maggid
nadhani umerudia yale yale ya wiki mbili zilizopita na hakuna jipya japo una uhuru wa ku-recyle mawazo yako kila wakati.
Kigezo chako cha uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi wa 2005 ni weak mno kwa sasa. Kuna mambo mengi yamebadilika ikiwamo chemistry ya siasa za uchaguzi. Fikiria haya:
-jk kudai miaka 5 ya kwanza alikuwa anajifunza kazi, sasa anaomba ili afanye kazi ni tamko la hatari. Watu walichagua rais kufanya kazi si kufanya mazoezi.
-ccm ilikuwa moja na imara wakati wa uchaguzi wa 2005 kuliko ilivyo sasa. Kuna wana ccm wengi watakaopigia upinzani kuliko idadi ya wapinzani wenyewe. Ushindi wa kikwete 2005 ulichangiwa na kura za wapinzani kuliko unavyoweza kutegemea sasa.
-jk aliridhi uchumi mzuri kutoka ben kuliko hali ya uchumi tuliyo nayo sasa.
-kampeini za uchaguzi wa 2005 zilifanywa na mtandao plus chama - hizi za sasa zinafanywa na familia -jk, salma, ridhiwani na miraji. Jioni hii jk amemuita makamba kulalamika kuwa kuna maeneo hayana mabango na anahitaji maelezo. Hii si kazi ya mgombea wa chama kikubwa!
Chemistry ya namna hii, haina nafasi katika matundu ya uchambuzi wako uliolalia "mazoea" na theory iitwayo "makambaism".
ukweli unauma na ni mchungu kama shubiri!!!