Mkapa aitosa CCM, aigomea kwenda Arumeru

Sio kweli, kama Mkapa amekataa kuzindua kampeni, hizo tarehe zitakuwa zimeingiliana tuu na ratiba zake kwa sababu ndani ya CCM rushwa is the order of the day!. CCM sio tuu inanuka rushwa bali ni imeoza kwa rushwa mpaka inatoa uvundo na la kuvunda siku zote halina ubani!. Kama kawaida wanaousikia huo uvundo wa rushwa, ni wale walioko nje ya CCM tuu!, kwa wana CCM wenyewe, pua zao zimeisha zoea hiyo harufu na hawaisikii kama unavyopita maeneo ya Feri, unapokelewa na harufu ila ukikaa kidogo tuu pua zinaizoea na huisikii tena!. Wenyewe wa Feri, hawaisikii kabisa!.

Ila pamoja na uoza wote huu wa rushwa huko CCM, matokeo ya uchaguzi huo ni mashindano kati ya udhalimu na uadilifu, uchafu wa rushwa vs usafi wa dhamira, ufalme vs ya demokrasia ya kweli, ukoloni wa kutawaliwa kifkra vs ya ukombozi wa kweli!. Nawahakikishia udhalimu, uchafu wa rushwa, ufalme, ukoloni wa kutawaliwa ki fikta ndio utashinda!. Naisubiri April 2 kuwathibitishia hili!.

Amini nawaambieni Udhalimu, Rushwa, Ufalme, Ukoloni wa Kifikra, Ufisadi, Udini, Ukabila na Utaifishaji wa Mali za Umma ni matokeo ya Ombwe la Uongozi hasa Rais; Kamwe havitadumu milele kwani mwisho wake umefika.

Je hamzioni dalili za mwisho wake? Maandamano kila kona ya nchi, Migomo kila pembe ya nchi na Wananchi kutokuwa na imani na Serikali yao. Amini nawaambieni mwisho wa hayo yote upo karibu sana. Uhuru dhidi ya uonevu ma watu wachache kuhodhi maliasili ya nchi unakuja kesho. Freedom is Comming Tomorrow guyz.
 
Ila pamoja na uoza wote huu wa rushwa huko CCM, matokeo ya uchaguzi huo ni mashindano kati ya udhalimu na uadilifu, uchafu wa rushwa vs usafi wa dhamira, ufalme vs ya demokrasia ya kweli, ukoloni wa kutawaliwa kifkra vs ya ukombozi wa kweli!. Nawahakikishia udhalimu, uchafu wa rushwa, ufalme, ukoloni wa kutawaliwa ki fikta ndio utashinda!. Naisubiri April 2 kuwathibitishia hili!.

Don't give up too easily! Waacha watu wapambane. There nothing wrong with trying hard, but it is insult to humanity not to try.
 
Mkapa hawezi kuitosa CCM kwani anajua vyema kuwa uwepo wa CCM kama chama chenye nguvu bungeni una maslahi makubwa kwake. Hawezi kukubali kukaa pembeni akiangalia jahazi linalomlinda asishtakiwe kwa ufisadi wake likizama na kumuacha akiwa uchi. Natarajia kuwa atafanya kampeni kubwa sana kwa CCM itakapofika mwaka 2015 wakati wa uchaguzi mkuu.
 
Wana ccm wao wanajua kuwa wameoza ndio maana wanajitaidi kuwatafuta wale watu ambao wananch hawawajui kuwa wameoza kwa ufsadi pamoja na uongoz m baya
 
UZINDUZI wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki kupitia Chama cha Mapinduzi uliokuwa ufanyike Machi 10 imeingia dosari kubwa kufuatia kukataa kwa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kufanya kazi hiyo.

Habariza kuaminika kutoka ndani ya CCM zimedai kuwa Mkapa amegoma kufungua kampeni hizo zilizokuwa zifanyike eneo la Usa River nje kidogo ya jiji la Arusha nakuna habari kuwa uongozi wa juu umelazimika kuahirisha na kusogeza mbele siku ya uzinduzi.

Ofisa mmoja mwandamizi wa CCM ameliambia Tanzania Daima kuwa Mkapa amechukua uamuzi huo baada ya kubainika kuwa ataaibika kutokana na msuguano mkali wa chini kwa chini baina ya makundi yaliyoibuka tangu wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Mtoa taarifa wetu amesema kuwa Mkapa ametoa sharti zito la kuutaka uongozi wa wilaya, mkoa na taifa kuhakikisha kuwa umeshughulikia kikamilifu msuguano wa makundi hayo, la sivyo hataweza kushiriki uzinduzi wa kampeni hizo. Habari zimedai kuwa Katibu wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda, Mkurugenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Elishiria Kaaya, na Mwenyekiti wa UVCCM mkoa, James Milya, wameitwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili msuguano huo.

Imedaiwa kuwa wengine walioitwa ni pamoja na wagombea wawili waliokuwa wakichuana kuwania kuteuliwa kugombea ubunge wa jimbo hilo, William Sarakikya, na Elirema Kaaya (ambaye aliwahi kushikiliwa na Takukuru akituhumiwa kutoa rushwa kwa wagombea).

Taarifa zimedai kuwa hali ndani ya chama hicho ngazi ya mkoa ni mbaya pamoja na wagombea walioangushwa na Siyoi Sumari kukubaliana kuwa wataungana pamoja kumpigia kampeni mwezao ili ashinde. Hata hivyo, habari zimethibitisha kuwa uhasama baina ya makundi hayo, lile la James Milya na Mary Chatanda, kwa upande mwingine, yamekuwa katika mvutano wa siku nyingi na kwamba uchaguzi huo mdogo umeibua uhasama huo.

Alipopigiwa simu kuthibitisha kusogezwa mbele kwa uzinduzi wa kampeni hizo na ukweli wa kugoma kwa Mkapa, Chatanda alidai kuwa yuko barabarani na akaombwa apigiwe simu kesho (leo). Hata hivyo, alipoambiwa ni jambo la dharura, alikata simu na kuzima.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM taifa, Nape Nnauye, alipoulizwa juu ya kukataa kwa Rais Mstaafu Mkapa, alikana kujua lolote huku akitaka mwandishi amuulize aliyemwambia habari hizi. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Arusha, James Millya, hakupatikana na mmoja wa watu wake wa karibu, alilieleza Tanzania Daima kuwa kiongozi huyo machachari wa UVCCM, alikuwa jijini Dar es Salaam kikazi.

Mkapa aliteuliwa hivi karibuni na makao makuu ya CCM kuzindua rasmi kampeni za ubunge wa jimbo hilo, ikidaiwa kuwa ndiye mmoja wa viongozi wachache wenye uwezo mkubwa wa ushawishi katika masuala ya kampeni. Itakumbukwa kuwa Mkapa ndiye aliyezindua na kisha kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga mkoani Tabora, ambako kampeni zake baina ya CCM na CHADEMA zilivunja rekodi kwa mbwembwe, mikikimikiki na tambo za kila aina ikiwa ni pamoja na matumizi makubwa ya fedha.

Uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki unatabiriwa kuwa utakuwa na ushindani mkubwa kati ya wagombea wawili wa vyama vya CCM (ambacho kimemsimamisha mtoto wa marehemu Jeremiah Sumari), Siyoi Sumari, na CHADEMA ambacho kimemteua Joshua Nassari kupeperusha bendera yake.


Source: Tanzania Daima

Craaaaaaaaaaaaaaaaaaap kumbe gazeti lenyewe ni la Tanzania Daima la watu ambao hufikiri kwa kutumia masaburi

 
kumbe jf nimegundua hamsomi habari mkaelewa!gazeti limesema mkapa amewapa sharti uongoz ccm mkoa na wilaya wautatue kwanza ndo akafungue kampeni,na najua hawez kukiangusha chama na atakwenda kufungua na kufunga kampeni,ushindi n wa ccm
 
kama mkapa amegoma wamtume kingunge ngombale mwiri nadhani ataimudu hii kazi.!
 
Sio kweli, kama Mkapa amekataa kuzindua kampeni, hizo tarehe zitakuwa zimeingiliana tuu na ratiba zake kwa sababu ndani ya CCM rushwa is the order of the day!. CCM sio tuu inanuka rushwa bali ni imeoza kwa rushwa mpaka inatoa uvundo na la kuvunda siku zote halina ubani!. Kama kawaida wanaousikia huo uvundo wa rushwa, ni wale walioko nje ya CCM tuu!, kwa wana CCM wenyewe, pua zao zimeisha zoea hiyo harufu na hawaisikii kama unavyopita maeneo ya Feri, unapokelewa na harufu ila ukikaa kidogo tuu pua zinaizoea na huisikii tena!. Wenyewe wa Feri, hawaisikii kabisa!.

Ila pamoja na uoza wote huu wa rushwa huko CCM, matokeo ya uchaguzi huo ni mashindano kati ya udhalimu na uadilifu, uchafu wa rushwa vs usafi wa dhamira, ufalme vs ya demokrasia ya kweli, ukoloni wa kutawaliwa kifkra vs ya ukombozi wa kweli!. Nawahakikishia udhalimu, uchafu wa rushwa, ufalme, ukoloni wa kutawaliwa ki fikta ndio utashinda!. Naisubiri April 2 kuwathibitishia hili!.
Mkuu Pasco unanifurahisha sana na comment zako, very said mkuu, pamoja.
 
Mkapa, at least, ameona tatizo
Gogoro la wagombea wakati wa kura za maoni linaweza kusababisha zaama kwa CCM
 
UZINDUZI wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki kupitia Chama cha Mapinduzi uliokuwa ufanyike Machi 10 imeingia dosari kubwa kufuatia kukataa kwa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kufanya kazi hiyo.

Habariza kuaminika kutoka ndani ya CCM zimedai kuwa Mkapa amegoma kufungua kampeni hizo zilizokuwa zifanyike eneo la Usa River nje kidogo ya jiji la Arusha nakuna habari kuwa uongozi wa juu umelazimika kuahirisha na kusogeza mbele siku ya uzinduzi.

Ofisa mmoja mwandamizi wa CCM ameliambia Tanzania Daima kuwa Mkapa amechukua uamuzi huo baada ya kubainika kuwa ataaibika kutokana na msuguano mkali wa chini kwa chini baina ya makundi yaliyoibuka tangu wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Mtoa taarifa wetu amesema kuwa Mkapa ametoa sharti zito la kuutaka uongozi wa wilaya, mkoa na taifa kuhakikisha kuwa umeshughulikia kikamilifu msuguano wa makundi hayo, la sivyo hataweza kushiriki uzinduzi wa kampeni hizo. Habari zimedai kuwa Katibu wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda, Mkurugenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Elishiria Kaaya, na Mwenyekiti wa UVCCM mkoa, James Milya, wameitwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili msuguano huo.

Imedaiwa kuwa wengine walioitwa ni pamoja na wagombea wawili waliokuwa wakichuana kuwania kuteuliwa kugombea ubunge wa jimbo hilo, William Sarakikya, na Elirema Kaaya (ambaye aliwahi kushikiliwa na Takukuru akituhumiwa kutoa rushwa kwa wagombea).

Taarifa zimedai kuwa hali ndani ya chama hicho ngazi ya mkoa ni mbaya pamoja na wagombea walioangushwa na Siyoi Sumari kukubaliana kuwa wataungana pamoja kumpigia kampeni mwezao ili ashinde. Hata hivyo, habari zimethibitisha kuwa uhasama baina ya makundi hayo, lile la James Milya na Mary Chatanda, kwa upande mwingine, yamekuwa katika mvutano wa siku nyingi na kwamba uchaguzi huo mdogo umeibua uhasama huo.

Alipopigiwa simu kuthibitisha kusogezwa mbele kwa uzinduzi wa kampeni hizo na ukweli wa kugoma kwa Mkapa, Chatanda alidai kuwa yuko barabarani na akaombwa apigiwe simu kesho (leo). Hata hivyo, alipoambiwa ni jambo la dharura, alikata simu na kuzima.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM taifa, Nape Nnauye, alipoulizwa juu ya kukataa kwa Rais Mstaafu Mkapa, alikana kujua lolote huku akitaka mwandishi amuulize aliyemwambia habari hizi. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Arusha, James Millya, hakupatikana na mmoja wa watu wake wa karibu, alilieleza Tanzania Daima kuwa kiongozi huyo machachari wa UVCCM, alikuwa jijini Dar es Salaam kikazi.

Mkapa aliteuliwa hivi karibuni na makao makuu ya CCM kuzindua rasmi kampeni za ubunge wa jimbo hilo, ikidaiwa kuwa ndiye mmoja wa viongozi wachache wenye uwezo mkubwa wa ushawishi katika masuala ya kampeni. Itakumbukwa kuwa Mkapa ndiye aliyezindua na kisha kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga mkoani Tabora, ambako kampeni zake baina ya CCM na CHADEMA zilivunja rekodi kwa mbwembwe, mikikimikiki na tambo za kila aina ikiwa ni pamoja na matumizi makubwa ya fedha.

Uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki unatabiriwa kuwa utakuwa na ushindani mkubwa kati ya wagombea wawili wa vyama vya CCM (ambacho kimemsimamisha mtoto wa marehemu Jeremiah Sumari), Siyoi Sumari, na CHADEMA ambacho kimemteua Joshua Nassari kupeperusha bendera yake.


Source: Tanzania Daima

Kwenye red hapo juu: sasa huyo Mkurugenzi wa AICC anahusika vipi na mambo ya CCM?
 
Naomba mnikumbushe siku ya mwisho bwm kuhutubia wakazi wa arusha. Siasa zimebadilika sana zaidi ya uwezo wake wa kufikiri na kaliona hilo ndo maana anasubiri kupima upepo kwanza kwenye uzinduzi wa cdm.
 
Kutakuwa na tatizo zaid mana hawa CCM wana nyuso za mbuzi, hilo kwao sio tatizo mana JK aliwanadi mafisadi bila hata aibu, sioni kwann Mkapa ajifanye ni mgeni na huo utaratibu.

haimpi shida hata yeye si fisadi tu umesahau Kiwira ???
 
Jamani, jamani, jamani, hii kali...! Mkapa mwenyewe ana zigo la tuhuma, sasa hiyo aibu itoke wapi? Nilidhani ndege wafananao huruka pamoja, yaani hadi nasikia kichefuchefu!

Watever the reason may be ila kama kweli kawapa ultimatum hiyo amenifurahisha......baba akijisaidia pasipostahili kwa ulevi hilo ni kosa. Lakini baba bora ni yule atakayekataza wengine kutenda kama yeye kwa kuwa amegundua makosa yake.

Hii ni busara kubwa sana..............Eeenh muumba mbingu na ardhi...utuangalie waja wako kwa huruma
 
Dhubutu yake uwagomee CCM mbona patawaka na kuchimbika kwa kwenda mbele.Angekuwa safi kama warioba angethubutu kusimama na kuwaambia sintoweza mpaka mtimize hili na lile.Lakini kwa kuwa nae ni mhusika wa yote yanayodeal ndani ya chama basi mzigo ni wake hakuna usaliti beba baba beba mzigo wetu wetu huo.

Hakuna wa kuutetea bali ni CCM wenyewe na yoyote yule mwenye maslahi vinginevyo kutoboka kwa mtumbwi waokozi ni abiria waliomo ndani ya mtumbwi na si vinginevyo.Vinginevyo kama ukikimbia kuokoa Jahazi hakika ujue kupiga mbizi,kwa kuwa wananchi ndio bahari yenyewe ambayo imebeba Jahazi la CCM.
 
Back
Top Bottom