaguliwa na rais hivyo ni vizuri mtambue nguvu ya Mkapa na kwa nini ametoa ushahidi unamlinda yeye na serikali yake. Hii haina maana kwamba JK hawezi kuweka mashtaka yanayowahusu viongozi waliokuwa ktk wizara yake kwa sababu nanua fika wakati wa Mkapa wapo mabolizi wengi tu waliokuwa maadui wa Mtandao..

Swala la muhimu kwetu sio kujigubika ktk unafiki na ushabiki wa JK na Mkapa bali tulitazame swala zima kwa maslahi ya taifa. kama kweli kulikuwepo na Ufisadi basi hakuna makosa Mahalu kufikishwa mbele ya sheria. Hao kina RACHEL siku yao inakuja na yatakuja maswali kaa haya kwani hata jambazi huwa halikosi watetezi.
 
Lakini hapa hata Ushahidi JK utatolewa mahakamani maana alishaliambia bunge (2004) akiwa waziri kuwa ununuzi umefanyika kwa kufuTA TARATIBU ZOTE ZA MANUNUZI so hata yeye anajua kuwa Mahalu hana kesi hapa serikali inatafuta mlango nwa kutokea tu,
 
UTETEZI uliotolewa mahakamani kwa njia ya maandishi na Rais mstaafu Benjamin Mkapa katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, imemuweka njia panda Rais Jakaya Kikwete, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Mkapa ambaye ni shahidi wa pili wa kesi hiyo alitoa utetezi huo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam hivi karibuni ambao unaweza kuandika historia mpya katika mwenendo wa kesi nchini, kupitia kiapo chake ambacho kiliwasilishwa mahakamani na wakili wa mshtakiwa huyo, Mabere Marando.
Duru za kisheria zililiambia gazeti hili kuwa utetezi wa Mkapa kwa Profesa Mahalu ambao umepingana na upande wa serikali, utamuweka njia panda Rais Kikwete kwani hawezi kuipinga serikali yake inayoendesha kesi hiyo.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata kutoka vyanzo vya kuaminika zinaeleza kwamba kabla ya Mkapa kuwasilisha utetezi wake kwa maandishi, zilifanyika juhudi kubwa za makusudi kujaribu kumzuia kiongozi huyo mstaafu kuchukua uamuzi huo.
Chanzo kimoja cha habari kinaeleza kuwa mmoja wa watu ambao walikuwa wakitarajiwa kumfikia Mkapa na kujaribu kumshawishi kuutafakari upya uamuzi wake huo ni Waziri Mkuu mstaafu.
Hata hivyo, Tanzania Daima Jumatano ilishindwa kuthibitisha iwapo viongozi hao wawili wastaafu walikutana na wakajadiliana kuhusu jambo hilo, kabla Mkapa hajawasilisha rasmi utetezi wake huo.
Katika moja ya vipengele 13 vya kiapo hicho, pasipo kutaja jina, maelezo ya Mkapa, yanamgusa moja kwa moja Rais Jakaya Kikwete ambaye wakati Mkapa akiwa madarakani alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mmoja wa wanasheria maarufu nchini ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe, alisema ushahidi wa Mkapa unaonyesha kuwa kila kilichofanywa na serikali yake wakati Kikwete akiwa Mambo ya Nje, kilikuwa sahihi na kilipata baraka za serikali.
“Kama Mkapa anasema kila kitu kilikuwa sahihi, Kikwete ambaye serikali yake ndiyo iliyofungua na kuendesha kesi hiyo, atakapotoa ushahidi wake, atawezaje kumpinga Mkapa, lakini pia atawezaje kuipinga serikali yake mwenyewe?” alisema.
Wakili huyo ambaye alisema anasubiri kwa hamu kuona mwisho wa kesi hiyo aliyoiita ya kihistoria, alisema kama Rais Kikwete akiamua kutoa ushahidi kuitetea serikali yake wakati Mkapa amekwishaiumbua kuna hatari ya kesi hiyo kuibua mgongano kati ya serikali ya Mkapa na ya Kikwete.
Alisisitiza kuwa Kikwete yuko njia panda kwani kama ataamua kuitetea serikali yake, maelezo aliyoyatoa bungeni kuhusiana na ununuzi wa jengo la balozi linalolalamikiwa, yatamweka katika wakati mgumu kisiasa na kisheria.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa Agosti 3, 2004, Kikwete alitoa maelezo bungeni kuhusu utata uliokuwapo awali kuhusu ununuzi wa jengo hilo la ubalozi.
Kikwete katika maelezo yake hayo ambayo yako pia katika kumbukumbu rasmi za Bunge (Hansard) anaeleza, “Mheshimiwa Naibu Spika mwaka 2001/02 wizara ilinunua jengo la ubalozi counsel katika ubalozi wa Rome katika jitihada za kuondokana na tatizo la kupanga majumba ya watu huko nje na pia kupunguza gharama za kuendelea kulipa pango la nyumba kila mwaka.
“Ununuzi wa jengo hili ulifuata taratibu zote za manunuzi ya majengo ya serikali kwa kuzishirikisha wizara za ujenzi, ardhi na maendeleo ya makazi pamoja na Wizara ya Fedha.
“...Jengo lilifanyiwa tathmini na wataalamu wetu na kukubaliana na ununuzi wa Euro 3,098,781.40 Machi 6, 2002 fedha za awamu ya kwanza katika ubalozi wa Rome zilipelekwa nazo zilikuwa shilingi 700,000,000 Juni 28, 2002 zilipelekwa shilingi 120, 000,000.
“Mwishoni mwa Agosti 26, 2002 zilipelekwa shilingi 1,000,000,000 jumla ya fedha zilizokuwa zimepelekwa zikafikia shilingi 2,900,000,000 na baada ya hapo ubalozi wetu ulitekeleza taratibu zote za ununuzi wa jengo na kumlipa mwenye nyuma kiasi hicho cha fedha,” alieleza Kikwete.
Hadi jana, Ikulu ilikuwa haijajibu ombi la wakili wa Mahalu, Mabere Marando, la kutaka afike mahakamani kutoa ushahidi wake juu ya kesi hiyo.
Akizungumza na gazeti hili jana, Marando alisema hawajapata majibu ya Ikulu, lakini pia hawana haraka sana kwani hata mshitakiwa mwenyewe (Mahalu), hajaanza kujitetea.
Marando alisema Katiba haimzuii Rais kuja kutoa ushahidi mahakamani, lakini kama atashindwa anaweza kutoa kwa maandishi kama alivyofanya Mkapa.
“Akishindwa kabisa kuja, basi tutaomba kesi iahirishwe hadi atakapomaliza muda wake wa urais 2015,” alisema Marando.
Gazeti hili lilipowasiliana na Msemaji wa Ikulu, Salva Rweyemamu, kwa njia ya simu kujua endapo Rais amekubali kutoa ushahidi katika kesi hiyo, hakuweza kupatikana kwani simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
Kama ilivyokuwa kwa Salva simu ya Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, ilikuwa ikiita muda mrefu bila majibu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi, pia hakuweza kujibu swali hilo.
Katika hati ya kiapo chake cha Machi 31 mwaka huu, ambayo imeandaliwa kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Nyaraka (The Registration of Documents Act, Cap. 117 of 2002), Mkapa anaeleza kuwa kila kilichofanywa na Mahalu kilikuwa sahihi na kilikuwa na baraka ya serikali aliyokuwa akiingoza toka mwaka 1995-2005.
Ushahidi huo wa rais Mkapa umeorodhesha maelezo yake yaliyoainishwa katika vipengele 13.
Mkapa katika utetezi wake huo anadai kuwa mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo la ubalozi lililoko katika mtaa wa Vialle Cortina d’Ampezzo 185 mjini Rome ulizingatia sera ya serikali ya upatikanaji au ujenzi wa majengo ya kudumu ya ofisi na makazi na kwamba ulizingatia maslahi ya taifa.
Hati hiyo ya kiapo ambayo tayari wakili Marando amesema ameishaiwasilisha pia Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Eliezer Feleshi, inaanza kwa kusema, “Mimi Benjamin Mkapa, mtu mzima, Mkristo, mkazi wa Dar es Salaam, ninaapa kama ifuatavyo, ’nilikuwa Rais mtendaji wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vipindi viliwili mwaka 1995-2005 na nina uhakika wa yote haya nitakayosema ndani ya kiapo hiki.’”
Katika kiapo hicho Mkapa anadai pia kuwa alifahamishwa na watendaji wa serikali aliyokuwa akiiongoza jinsi mchakato uliofanyika na ripoti za uthamini wa serikali zilizotumika katika kufikia hatua ya kununua jengo hilo la ubalozi.
Anadai kuwa tathmini ya jengo hilo ambalo Mahalu anadaiwa kufanya udanganyifu na wizi kwa kulipa fedha kinyume na ilivyotajwa katika mkataba ambayo ilifanywa na serikali ya awamu ya tatu kupitia wizara mbili tofauti, Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Ardhi na Maendeleo Mijini.
Anaendelea kudai kuwa anatambua kuwa ripoti ya serikali ya uthamini wa jengo hilo iliandaliwa na Wizara ya Ujenzi kwa kiwango cha dola za Marekani milioni tatu na Wizara ya Ardhi kwa thamani ya euro milioni 5.5.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo kupitia mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulikuwa wa aina mbili, mmoja ni rasmi na mwingine wa kibiashara na kuongeza kuwa kwa mujibu wa taratibu ya serikali ya Italia na kuwa hilo lilifanyika kwa baraka za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Shahidi huyo wa Mahalu anadai pia kuwa kwa mujibu wa kiapo chake anakumbuka vyema taarifa ya serikali iliyotolewa bungeni Agosti 3 mwaka 2004 iliyosema na kuthibitisha kuwa taratibu zote zinazohusiana na manunuzi ya jengo kwa mujibu wa maelekezo ya serikali, zilifuatwa na kwamba muuzaji wa jengo hiilo alilipwa fedha zote.
Akimwelezea Mahalu katika utetezi wake, Mkapa alidai katika kipindi chote alichokuwa Rais wa nchi alifanya kazi na mshtakiwa huyo katika nyadhifa mbalimbali za utumishi wa umma na kwamba mshtakiwa huyo ni mtu wa tabia njema, mkweli, mwaminifu na mchapaji kazi.
Mkapa anahitimisha utetezi wake kwa kueleza kuwa kutokana na mwenendo huo wa kutukuka, Rais wa Italia alimpatia moja ya tuzo za heshima yenye hadhi ya juu kabisa ya taifa hilo Profesa Mahalu, muda mrefu baada ya balozi huyo kuwa ameshaondoka nchini humo.
Katika kesi hiyo namba 1/2007, inayosikilizwa na Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Kisutu, Ilivin Mugeta, Mahalu anashtakiwa pamoja na Grace Martin.
Mahalu na Martin wanatuhumiwa kwa wizi wa sh bilioni tatu katika ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Rome.
Mapema mwaka 2007, Jamhuri kupitia mawakili wake toka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ben Lincoln na Ponsian Lukosi, iliwafikisha mahakamani hapo kwa mara ya kwanza washtakiwa hao kwa makosa ya uhujumu uchumi. Mahalu anakusudia kupeleka jumla ya mashahidi 10.
Mashahidi hao ni mteja wake (Mahalu), Mkapa, Rais Jakaya Kikwete, kwani wakati akinunua jengo hilo ndiye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na ndiye aliyempa nguvu ya kisheria ya kuendelea na ununuzi wa jengo hilo, aliyekuwa waziri wa Ujenzi wa John Magufuli.
Mashahidi wengine ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba ambaye pia anakabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bil. 11.7.
 
You are better than this! Yaani badala ya nyie kushangazwa na kitendo cha Mkapa kujishushia hadhi yake kwa sababu tu ya urafiki, sasa mnamshutumu Kikwete kwa kufanya kitu ambacho asingefanya mngemlaumu. Sisi wengine tunajua kabisa juhudi ambazo Mkapa alizifanya kuhakikisha kwamba Mahalu hashitakiwi kwa sababu tu ya urafiki wao. Lakini ukweli ni kwamba ushahidi uliotolewa mahakamani umemuumbua Mahalu na ndiyo Maana Marando na wenzake walihaha sana kukimbia kila mahakama ili Mahalu asijitetee wakati tayayri kuna uamuzi wa kwamba ana kesi ya kujibu.

Hii affidavit ya Mkapa ilikuwa itumike kuombe Nolle Prosequi lakini Mkurugenzi wa Mashitaka alipokataa ndo sasa wakaamua kuitoa hadharani ili kutafuta public sympathy, na huyu Marando akawa anatamba kwamba sasa wanaandika barua ya kuomba Kikwete akatoe ushahidi halafu wai-leak kwenye press na kweli wakafanya hivyo. Hivi mpaka hapo hamuoni kwamba kuna tatizo hapa. Tena wanaofanya hivyo ndiyo wale wanaojifanya kupambana na ufisadi (Marando akiwa Chadema) na huku akifanya mambo ambayo mengine ni kinyume na maadili ya taaluma yake. Nchi hii ni ya ajabu sana. Mtu akiwa mwizi wa mali ya umma watu wanamuona kama shujaa na kumpongeza. Hivi kuna nini cha kupongeza hapa wakati profesa mzima wa sheria anafanya forgery ya wazi na ya kitoto ili kukomba hazina ya nchi? Halafu nyie hao hao mnapigia kelele ufisadi mwingine wakati huu wa Mahalu mnauchekea!

Mbopo,
3 Aug 2004 wakati JK anatoa report ya wizara yake pale Mjengoni kuwa manunuzi ya mjengo huo hauna mushkeli na yamefata taratibu zote za manunuzi za serikali,.......
Hapa alikuwa anongelea jengo gani?
Hapa naye alikuwa MWIVI ila sasa kama RAIS kaacha WIVI?
Ama alikuwa KILAZA na alikuwa asoma kitu asokijua kama JUHA ili siku iingie akakunje mshiko dirishani?

Je JK hapa alikuwa ana FORGE nini?
 
Mimi nafikiri wewe ume-widen scope ya discussion na kwa namna hiyo huwezi kupata sense ya tunachuzungumza. Issue hapa ni whether Mahalu ameonewa au la kwa kumfungulia mashtaka. Kati ya wote waliotoa utetezi kwa Mahalu kwa kutumia hoja yao hiyo hawajaonyesha kwamba (a) kuna bifu kati ya Rais na Mahalu; (b) kwamba wizi huo haujafanyika na wala Mahalu hajahusika; (c) kwamba mashitaka hayo yamchochewa na chuki tu aliyonayo rais dhidi ya Mahalu. Lakini kilichojitokeza hapa ni kwamba eti kwa sababu Mkapa anakwenda kutoa ushahidi mahakamani, basi Mahalu ameshinda kesi na kwamba yeye Mahalu ameonewa.

Huu ni mtazamo finyu na hupati sababu yoyote ya kufikia conclusion hiyo zaidi ya chuki ambayo watu wanayo dhidi ya rais. Mahalu ana kesi ya kujibu and it doesn't matter who he brings as a witness lakini kudhani kwamba ushahidi wa Mkapa ndiyo ukweli wa mambo ni kutokuelewa mambo kwa hali ya juu kwa sababu kama inadhaniwa kwamba Mkapa ni msafi basi wangeangalia jinsi watu wote aliokuwa amewaamini wakati wa utawala wake walivyozalisha makashfa. Muangalie Ballali, Mramba, Yona, Mgonja, Mahalu, Kitine, Kigoda na wengine wengi na yuko tayari kuwatetea wote hao.

Mimi nafikiri tumejikita kudhani kwamba mafisadi ni wale tu waliotajwa Mwembe yanga na Tabora na kwamba wale ambao wanachukuliwa hatua kivingine basi hao si mafisadi bali ni maadui wa JK ambao ana bifu nao. Much as kuna safari ndefu katika kuchukua hatua dhidi ya hao waliotajwa, lakini ukweli ni kwamba hatua hizi zinatia moyo. Kwa mwenendo huu ni wazi kwamba very soon tutaambiwa kwamba hata Yona, Mramba na Mgonja tutaambiwa wanaonewa. This is unfair to the war against corruption.

toka jana nakamwambia kijana hii kesi wewe umeanza kuisikia mahakamani lakini kiini cha kesi hukijui hata kidogo....juu unaona wizi wa bilion 3 lakini ki - ukweli hakuna wizi na hili jk aliwahi kulikiri bungeni.......kuna sababu nyingine lakini unang'ang'a tu......toka jana nakamwambia mahalu atashinda kesi......
 
Ndugu yangu Mbopo inaonekana huelewi kabisa mfumo wa serikali unavyokwenda, hakuna manunuzi au malipo ya serikali yanayoweza kufanywa na mtu mmoja hiyo kitu haipo dunia yeyote ile. Kesi ya Mahalu na Liyumba zinafanana kabisa. Ukifanya maamuzi serikalini kwa kutofautiana na wanasiasa lazima yatakukuta yakina Mahalu na Liyumba utakuja amini tu iwe leo au kesho. Hawa watu walifanya kazi tofauti na wanasiasa waliopo that's why wanalipiza kisasi, ni kesi za kisiasa but nakuhakikishia hizi kesi wote watashinda kamwe ukweli hauwezi kufichika milele.
 
Sisi wengine tusiokuwa wanasheria ni vigumu kujua kinachoendelea; mimi nilidhani ushahidi muimu ni wa yule aliyetuuzia jengo hilo, akidhibitisha ya kwamba fedha alizolipwa ni kidogo ya zile ambazo serikali ya Tanzania ilitoa, wizi unakuwa umedhibitika bila ya kujali JK au Mkapa wanasemaje.
 
Some of you guys need to differentiate FACTS from FICTION in this discourse. I am quoting, "Muangalie Ballali, Mramba, Yona, Mgonja, Mahalu, Kitine, Kigoda na wengine wengi na yuko tayari kuwatetea wote hao".
I dare say, IT IS A FACT that USHAHIDI WA MKAPA katika yote hayo utawaumbua wengi. Sasa if Feleshi reads this, let him deny the fact kwamba hakwenda kumsihi BWM to withdraw the said affidavit. WHY?
Answer: Ushahidi wa BWM umevuruga intention ya kumfunga Mahalu which is precisely what WABAYA wake have sought all along. Ndiyo, the DEFENCE has been buisy averting just that. Hata kama wamezunguka wapi na wapi, hiyo ni haki yao. Wewe ungefanya hivyo hivyo kama unaninginizwa as is the case katika hili suala.

You go asfar as saying, "Kwa mwenendo huu ni wazi kwamba very soon tutaambiwa kwamba hata Yona, Mramba na Mgonja tutaambiwa wanaonewa. This is unfair to the war against corruption"
That is fiction!
 
Back
Top Bottom