wanajaribu kutafuta lugha ya kulipush jambo hili mbele ili waweze kuenjoy utawala ndani ya katiba iliyopo.Mbona jamani tunataka kuwa semea wengi? tuache watu wajisemee wenyewe jamani, tusiendeshwe kwa mhemko mtu anasema nchi isiendeshwe na kundi flani la watu wakati huohuo anatuasa vijana tupambane ipatikane katiba mpya we umejuaje mimi naihitaji katiba mpya ama la wakati hata hiyo iliyopo siijui na sijui mapungufu yake? Ndugu zangu labda tujaribu kukumbuka waliyotueleza wanazuoni wetu pale Nkrumah Hall Chuo Kikuu cha Nchi Prof. Issa Shivji, Jenerali Ulimwengu na Azavel Feza Lwaitama kuwa tusiwasemee watu tuwaache waseme wenyewe na ndiyo maana katika kongamano lile walikua wanaangalia mambo makuu matatu 1. Je ipo haja au kuna uhitaji wa katiba mpya? 2. Kama ipo haja au hii iliyopo ibadilishwe, je iwe na maudhui gani? 3. Je mchakato upi utumike kupata katiba hiyo? walisisitiza kuwa haya majibu yote yanapaswa kujibiwa na wananchi na siyo mtu au chama fulani. Tunacho paswa kuangalia je kamati hiyo itatoa majibu kwa nani? itatumia adidu rejea zipi au za mfumo upi? wananchi watapewa uwanja uhuru wa kuelimishwa kabla ya kutoa maoni? Tukisema hoja ipelekwe bungeni tumeshatahadharishwa kuwa idadi ya wabunge wa CCM ni kubwakuliko upinzani hivyo tusishangae ikarudi katiba ya CCM kama Shivji aliyotuelimisha. Sidhani kama tukiandamana nchi nzima ndiyo itakua katiba mpya kama alivyosema mwanasias flani siku ya kongamano kuwa damu ya Arusha ndiyo dibaji Lazima kuwa na organ au chombo kitakacho ratibu swala zima kinaweza kuwa cha rais au bunge na si vinginevyo. Ujue katiba inabadilishwa na katiba na siyo vinginevyo.