Mkanganyiko wa Maadili ya Madaktari wakati wa Migomo

Ndugu wanajamvi wenzangu naomba tudiscuss hii kitu,jana kupitia vyombo mbalimbali vya habari madaktari takribani 200 ambao walikuwa katika mafunzo ya vitendo/Interns waliamua kuomba msamaha kwa serikali na watanzania kwa ujumla kwa kitendo chao cha mgomo ambao ulileta madhara ya baadhi ya wagonjwa kufariki kwa kukosa matibabu nk. Binafsi nimeshindwa kuwaelewa kilichowatuma kuja kuomba msamaha ni njaa kutokana na wengi wao kufutiwa vyeti vya usajili kama professional doctors ambayo ingewapelekea kukosa sifa za kuajiriwa au ni kujutia athari zilizosababishwa na mgomo wao ikiwemo vifo vya watanzania ambo ni innocent? Je ni kweli kwamba sababu za wao kugoma hazikuwa na mashiko yoyote na ndio maana wakaamua kuomba msamaha au yale yaliyowafanya kugoma yote yametekelezwa kwa kiwango cha kuridhisha?
Je ni sawa kwa wao kuomba msamaha serikali na watanzania kwa sasa au ni kama wamepotea hawajui what to do and what will come next?

Nawasilisha hoja.


Source:media (tv's and news papers)
 
'Wote wale ni vijana wa Chama cha Mapinduzi.Na wamefanya vile 'strategically' ili kumpa hadhi Rais na Serikali yake' amesema mmoja wa Madaktari Bingwa wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili niliyezungumza naye muda mfupi uliopita.'Migomo inaratibiwa naviongozi wetu.Kama mtu hataki,huwa hatumlazimishi.Wao walikuwa wapi muda wote na hata kugoma? Wote wale ni UVCCM.' aliongeza. Kuna taarifa kuwa Nape Nnauye alizungumza na watioa tamko kabla ya kulitoa tamko lao. Usaliti juu ya usaliti.
 
Weka source Mkuu Mzee Tupatupa,..ila si taarifa za kushangaza kwani yule Sr.Paul Swakala alikuwa pale Bugando kama kadi enzi za uongozi wake(this was known)
 
Ngiri ukimjkimbiza sana akiona anazidiwa huwa anakugeukia na kuamza kukukimbiza wewe. Na paka ukimpiga sana huwa anabadilika na kuanza kukurarua. Ila Ngiri anaendelea kubaki ngiri na paka anabaki kuwa paka! Hao madaktari kama waliamini kile walichokuwa wanakigomea watageuka kama ngiri au kubadilika kama paka, na watakuwa vichomi kwa serikali.
Naamini hivyo!
 
Nakumbuka wakati niko shule nilishalazimishwa kuandika barua ya kukiri hata yale makosa ambayo hayakuwa yangu ili suspension iondolewe, lakini niliona ni ujinga mtupu ndio ingekuwa kama reference yao kwa next time kama nitakuwa na kosa kunifukuza shule.

Sasa mimi nikajiuliza hii shule ni Private kwa nini nisome kwa vitisho vya kuogopa kufukuzwa? nikahama shule, na ikumbukwe kipindi chetu hakukuwa na shule Private zaidi ya shule za Wazazi.

Back to topic hawa Interns hakuna mwenye ubavu wa kusurvive street, na hiyo statement wameandikiwa huyo anayejifanya ndio kiongozi wao yeye amesaini tu ili waweze kurudishwa kibaruani. hapo JK kicheko mpaka jino la mwisho yeye ndio muajiri namba 1.
 
Nilidhani umebadilika kidogo siku hizi kumbe ni kweli "maji huwa hayasahau baridi!" na "mwendawazimu huwa haponi, anapata nafuu tu!"
 
Vipi Dr Slaa si alijifanya kudandia hoja ya madaktari pamoja na nyie Pro-Chadema saizi mnang'aa sharubu tu baada madaktari kuomba msamaha.

Hawa ni Interns, ni wanafunzi kwa njia ya vitendo na siyo Madaktari.
source: Jakaya Kikwete.

N:b'
Daktari Bingwa wa upasuaji wa watoto Catherine Mng'ong'o ameshaacha kazi rasmi Muhimbili. nyinyi chekeleeni ujinga tu, sisi tunaouuguza ndio tunajuwa nini kinaendelea. hii siyo siasa japo mnataka kuifanya siasa.
 
The faint heart never won. Doctors must bodly step forward and demand their rights. Industrial action is about defiance and not compliance.
 
hata mi nilihisi kitu hicho maana haiingii akilini wagome kwa mbwembwe vile halaf eti waje waombe msamaha kirahisi vile...it is fishy!
 
Kuna Mtu amenimegea tetesi kwamba wamepewa Pesa nyingi na Ikulu wakutane na madactari woote waliowekwa pembeni wawa-convice kwamba wataomba msamaha kwa niaba yao na Serikali itatoa tamko la kuwasamehena itawarudisha.
 
Wait a minute, ni madaktari Bingwa au ni wanafunzi kwa njia ya Vitendo ambao wamefutiwa leseni zao? msichanganye habari tafadhali.

Hawa JK hawatambui kama ni madaktari bali ni interns ( wanafunzi kwa njia ya vitendo ). siwezi kuwashangaa kwa hilo hawana ubavu wa kufia wanachoamini bali njaa ya muda mfupi imewanyong'onyesha na kukubali kutumiwa.

Lakini all in all swala hili haliwezi kutuondowa kwenye hoja ya mauwaji ya Mwangosi.
 
Back
Top Bottom