Mjengwa katika kampeni za Kikwete 2010?

Pity you Mjengwa; The wind of change is blowing brother, naona unajaribu kuzuia maji yanayotiririka.
 
Ni vyema ukatuambia tathimini yako umefanya maeneo yapi? Ili tukupime kwa kile unachokisema na hali halisi ya kisiasa katika maeneo husika na sio hisia au utabiri kama wa yule mzee
 
Analysis ya Mjengwa iko based on interpolation . Lakini tatizo la interpolation kwenye siasa ni kuwa wapiga kura wengi si makada wa vyama vya siasa. Hawa ndio wanaoleta serikali. Mtizamo wake wa vijijini ni ule wa Lupembe ambapo wazee walimwambia JK kuwa mtu ana baba mmoja. Na kwa wao baba wa siasa ni CCM. Hili ni tatizo ambalo vyama vya upinzani vinatakiwa lishughulikie, kamwe CCM haitawaamsha watu wenye mtizamo huo haswa walioko vijijini! Kwa vyama vya Upinzani analysis ya Mjengwa yaonyesha ushabiki wake kwani angekuwa na takwimu alizofanya yeye au mtu mwingine basi na wengine wngelizipitia ili kuona kama kwenye maeneo mengine majibu yatakuwa hayohayo. Huo ndio udhaifu wa mwandishi takwimu zake kazichukua Lupembe sasa hamishia hizo Bukombe au Lindi uone kama kuna mlingano.
Kuwa kada wa CCM si tatizo kama ni propaganda zifanyiwe kazi. Japo CCM wanaweza kushinda uraisi, kazi ya wapiga kura ni kuchagua wabunge wengi kutoka upinzani ili Bunge liwe na nguvu ya kuisimamia serikali. Hili litatuhakikishia chama kinachoongoza serikali kitatekeleza ilani yake ya uchaguzi, na si baada ya mwaka mmoja tusikie kuwa haitekelezeki au sikuiasisi.
Matayarisho yanayofanywa sasa na akina Mjengwa na pia viongozi wa dini kuomba matokeo ya uchaguzi yakubalike ni ya kisaikolojia na kuhalalisha uwizi wa kura, wangelifanya hayo mwanzo wa kampeni! Tukumbuke kwa nini matokeo ya Dar kwenye uchaguzi wa kwanza yalzuiwa na kurudiwa. Je CCM watakuwa waungwa na kukubali endapo watapoteza viti muhimu?
 
Kijana yuko kazini!

90cart01102006oo6.jpg
 
Huu ni uchambuzi dhaifu ukiwa umejikita katika siasa za kukariri na mazoea. Kwa kutojua au kwa nia mbaya muandishi anajaribu kutumiaminisha katika ukubwa wa mtandao(mabolizi wa nyumba kumi) na uchaguzi wa serekali za mitaa kama nguzo yake ya uchambuzi.

Tayari kwa mfumo wa sasa tumeona idadi ya wenyeviti wa serekali za mitaa na mabalozi wa nyumba kumi kumi hawana athari yoyote katika uchaguzi mkuu. Ikumbukwe idadi ya watu wanaoshiriki uchaguzi wa serekali za mitaa ni wachache mno katika kiwango cha kupuuzwa katika matokeo ya uchaguzi mkuu na pia CCM huwa unajisimamia yenyewe moja kwa moja walau kwenye uchaguzi mkuu huwa wanajificha nyuma ya pazia la NEC.

Ukweli ni kwamba hawa mabalozi hawana ushawishi tena ndio maana CCM wanalazimika kutumia mabasi na malori ili kuokoa mikutano yao ya kampeni. Mabolozi hawana ushawishi wa kuwaelekeza wananchi wakahudhurie mikutano ya ccm, Dr. Slaa anapofanya kampeni, watu husukumwa na dhamiria yao, nguvu na imani yao kwa mgombea pamoja na ubora wa ujumbe unaotolewa(ubora wa ilani).

Ubora wa ujumbe ni jambo ambalo mchambuzi ameliepuka kwa maksudi, ya kwamba CCM inalazimika kufanya matamasha ya sanaa kuvutia watu. Kumbukumbu kubwa mwananchi anayobaki nayo baada ya kudhuria mikutano ya slaa ni mabadiliko ya mifumo,mfano elimu na afya bure,ujenzi wa makazi bora na uwajibikaji utaookao ondoa ufisadi, wakati kwa kikwete kumbukumbu kubwa ni ngojera toka kwa wasanii mbalimbali.

Majjid kwa maksudi anaepuka kutafakari chaguzi ndogo za Tarime,Busanda na Biharamlo. Busanda CCM ilikuwa na mitaa mingi ikifuatiwa na CUF, na mwaka 2005 CUF ndio ilishika nafasi ya pili lakini ulipokuja uchaguzi mdogo CHADEMA ilitangazwa mshindi wa pili ikiwa ina zaidi ya asilimia 40 ya kura, Biharamlo nguvu za awali zilikuwa ni CCM na TLP lakini CHADEMA ikatangazwa kwa zaidi ya asilimia 45 ya kura.Uwekezaji wa Operation Sangara ni jambo ambalo mchambuzi huyu kwa makusdi amepuuza ili kukidhi malengo ya chapisho lake.

CHADEMA imefanya uwekezaji mkubwa sana wa kisiasa katika miaka mitano iliyopita sasa ni suala la uamsho tu,ubora wa wagombea wake ni ziada katika uchaguzi huu, yoyote mwenye akili timamu atatambua CHADEMA haina nafasi haba katika kinyan'ganyoro cha madaraka ya nchi.



Ushiriki wa wanafamilia za JK pia umetajwa kama nguvu nyingine ya JK wakati ni udhaifu! Wanafamilia hawa hawana athari kubwa na ya jumla kwa kura. Sehemu kubwa ya mikutano yao ni ya ndani, na inawafikia watu ambao tayari ni wanachama wa CCM na pengine wamekwisha amua kuwapigia kura mda mrefu(sehemu ya asilimia arubaini zinazozungumzwa). Wanatumia rasilimali nyingi kuwafikia watu walewale na sehemu kubwa zimegeuka kuwa tume za upatanishi baada ya mizengwe ya ndani badala ya timu za kampeni, hapa ndipo wanazidi kuyapanua makundi kwa kuyatambua rasmi hii inawaongezea nguvu zaidi wapinzani. Harakati hizi zinawaumiza zaidi ya kuwaimarisha.Taswira ya kampeni za ufamilia ni mzigo na sio ya msaada kwa CCM.

Kuna wimbi kubwa mno lenye muelekeo wa kutambua CHADEMA kama jukwaa halisi la kubeba mabadiliko tarajiwa, na muenekeno unaonekana kwa wanaharakati na watu wanaoheshimika katika jamii kuiunga mkono, wananchi wameamua kuonganisha nguvu kupitia CHADEMA hili kwa maksudi amelipuuza sambamba na utendaji mbovu wa serekali ya CCM katika miaka mitano iliyopita,baadala yake ameipa CCM mamlaka ya kimungu ya kwamba wananchi ni vipofu na wataipigia tu kura ccm, eti kura za mazoea, ni huko vijijini ambako wananchi wameonyesha ujasiri wa kumzomea mgombea wa CCM.

Kwa Ujumla,uchambuzi wa Majid umebainisha lengo lake halisi. Kwa kuepuka masuala mengi yanaoendelea kujitokeza na mwenendo mzima wa kampeni na hali ya kisiasa kwa sasa na hatimae kujikita katika siasa za mazoea na mizania dhaifu ni vema tukahitimisha kwamba anajaribu kutetea uhuni uliopangwa na kuna msukumo wa maslahi binafsi. Tumemsoma na ajue tu nchi imevimba asijichumie laana ya wana wa ardhi.
 
Hivi gazeti lake alilolianzisha limeishia wapi, lilikuwa linaitwa something ..Jamii>

Hakuna ubaya kutoa analysis kama hii. Tatizo ni pale inapokosa basis, analysis imekaa kitabiri wakati tunajua mtabiri tunaye mmoja tu nchi hii. Angetuambia amewahoji watu kadhaa sehemu kadhaa au angetumia matokeo fulani, lakini sasa unalala leo unapata hisia kwamba CUF itakuwa ya kwanza, kesho unapata hisia zingine kwamba CHADEMA itakuwa ya nne, then unaandika makala, ebo!! Mbona wanaoota wapo wengi tu, lakini hawawezi kuandika kwa sababu ndoto haziwezi kuwa basis ya makala!!

Dr, nimeisoma makala ya huyu Bwana mara mbili. jambo ambalo naona linaweza kuwa sahihi kwake ni kwamba makala hii imejaa hisia and 'wishes' ambazo kimsingi ndizo anazotaka ziwe. Ni mchanganuo mzuri lakini umekaa kihisia zaidi na kufata historia ambayo hata hivyo kwa mwaka huu haina mashiko sana kwa sababu zifuatazo.

1. Ni dhahiri kama Lipumba alipata kura nyingi 2005 kumzidi Mbowe, influence ya Zanzibar haiepukiki. CUF inanguvu zanzibar na hatupingi hilo. Hata hivyo tofauti ya kura laki tano si yakuweza kutosha kutoa tathmini ya mwaka huu hasa ukizingatia mabadiliko makubwa ambayo yametokea.

2. Ingawa CUF ilishinda kwa wingi wa kura, ni dhahiri chadema walikuwa kwenye nafasi nzuri kwa wabunge. Hii inatosha kuweka picha halisi ya mambo yalivyo. ikiwa mgombea yuleyule kwa mwaka 2005 hakuweza kupata mbunge hata mmoja bara, kwa nini, katika misingi ya historia hiyohiyo ambayo maggid anaiamini, CUF waweze kupata wabunge 10 mpaka kumi na tanu pwani na kusini?

3. Uchambuzi wake ama unalenga kuwaaminisha watanzania kitu ambacho sicho, au una upendeleo wa dhahiri. Ikiwa anaweza kuiona nguvu ya Lipumba kusini na pwani, anashindwa nini kuiona nguvu ya Dr Slaa katika maeneo mengi ya nchi yetu?
 
Mmmhhh!
Kazi kweli kweli!
Bwana Maggid kuna tofauti kubwa kati ya fikra huru na biased expression of thought.
Makala yako ni dhahiri ina ujumbe wenye nia ya kushawishi kiupotoshaji kwa manufaa ya kisiasa.
Sababu ni nyingi na nitaziainisha:

1.Unasema "WENYE kupanga mikakati ya kivita wanajua, kuwa matokeo ya ushindi wa kivita hufahamika kabla risasi ya kwanza kupigwa. Inahusu matayarisho, malengo, mbinu na mikakati."
Historia na hata matokeo ya vita vya hivi karibuni yanathibitisha kwamba premise yako ni false!Wamarekani walipoingia vietnam waliamini watashinda kwa vile walikuwa na "matayarisho, malengo, mbinu na mikakati."Lakini leo tunajua kilicho wakuta mpaka wakakimbia bila ushindi.Wavietnam walizidiwa kila kitu,Pesa,Vifaa,Nyenzo za kivita,ujuzi na uzoefu wa kivita....Lakini walikuwa na kitu ambacho haya yote yasingeweza kukishinda "the human will" na determination yao.Vivyo hivyo Somalia.

2.Unasema "Leo, zikiwa zimebaki wiki nne kabla ya siku ya uchaguzi naiona hali iliyobadilika katika uwanja huu wa mapambano ya kisiasa. Naiona hali ifuatayo kama uchaguzi ungefanyika kesho".Hivi nini hasa kilichobadilisha hali hiyo ya mapambano ya kisisasa?Ahadi hewa na zisizotekelezeka za Kikwete?Taarifa za upotoshaji katika vyombo vya habari vya serikali?Ni nini hasa?Au container ya vifaa vya CCM vilivyoingizwa juzi?Makala yoyote yenye kutoa conclusions lazima ieleze conclusions hizo zimefikiwaje,kwa kutumia utaratibu upi na sample iliyotumika ilikuwa na muundo upi na ya ukubwa gani ili tuweze kuverify conclusions zako sio kutumia tu abstract conceptualizations!

3.Unasema bila haya "Huko nyuma nilibainisha, kuwa viashria vya jamii inayotaka mabadiliko vimeshaonekana. CCM itakuwa na mawili ya kuchagua; kuchukua jukumu la kuyaongoza mabadiliko hayo au kusubiri kuzamishwa na mkondo wa maji ya mabadiliko hayo"
False again!CCM si sehemu ya mabadiliko unayoyataja,Kwa kweli CCM ndio chanzo cha kiu ya mabadiliko hayo!Sasa unaposema CCM ichukue jukumu la kuyaongoza mabadiliko hayo unataka kutuambia kuwa SASA mbu anaweza kuongoza kampeni ya kutokomeza malaria kwa mafanikio!
Wewe Majjid vipi?Chadema wanasema tunataka gharama za kuwekeza katika elimu na afya zibebwe na serikali,CCM wanasema hayo hayawezekani!Halafu hao hao CCM ndio wasimamie kiu ya watanzania kupata elimu bora na si bora elimu kama kipaumbelele cha uwekezaji
wa Taifa?
Pili,Kwa taarifa yako mkondo wa maji hautakuja 2015! Uko sasa!Mkondo ni 2010 si 2015!

4.Angalia taarifa hii; Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Oktoba mwaka jana ulimalizika kwa kukipa ushindi mnono Chama Cha Mapinduzi. Chama hicho kilipata ushindi wa asilimia 91.71 za kura, kikifuatiwa kwa mbali na CUF iliyopata asilimia 3.94 na Chadema asilimia 2.76.
uchaguzi wa serikali za mitaa haukuwa na hamasa wala haukuamsha hisia zenye wimbi la mabadiliko kama ilivyo sasa!Watanzania wengi bado tulikuwa na chembe chembe za matumaini kwamba hali itaboreka,Kwamba CCM itajisafisha,lakini sasa ni dhahiri kuwa CCM haiwezi kujisafisha!Uchafu wao uko ndani ya mwili wenyewe,si kwenye nguo au ngozi tu bali ndani kabisa.Its in its very DNA if you will.Tumeona kwenye uteuzi wao,tumeona kwenye kulana wenyewe kwa wenyewe bila aibu-rejea masakata la Bashe,Mwakalebele,DED arusha,DED hai,DC kasulu,Na kadhalika mara kumi!

5. Mwanakijiji atatembea kwa miguu kilomita kumi kwenda kuhudhuria mkutano wa CCM. Atakwambia amepewa taarifa ya mkutano na Balozi wake wa Nyumba Kumi. Hivyo basi, CCM wanajivunia mtandao wao wa kichama kuanzia ngazi ya Balozi wa Nyumba Kumi, shina, tawi na kuendelea. Na hata mtandao wa Kiserikali.
Hilo tunalijua,N hasa hili la pili la mtandao wa Kiserikali.Ingawa wengi wa wanavijiji hao hawakuwa na mahali pa kukimbilia kwa maana ya "Credible and strong opposition" sasa wanapo!Tofauti na mawazo yako mimi natembea sana vijijini na huko nimekuta mwamko wa ajabu.Alama zinazoonekana bado ni za CCM kama vile mabango,picha,bendera nk lakini mioyo ya watu wengi ambao walikuwa wanachama na wapenzi wa CCM haiko tena huko!Wanaona afadhali upinzani kwa vile hali ya maisha imezidi kuwa duni kupindukia!Mfumuko wa bei haushikiki,bei za mazao hazijaboreka,Gharama za matibabu zinapanda kila siku,maji hakuna,umeme ndio ndoto ya alinacha....KIMSINGI WANAJIULIZA AHADI YA "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA" IKO WAPI?NA KWA NINI KIKWETE HUYU HUYU ANATULETEA AHADI NYINGINE WAKATI ILE TULIYOIPENDA KUKAMCHAGUA YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA HAJATUTIMIZIA?No,Majjid!Kikwazo nambari wani kwa watanzania kuingoa CCM sio wanachama,wapenzi wala wananchi wa vijijini na watanzania kwa ujumla wao!Ni mfumo ulioko madarakani!Ni serikali inayojitahidi kila kukicha kukikicha chama tawala unfair advantage!

6.Unasema "Inaonekana sasa, kuwa zama za ' First Lady' kuwa ' Mama wa nyumbani' Ikulu zimepita. Ni dhahiri, kuwa kwa mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete, amenufaika sana na ushiriki wa karibu wa mkewe na mwanawe Ridhiwani. Na si kwa Jakaya Kikwete tu, CCM kama chama, wagombea ubunge wake wananufaika kwa kiasi kikubwa na uwepo wa Mama Salma Kikwete na Ridhiwani kwenye kampeni.

Wote wawili, Salma Kikwete na Ridhiwani Kikwete wana mvuto wa kisiasa unaoongezewa nguvu na wao kuwa wanafamilia ya Rais aliye madarakani na ambaye bado, kiukweli, ana mvuto kwa Watanzania walio wengi."
Ukweli ni kwamba mvuto wa kikwete umepungua sana sana!Hivi sasa hana analoweza kujivunia katika utawala wake wa miaka mitano.Na ndio maana hata kauli mbiu yao ya "Maisha bora kwa kila mtanzania" si tu kuwa wameizika rasmi lakini hata kutamkika haitamkiki.Hata yeye binafsi anaona kuwa kutamka kauli mbiu hiyo kwa sasa ni kejeli kwa watanzania.Na kwa raisi mwenye sifa ya kuropoka na kutotumia busara katika kauli zake kama kiongozi wa nchi-kuliona hili basi ujue ameboronga kweli kweli!(Rejea kauli zake kuhusu wanafunzi na waathirika na ukimwi,Ukitaka kula lazima na wewe uliwe n.k)
Salma na Ridhiwani!
Salma asingekuwa anatumia rasilimali zetu sote kwa kampeni ya mumewe nadhani baadhi yetu tusingejali sana kwa vile ukweli ni kwamba hana ujumbe mpya wenye mvuto kwa watanzania.Binafsi nadhani ana "add insult to injury" kwa wengi wanaochambua masuala ya nchi yetu.Hanishawishi kwamba kikwete ni bora....On the contrary mm namwona kama kielelezo cha udhaifu wa kikwete mwenyewe na serikali yake.
Ridhwani!Hivi maggid unapozungumzia mvuto wa kisiasa unamaana nisha nini hasa?Haiba?Smiling faces?Ninavyo jua mimi mvuto wa kisiasa unatokana pamoja na mambo mengine ni falsafa inayotegemeza convictions zake, uwezo wa kupanga na kuelezea hoja zenye mafiko,Uzito na umuhimu wa ujumbe anaouwasilisha muhusika na jinsi muhusika anavyo fanikiwa kujitanabasisha na wanaomtazama au kumsikiliza.Katika haya yote sioni jinsi huyu bwana mdogo anavyofiti.Picha tunayoipata wengi linapotajwa jina lake ni mtoto wa baba (au mama),aliyeoteshwa kama uyoga kwenye medani za siasa za kitaifa bila kuwa na merits,anayetafuta cheap popularity lakini mwenye visasi na visa.Hatuona chochote kinacho mdifine yeye kama yeye anachoweza kukitumia kuwa impress watanzania.He is just another liability!

7. Udhaifu wa CHADEMA
Unajidhihirisha kwenye eneo la oganaizesheni na kifedha. Hilo nililibainisha katika makala yangu yaliyopita. Bado CHADEMA haina uwakilishi mpana katika ngazi za mashina na matawi. Niliandika, kuwa Dr Slaa anaweza kutua na helikopta Pawaga Iringa, lakini mara ile akiruka, huku nyuma hakuna watendaji wa CHADEMA wa kufanya kazi ya CHADEMA. Kuna taarifa pia za wagombea wake ubunge na udiwani kukosa nguvu za kifedha kuendesha kampeni .Hapa walau umesema ambacho wengi wetu tumekiona na ni changamoto ya kweli(Rejea post yangu juu ya kujitoa kwetu katika struggle ya kuleta mabadiliko jana hapa JF).Ingawa si kweli kwamba chadema haina uwakilishi katika ngazi za mashina na matawi.cha msingi hapa ni kukubali kuwa bado tuna kazi kubwa ya kufanya ingawaje haimananishi kwamba tuwaache CCM watupeleke ICU mwaka huu wakati tukiimarisha ngazi hizi tajwa,la hasha,ni afadhali turekebishe mapungufu haya wakati jahazi liko katika mikono salama ya Dr.Slaa.Hili la kukosa fedha limo ndani ya uwezo wetu,Kama kweli tunayahitaji mabadiliko yatakayotuletea Tanzania yenye neema ni lazima yatugharimu.Ni lazima tujitoe kwa hali na mali ili kuliangamiza zimwi liitwalo CCM.
Sijui kama utanikumbuka rafiki yangu maggid,Enzi zile za JKT Itende pale mbeya,enzi ambazo tulisafirishwa bure kwa warranti kwenda kujenga nchi yetu baada ya kusomeshwa kwa gharama za serikali zilizochangiwa na wananchi wote!
Enzi zile ambapo watumishi walikuwa wakiwajibika na kutimiza wajibu wao,Enzi ambazo kauli za kiongozi wa nchi ilikuwa ikimaananisha utashi wetu kama taifa,Enzi ambapo watoto hawakuwa wapiga debe wa baba zao,Enzi ambayo kichefuchefu cha kiongozi mkuu anayewasafisha na kuwakumbatia mafisadi papa bila aibu na kisha kutugeukia na kutuomba kura hakikutusumbua kama sasa!Enzi ambayo tuliamini katika kuweza na si katika mawazo mgando ya HAIWEZEKANI!!Enzi ambayo ilikuwa AIBU kuwa omba omba wakati sasa ni fahari ya TAIFA!
Nitaendelea kukufunulia udhaifu wa hoja na mkakati wenu kesho panapo majaaliwa.

:llama:

"True freedom must be expressed through the human ability to think critically, to analyze and to make informed decisions about oneself, his society and the world "- Sidanganyiki2010
 
Unaota!!! Vijijini watu wamebadilika sana juzi nilikuwa naongea na rafiki yaku kutoka kyela anasema kabisa wanavijiji wanamwambia Mwakyembe ubunge tunakupa lakini swala la Urais kikwete si chaguo letu safari hii. Geita vijijini wananchi wanasema kabisa safari hii ni Dr. Slaa. Musoma vijijini walimu wanasema waziwazi kuwa tunampa Dr. Slaa. Sasa wewe unatoa tu maelezo bila data.

Tunajuaje kama hizo simu ulikuwa umepiga tayari ushakula bange zako na uliyokuwa unayasikia siyo uliyokuwa unaambiwa? :tonguez:
 


Maggid mark my words, matokeo ya ucahaguzi huu yatakushangaza sana kama tathmini yako ndiyo hiyo!!!!!!!! Kwa uhuru huo huo unaouzungumzia, this is my prediction

Wa kwanza Dr. Slaa, wa pili JK na wa tatu Lipumba.......... haha ahaha ahahah

Maggid anajua kabisa anachokifanya. Hawa ni wale waliotumwa kufanya kazi za propaganda kupitia magazeti. Lakini ukweli halisi wanaufahamu.

Kama alivyosema Kitila hapo nyuma, hivi huyu bwana anafikiri JF ni mambumbu kiasi cha yeye kulala na kuota hivi au kuhisi hivi then atuletee ndoto au hisia zake. Hawa ni wale watu wanaojari matumbo yao tu. Baada Tarehe 31 October, matokeo yakitoka kinyume na anavyotegemea utaona anaandika tofauti na ikiwezekana yeye ndiye atakuwa wa kwanza kumsema huyo mshikaji wake vibaya kwenye hizo hisia zake. Watu wa type hii ni kama Yuda........!!!!!!
 
nichukue fursa hii kumpa pole ndugu Maggid, tathmini yake haina uhalisia kabisa. historia ya 2005 na uchaguzi wa serikali za mitaa siyo vigezo vya sasa. hilo limedhihirika katika chaguzi ndogo zilizofanyika baada ya 2005. chaguzi za serikali za mitaa hazina hamasa kama uchaguzi mkuu, hata usimamizi wake uko kwenye ofisi ya waziri mkuu. naamini kabisa ushindi upo kwa Slaa kama mimi na Maggid tutampa kura zetu. Namuomba huyu ndugu atoe kura yake kwa Slaa halafu aje kutoa tathmini baada ya uchaguzi.
 
mjengawa,Michuzi, Jiachie.Original comedy wote hawa ni vibaraka tu wa ccm so haina haja ya kujenga nao hoja yoyote ile.kimsingi hawana jipya wameshapewa tshirt na vijisenti ndo vinawasumbua waende huko huko kwa mafisadi wao waendelee kuwaandika kwenye blog's zote
 
Magid Mjengwa,
Pole kaka na kazi.
Makala yako ni nzuri kutegemea ni nani anasoma, wala huna sababu ya kusema utaudhi wengi, hii ni jamiiforums.
Mimi nashindwa kukuelewa baada ya kusoma na kuona ni makala zile zile za siku zote. Nilitegemea wewe kama mwandishi wa habari kama sijakosea, ungekuja na tathimini yakinifu ya uchaguzi wa 2010 badala ya kutumia takwimu za zamani ambazo zinaweza zisifanyekazi mwaka huu. Dr Slaa alishinda ubunge Karatu 1995 bila ya kuwa na madiwani kama sio mmoja vilevile Dr walid amani kaburu, Lyatonga mrema Temeke, Makongoro nyerere Arusha nk.

Nilitegemea kwa kuwa wewe unabahati ya kukutana na wapiga kura katika pita pita zako ungeleta takwimu hata kama sio rasmi. Mfano ungewauliza wapiga kura kila unapopita usingekosa kumi au ishirini kwa jimbo moja na kuweka viswali virahisi angalau mmbunge na raisi ukaweka vyama, ungeweza kuja na picha ambayo tusingeweza kuweka walakini na kazi yako ya uandishi.

Nikijaribu kufuatilia makala zako, naona kama vile unaogopa kitu fulani kwahiyo huna jinsi ila kuna wakati unakuwa wewe kuna wakati inabidi uridhishe upande. Inaniwia vigumu kama Synavote wameminya matokeo ya utafiti ulioonyesha Dr.Slaa anashinda. Vilevile matokeao ya maoni kwenye majimbo mbali mbali yanaonyesha jinsi wapinzani wanavyokubalika sio Chadema pekee kuna baadhi Chadema, CUF. Kizazi hiki tunatakiwa kuwa tofauti kidogo badala ya kuandika ukiwa chumbani twendeni kwenye maeneo ya tukio na tuandike habari inayotokea.

Sina chanzo za habari zako, ila nanona umetumia uchaguzi wa mwaka 2005. Mapinduzi ya demokrasia duniani huwa yanashangaza wengi, watawala wengi wanashtukizwa ndio maana wengi wanaishia kuleta vita, kama Mugabe, nk. Wamarekani waliamini Obama hawezi kuwa Raisi kwani ni mweusi na kazaliwa na baba mwafrika. Walishangaa sana walipomkuta Ikulu, mpaka hivi leo wapo amabao hawaamini.

Sikulazimishi uandike habari ambayo unaona si ya kweli, lakini habari yako haina mshiko wowote. Tukiangalia mwamko wa wananchi mwaka huu tunaona uko juu, elimu ya uraia na uchaguzi na watu kujua haki zao imepanda, watu wa kada mbali mbali wameanza kuamini kuwa wapinzani nao wanaweza kuleta mabadiliko. Majimbo mengi wamesimama wagombea ambao wanaeleweka na wananchi tofauti na miaka mingi, wachangiaji wamaeongezeka wanakisaidia chama hii ikiwa ishara ya kukubalika.

Ni wabunge wangapi Chadema inaweza kupata, Tendwa alisema 80-100, wewe mjengwa unasema wachache kuliko wa CUF, Chadema wanasema zaidi ya 100. Na sisi tunasema tutawapata wengi kwani mori upo juu. Sisi tuliopo kwenye uhamasishaji kuanzia ngazi za matawi tunapata matumaini makubwa, tunaona tofauti yawananchi wa leo na 1995.

Ndugu Mjengwa Duniani hakuna kampuni ya poll ya chumbani, zote zinakwenda kufanya kazi na kuuliza wapiga kura waliojindikisha, na sayansi hiyo inafanya kampuni hizo zisitofautiane kwenye majibu yao kwa asilimia nyingi. Mara nyingi wanasema ukweli kutokana na hali halisi. Sasa wewe kuja na takwimu za chumbani sio za kisayansi kwenye dunia ya leo ukiwa mwandishi unakuwa umeshindwa kazi yako. Takwimu za ukweli hakuna wa kuziogopa wala kuchukia labda mwehu kama wananchi watasema tunamchagua Mjengwa huwezi kataa. Ila kutumia kalamu kuwa mtabiri kama shekhe Yahaya ni usaliti wa elimu ya uandishi wa habari. Kazi kubwa ya waandishi ni kuelimisha umma kwa kutumia vyanzo vya ukweli na habri zilizotafitiwa.

Unapima mwendo wa uchaguzi kwa kuuliza wapiga kura kwa wakati huo. Siasa za Tanzania zinabadilishwa na nani anagombea wakati huo, bado hatuna siasa za kichama sana, watu wanaswing na mgombea na rushwa wakati mwingine inahamisha wapiga kura. Sasa badala ya kutuletea matokeo ya maruhani anza kujadili jimbo kwa jimbo au mgombea kwa mgombea.[/QUOTE
]

Hapo Kwenye red, umemwambia ukweli. How much money amepokea mpaka awe blind kiasi hiki? Sijui kama nitasoma tena makala zake kwenye gazeti nilipendalo la Raia Mwema.
Yafaa watu wajue kwamba pesa si kila kitu duniani, lazima uheshimu utu wako!
Mjengwa? NO!!!!!!
 
Mjengwa bwana anajulikana huyu katika mambo makuu mawili (kwa mtazamo wangu); ukichunguza sana kwa makini machapisho yake, ninashawishika kuamini ama ni kada wa kile chama kikongwe (japo hataki kuweka bayana); ama pia ni mfurukutwa wa zile siasa zinazoleta shida kati ya watu (za kiimani). Anyway, huu ni mtazamo wangu lakini nina uhakika siku moja nitakuja kuwa proved right. Ni sawa na usanii niliuona 2005 na kutokutoa kura yangu kwa "tumaini jipya". Madudu yalivyoanza moyoni nilipata amani maana nilijua kuwa nilikuwa sahihi kwa wakti ule (japo kwa hisia tu). Kuhusu Mjengwa.... tusubiri tuone... ndio wakuu wa wilaya wateule hawa wanaokuja...time will tell

It is before he wrote "ABRAKADABRA"
 
Lengo ni kututayarisha kisaikolojia kwa mchezo mchafu wenye baraka za dola na hivyo kupunguza hasira za wananchi dhidi ya kitendo kama hicho. Mfano moja mzuri ni kufichwa kwa matokeo ya kura ya maoni iliyoendeshwa na Synovate yaliyompa Dr. Slaa ushindi. Hatudanganyiki !

Na lengo la hizi polls za JF zinatolewa offline kwa ajili ya matengenezo halafu baada ya matokeo kuchongwa zinarudishwa je ni kwa ajili ya kujitayarisha kisaikolojia?

Synovate wenyewe wamekataa kuwa hawajawahi kufanya hiyo kura ya maoni, sasa kama siyo kuathirika kisaikolojia basi kulazimisha kitu ambacho hakipo sijui ni maradhi ya aina gani. :tonguez:
 
Back
Top Bottom