Katika hali ya kutapatapa na kuhakikisha mafisadi hawaguswi, juhudi za maksudi zimeanza kuchagiza kuzibwa midomo watu wote wanaojaribu kuongea ukweli.
Jitihada hizo zimeanza na gazeti la Rai, toleo la jana.
Katika gazeti hilo, mwandishi amelituhumu mwanahalisi kwamba ni jukwaa linalotumiwa na wabaya wa JK ili kuiangusha serikali.
Wanadai Mwanahalisi limejiandaa kuuhadaa umma kuwa JK hafai kwa kumhusisha JK na ufisadi wa nci hii na kusema yeye ni sehemu ya ufisadi au ni mfadhili wa uozo huo.
Wanalinukuu gazeti la Mwanahalisi la Jumatano hii kwa kujaribu kuonyesha uhusiano wa Manji, Rostam na Kagoda.
Pia wamechukizwa na makala inayosema "JK, jisafishe Kwanza mwenyewe kabla ya kusafisha CCM" nk. Wakati huo huo, Gazeti la mwanahalisi limeripoti kwamba toleo lao la wiki iliyopita lilihujumiwa kwa baadi ya vizito kununua nakala nyingi kwenye mikoa ya Mbeya ili watu wakose kusoma habari za Dowans nk ilki kuzia wananchi kupata welewa wa nini kilijiri katika mkataba huo wa kinyonyaji.
Kwa upande wa Mengi, anatuhumiwa kwamba ni mwanasiasa popo, kwani yuko CCM lakini ndiye kinara wa kutumia magazeti ya Mwanahalisi kumzunguka Kikwete.
Isitoshe ,Sitta anatuhumiwa kwamba anatumia uwepo wake kwenye CCM na Kamati kuu ili kumdoofisha JK, kwa kutoa siri za ndani ambazo Mwandishi anasema ni za kupikwa.
Katika makala hiyo, hakuachwa kuhusishwa Slaa na maandamano ya vyuo vikuu, na pia sehemu zinginezo. Wakimkandia Mengi, wamesema ni mfanyabiashara anayejifanya mzalendo na mwenye huruma wakati ni kinyume chake!
Wanahitimisha kwa kutaka vyombo vya usalama kuwadhibiti akina Mwanahalisi, Sitta na wenzake, na watu kama Mengi, kwani ni hatari kwa usalama wa taifa 'lililozoea amani na utulivu". Wanazidi kumpaka mafuta JK kwa kusema ndiye raisi pekee ambaye ameonyesha wazi kuchukia rushwa na kwamba amechukua hatua ya kuipa meno TAKUKURU na kwamba kesi kadhaa za ufisadi zimepelekwa mahakamani.
KAZI NDO IMEANZA........
Jitihada hizo zimeanza na gazeti la Rai, toleo la jana.
Katika gazeti hilo, mwandishi amelituhumu mwanahalisi kwamba ni jukwaa linalotumiwa na wabaya wa JK ili kuiangusha serikali.
Wanadai Mwanahalisi limejiandaa kuuhadaa umma kuwa JK hafai kwa kumhusisha JK na ufisadi wa nci hii na kusema yeye ni sehemu ya ufisadi au ni mfadhili wa uozo huo.
Wanalinukuu gazeti la Mwanahalisi la Jumatano hii kwa kujaribu kuonyesha uhusiano wa Manji, Rostam na Kagoda.
Pia wamechukizwa na makala inayosema "JK, jisafishe Kwanza mwenyewe kabla ya kusafisha CCM" nk. Wakati huo huo, Gazeti la mwanahalisi limeripoti kwamba toleo lao la wiki iliyopita lilihujumiwa kwa baadi ya vizito kununua nakala nyingi kwenye mikoa ya Mbeya ili watu wakose kusoma habari za Dowans nk ilki kuzia wananchi kupata welewa wa nini kilijiri katika mkataba huo wa kinyonyaji.
Kwa upande wa Mengi, anatuhumiwa kwamba ni mwanasiasa popo, kwani yuko CCM lakini ndiye kinara wa kutumia magazeti ya Mwanahalisi kumzunguka Kikwete.
Isitoshe ,Sitta anatuhumiwa kwamba anatumia uwepo wake kwenye CCM na Kamati kuu ili kumdoofisha JK, kwa kutoa siri za ndani ambazo Mwandishi anasema ni za kupikwa.
Katika makala hiyo, hakuachwa kuhusishwa Slaa na maandamano ya vyuo vikuu, na pia sehemu zinginezo. Wakimkandia Mengi, wamesema ni mfanyabiashara anayejifanya mzalendo na mwenye huruma wakati ni kinyume chake!
Wanahitimisha kwa kutaka vyombo vya usalama kuwadhibiti akina Mwanahalisi, Sitta na wenzake, na watu kama Mengi, kwani ni hatari kwa usalama wa taifa 'lililozoea amani na utulivu". Wanazidi kumpaka mafuta JK kwa kusema ndiye raisi pekee ambaye ameonyesha wazi kuchukia rushwa na kwamba amechukua hatua ya kuipa meno TAKUKURU na kwamba kesi kadhaa za ufisadi zimepelekwa mahakamani.
KAZI NDO IMEANZA........