Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Jk alifikiri ya kuwa watanzania watamchagua kwa sababu ya ahadi za miaka mitano ijayo......Hilo lilikuwa ni kosa lake la kwanza...........Watanzania walitaka tathmini ya miaka mitano iliyopita ambayo Jk hakuwapa...........sasa bila kujua CCM na JK wake walikwama wapi ni vigumu kwa wapigakura kuendelea kuwaamini na ahadi zao lukuki ambao utekelezaji wake umethibitika ni wa kusuasua.
Wapigakura walitaka kujua mikakati ya JK kupambana na ufisadi ambao ndicho kiini kikubwa cha umasikini wetu na huduma za umma kudorora lakini JK hakutaka kushibisha shauku za wapigakura kwenye maeneo haya!!!!!!!!!!!
JK alifikiria uongozi ni kufanya utakavyo lakini hivi karibuni atajifunza ya kuwa uongozi ni kufanya yale ambayo wapigakura wanataka na ukija na ajenda zako za siri na wapigakura wakizijua basi umekwisha watakukataa...
La kushangaza zaidi ni kwa nini Jk hakutaka kutumia muda mwingi kuzungumzia mafanikio ya serikali yake kwa miaka mitano iliyopita? Ungelitegemea ya kuwa kama kazi tuliwatuma waliifanya vizuri basi wangelikuwa na mengi ya kujigamba lakini Jk aonekana kama ndiyo anaomba kwa mara ya kwanza ridhaa ya kuongoza nchi...wakati siyo kweli .......Hili litamgharimu sana
Kiongozi uliyeko madarakani kwa miaka mitano hupaswi kuwa unatoa ahadi ila unapaswa kuwakumbusha wapigakura kile ulichokifanya na kukaa kimya juu ya kile alichokifanya wapigakura watafikiria ya kuwa JK na CCM pengine hakuna walilolifanya na kuwaadhibu kwa kura zao.........Haitoshi kwa JK kung'aka ya kuwa kuna mengi tuliyoyafanya....wapigakura watauliza ni yepi mkuu siku ya kupiga kura.....na hicho kitakuwa ni kilio na kusaga meno kwake JK na CCM yake........Hivi sasa tunaita CCM ni mali ya JK kwa sababu hakutaka kuimilikisha kwa wananchama wa CCM au hata viongozi wake pale aliposema suala la Uraisi ni la kifamilia..........na ndiyo maana kwenye kampeni zake ni yeye, mkewe na wanawe ndiyo wanahangaika kutafuta kazi ya umma...na wapigakura wanajiuliza hivi hawa wanafamilia ya JK wakikipata hiki kibarua tena watamhudumia nani kama siyo kujihudumia wenyewe?
Eneo ambalo Jk alitakiwa atumie muda mwingi kuwahabarisha wapigakura lilikuwa ni matatizo ya kiuchumi lakini yeye ametumia muda wake mwingi kuvijenga vyama vya upinzani kwa kuviita "photocopy" na vya muda tu. Wapigakura wanaujua uwezo wa vyama vya upinzani hivyo hawakuhitaji JK kuwafundisha somo hilo....
Jk hakuzungumzia matatizo ya kiuchumi na kuwaacha wapigakura kuamini ya kuwa yupo mbali nao na hivyo haguswi na adha kadha wa kadha zinazowakabili na mshahara wake ni kumfuta kazi J2 ijayo.......Kwa lugha ya kimombo husema: "JK is out of touch, insulated and out of reach to commoners......."
Jk baada ya kufilisika kisiasa akaanza kushutumu vyombo vya habari, viongozi wa dini na baadhi ya waumini wa madhehebu zisizokuwa zake ya kuwa wanamchukia kwa sababu ya imani yake ya kidini akisahau ya kuwa miaka mitano tu iliyopita watu hao hao anaowakosea adabu leo ndiyo wengi wao waliompa hiyo dhamana ya kuliongoza taifa hili.
Shukrani ya JK sasa ni kuwaita wadini kwa minajili ya kuficha udhaifu wake wa kuwa kiongozi mdhaifu....Kwa hali hii, Jk amewanyima wapigakura mwanya wa kumsaidia kumrekebisha na hivyo kuwahamasisha kumfukuza kazi kiongozi huyu dhaifu mwenye malalamiko na visingizio visivyokuwa na mwisho......
Badala ya Jk kuhubiri udini na ukabila mambo ambayo bado hayajaota mizizi hapa nchini angeliwauliza watanzania kwa unyenyekevu sana hivi ni wapi nimekosea?
Hapo wapigakura wangemwona kumbe ana nia ya kujirekebisha lakini mkakati wake wa kuwalaumu wapigakura kwa kubuni bila ushahidi wowote kuwa changamoto zinazotukabili ni udini na ukabila yaelekea JK hata hajui nchi hii inatoka wapi, iko wapi na inaeleka wapi...na kiongozi wa jinsi hii, namna ya kumuenzi ni kumstaafisha kwa nguvu za kura zetu siku ya J2 ijayo............hatuna namna nyingine ila hiyo.......
Uongozi shupavu ni kujipima, kuuliza na kushirikisha wenzio na wala siyo kuwaonyesha ubaguzi, ulafi wa madaraka na ubinafsi hata kubinafsisha ofisi ya umma kuwa sasa ni miliki ya familia yako JK...........Lakini nina habari njema kwa JK ya kuwa baada ya kura kupigwa huo mzigo hautakuwa "headache" yake tena kwani wapigakura watamkabidhi raia mwingine ambaye safari hii anafahamu fika kuwa uongozi wa umma ni shirikishi na wala siyo suala la kifamilia..
BYE-BYE JK..........BUT........ WELCOME DR. SLAA AND CHADEMA.........................
Wapigakura walitaka kujua mikakati ya JK kupambana na ufisadi ambao ndicho kiini kikubwa cha umasikini wetu na huduma za umma kudorora lakini JK hakutaka kushibisha shauku za wapigakura kwenye maeneo haya!!!!!!!!!!!
JK alifikiria uongozi ni kufanya utakavyo lakini hivi karibuni atajifunza ya kuwa uongozi ni kufanya yale ambayo wapigakura wanataka na ukija na ajenda zako za siri na wapigakura wakizijua basi umekwisha watakukataa...
La kushangaza zaidi ni kwa nini Jk hakutaka kutumia muda mwingi kuzungumzia mafanikio ya serikali yake kwa miaka mitano iliyopita? Ungelitegemea ya kuwa kama kazi tuliwatuma waliifanya vizuri basi wangelikuwa na mengi ya kujigamba lakini Jk aonekana kama ndiyo anaomba kwa mara ya kwanza ridhaa ya kuongoza nchi...wakati siyo kweli .......Hili litamgharimu sana
Kiongozi uliyeko madarakani kwa miaka mitano hupaswi kuwa unatoa ahadi ila unapaswa kuwakumbusha wapigakura kile ulichokifanya na kukaa kimya juu ya kile alichokifanya wapigakura watafikiria ya kuwa JK na CCM pengine hakuna walilolifanya na kuwaadhibu kwa kura zao.........Haitoshi kwa JK kung'aka ya kuwa kuna mengi tuliyoyafanya....wapigakura watauliza ni yepi mkuu siku ya kupiga kura.....na hicho kitakuwa ni kilio na kusaga meno kwake JK na CCM yake........Hivi sasa tunaita CCM ni mali ya JK kwa sababu hakutaka kuimilikisha kwa wananchama wa CCM au hata viongozi wake pale aliposema suala la Uraisi ni la kifamilia..........na ndiyo maana kwenye kampeni zake ni yeye, mkewe na wanawe ndiyo wanahangaika kutafuta kazi ya umma...na wapigakura wanajiuliza hivi hawa wanafamilia ya JK wakikipata hiki kibarua tena watamhudumia nani kama siyo kujihudumia wenyewe?
Eneo ambalo Jk alitakiwa atumie muda mwingi kuwahabarisha wapigakura lilikuwa ni matatizo ya kiuchumi lakini yeye ametumia muda wake mwingi kuvijenga vyama vya upinzani kwa kuviita "photocopy" na vya muda tu. Wapigakura wanaujua uwezo wa vyama vya upinzani hivyo hawakuhitaji JK kuwafundisha somo hilo....
Jk hakuzungumzia matatizo ya kiuchumi na kuwaacha wapigakura kuamini ya kuwa yupo mbali nao na hivyo haguswi na adha kadha wa kadha zinazowakabili na mshahara wake ni kumfuta kazi J2 ijayo.......Kwa lugha ya kimombo husema: "JK is out of touch, insulated and out of reach to commoners......."
Jk baada ya kufilisika kisiasa akaanza kushutumu vyombo vya habari, viongozi wa dini na baadhi ya waumini wa madhehebu zisizokuwa zake ya kuwa wanamchukia kwa sababu ya imani yake ya kidini akisahau ya kuwa miaka mitano tu iliyopita watu hao hao anaowakosea adabu leo ndiyo wengi wao waliompa hiyo dhamana ya kuliongoza taifa hili.
Shukrani ya JK sasa ni kuwaita wadini kwa minajili ya kuficha udhaifu wake wa kuwa kiongozi mdhaifu....Kwa hali hii, Jk amewanyima wapigakura mwanya wa kumsaidia kumrekebisha na hivyo kuwahamasisha kumfukuza kazi kiongozi huyu dhaifu mwenye malalamiko na visingizio visivyokuwa na mwisho......
Badala ya Jk kuhubiri udini na ukabila mambo ambayo bado hayajaota mizizi hapa nchini angeliwauliza watanzania kwa unyenyekevu sana hivi ni wapi nimekosea?
Hapo wapigakura wangemwona kumbe ana nia ya kujirekebisha lakini mkakati wake wa kuwalaumu wapigakura kwa kubuni bila ushahidi wowote kuwa changamoto zinazotukabili ni udini na ukabila yaelekea JK hata hajui nchi hii inatoka wapi, iko wapi na inaeleka wapi...na kiongozi wa jinsi hii, namna ya kumuenzi ni kumstaafisha kwa nguvu za kura zetu siku ya J2 ijayo............hatuna namna nyingine ila hiyo.......
Uongozi shupavu ni kujipima, kuuliza na kushirikisha wenzio na wala siyo kuwaonyesha ubaguzi, ulafi wa madaraka na ubinafsi hata kubinafsisha ofisi ya umma kuwa sasa ni miliki ya familia yako JK...........Lakini nina habari njema kwa JK ya kuwa baada ya kura kupigwa huo mzigo hautakuwa "headache" yake tena kwani wapigakura watamkabidhi raia mwingine ambaye safari hii anafahamu fika kuwa uongozi wa umma ni shirikishi na wala siyo suala la kifamilia..
BYE-BYE JK..........BUT........ WELCOME DR. SLAA AND CHADEMA.........................