jamadari
JF-Expert Member
- Feb 13, 2010
- 295
- 92
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, imemkingia kifua Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, kuwa alitaja mali zake wakati akitoka madarakani.
Kwa mujibu wa sekretarieti hiyo, Mkapa ambaye alikuwa Rais kati ya mwaka 1995 hadi 2005, aliwasilisha tamko la mali zake baada ya kumaliza awamu yake ya uongozi.
Sekretarieti hiyo ilisema Mkapa alifanya hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 9(1) D cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995. Tamko la sekretarieti hiyo linafuatia taarifa zilizotolewa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni kuwa Mkapa alitangaza mali zake wakati anaingia madarakani mwaka 1995 lakini alipoondoka mwaka 2005 hakufanya hivyo.
Sekretarieti inakanusha taarifa kwamba Mkapa hakutangaza mali zake, ni uongo na huenda imetolewa kwa nia mbaya, ilisema sehemu ya taarifa ya sekretarieti hiyo.
Hata hivyo, sekretarieti hiyo imeshindwa kuweka wazi iwapo ilienda kuhakiki mali za Mkapa ili kujiridhisha kuwa kile alichojaza kwenye fomu kinalingana na hali halisi ya mali zake.
Sheria inasema sekretarieti itahakiki mali za kiongozi wa umma lakini hairuhusu kutangaza mtu anayeenda kuhakikiwa mali zake, mfano hatuwezi kusema leo tunaenda kuhakiki mali za mtu fulani Vile vile hatuwezi kusema kuwa tulihakiki mali za Mkapa au la, alisema Mataula.
CHANZO: NIPASHE
Kwa mujibu wa sekretarieti hiyo, Mkapa ambaye alikuwa Rais kati ya mwaka 1995 hadi 2005, aliwasilisha tamko la mali zake baada ya kumaliza awamu yake ya uongozi.
Sekretarieti hiyo ilisema Mkapa alifanya hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 9(1) D cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995. Tamko la sekretarieti hiyo linafuatia taarifa zilizotolewa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni kuwa Mkapa alitangaza mali zake wakati anaingia madarakani mwaka 1995 lakini alipoondoka mwaka 2005 hakufanya hivyo.
Sekretarieti inakanusha taarifa kwamba Mkapa hakutangaza mali zake, ni uongo na huenda imetolewa kwa nia mbaya, ilisema sehemu ya taarifa ya sekretarieti hiyo.
Hata hivyo, sekretarieti hiyo imeshindwa kuweka wazi iwapo ilienda kuhakiki mali za Mkapa ili kujiridhisha kuwa kile alichojaza kwenye fomu kinalingana na hali halisi ya mali zake.
Sheria inasema sekretarieti itahakiki mali za kiongozi wa umma lakini hairuhusu kutangaza mtu anayeenda kuhakikiwa mali zake, mfano hatuwezi kusema leo tunaenda kuhakiki mali za mtu fulani Vile vile hatuwezi kusema kuwa tulihakiki mali za Mkapa au la, alisema Mataula.
CHANZO: NIPASHE