Mjukuu ambaka bibi yake, amuua

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080
KIJANA mmoja mwenye umri wa miaka 27 anatuhumiwa kumbaka kikongwe wa miaka 70, ambaye anasadikiwa kuwa ni bibi yake, na baadaye kumuua kwa kumchinja.

Kikongwe huyo, Kulwa Mahona, ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Mwagala, Kata ya Ibadakuli, aligundulika kufanyiw aunyama huo Mei 19 majira ya asubuhi.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Leonard Mayunga James aliiambiwa Mwananchi kuwa kijana huyo, ambaye jina tunalihifadhi, alimuua kikongwe huyo usiku wa manane baada ya kumuingilia nyumbani kwake alikokuwa amelala.
Alisema kijana huyo alianza unyama huo kwa kumbaka kwa nguvu na baadaye kumchinja shingoni baada ya kugundua kuwa kikongwe huyo alimgundua mbakaji.

Kijana huyo alitoroka baada ya akiamini kuwa ameshamuua kikongwe huyo, lakini kaka wa kijana huyo alipofika eneo hilo majira ya asubuhi alimkuta mzee huyo akiwa taaban kutokana na majeraha yaliyokuwa shingoni kwake na akawaita majirani.

Mwenyekiti huyo wa kijiji alisema kikongwe huyo alimudu kusimulia wanakijiji waliowahi kufika eneo hilo jinsi aliyofanyiwa ukatili na kijana huyo kutokana na ukweli kwamba wakati huo alikuwa akimudu kuongea.
Alisema waliamua kuripoti polisi na kuchukua fomu kwa ajili ya matibabu, lakini ilipotimia saa 9:00 alasiri kikongwe huyo alifariki wakati akiendelea kupatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Shinyanga.

Mtoto wa marehemu, John Njige alisema kuwa alipata taarifa za tukio hilo juzi asubuhi na kumkuta mama yake akiwa hospitalini na kwamba alipata nafasi ya kuzungumza nae kabla hajafariki dunia.
Kaimu kamanda wa polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Isaya Nganga alisema alikuwa hajapata taarifa kamili za tukio hilo.
Wakati huohuo, mwanafunzi mmoja wa darasa la sita anayejulikana kwa jina la Isaya Magese, 14, ameuawa kwa kuchomwa kisu na mwanafunzi mwenzake katika sehemu ya titi lake la kushoto
Kaimu kamanda wa polisi mkoani Shinyanga, Charles Nyanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 16 mwaka huu majira ya saa 1:00 jioni katika Kijiji cha Kisesa kilicho katika Kata ya Kolandoto, Shinyanga.

Alisema aliyefanya mauaji hayo, jina tunalihifadhi kwa sababu za kimaadili, ni mtoto wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sabamtaja aliyefanya mauaji hayo kuwa ni Shija Ndohoi (16) ambaye pia ni mwanafunziwa darasa la saba. Wote ni wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kisesa.

Kamanda Nyanda alisema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni ushabiki wa mpira ulioambatana na kurushiana maneno, huku Isaya akidaiwa kumwambia mwenzake kuwa anavuta bangi na kumuudhi mpinzani wake.
Jeshi la Polisi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo na linajiandaa kumpandisha kizimbani.

Mjukuu ambaka bibi yake, amuua
 
Back
Top Bottom