Mjadala wa katiba mpya ITV; Mnyika, Tambwe Hizza na Dr. Mvungi

Mbona jamani tunataka kuwa semea wengi? tuache watu wajisemee wenyewe jamani, tusiendeshwe kwa mhemko mtu anasema nchi isiendeshwe na kundi flani la watu wakati huohuo anatuasa vijana tupambane ipatikane katiba mpya we umejuaje mimi naihitaji katiba mpya ama la wakati hata hiyo iliyopo siijui na sijui mapungufu yake? Ndugu zangu labda tujaribu kukumbuka waliyotueleza wanazuoni wetu pale Nkrumah Hall Chuo Kikuu cha Nchi Prof. Issa Shivji, Jenerali Ulimwengu na Azavel Feza Lwaitama kuwa tusiwasemee watu tuwaache waseme wenyewe na ndiyo maana katika kongamano lile walikua wanaangalia mambo makuu matatu 1. Je ipo haja au kuna uhitaji wa katiba mpya? 2. Kama ipo haja au hii iliyopo ibadilishwe, je iwe na maudhui gani? 3. Je mchakato upi utumike kupata katiba hiyo? walisisitiza kuwa haya majibu yote yanapaswa kujibiwa na wananchi na siyo mtu au chama fulani. Tunacho paswa kuangalia je kamati hiyo itatoa majibu kwa nani? itatumia adidu rejea zipi au za mfumo upi? wananchi watapewa uwanja uhuru wa kuelimishwa kabla ya kutoa maoni? Tukisema hoja ipelekwe bungeni tumeshatahadharishwa kuwa idadi ya wabunge wa CCM ni kubwakuliko upinzani hivyo tusishangae ikarudi katiba ya CCM kama Shivji aliyotuelimisha. Sidhani kama tukiandamana nchi nzima ndiyo itakua katiba mpya kama alivyosema mwanasias flani siku ya kongamano kuwa damu ya Arusha ndiyo dibaji Lazima kuwa na organ au chombo kitakacho ratibu swala zima kinaweza kuwa cha rais au bunge na si vinginevyo. Ujue katiba inabadilishwa na katiba na siyo vinginevyo.
wanajaribu kutafuta lugha ya kulipush jambo hili mbele ili waweze kuenjoy utawala ndani ya katiba iliyopo.
 
Kuhusu malipo ya DOWANS! Nimeshangaa sana kamati kuu ya CCM kuja na tamko kuwa kuilipa DOWANS hakuepukiki kwa kuwa ni swala la kisheria!!! Pamoja na kusema kuwa Serikali isubiri kutoa malipo kwa kuwa kuna-watz waliokataa rufaa kauli hiyo ni kama inabariki na hata kuinfluence maamuzi ya mahakama ambayo kismsingi wateule wake wote wanatokana na Chama Cha Mapinduzi. I am totally disappointed!
 
Ushauri kwa CCM: Mijadala mikubwa kama ya katiba wajitahidi kupeleka mtu mwenye kuelewa mambo vinginevyo itakuwa mnafanya kama maigizo na kutoa hoja za kitoto. Kwa mfano mjadala wa katiba wa ITV, Tambwe Hiza kaongea nini? Alikuwa kama mtoto wa primary school. Ebu kuweni makini na mambo ya msingi.
 
Wakuu, kwetu hatukuwa na umeme. Shukrani kwa kutupatia wasifu wa tambwe, mtoa upupu. Tunaomba itv wasimwalike tena ili watu wapate hoja za kupost hapa kutuelimisha


Unaajua kwa mara ya kwanza ndio nimemuona na kumsikia huyo Tambwe. Nilikuwa nawahurumia washiriki wa kipima joto pamoja na Masako kwani huyo Hiza alionekana kabisa amekuja kupoteza muda na kuufanyia fujo mdahalo. Yaani hata wanafamilia wake kama walikuwa wanaufuatilia mdahalo huo watakuwa wanajuta kuwa na uhusiano naye, it is shameful and a joke of a man!!!!
 
Mi naona swala la katiba limekuwa katika mdomo wa kila chama,ama kweli wote hamna huruma na watanzania wanaowaona.kama kweli mnatetea maslahi ya watanzania tunaomba kuanza shule watu wasomekatiba waijue
 
Akina Tambwe Hiza, Yusufu Makamba, yule mama wa CCM Arusha, ndiyo viongozi waandamizi wa chama tawala ambacho kinaota ndoto ya sera za kushika hatamu!!!!!!!!!!!!!!! Shame!!!!!! Siasa ya vyama vingi ina umri wa mtu mzima-hii ni serikali ya awamu sijui ni ya ngapi vile???????????
Kwa mwelekeo huu wa CCM, ukombozi uko just next door-hizi ni ishara za Mungu, si za wanadamu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Nchi hii ni mali ya Mungu, siyo ya mashetani yanayomlinda rais wake!!!!!!!!!!!!!!! Majira ya Mungu ya kukomboa taifa hili yamefika!!!!!!!!!!!!!!!!-is just next door!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Tukio hili litakavyotokea wengi hawataamini macho na masikio yao-itatokea kama muujiza mkubwa kwa taifa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
tambwe hiza!!hao itv wametumia kigezo gani kumualika mtu wa aina hii au swala la katiba wanataka kuligeuza kuwa propoganda?ndo kazi ya huyu bwana cjawahi kumsikia akiongea point hata 1tu katika maisha yangu.
huyu alitumwa na ccm kwa sababu hawana maelezo yoyote yenye maana ambayo watayatoa kwa wananchi ndo wakaamua wamtume huyu mbwa aende kubweka tu mule ili mjadala usieleweke, ndo maana alikuwa anabweka tu mule mwanzo mwisho anachokisema hakieleweki.

 
Back
Top Bottom