Mjengwa alonga 'live'!

magoma

New Member
Mar 2, 2009
4
0
Hii ni kutoka mjengwablog...


Katika kila tufanyalo, tukumbuke, kuwa kuna Watanzania wenzetu kwa mamilioni ambao hawana huduma muhimu kwa mwanadamu. Kuna lazima ya sauti zao kusikika;

SIKILIZA:

[mp3]http://kwanzajamii.podomatic.com/enclosure/2009-03-24T12_18_02-07_00.mp3[/mp3]
 
Mkuu Magoma hongera kwa kutupa habari za Mjengwa, naona una posts 4 humu JF, na zote ni threads ulizoanzisha kuhusu Mjengwa. Na hizo "threads" ni zifuatazo:-
Mjengwa alonga 'live'!
Mjengwa atangaza rasmi gazeti jipya
Mjengwa ajibu: Tumejipanga upya,Tunakuja!
Mjengwa:Nimepumzika Kuandikia Rai Mwema

magoma
Junior Member
Join Date: Mon Mar 2009
Posts: 4
Thanks: 0
Thanked 4 Times in 2 Posts
 
Msimamo wa gazeti jipya la ' Kwanza Jamii' na timu yao. Iko kwenye mjengwablog.
Sumaku.

TAHARIRI: HUU NDIO MSIMAMO WETU
NDUGU Msomaji, leo Jumanne Machi 31, 2009 , Tanzania kama nchi imeendelea kufurahia uhuru wa kutoa maoni kwa njia ya vyombo vya habari. Hii ni kwa kuwa na gazeti jipya na huru la ‘Kwanza Jamii’. Hivyo basi, unalolisoma sasa kwa mara ya kwanza ni gazeti la ‘ Kwanza Jamii’. Kama ilivyo kwa jina lake, ni gazeti la jamii, ni gazeti lako.

Kwanza Jamii ni gazeti la kijamii lililoanzishwa na wanajamii kwa ajili ya wanajamii wa Kitanzania ndani na nje ya mipaka yetu. Pamoja na nia ya kibiashara kwa maana ya kupata faida, waanzilishi wa gazeti hili wamesukumwa na vipaumbele vikuu viwili; mosi, tunaamini kwamba nchi hii imejaaliwa kuwa na vyombo vingi vya habari vinavyojumuisha redio , magazeti na televisheni.
Na tunaamini pasi na shaka, kuwa kuna Watanzania wengi hawapajapata nafasi ya kutosha kutoa maoni yao kwa nia ya kushauri, kukosoa, na hata kupongeza juu ya mustakabali wa mwenendo mzima wa utendaji wa vyombo mbalimbali vya usimamizi wa rasilimali za umma na usimamizi wa mifumo mbalimbali ya kiutawala.
Hivyo basi, Kwanza Jamii tuna azma ya kupanua wigo kwa Watanzania kupata nafasi hiyo ya kupata habari, kuelimika na kuburudika . Si hivyo tu, na hata Watanzania wenyewe, kupitia kalamu zao, kompyuta na simu zao, kusema yale wanayotaka kusema kupitia gazeti hili. Maana, Kwanza Jamii ni gazeti lao bila kujali tofauti za kikabila, kidini na kirangi.
Pili, zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanaishi vijijini. Kwanza Jamii litashirikiana kwa karibu na ndugu zetu hao ili kubaini kero, karaha, taabu na hata raha wanazozipata kwenye maeneo yao hayo. Ingawa jambo hilo lina gharama, lakini tunaahidi kujitahidi kuwafikia Watanzania wenzetu hawa kwa namna moja au nyingine.
Tunajua , kuwa wapo wenzetu mahodari wa kusema bayana kwa nia njema, lakini pia, miongoni mwa asilimia 80 hiyo ya Watanzania, wapo wasioridhishwa na mambo fulani fulani kwenye mfumo wetu wa kimaisha. Hata hivyo, kwa sababu mbalimbali, hawana uwezo wa kunyanyua kalamu au ndimi zao na kukemea. Hawa tunawaomba wasifadhaike na kukata tamaa.
Kwanza Jamii tumejipanga na tumewaletea wachambuzi wanazuoni na wasio wanazuoni. Ni wachambuzi mahiri kabisa katika maeneo yao. Na tuamini, kuwa wapo tayari kuwaondoa upweke na kusemea mioyo yenu kwa nia njema kabisa ya kushiriki kuijenga nchi yetu. Maana, hawa ni wasomi waliosomeshwa kwa kodi za wanajamii walio wengi wa kule vijijini. Ni jukumu la wasomi hawa kuanza kutumia maarifa yao kuisaidia jamii pana walioiacha nyuma yao.
Na katika zama hizi za kuwafichua wabadhilifu wa mali za umma waliojipatia jina jipya la mafisadi, inasemwa mitaani, kuwa mafisadi hao wameanzisha, na wanaendelea kuanzisha na hata kuvifadhili vyombo vya habari na wanahabari wenyewe kwa nia ya kufunika maovu yao. Sisi- Kwanza Jamii, tunaomba tujipambanue kungali mapema, kuwa gazeti hili halikuanzishwa kwa faida iliyotokana na shughuli zozote za kifisadi.

Hivyo basi, tunatoa wito kwa wale wote wanaojijua, kuwa wanachuma mali zao kwa njia za kifisadi, kuwa gazeti hili si mahali salama pa kukimbilia ili kuwapakizia ubaya wale waliobaini unyang’au wao. Kwanza Jamii tunaahidi pia kushirikiana na wale wote wanaokandamizwa kutokana na mfumo wa uongozi kwenye vijiji vyao, mitaa yao, makazini na hata majumbani mwao. Ingawa , katika kufanya hivyo, hatuko tayari kuingilia uhuru wa familia bila utashi wa wahusika. Kwamba tutazingatia miiko ya taaluma ya uandishi wa habari. Na tukumbuke, hakuna uhuru usio na mipaka.
Kwanza Jamii tutapigana bega kwa bega na wale wote walio tayari na wenye dhamira ya dhati ya kupambana na maovu katika jamii yetu. Kwanza Jamii tutakosoa kwenye makosa na tutashauri penye mkanganyiko. Lakini pia hatutasita kusifu na kupongeza panapostahiki.
Kwanza Jamii hatutamwonea mtu au taasisi yeyote ile kwa dhamira na makusudi ya kutaka kuonea. Na katu hatutomwogopa wala kumwonea aibu yeyote atakayekiuka utaratibu wa kisheria tuliojiwekea katika mfumo wa maisha yetu, uongozi wetu, siasa zetu na tamaduni zetu .
HUU NDIO MSIMAMO WETU.
 
Back
Top Bottom