Sipo
JF-Expert Member
- Jul 25, 2008
- 2,139
- 91
Kuna tatizo la kujieleza wakati muomba kazi anapoenda kwenye usaili. Uzoefu unaonyesha kuwa wasailiwa wengi huwa wanachanganyikiwa na kushindwa kujibu maswali kwa ufasaha na kujikuta wanakosa kazi.
Thread hii lengo lake ni sisi wanaJF kuelezana mambo ya muhimu ya kufanya/kuzingatia wakati wa kufanyiwa usaili.
Karibuni
---------------
phil_kabuje: Epuka lugha hizi za mwili (body languages) wakati wa kufanya usaili (interview)
1.Epuka kukunja mikono yako kifuani hii huonyesha kujiamini kupita kiasi, dharau au wakati mwingine huashiria kutokubaliana na kile kinachozungumzwa
2. Kama umesimama, jitahidi unyooke, epuka kuegamia ukuta au kupishanisha miguu (kuchora alama ya X). Kama umekaa usiegamie sana kiti kwani hii huonyesha ishara ya uvivu. Kaa ukiwa umenyooka
3. Epuka kuwa wakwanza kukwepesha macho kwa haraka unapomuangalia anayekufanyia usaili au aliyekuuliza swali. Hii huonyesha kukosa kujiamin au tabia ya udokozi. Daima angalia mbele usiiname chini unapoulizwa maswali
4. USITAFUNE KITU chochote mdomoni iwe pipi au vidole vyako (hasa kwa wanawake)
5. Usionyeshe Ishara yoyote mbaya unapomzungumzia muajiri wako aliyepita (hata kama ndiye sababu ya wewe kuacha kazi)
6. Usiwanyooshe vidole wanaokufanyia usaili
7. Usitikise sana kichwa kupita kiasi. Ni vizuri kutikisa kichwa unapoonyesha kuelewa kile unachoambiwa, lakini mara nyingine inawezekana ukaulizwa swali la mtego ambalo hutakiwi kukubali!
8. Usiweke mikono nyuma au mfukoni unapoingia ndani au ukiwa umesimama. Hii hunyesha hali ya kutotaka kuwa muwazi, au majivuno.
9. Unachokizungumza kifanane na uso wako. Mfano unapozungumzia kitu kinachokufurahisha halafu una sura nzito, una hatari! Jitahidi kutoa tabasamu kila unapoulizwa swali au kuelezea kitu
10. Usiangalie sana juu ishara ya kukumbuka kitu. Hii huonyesha kutokuwa na hakika ya kile unachokizungumza!
Thread hii lengo lake ni sisi wanaJF kuelezana mambo ya muhimu ya kufanya/kuzingatia wakati wa kufanyiwa usaili.
Karibuni
---------------
phil_kabuje: Epuka lugha hizi za mwili (body languages) wakati wa kufanya usaili (interview)
1.Epuka kukunja mikono yako kifuani hii huonyesha kujiamini kupita kiasi, dharau au wakati mwingine huashiria kutokubaliana na kile kinachozungumzwa
2. Kama umesimama, jitahidi unyooke, epuka kuegamia ukuta au kupishanisha miguu (kuchora alama ya X). Kama umekaa usiegamie sana kiti kwani hii huonyesha ishara ya uvivu. Kaa ukiwa umenyooka
3. Epuka kuwa wakwanza kukwepesha macho kwa haraka unapomuangalia anayekufanyia usaili au aliyekuuliza swali. Hii huonyesha kukosa kujiamin au tabia ya udokozi. Daima angalia mbele usiiname chini unapoulizwa maswali
4. USITAFUNE KITU chochote mdomoni iwe pipi au vidole vyako (hasa kwa wanawake)
5. Usionyeshe Ishara yoyote mbaya unapomzungumzia muajiri wako aliyepita (hata kama ndiye sababu ya wewe kuacha kazi)
6. Usiwanyooshe vidole wanaokufanyia usaili
7. Usitikise sana kichwa kupita kiasi. Ni vizuri kutikisa kichwa unapoonyesha kuelewa kile unachoambiwa, lakini mara nyingine inawezekana ukaulizwa swali la mtego ambalo hutakiwi kukubali!
8. Usiweke mikono nyuma au mfukoni unapoingia ndani au ukiwa umesimama. Hii hunyesha hali ya kutotaka kuwa muwazi, au majivuno.
9. Unachokizungumza kifanane na uso wako. Mfano unapozungumzia kitu kinachokufurahisha halafu una sura nzito, una hatari! Jitahidi kutoa tabasamu kila unapoulizwa swali au kuelezea kitu
10. Usiangalie sana juu ishara ya kukumbuka kitu. Hii huonyesha kutokuwa na hakika ya kile unachokizungumza!