kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita nilikuletea mada iliyohusu penzi la kweli halionekani kwa macho. Bila shaka bado unatafakari ili uweze kutoa maoni yako kuhusiana na yale niliyochombeza kama mtohoaji(mchokoza mada).
Naam. Leo ngoja nikusimulie tafrani nyingine niliyonasa katika pitapita zangu. Si unajua tena mitikisiko ilivyo mingi ndani ya ndoa? Hebu sikiliza visa hivi viwili nilivyonasa kwa wakati mmoja.
Hivi majuzi nikutana na dada mmoja rafiki yangu ambaye tuliachana mwaka 1975 wakati tukiwa sekondari. Kwa kuwa ilikuwa tuko barabarani, tukakubaliana tutafute sehemu ya kupata soda ili tueleweshane vema kuhusu maisha tokeo wakati ule. Tukaketi sehemu tukaagizia soda.
Akanisimulia misukosuko yake ya maisha hadi kufikia pale alipo. Wakati, akinisimulia, jirani aliketi binti mmoja akila chipsi zake. Ghafla akavuka kiti na kuomba kujumuika nasi kwa kile alichosema alivutiwa na mazungumzo yetu kwani naye alipata msukosuko wa kindoa unaofanana na maelezo ya yule mama rafiki yangu.
Mpenzi msomaji, nikudokeze kwa kifupi kwanza kilichomsibu mama yule, halafu alichoeleza binti huyo, tatizo ambalo linalandana kabisa na la mwenzake. Tukiwa sote tunasikiliza, mama huyu rafiki yangu akasema;
Ndoa yangu ilipata misukosuko mingi sana. Lakini hatimaye tukaachana kwa talaka baada ya kuona siwezi kupambana nisije nikapoteza maisha huku naona. Namshukuru Mungu hivi sasa niko huru nalea wanangu na wajukuu.
Tuliishi na mume wangu na kubahatika kupata watoto wanne, wakiwemo mapacha. Tukajenga nyumba tatu. Mume wangu akaanza vituko wakati nikiwa na mimba ya mtoto wa mwisho. Akaanza kulala nje, kumbe alikuwa na mwanamke anataka kumuoa.
Akafungua kesi ya talaka mahakamani nami nikawa nakwenda kusikiliza huku ni mjamzito. Huku kesi iko mahakamani mume huyu akawa ametangaza ndoa kuoa mwanamke mwingine. Nilipopata tarifa nikatinga kanisani na cheti changu cha ndoa kuzuia hadi kesi ya mahakamani imalizike.
Ndoa hiyo batili ikapigwa stop.
Baada ya kuona nataabika huku mjamzito, siku ya kesi ikabidi nikubali talaka ili niepuke usumbufu. Nikapokea talaka yangu, katika mali nikapewa nyumba ambayo naishi hivi sasa hapa Dar.
Bwana yule akaendelea na mipango yake ya harusi na kumuoa aliyekuwa anamzuzua. Ni miaka kibao hadi leo hii hakabatika kupata mtoto. Na bwana huyo inaonekana anajuta kwani amekazana sana kuwasiliana nami akisingizia kuwaona wanawe. Mimi ndiyo wala sina habari naye.
Na dada yake ambaye alinichukia sana tena pale nilipozaa mapacha, naye alipoolewa akafululiza mapacha wawili mara tatu(jumla watoto sita). Ilifikia hatua akaja kuniomba msamaha kwa kauli zake mbovu na zilizojaa kejeli.
Naam mpenzi msomaji, hicho ndicho kisa cha mama yule rafiki yangu. Sasa huyu binti naye alikuwa na machungu yake ambapo bwana aliyezaa naye watoto wawili, amemtosa na kwenda kufunga ndoa na mwanamke mwingine.
Nilimwambia tufunge ndoa akaniambia nisiwe na haraka. Lakini nikashangaa ametangaza ndoa na mwanamke mwingine na kuniacha solemba. Chumba nilichokuwa nimepanga nikaachia na kwenda kuishi kwa mamangu.
Kazi niliyokuwa nafanya nikapunguzwa hivyo nikaanza kusaka kibarua. Bahati nzuri hivi karibuni nimpata kazi kwenye hospitali moja sehemu ya mapokezi. Namshukuru Mungu kwani hivi sasa nimetulizana kimawazo.
Kinachonishangaza ni kwamba inaonekana anajutia uamuzi wake wa kuoa kwani amekuwa na harakati za kunitafuta na kutaka tuzungumze jambo ambalo sijampa nafasi kwa jinsi alivyoniumiza pale alipoacha kunioa akamtafuta mwanamke mwingine. Sitaki hata kumsikia na ndio maana dada hapa alipokuwa anasimulia kisa chake nikakifananisha na hicho cha kwangu, anamaliza kusema binti huyu.
Mpenzi msomaji, bila shaka umewasikia kinamama hawa ambao waume zao wamewazalisha watoto kisha kuwatosa na kwenda kufunga ndoa na wanawake wengine. Lakini huko walikoegemea hawana raha wana kila dalili ya kujutia. Upo hapo? Ama kwa hakika Maisha Ndivyo Yalivyo.
Mpenzi msomaji wangu, baada ya kuwasikiliza kwa makini kinamama hawa, lipo swali moja nilijiuliza kwamba ni kwanini mwanaume azae na mwanamke na kuishi nae kama mkewe halafu ghafla anambadilikia na kuanzisha zogo la kumuacha kisha kwenda kuoa mwanamke mwingine tena kwa ndoa?
Swali hili limenipa mawazo mengi. Kwa kifupi niseme tu kwamba inawezekana baada ya mume kumpima kwa muda mkewe huyo amegundua mapungufu yake na hivyo akaona hamhitaji tena anataka chungu kipya. Zipo sababu kibao zilizojificha ambazo wanazijua wanadoa wenyewe, udhaifu wao. Mwingine ni tamaa tu za mwili na macho kodo asiyetaka kinachopita mbele ya macho yake kimpite bila kuteta nacho. Si unajua tena utaona kizuri leo na kesho ukipita utaona kizuri zaidi ya kile cha jana? Hivyo ndivyo zilivyo tamaa za mwili wa binadamu, hautosheki.
Wakati mwingine mwanaume anamuacha huyu na kumuoa yule japo wameishi naye kutokana na tabia ya huyo anayeachwa. Pengine ni mzururaji, hasemi ukweli, mvivu na kadhalika.
Mwingine huchukua hatua ile kutokana na ukorofi wa dada zake(mawifi). Mawifi wengine ndio wanaobomoa ndoa za kaka zao. Kama mke wa kaka yao hataki msongamano nyumbani kwake, au hakubaliani na kila jambo walitakalo mawifi au wakwe, lazima mama huyu atatikiswa tu.
Na mara nyingi imetokea wanaume kuwasikiliza zaidi dada zao kuliko wake zao. Matokeo yake ndio kama hayo jamaa hufikia hatua na ama kumtimua mkewe au kufutilia mbali mipango mizuri ikiwemo kufunga ndoa au kudiriki hata kutoa talaka kutokana na maneno ya fitina.
Kwa leo msomaji wangu naishia hapa na kama unacho kisa nitumie tujadili kwa pamoja kupitia e-mail hapa chini.
Barua pepe: fwingia@yahoo.com
Naam. Leo ngoja nikusimulie tafrani nyingine niliyonasa katika pitapita zangu. Si unajua tena mitikisiko ilivyo mingi ndani ya ndoa? Hebu sikiliza visa hivi viwili nilivyonasa kwa wakati mmoja.
Hivi majuzi nikutana na dada mmoja rafiki yangu ambaye tuliachana mwaka 1975 wakati tukiwa sekondari. Kwa kuwa ilikuwa tuko barabarani, tukakubaliana tutafute sehemu ya kupata soda ili tueleweshane vema kuhusu maisha tokeo wakati ule. Tukaketi sehemu tukaagizia soda.
Akanisimulia misukosuko yake ya maisha hadi kufikia pale alipo. Wakati, akinisimulia, jirani aliketi binti mmoja akila chipsi zake. Ghafla akavuka kiti na kuomba kujumuika nasi kwa kile alichosema alivutiwa na mazungumzo yetu kwani naye alipata msukosuko wa kindoa unaofanana na maelezo ya yule mama rafiki yangu.
Mpenzi msomaji, nikudokeze kwa kifupi kwanza kilichomsibu mama yule, halafu alichoeleza binti huyo, tatizo ambalo linalandana kabisa na la mwenzake. Tukiwa sote tunasikiliza, mama huyu rafiki yangu akasema;
Ndoa yangu ilipata misukosuko mingi sana. Lakini hatimaye tukaachana kwa talaka baada ya kuona siwezi kupambana nisije nikapoteza maisha huku naona. Namshukuru Mungu hivi sasa niko huru nalea wanangu na wajukuu.
Tuliishi na mume wangu na kubahatika kupata watoto wanne, wakiwemo mapacha. Tukajenga nyumba tatu. Mume wangu akaanza vituko wakati nikiwa na mimba ya mtoto wa mwisho. Akaanza kulala nje, kumbe alikuwa na mwanamke anataka kumuoa.
Akafungua kesi ya talaka mahakamani nami nikawa nakwenda kusikiliza huku ni mjamzito. Huku kesi iko mahakamani mume huyu akawa ametangaza ndoa kuoa mwanamke mwingine. Nilipopata tarifa nikatinga kanisani na cheti changu cha ndoa kuzuia hadi kesi ya mahakamani imalizike.
Ndoa hiyo batili ikapigwa stop.
Baada ya kuona nataabika huku mjamzito, siku ya kesi ikabidi nikubali talaka ili niepuke usumbufu. Nikapokea talaka yangu, katika mali nikapewa nyumba ambayo naishi hivi sasa hapa Dar.
Bwana yule akaendelea na mipango yake ya harusi na kumuoa aliyekuwa anamzuzua. Ni miaka kibao hadi leo hii hakabatika kupata mtoto. Na bwana huyo inaonekana anajuta kwani amekazana sana kuwasiliana nami akisingizia kuwaona wanawe. Mimi ndiyo wala sina habari naye.
Na dada yake ambaye alinichukia sana tena pale nilipozaa mapacha, naye alipoolewa akafululiza mapacha wawili mara tatu(jumla watoto sita). Ilifikia hatua akaja kuniomba msamaha kwa kauli zake mbovu na zilizojaa kejeli.
Naam mpenzi msomaji, hicho ndicho kisa cha mama yule rafiki yangu. Sasa huyu binti naye alikuwa na machungu yake ambapo bwana aliyezaa naye watoto wawili, amemtosa na kwenda kufunga ndoa na mwanamke mwingine.
Nilimwambia tufunge ndoa akaniambia nisiwe na haraka. Lakini nikashangaa ametangaza ndoa na mwanamke mwingine na kuniacha solemba. Chumba nilichokuwa nimepanga nikaachia na kwenda kuishi kwa mamangu.
Kazi niliyokuwa nafanya nikapunguzwa hivyo nikaanza kusaka kibarua. Bahati nzuri hivi karibuni nimpata kazi kwenye hospitali moja sehemu ya mapokezi. Namshukuru Mungu kwani hivi sasa nimetulizana kimawazo.
Kinachonishangaza ni kwamba inaonekana anajutia uamuzi wake wa kuoa kwani amekuwa na harakati za kunitafuta na kutaka tuzungumze jambo ambalo sijampa nafasi kwa jinsi alivyoniumiza pale alipoacha kunioa akamtafuta mwanamke mwingine. Sitaki hata kumsikia na ndio maana dada hapa alipokuwa anasimulia kisa chake nikakifananisha na hicho cha kwangu, anamaliza kusema binti huyu.
Mpenzi msomaji, bila shaka umewasikia kinamama hawa ambao waume zao wamewazalisha watoto kisha kuwatosa na kwenda kufunga ndoa na wanawake wengine. Lakini huko walikoegemea hawana raha wana kila dalili ya kujutia. Upo hapo? Ama kwa hakika Maisha Ndivyo Yalivyo.
Mpenzi msomaji wangu, baada ya kuwasikiliza kwa makini kinamama hawa, lipo swali moja nilijiuliza kwamba ni kwanini mwanaume azae na mwanamke na kuishi nae kama mkewe halafu ghafla anambadilikia na kuanzisha zogo la kumuacha kisha kwenda kuoa mwanamke mwingine tena kwa ndoa?
Swali hili limenipa mawazo mengi. Kwa kifupi niseme tu kwamba inawezekana baada ya mume kumpima kwa muda mkewe huyo amegundua mapungufu yake na hivyo akaona hamhitaji tena anataka chungu kipya. Zipo sababu kibao zilizojificha ambazo wanazijua wanadoa wenyewe, udhaifu wao. Mwingine ni tamaa tu za mwili na macho kodo asiyetaka kinachopita mbele ya macho yake kimpite bila kuteta nacho. Si unajua tena utaona kizuri leo na kesho ukipita utaona kizuri zaidi ya kile cha jana? Hivyo ndivyo zilivyo tamaa za mwili wa binadamu, hautosheki.
Wakati mwingine mwanaume anamuacha huyu na kumuoa yule japo wameishi naye kutokana na tabia ya huyo anayeachwa. Pengine ni mzururaji, hasemi ukweli, mvivu na kadhalika.
Mwingine huchukua hatua ile kutokana na ukorofi wa dada zake(mawifi). Mawifi wengine ndio wanaobomoa ndoa za kaka zao. Kama mke wa kaka yao hataki msongamano nyumbani kwake, au hakubaliani na kila jambo walitakalo mawifi au wakwe, lazima mama huyu atatikiswa tu.
Na mara nyingi imetokea wanaume kuwasikiliza zaidi dada zao kuliko wake zao. Matokeo yake ndio kama hayo jamaa hufikia hatua na ama kumtimua mkewe au kufutilia mbali mipango mizuri ikiwemo kufunga ndoa au kudiriki hata kutoa talaka kutokana na maneno ya fitina.
Kwa leo msomaji wangu naishia hapa na kama unacho kisa nitumie tujadili kwa pamoja kupitia e-mail hapa chini.
Barua pepe: fwingia@yahoo.com