Mizimu Ndani Ya CCM.....UV-CCM Tuko Tayari Kuwaongoza Vijana Kwenda CHADEMA

Muke Ya Muzungu

JF-Expert Member
Jun 17, 2009
3,444
264
Kwa wale mnaofatilia maswala ya kisiasa, nadhani mmejiuliza ni kwanini kijana February Ma-ropes amekuwa kimbelembele sana, yaani amekuwa kama ndiye waziri wa nishati?? Amekuwa akijifanya mchapakazi sana, asiye na uhusiano na serikali ya JK, huyu kada wa Mafisadi, RA na EL ana mengi mazito.........UV....CCM tumemstukia tunaanza kuyamwaga. Ikiwa Hawatakubali mabadiliko ya Kweli, Tunaelekea CHADEMA
**************************

Mimi ni mjumbe kwenye kamati kuu ya UV-CCM; Mwezi February, niliandika taarifa kuhusu kudorora kwa uhusiano kati ya mkuu wa kaya na katibu mkuu wa chama tawala mzee Yusuf Ma-Ropes, lakini moderator akaja kuliondoa. Kwa sasa taarifa zimeshavuja kwamba Sekretarieti nzima ya Chama Tawala Imejiuzulu na uchaguzi wa viongozi wapya ni hapo kesho.

Hapa nipo Dodoma na mambo siyo mazuri. Wajumbe wa kamati kuu wamekuwa wakimlaumu katibu mkuu kuwa chanzo cha kuchukiwa kwa chama tawala. Ila ukweli wa mambo ni kwamba, mambo ni mazito zaidi ya tunavyoyafikiria. Uhusiano kati ya mkuu wa kaya "Jokabaya Mrishole Kiwete na Mzee wa Mipasho Yufusu Ma-Ropes umedorora kwa kiasi kubwa kweli. Kwanza, Mkuu wa Kaya Jabaya Kiwele, alimlaumu sana Mzee wa Mipasho Y. Ma-Ropes, kuingilia machakato mzima wa kura za maoni ndani ya chama tawala, kwa bahati alifanikiwa kuwaingiza aliowataka pamoja na mwanaye.

Mzee maropes alionekana kuwatoa viongozi waliochaguliwa kihahali na kuwaingiza watu wake. Hii ilikuwa ni dhahiri kule kwa Bashe, na hata kwa mzee Shelukindo, chama tawala kilitumia nguvu ya chama na serikali kuhakikisha mwanaye mzee maropes, Yaani Kijana February Ma-Ropes kutwaa ubunge wa Jimbo la Bumbuvili..Siyo hayo tu, tangu mwanzo, Mzee maropes alishasuka dili na mzee wa kaya kwamba mara tu mwanayee anapoutwaa ubunge, apewe uwaziri.

Hii ilikuwa ni dili iliyokuja kuharibika baada ya Usalama kupata taarifa kutoka kwa wamarekani kwamba mwanaye Ma-ropes alishiriki kwenye mambo ya kighaidi mtandaoni kwa kumtishia binti wa kifamilia moja tajiri sana huko marekani. Kwani hii ilimuwepa pabaya mzee wa kaya, alilijibu swala hilo mwenyewe Baada ya kupokea hizo taarifa. Mkuu wa kaya alibadilika ghafla na kutupilia mbali pendekezo la kumpa uwaziri kijana February, kwani hapo mwanzo huyu kijana pia alikoroga na kumpa kashfa kubwa kwenye mradi wa malaria nomore. Hasira zilimjaa mzee maropes baada ya mwanaye kutoswa, ambaye alilazimika kuingia kwenye siasa za makundi kisirisiri. Mzee maropes aliingia kwenye kundi la wakina RA na EL

Kwa sasa, Mzee maropes, kamsukuma mwanaye pia kwenye kundi la Rosutamu Azize, na Edwardo Lowassana. Kijana February, amejenga bifu na mkuu wa kaya, baba yake naye hivyo hivyo ingawa hawezi kuonyesha kwenye umma kwani ni lazima washirikiane katika maswala ya kikazi. Mzee wa mipasho Y--Ma-Ropes, amepania kuwaacha wanaye kwenye nafasi nyeti. Mpango mzima ni kuwanadi kwenye media kuwa wachapakazi, hasa Mwambao wa Vodacom na February wa Bumbuvili. Lengo ni kumuacha bintiye mkuu wa mkoa, au mbunge viti maalum na kijana waziri. Kwa hiyo ushirikiano wake na RA na EL ni wa kwa manufaa binafsi na familia yake. Hatuwezi kukubali, kwani huyu February, anajaribu kutuvuruga hata sisi UVCCM

Kwa sasa huyu mzee ana bifu za kichinichini na JK kwa maana JK hakumchagua mwanaye kuwa Waziri. Basi hapo, akajiingiza kwenye mtandao wa RA na EL ili mwanaye awepokwenye baraza lijalo. Kwa hiyo tusibirini ni yapi yatajitokeza Dodoma Kesho, nitawahabarisheni zaidi... mara mambo yakizidi kushuka. Hatutaweza kuliongoza Chama ikiwa mabadiliyo tunayaoyataka hayatazingatiwa. Tuko Tayari Kwenda CHADEMA
 
ChAdema at work. Msitake kutudangannya watu waxzima na akili zetu. Mtawapata hao hao mafala kuwarubuni. Ulikolala wewe, sisi tushapapita toka juzi. Mnafik.
 
Endelea kutupasha yanayojiri Dodoma !!! Kuhusu kujiunga na CDM Karibu tunakusubiri ila tu kama huna sifa ya fisadi na kwamba huji kwa sababu umekosa madaraka huko kwa mafisadi wa CCM !!!.
 
NYOOOTE MNAKARIBISHWA CHADEMA BILA UBAGUZI ILMRADI TU KWANZA UWE NI MUUMINI KATIKA FALSAFA YETU YA 'UMMA KWANZA' NA KUWA TAYARI KULITETEA HILI WAKATI WOTE MCHANA AU USIKU, SIRINI AU MBELE YA HADHARA!!!!!!!!!!!!

Ewe Watanzania wenzetu mlioko bado ndani ya HILO SANAMU LA CHAMA CHA MAPINDUZI KOTE BARA NA VISIWANI, mnakaribishwa saaana kujiunga na CHADEMA au chama chochote cha upinzani nchini, kadiri ya mapenzi yako yanavyokutuma.

Ila tu ni kwamba huku kwetu CHADEMA tutavutiwa zaidi na ujio wako endopo kwanza ni kweli kabisa unaamini katika Falsafa yetu Mpya sana nchini inayosisitiza na kuaini katika dhana ya 'NGUVU NA MAMLAKA YA UMMA' katika katika masuala yooote ya kiutawala na kujiletea maendele.

Na kwamba kweli uko tayari kukana utawala wa KIFISADI na kule kuchukia wakati wote MAFISADI na machungu wanaosababishia taifa letu kwa kuchukua serikali yoote mateka yake na kuponda raha na raha na rasilmali zetu bila huruma; hivyo unaona ni vema utawala wa nchi kurejeshwa kwa wananchi na Maslahi ya Umma kuwa mbeeele wakati wote.

Endapo unajiona ni mtu huyu mwenye sifa zinazoelezewa hapo juu basi ujue tangu majuzi tu kadi yako ya uanachama CHADEMA kinakusubiri bila ubaguzi wowote kirangi, jinsia, dini na madhehebu zake, elimu, ukanda, kabila, kipato, umri wala kijiji au mtaa unakoishi.

Tofauti na hapo, CHADEMA hakipo tu kwenye window-shopping kupokea hata yule ambaye ni wazi ndiye aliyesababisha au kuhiari kutekeleza uwakala wa kufanya utawala wa umma kuondaka na machungu kutukumba kote nchini na wala si kujidakia tu hata chukizo la jamii yetu!!
 
ChAdema at work. Msitake kutudangannya watu waxzima na akili zetu. Mtawapata hao hao mafala kuwarubuni. Ulikolala wewe, sisi tushapapita toka juzi. Mnafik.

Mwaka huu mtaweweseka sana.Mara mchawi Chadema,mara mchawi Lowassa,et al.Mtamtimua hadi Kikwete lakini tutarajie nini kutoka chama cha kijambazi?Hizo zote ni laana za kuwadhulumu walalahoi haki zao na kuwaua wanapodai haki zao.

Watu wazima hovyooo!!!
 
Vijana wote makini wako CDM, ni vijana gani hao wanaosubiri kukokotwa na huyu kama si mazuzu wenzake!
 
Kafa Nyerere aliyeianzisha itakuwa CCM. Na Yesu jee, tena Mungu, "kafa". Itakuwa chama.

Unaanza kupayuka wewe!, mambo ya Mungu usiyafananishe na ya Mafisadi, usipende kututafutia balaa huku. Acha ccm ife yenyeweeee! Kama unataka kufa nayo kufa mwenyewe lakini huki usimchanganye YESU, tuko makini sana kuangalia usitupotezee mwelekeo! Ala!
 
Hivi nani kasema Chadema ni jalala la kutupa takataka zinazotoka ccm? Mafisadi, watu wenye fikra uvundo, wasiojua kwa nini sisi ni masikini, wanaopiga raia risasi na mabomu, wanaokandamiza uhuru wa kujieleza.
 
Freedom of mind is a freedom of soul, ccm in a deep internal-conflict and leadership crisis. Wishing ccm a quick recovery from its current ICU status - MCHEKECHONI.
 
Jamani tusidanganye kwamba kwa kuvunja CC JK kafanya la maana la hasha, huo ni uoga wake wa kufanya maamuzi magumu. Tena ni kupoteza muda na kuzidi kujidharaulisha manake watanzania watashangaa wakijua kwamba karibu wajumbe wote wa CC watarudi kwenye hiyo anayodai mpya wakati ni viraka kama anavyotaka kufanya kwenye katiba. Huyu bwana ni kituko inamaana hajui kwamba ni wajumbe karibu 7 tu ambao anaweza kuwafukuza wengine hana uwezo nao kwa sababu katiba yao hairuhusu mf. wenyeviti wa jumuia zao zote wanarudi akiwemo Bashe watakayemchagua kuwa mwenyekiti wa UVCCM. makamu mwenyekiti wa zanzibar anaingia kwa mujibu wa sheria, wakina mzee malecela ni wajumbe wa kudumu hana uwezo wa kuwaondoa. Kwa hiyo amevunja CC kwa ajili ya kuwatoa wakina RA? si woga huo kwa nini asingewashauri wajiuzulu wangekataaa angeenda NEC kuwashtaki na kupendekeza wafukuzwe wangefukuzwa ndipo CCM wangeanza kupata masikio. Hii ya sasa imezidi kumharibia kwa kuwadhalilisha hata wale wasiokua na matatizo. Kiongozi muoga hawezi kuikoa nchi wala chama chake. Huyo ndio JK wetu lord have mercy. Sasa zanzibar wamechana mapendekezo ya muswada hadharani tena mbele ya sitta mnafiki, nimeshangaa pia kumsikia Nape akiushabikia mswada kisa kapewa u DC, nakubaliana na Mrisho Gumbo , hawa wanafikiri kwa matumbo sitta keshakua mchawi na nape yuko mbioni
 
Unaanza kupayuka wewe!, mambo ya Mungu usiyafananishe na ya Mafisadi, usipende kututafutia balaa huku. Acha ccm ife yenyeweeee! Kama unataka kufa nayo kufa mwenyewe lakini huki usimchanganye YESU, tuko makini sana kuangalia usitupotezee mwelekeo! Ala!

Mkuu umenena.....mambo ya Mungu ni yakuogopa sana.....maana tusije tukashangaa ukitaku-login JF inagoma kumbe tumekwishabeba laana.....
YA MUNGU TUMPE MUNGU KWA NGUVU ZOTE NA YA MAFISADI TUYAPINGE KWA NGUVU ZOTE...............
 
Kafa Nyerere aliyeianzisha itakuwa CCM. Na Yesu jee, tena Mungu, "kafa". Itakuwa chama.
mbona humsemi yule aliyefukiwa nusu ili baada ya ck mtangaze kafufuka kama Yesu?kabla ya cku kufika Nguruwe ikampitia na kumla,na ndio ukawa mwisho wa uhai wake.au mnafikiri hatujui kwa nn hamli KITIMOTO!
 
Sidhani kama tutahitaji makpi ya CCM waendelee huko huko kwao maswala ya kuunga mkono chama chetu cha CDM hamkatazwi sisi tupo kikazi tu sio kimaslahi ya watu wachache.

Tafadhali tunawaomba msituingize kweny mambo yenu ya kishenzi na kiutahaira yaani kwanza huyo february ana DOMO kama bakuli la maharage akaimbe mipasho sio aongelee maswala ya umeme swala hilo tunae mtu wetu makini mchapa kazi na mwadilifu mwenye akili timamu MNYIKS sio kama nyie sisi hatutaki MIPASHO
 
Back
Top Bottom