mpemba mbishi
JF-Expert Member
- Nov 27, 2011
- 1,132
- 185
Chama cha mapinduzi kimepanga mbinu tofauti kuhakikisha katiba mpya inayotarajiwa kutungwa na watanzania haitoweza kutumika wakati wa uchaguzi mkuu ujao (2015).
Kwa mujibu wa wajumbe wa CCM (zanzibar) waliorudi tanzania bara hivi karibuni, wamenukuliwa wakisema kuwa mikakati hiyo ni ya aina mbili:
1) KUISHINIKIZA TUME YA KATIBA KUINGIZA MAMBO AMBAYO YATAWAKERA WAZANZIBAR KUHUSU MUUNGANO JAMBO AMBALO LITAPELEKEA KUPIGA KURA YA KUIKATAA KATIBA MPYA WAKATI ITAKAPOITISHWA KURA YA MAONI. Katika kufanikisha hili tayari mapendekezo ya awali yapo mbioni kuwasilishwa tume ya katiba ili yaingizwe kwenye katiba. Moja ya pendekezo hilo ni KUWEPO KWA MFUMO WA MUUNGANO WA SERIKALI MBILI jambo ambalo linapingwa vikali na wazanzibar.
2) Mkakati mwengine ni KUWATUMIA BAADHI YA WANASIASA AU VYAMA VYA SIASA KUWEKA PINGAMIZI MAHKAMANI ILI MUDA WA KUKAMILISHA MCHAKATO HUO USIFANIKIWE. Katika hili serikali na CCM imepanga kujitetea kuwa ilikuwa na nia njema lakini vyama vyenyewe vya upinzani ndio vilivyochelewesha mchakato huo.
Pia wamedai watatumia mkakati mwengine iwapo mbinu hizo hazitofanikiwa. Hata hivyo mwandishi wa habari hii hakufanikiwa kupata mkakati wa tatu iwapo njia hizo hazitozaa matunda, lakini bado ninaendelea kutafuta kujua ni njia gani hiyo wanatarajia kuichukua.
Kwa mujibu wa wajumbe hao kutoka zanzibar wamesema kuwa wana ccm wenzao kutoka bara sasa hivi hofu yao ni chadema, hivyo basi iwapo katika mpya itatumika katika uchaguzi mkuu ujao (2015) inaweza kuhatarisha wao kubaki madarakani kwa vile tume huru ya uchaguzi itakuwa ni pigo kubwa kwa ccm.
Mmoja ya wajumbe hao Alipoulizwa iwapo ni mkakati gani ambao anategemea kuwa utafanikiwa alidai kuwa ni ule mkakati wa kwanza wa kuweka vipengele na vizuizi ambavyo vitawafanya wazanzibar kuichukia katiba mpya na kupelekea kuikataa wakati wa kura ya maoni jambo ambalo litakuwa ni pigo kwa chadema ambacho kimepanga kutumia tume huru ya uchaguzi kujikita madarakani.
Habari hizi huenda zikawa na ukweli fulani kwa vile uvumi umeenea hapa zanzibar kuwa kama HAKITOWEKWA KIPENGELE CHA KUJADILIWA MUUNGANO (KUWEPO AU KUTOKUWEPO) basi wazanzibar watahamasishwa kupiga kura ya hapana wakati ukifika jambo ambalo litafanikiwa kwa kura nyingi.
(WAKATI NDIO AMBAO UTATHIBITISHA UKWELI AU UONGO WA TETESI HIZI.)
TUJADILI NA NINI KIFANYIKE KUZUIA MBINU HIZI CHAFU.
Kwa mujibu wa wajumbe wa CCM (zanzibar) waliorudi tanzania bara hivi karibuni, wamenukuliwa wakisema kuwa mikakati hiyo ni ya aina mbili:
1) KUISHINIKIZA TUME YA KATIBA KUINGIZA MAMBO AMBAYO YATAWAKERA WAZANZIBAR KUHUSU MUUNGANO JAMBO AMBALO LITAPELEKEA KUPIGA KURA YA KUIKATAA KATIBA MPYA WAKATI ITAKAPOITISHWA KURA YA MAONI. Katika kufanikisha hili tayari mapendekezo ya awali yapo mbioni kuwasilishwa tume ya katiba ili yaingizwe kwenye katiba. Moja ya pendekezo hilo ni KUWEPO KWA MFUMO WA MUUNGANO WA SERIKALI MBILI jambo ambalo linapingwa vikali na wazanzibar.
2) Mkakati mwengine ni KUWATUMIA BAADHI YA WANASIASA AU VYAMA VYA SIASA KUWEKA PINGAMIZI MAHKAMANI ILI MUDA WA KUKAMILISHA MCHAKATO HUO USIFANIKIWE. Katika hili serikali na CCM imepanga kujitetea kuwa ilikuwa na nia njema lakini vyama vyenyewe vya upinzani ndio vilivyochelewesha mchakato huo.
Pia wamedai watatumia mkakati mwengine iwapo mbinu hizo hazitofanikiwa. Hata hivyo mwandishi wa habari hii hakufanikiwa kupata mkakati wa tatu iwapo njia hizo hazitozaa matunda, lakini bado ninaendelea kutafuta kujua ni njia gani hiyo wanatarajia kuichukua.
Kwa mujibu wa wajumbe hao kutoka zanzibar wamesema kuwa wana ccm wenzao kutoka bara sasa hivi hofu yao ni chadema, hivyo basi iwapo katika mpya itatumika katika uchaguzi mkuu ujao (2015) inaweza kuhatarisha wao kubaki madarakani kwa vile tume huru ya uchaguzi itakuwa ni pigo kubwa kwa ccm.
Mmoja ya wajumbe hao Alipoulizwa iwapo ni mkakati gani ambao anategemea kuwa utafanikiwa alidai kuwa ni ule mkakati wa kwanza wa kuweka vipengele na vizuizi ambavyo vitawafanya wazanzibar kuichukia katiba mpya na kupelekea kuikataa wakati wa kura ya maoni jambo ambalo litakuwa ni pigo kwa chadema ambacho kimepanga kutumia tume huru ya uchaguzi kujikita madarakani.
Habari hizi huenda zikawa na ukweli fulani kwa vile uvumi umeenea hapa zanzibar kuwa kama HAKITOWEKWA KIPENGELE CHA KUJADILIWA MUUNGANO (KUWEPO AU KUTOKUWEPO) basi wazanzibar watahamasishwa kupiga kura ya hapana wakati ukifika jambo ambalo litafanikiwa kwa kura nyingi.
(WAKATI NDIO AMBAO UTATHIBITISHA UKWELI AU UONGO WA TETESI HIZI.)
TUJADILI NA NINI KIFANYIKE KUZUIA MBINU HIZI CHAFU.