Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Miaka nenda rudi tumesikia "mafuriko" na kila mafuriko yanapotekea utasikia "mabondeni". Kila mafuriko yanapotokea zinapigwa picha ya jinsi watu wanavyoweza kusurvive mafuriko hayo. Tumeandika hapa mara nyingi na picha nyingi za mafuriko katika Jiji la
Dar zimewekwa. Tumeona watu wakiendesha magari na pikipiki kwenye mitaa iliyojaa maji na pia tumeona watu wengine wakibebwa mgongoni (kwa ada fulani) kuhamishwa toka upande mmoja kwenda mwingine.
Kwenye baadhi ya maofisi kuna matairi yamepangwa au matofali ambayo yamekaa hapo kwa ajili ya wakati wa mafuriko ambapo watu huwezi kutumia na sehemu nyingine kuna watu huweka matairi au matofali na kuwatoza watu fedha kwa kupita wakati wa mafuriko na kweli kabisa wapo watu wanapita na kulipa bila kufikiria.
Jiji la Dar ni miongoni mwa miji midogo kabisa kijiografia labda kuliko mji mwingine wowote Tanzania. Lakini tunaweza kusema pasipo shaka kuwa kushindikana kwa kutengenezwa kwa mfumo mzuri wa maji ya mafuriko (storm water) na maji machafu (sewage system) ni dalili tu kuwa tuna wasomi wengi na wanasiasa wengi ambao wanaishi Dar lakini wote hawa wameshindwa kabisa kutafuta suluhisho la tatizo la mafuriko.
Sasa hivi magenius wetu wameamua kuja na mradi mkubwa wa mabasi yaendayo kasi ambayo nayo kwa hakika yatapita kwenye njia hizi za mafuriko. Licha ya mradi huo mradi mwingine wa mabilioni umebuniwa wa kujenga mabarabara ya juu kwa juu ili na sisi tuweze kupiga picha nyingi na kuonesha kuwa na sisi "tunazo". Ukijumlisha na mradi wa daraja kubwa la Kigamboni ni wazi kabisa kuwa Watanzania wanaonekana wanaweza! Lakini unajiuliza kwanini wameshindwa hili la kuhakikisha jiji halifuriki kila mvua ikinyesha?
Dar zimewekwa. Tumeona watu wakiendesha magari na pikipiki kwenye mitaa iliyojaa maji na pia tumeona watu wengine wakibebwa mgongoni (kwa ada fulani) kuhamishwa toka upande mmoja kwenda mwingine.
Kwenye baadhi ya maofisi kuna matairi yamepangwa au matofali ambayo yamekaa hapo kwa ajili ya wakati wa mafuriko ambapo watu huwezi kutumia na sehemu nyingine kuna watu huweka matairi au matofali na kuwatoza watu fedha kwa kupita wakati wa mafuriko na kweli kabisa wapo watu wanapita na kulipa bila kufikiria.
Jiji la Dar ni miongoni mwa miji midogo kabisa kijiografia labda kuliko mji mwingine wowote Tanzania. Lakini tunaweza kusema pasipo shaka kuwa kushindikana kwa kutengenezwa kwa mfumo mzuri wa maji ya mafuriko (storm water) na maji machafu (sewage system) ni dalili tu kuwa tuna wasomi wengi na wanasiasa wengi ambao wanaishi Dar lakini wote hawa wameshindwa kabisa kutafuta suluhisho la tatizo la mafuriko.
Sasa hivi magenius wetu wameamua kuja na mradi mkubwa wa mabasi yaendayo kasi ambayo nayo kwa hakika yatapita kwenye njia hizi za mafuriko. Licha ya mradi huo mradi mwingine wa mabilioni umebuniwa wa kujenga mabarabara ya juu kwa juu ili na sisi tuweze kupiga picha nyingi na kuonesha kuwa na sisi "tunazo". Ukijumlisha na mradi wa daraja kubwa la Kigamboni ni wazi kabisa kuwa Watanzania wanaonekana wanaweza! Lakini unajiuliza kwanini wameshindwa hili la kuhakikisha jiji halifuriki kila mvua ikinyesha?