Mjengwa uso kwa uso na simba wa mikumi!

jamadari

JF-Expert Member
Feb 13, 2010
295
92
Jumapili ya Februari 20 sitaishi nikaisahau. Nilifika Mikumi National Park Jumamosi alasiri kwa mapumziko ya usiku mmoja kabla ya kuendelea na safari yangu ya Dar nikitokea Iringa. Usiku wa kuamkia Jumapili simba waliunguruma karibu kabisa na Mikumi Wildlife Camp nilikofikia banda namba 9 lijulikanalo kama Kongoni. Niliamka kunako saa kumi na mbili. Mmoja wa wafanyakazi wa kambi hiyo akaniambia simba watatu wako umbali wa mita mia tano kutoka kambini. Nikaenda haraka kuwaangalia; dume mmoja na majike mawili. Nikapiga picha kadhaa. Simba dume alionyesha kukasirika sana, aliniangalia kwa macho makali Kisha akanifokea, akijiandaa kurukia mlango wa gari. Nikafunga kioo na kuondoka haraka sehemu hiyo. Nikarudi kambini na kwenda moja kwa moja kupata kikombe changu cha chai. Nikiwa njiani kurudi kwenye banda langu, majira ya saa moja na nusu asubuhi, ghafla nikamwona simba yule dume akinijia akitokea banda namba kumi liitwalo Kanga. Nywele zilinisisimka,nilitamani ardhi ipasuke. Hakukuwa na mtu mwingine yeyote. Sikupiga kelele, maana ningemchanganya zaidi simba yule. Nikabaki nikimwangalia simba yule machoni huku nikirudi kinyumenyume kurudi ilipo ofisi ya mapokezi. Kamwe usimgeuzie simba kisogo. Ukimtazama machoni anaweza kugeuka na kutafuta njia nyingine, simba ni mnyama mwenye kuona haya. Na hakika, simba alitoka kwenye njia niliyokuwa nikiifuata na kuelekea kwenye banda lingine mkono wa kulia, aliachana na mimi. Haraka nikakimbia kuwajulisha baadhi ya wafanyakazi wachache waliokuwapo pale kambini. Kazi ikawa kuwataarifu kwa haraka wageni wote ( watalii) waliokuwapo kambini pale kuwa ' kambi imevamiwa na simba watatu'. Simba dume ameondoka banda namba 10 na kuwaacha majike wake wawili wakiwa mlangoni. Nikiwa na wafanyakazi watatu wa kambi hiyo, tukajipanga kwa haraka kuhakikisha wageni wote walio mabandani wanabaki ndani ya mabanda hayo kwa usalama wao, na walio nje kwenye restaurant watafute haraka sehemu za kujihifadhi. Maana simba walianza kupita banda moja baada ya jingine. Tukaanza kufuatilia nyendo za simba wale pale kambini ili kuhakikisha usalama wa wageni. Niliweza pia kupiga picha nyingi za karibu. Simba dume ndiye aliyeanza kuondoka eneo la kambi baada ya nusu saa na kuwaacha majike wawili. Hao majike tulifanikiwa kuwadhibiti kwa kutumia mlio wa gari na kuwasukuma umbali ambao uliruhusu wageni kutoka mabandani na walio nje kwenda kuchukua mizigo yao. Niliondoka Mikumi huku kukiwa na taarifa za kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa simba wale kurudi tena eneo la kambi hiyo. Kwa picha zaidi za tukio hilo, tembelea; http://mjengwa.blogspot.com/
 
Jumapili ya Februari 20 sitaishi nikaisahau. Nilifika Mikumi National Park Jumamosi alasiri kwa mapumziko ya usiku mmoja kabla ya kuendelea na safari yangu ya Dar nikitokea Iringa. Usiku wa kuamkia Jumapili simba waliunguruma karibu kabisa na Mikumi Wildlife Camp nilikofikia banda namba 9 lijulikanalo kama Kongoni. Niliamka kunako saa kumi na mbili. Mmoja wa wafanyakazi wa kambi hiyo akaniambia simba watatu wako umbali wa mita mia tano kutoka kambini. Nikaenda haraka kuwaangalia; dume mmoja na majike mawili. Nikapiga picha kadhaa. Simba dume alionyesha kukasirika sana, aliniangalia kwa macho makali Kisha akanifokea, akijiandaa kurukia mlango wa gari. Nikafunga kioo na kuondoka haraka sehemu hiyo. Nikarudi kambini na kwenda moja kwa moja kupata kikombe changu cha chai. Nikiwa njiani kurudi kwenye banda langu, majira ya saa moja na nusu asubuhi, ghafla nikamwona simba yule dume akinijia akitokea banda namba kumi liitwalo Kanga. Nywele zilinisisimka,nilitamani ardhi ipasuke. Hakukuwa na mtu mwingine yeyote. Sikupiga kelele, maana ningemchanganya zaidi simba yule. Nikabaki nikimwangalia simba yule machoni huku nikirudi kinyumenyume kurudi ilipo ofisi ya mapokezi. Kamwe usimgeuzie simba kisogo. Ukimtazama machoni anaweza kugeuka na kutafuta njia nyingine, simba ni mnyama mwenye kuona haya. Na hakika, simba alitoka kwenye njia niliyokuwa nikiifuata na kuelekea kwenye banda lingine mkono wa kulia, aliachana na mimi. Haraka nikakimbia kuwajulisha baadhi ya wafanyakazi wachache waliokuwapo pale kambini. Kazi ikawa kuwataarifu kwa haraka wageni wote ( watalii) waliokuwapo kambini pale kuwa ' kambi imevamiwa na simba watatu'. Simba dume ameondoka banda namba 10 na kuwaacha majike wake wawili wakiwa mlangoni. Nikiwa na wafanyakazi watatu wa kambi hiyo, tukajipanga kwa haraka kuhakikisha wageni wote walio mabandani wanabaki ndani ya mabanda hayo kwa usalama wao, na walio nje kwenye restaurant watafute haraka sehemu za kujihifadhi. Maana simba walianza kupita banda moja baada ya jingine. Tukaanza kufuatilia nyendo za simba wale pale kambini ili kuhakikisha usalama wa wageni. Niliweza pia kupiga picha nyingi za karibu. Simba dume ndiye aliyeanza kuondoka eneo la kambi baada ya nusu saa na kuwaacha majike wawili. Hao majike tulifanikiwa kuwadhibiti kwa kutumia mlio wa gari na kuwasukuma umbali ambao uliruhusu wageni kutoka mabandani na walio nje kwenda kuchukua mizigo yao. Niliondoka Mikumi huku kukiwa na taarifa za kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa simba wale kurudi tena eneo la kambi hiyo. Kwa picha zaidi za tukio hilo, tembelea; http://mjengwa.blogspot.com/

Lazima nywele zikusisimke Mkuu na shukuru Mungu sana uliwahi kumuona kabla hajakuvamia. Ukiwa maeneo ya mbuga za wanyama inabidi uwe extra careful ama unaweza kujeruhiwa vibaya sana au hata kukutana na umauti.
 
Jumapili ya Februari 20 sitaishi nikaisahau. Nilifika Mikumi National Park Jumamosi alasiri kwa mapumziko ya usiku mmoja kabla ya kuendelea na safari yangu ya Dar nikitokea Iringa. Usiku wa kuamkia Jumapili simba waliunguruma karibu kabisa na Mikumi Wildlife Camp nilikofikia banda namba 9 lijulikanalo kama Kongoni. Niliamka kunako saa kumi na mbili. Mmoja wa wafanyakazi wa kambi hiyo akaniambia simba watatu wako umbali wa mita mia tano kutoka kambini. Nikaenda haraka kuwaangalia; dume mmoja na majike mawili. Nikapiga picha kadhaa. Simba dume alionyesha kukasirika sana, aliniangalia kwa macho makali Kisha akanifokea, akijiandaa kurukia mlango wa gari. Nikafunga kioo na kuondoka haraka sehemu hiyo. Nikarudi kambini na kwenda moja kwa moja kupata kikombe changu cha chai. Nikiwa njiani kurudi kwenye banda langu, majira ya saa moja na nusu asubuhi, ghafla nikamwona simba yule dume akinijia akitokea banda namba kumi liitwalo Kanga. Nywele zilinisisimka,nilitamani ardhi ipasuke. Hakukuwa na mtu mwingine yeyote. Sikupiga kelele, maana ningemchanganya zaidi simba yule. Nikabaki nikimwangalia simba yule machoni huku nikirudi kinyumenyume kurudi ilipo ofisi ya mapokezi. Kamwe usimgeuzie simba kisogo. Ukimtazama machoni anaweza kugeuka na kutafuta njia nyingine, simba ni mnyama mwenye kuona haya. Na hakika, simba alitoka kwenye njia niliyokuwa nikiifuata na kuelekea kwenye banda lingine mkono wa kulia, aliachana na mimi. Haraka nikakimbia kuwajulisha baadhi ya wafanyakazi wachache waliokuwapo pale kambini. Kazi ikawa kuwataarifu kwa haraka wageni wote ( watalii) waliokuwapo kambini pale kuwa ' kambi imevamiwa na simba watatu'. Simba dume ameondoka banda namba 10 na kuwaacha majike wake wawili wakiwa mlangoni. Nikiwa na wafanyakazi watatu wa kambi hiyo, tukajipanga kwa haraka kuhakikisha wageni wote walio mabandani wanabaki ndani ya mabanda hayo kwa usalama wao, na walio nje kwenye restaurant watafute haraka sehemu za kujihifadhi. Maana simba walianza kupita banda moja baada ya jingine. Tukaanza kufuatilia nyendo za simba wale pale kambini ili kuhakikisha usalama wa wageni. Niliweza pia kupiga picha nyingi za karibu. Simba dume ndiye aliyeanza kuondoka eneo la kambi baada ya nusu saa na kuwaacha majike wawili. Hao majike tulifanikiwa kuwadhibiti kwa kutumia mlio wa gari na kuwasukuma umbali ambao uliruhusu wageni kutoka mabandani na walio nje kwenda kuchukua mizigo yao. Niliondoka Mikumi huku kukiwa na taarifa za kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa simba wale kurudi tena eneo la kambi hiyo. Kwa picha zaidi za tukio hilo, tembelea; http://mjengwa.blogspot.com/

Pole kwa yaliyokukuta na hongera kwa ujasiri
 
Sikupiga kelele, maana ningemchanganya zaidi simba yule. Nikabaki nikimwangalia simba yule machoni huku nikirudi kinyumenyume kurudi ilipo ofisi ya mapokezi. Kamwe usimgeuzie simba kisogo
Nimeshika pumzi yangu, nahisi ningekuwa mimi ningepiga yowe kubwa, ama ningekufa kabla hajanifikia.
 
Aisifuye mvua imemnyea.
Nimeipenda sana mbinu ya kuangaliana na simba.
Bora wewe uliikumbuka hiyo, maana nadhani mimi wangekuta soli za safari boot yangu tu, maana niliisahau nikiwa mdogo.
 
Amaaaa, kumbe Mjengwa ndiye Jemadari? Nilimfahamu sana kwenye Tanzanet enzi hizo. Unaona hadithi za babu zinavyosaidia? Kumtazama simba usoni ana haya sana. ndiyo maana akimtafuna mtu anauacha uso na viganja vya mikono na mikguu. Tumbo na minofu huenda sambamba navyo.
 
01.jpg

03.jpg

02.jpg

11.jpg

16.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom