Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
Ule mkakati unaoratibiwa na Sheikh Ponda Issa Ponda wa kushawishi waislam wasishiriki zoezi la sensa lililoanza leo linaelekea kutopata mafanikio baada ya waislam walioweka mabango majumbani kwao ya kutokuhesabiwa kukubali wenyewe kuhesabiwa bila kikwazo.
Shuhuda wa habari hizi ambaye ni mimi mwenyewe nimeshuhudia makumi ya waislam wakihesabiwa kuanzia ubungo jirani na mitambo ya umeme ya Aggreco hadi mabibo ambapo waliohesabiwa walisema wanahesabiwa kwakuwa hawataki 'maneno' na serikali.
Walidai kuwa wanaunga mkono hoja za wenzao za kutokuhesabiwa lakini wakasema serikali ikiamua jambo haishindwi hivyo wanaepuka kitakachofuata baada ya huo mgomo.
Maeneo ya Mburahati, kigogo nq Luhanga mwitikio wa kuhesabiwa umekuwa mzuri, ingawa wapo wachache waliogoma lakini zimesikika lawama kutoka kwa baadhi ya Maustaadh wakilalamika KUSALITIWA na wenzao ambapo wamelia na WOGA wa waislam kwenye mambo aliyoyaita ya msingi.
Karani wa Sensa aliyekuwepo Mabibo -Sahara na Mabibo Muleba hadi jirani na Mabibo External wamesema hadi muda huu zoezi liko vizuri na wachache waliogoma watashughulikiwa.
Wamesema jukumu lao ni kuandikisha na kaya itakayogoma itapelekwa kwa mwenyekiti wa serikal za mtaa ambaye naye atawahesabu, wakimgomea huyovndipovwatakapochukuliwa na polisi kwenda kuhesabiwa kinguvu rumande wakati huo wakisubiri vifungo.
Afisa mtendaji wa kata ya Mabibo amesema kama waislam wataendelea na mchezo huu wa kijinga watakuwepo wengi watakaopoteza ajira maana serikali imejipanga kuwafunga wote watakaogoma kuhesabiwa
Shuhuda wa habari hizi ambaye ni mimi mwenyewe nimeshuhudia makumi ya waislam wakihesabiwa kuanzia ubungo jirani na mitambo ya umeme ya Aggreco hadi mabibo ambapo waliohesabiwa walisema wanahesabiwa kwakuwa hawataki 'maneno' na serikali.
Walidai kuwa wanaunga mkono hoja za wenzao za kutokuhesabiwa lakini wakasema serikali ikiamua jambo haishindwi hivyo wanaepuka kitakachofuata baada ya huo mgomo.
Maeneo ya Mburahati, kigogo nq Luhanga mwitikio wa kuhesabiwa umekuwa mzuri, ingawa wapo wachache waliogoma lakini zimesikika lawama kutoka kwa baadhi ya Maustaadh wakilalamika KUSALITIWA na wenzao ambapo wamelia na WOGA wa waislam kwenye mambo aliyoyaita ya msingi.
Karani wa Sensa aliyekuwepo Mabibo -Sahara na Mabibo Muleba hadi jirani na Mabibo External wamesema hadi muda huu zoezi liko vizuri na wachache waliogoma watashughulikiwa.
Wamesema jukumu lao ni kuandikisha na kaya itakayogoma itapelekwa kwa mwenyekiti wa serikal za mtaa ambaye naye atawahesabu, wakimgomea huyovndipovwatakapochukuliwa na polisi kwenda kuhesabiwa kinguvu rumande wakati huo wakisubiri vifungo.
Afisa mtendaji wa kata ya Mabibo amesema kama waislam wataendelea na mchezo huu wa kijinga watakuwepo wengi watakaopoteza ajira maana serikali imejipanga kuwafunga wote watakaogoma kuhesabiwa