Mitazamo na tathmini ya Uchaguzi 2015

CONFLICT OF INTEREST (COI) YAANI MGONGANO WA MASILAHI

Mgongano wa masilahi ni mwingiliano wa masilahi ya mtu/taasisi/shirika yawezayo kukwaza utashi au matakwa katika kutekeleza majukumu

Tumeona jinsi mgongano wa masilahi ulivyoleta kizaa zaa bungeni. Matatizo yanajengwa na mgongano wa masilahi (COI)

Kwa mfano huo, bunge la 11 limeanza vibaya sana, hata kupelekea Spika/Serikali kujichanganya

MASHIRIKA YACHANGIA HAFLA YA BUNGE

Hafla ya bunge imetokana na michango nje ya pesa za bunge au serikali. Pengine ni ya makampuni, mashirika n.k.

Hilo lilisemwa kwa kuzingatia ukweli kuwa milioni takribani 250 ni nyingi kutoka bajeti ya umma
Yangekuwepo malalamiko juu ya matumizi mabaya ya fedha za umma

Rais aliamua sehemu kubwa ipelekwe hospitali ya Muhimbili kununua vitanda

Mchana kabla, Rais lihutubia bunge na kutilia mkazo suala la kupambana na rushwa
Alisema kazi hiyo ni ngumu kwasababu ina watu wazito na kuliomba taifa limuombee afanikiwe

SIKU ZA NYUMA

Wabunge kadhaa walituhumiwa kwa kuwa na mgongano wa masilahi.
Wengine wakisemwa kuchukua posho kutoka serikali na kule kwenye mashirika wanakofanya kazi zinazohusu bunge

Iliwahi kupendekezwa wabunge wasiwe wajumbe wa bodi za taasisi au mashirika ili kukwepa mgongano wa masilahi

INASHANGAZA

Kuwa bunge linalosubiri miswada mbali mbali ya kupambana na rushwa, limeingia katika mgongano wa masilahi
Inawezejanaje chombo cha umma kinachotunga sheria na kusimamia serikali kupokea pesa za nje?

Bunge litawezaje kuwa huru ikiwa tayari linapokea 'misaada' nje ya utaratibu unaolizewesha kuwa huru bila (COI)?
Lakini pia pesa hizo hazikupaswa kuelekezwa katika matumizi ya umma.

Haina maana kuwa pesa hizo ni haramu, la hasha! bali zinaleta mgongano wa masilahi

Tumeona matatizo yaliyopo yanayotokana na migongano ya masilahi, je tunahitaji somo zaidi?

Haya yanatokea kwasababu hakuna umakini katika kusimamia sheria, kanuni, maadili na taratibu zetu

Tunaweza kuishi kwa kupinda pinda tu mambo, bora liende

Tusipobadilika, hatutafanikiwa. Tunaona matatizo hatujifunzi, tunarudia mako

Tusemezane
 
SUALA LA ZNZ

NINI HASA KINACHOJADILIWA NYUMA YA PAZIA?

Yamekuwepo majadiliano nyuma ya pazia kumaliza mgogoro visiwani
Utata wa majadiliano hayo ni matokeo ya hatma ya chaguzi siku za baadaye na hatma ya ZNZ kwa sasa

Uchaguzi ni maamuzi ya wananchi kuhusu kundi gani au akina nani wapewe uongozi wa taifa
Tataratibu zetu tulizojiwekea ni mshindi kwa kura nyingi. Zipo nchi ambazo mshindi hupatikana kwa 2/3

Kwamba, uchaguzi wa marudio hufanywa kuondoa vyama vyenye ushindi kidogo kuwezesha mshindi kwa 2/3
Utaratibu wetu ulibadilika wakati fulani na mshindi kupewa yote 'winner takes it all'

Wakati majadiliano yakiendelea, tunasikia miongoni mwa waliopo mezani wakitangaza uchaguzi kurudiwa
Hoja kubwa imehama kutoka sababu za kurudia uchaguzi na kama zipo sheria kurudia uchaguzi

Tuangalie nadharia mbili kuu. Kwanza, upande mmoja unataka matokeo yote yatangazwe na mshindi atangazwe
Upande mwingine unataka uchaguzi urudiwe bila sababu za ''kisheria'' na mantiki

Nadharia ya uchaguzi kurudiwa inahojiwa na wengi kama upo uwezekano huo
Uwezakano upo, hata kama upande mmoja utasusia. Mfano, CUF wakisusia haliondoi ukweli uchaguzi unaweza kurudiwa

Sababu zinazoweza kufanikisha hilo ni ukweli kuwa uchaguzi ni wa vyama vingi. Visiwani vipo vyama vingi.

Uchaguzi ukiitishwa upo uwezekano wa vyama vingine kuingia katika kinyang'anyiro
Matokeo ya uchaguzi huo yatakuwa halali kwa maana ya uchaguzi na mshindi atatangazwa

Nadharia ya kwanza, kama upande mwingine utaendelea na hoja ya matokeo kutangazwa kama yalivyo na upande wa pili kugomea , hatma ya nchi kwa ujumla itakuwa na walakini mkubwa

Mkwamo wa suluhu ya ZNZ una atahari za kiuchumi kwa nchi hiyo. Athari hizo zinaweza kusambaa hadi Tanzania bara

Tanzania bara itabidi ichukue jukumu la kuhudumia wananchi wa ZNZ wakati wote wa mkwamo kiuchumi

Ndio maana tunauliza, hili suala hatma yake ipoje na nini mustakabali wa chaguzi zetu siku za usoni?
Wapi maamuzi ya wananchi, wapi sheria na taratibu zetu zinazotuongoza katika kujitawala?

Tusemezane
 
SUALA LA ZNZ LINAIGUSA JMT KWA KIASI KIKUBWA

LINAWEZA KUWEKA AU KUBOMOA MISINGI WA MUUNGANO

Tumesoma maoni sehemu mbali mbali kuhusu ZNZ. Baadhi ya wananchi wanaamini hilo ni tatizo la ZNZ pekee

Tukiwa nchi zilizoungana, tatizo hilo linagusa JMT kijamii, kisiasa na kiuchumi

Kijamii ni pale ambapo jamii za pande mbili zinapojikuta zikiwa katikati ya mgogoro kwa namna tofauti
Jamii zinazoishi sehemu zote na hapa tuseme maingiliano ya kijamii na hasa kwa upande wa WZNZ waishio bara

Kiuchumi ni kwa jinsi nchi zinavyounganishwa kijiografia. Huduma za kijamii, kibiashara n.k. zimeathirika
Kupungua kwa watalii kumeathiri uchumi wa ZNZ unaotegemea huduma.

Usafirishaji wa mizigo na bidhaa nao umeathirika. Hivyo, matatizo ya ZNZ yatabebwa na Tanganyika kwani ndivyo ilivyo

Kisiasa kuna tatizo kubwa. Kabla,kulikuwa na hoja za namna ya muungano ulivyo.
Kuvunjika kwa BMLK ni kielelezo cha ukubwa wa tatizo.

Lakini kwa haraka haraka tunaweza kuona mambo yanayoweza kuimarisha au kubomoa misingi ya muungano

Kwa mfano, Rais wa JMT anatarajiwa kutangaza baraza la mwaziri.

Katika mambo ya muungano, viongozi huchaguliwa kutoka pande zote. Hilo limekuwa lalamiko kubwa kwa upande wa ZNZ

Katiba inasema mwaziri watatokana na wabunge wa kuchaguliwa.
Wabunge wa kuchaguliwa kutoka ZNZ wapo na miongoni mwao watateuliwa kuwa mwaziri au manaibu katika JMT

Haieleweki katika mkwamo uliopo nini kitatokea. Yapo mawili yanayoweza kujitokeza

Kwanza, Rais akiteua mawaziri miongoni kutoka ZNZ, maana yake watapaikana kwasababu wametokana na uchaguzi uliosimamiwa na NEC. Hata hivyo kuna tatizo.

Kama ZEC ina dai ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi, na kama WZNZ waliopiga kura 5 ndio hao waliochagua wabunge, uhalali wa wabunge hao unakuwaje?

Hoja hapa ni kuwa wabunge kutoka ZNZ wanawezaje kupatikana wakiwa 'safi' ikiwa kulikuwa na ukiukwaji wa uchaguzi katika kundi lile lile lililochagua Wawakilishi , Rais wa ZNZ na madiwani na Rais wa JMT?

Pili, endapi Rais ataweka kiporo uteuzi wa WZNZ katika baraza la mawaziri, je sura ya muungano inakuwaje?
Na je yale madai kuwa JMT ni Tanganyika yenyewe hayatapa nguvu siku za baadaye?

Yapo mengi yanayotatiza , kwa uchache pengine na ububusa wa kuelewa tuangalie machache kidogo kidogo

Tusemazane
 
SIASA NI ELIMU YA SANAA NA SAYANSI
TUNAWELEWA WANASIASA JUU JUU
WANATUJUA, WANATUMIA MAKOSA YETU VEMA KULIKO YAO

Katika nchi masikini kama zetu siasa ni kazi ya kupandia ngazi au kujaza matumbo.

Tunawaona wanasiasa kama wabiga kelele na wabwabwaji.

Kwasababu hatuwafahamu, nao , wanatufahamu vema siku zote hutumia makossa yetu kwa faida zao


Wanasiasa wanajua kubadili ukweli kuwa uongo na kinyume chake.

Alieyjuwa Waziri mkuu wa Uingereza maarufu Winston Churchill aliulizwa mwanasiasa ni nani?

Churchill alijibu (sio tafasiri rasmi) '' Ni mtu anayekwambia kitakachotokea leo, kesho, wiki au mwaka ujao na wakati utakapofika ataweza kukuambia kwanini hakikutokea''

Wanasiasa ni watu makini, wenye subiria na mikakati mizito hata kama inaonekana ya kipuuzi

Ni watu wanaojua kutumia muda na matukio wakaweza kufanya kwa wakati ‘timing'

Kwa mfano, wakati wa mchakato wa katiba mpya, baadhi ya wanasiasa walisema hawakubaliani na mchakato. Walikuwa na subira, wakati ulipofika wakafanya timing.

Kwanza, kuwaondoa wajumbe wa tume ya Warioba wasishiriki BMLK, halafu kumchagua Spika atakayesimamia masilahi na mwisho kufinyanga kanuni ili ziwape nafasi za kufanya yao

Baada ya kufanikiwa na kisha kushindwa, wakabadili hoja. Kwamba, kuvunjika kwa bunge ni kwasababu UKAWA wanataka Serikali 3. Ikavuma masikioni na watu kusahau kuwa hoja ya UKAWA ilikuwa kufuata maoni ya tume kama yalivyotolewa.

Hadi leo wanasema bunge liliharibika kwasababu UKAWA wanataka serikali 3

Wanageuza uongo hadi unakuwa ukweli

Ndivyo ilivyo sasa hivi. Wanasiasa wana subira kuhusu suala la ZNZ.

Hawana ''haraka'' kwasababu hulka yao ni ‘subira' timing na utendaji (execution)
Tayari wamefanikiwa kugeuza ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli.

Hoja inayotawala ni kama uchaguzi utarudiwa na lini. Hoja ya kwanini uchaguzi urudiwe , kwa misingi gani, sheria gani, utaratibu gani unaochagua kura za JMT na SMZ kwa wapiga kura wale wale imekufa

Wanachosubiri kutumbia yal Churchill, wanakuja kutueleza kwanini uchaguzi ni halali ukawa haramu halafu halali

Tusemezane
 
''MWAFAKA UNATAFUTWA''

KURA ZA WANANCHI PEMBENI, SASA NI VIKAO VYA MUAFAKA


Kumekuwepo na kauli kutoka pande zote kuwa muafaka unatafutwa.
CUF wakisema hoja yao ipo pale pale, CCM wakisisitiza kuna muafaka unatafutwa na majadiliano yanaendelea

Hapa kuna kitu cha kusikitisha sana. Kura za Wazanzibar ni malaki. Uchaguzi uliitishwa ili kupata uongozi
Hivi kuna muafaka gani katika kura za wananchi? Si muafaka ni kuhesabu kura na kutangaza matokeo au vinginevyo

Kinachoonekana, vikundi vya watu vinakaa mezani kuamua 'muafaka' wa kura za wananchi
Si kuwa kura za wananchi zinatoa muafaka kwa vikundi! bali kinyume chake

Hili linajenga hisia mbaya kuhusu demokrasia ya nchi yetu.
Si kuwa linaharibu taswira bali linatuondolea ile heshima tuliyokuwa nayo (moral authority) ya kusaidia wenzetu

Ni jambo linalotia shaka sana kuhusu upigaji wa kura siku za baadaye

Wananchi wengi watakata tamaa wakijua kura zao haziheshimiwi bali muafaka wa viongozi

Hao viongozi wanaokaa kutafuta muafaka, lini waliuliza wananchi kuhusu hilo?

Watarudi lini kueleza kuhusu kura za wananchi zilizowekwa pembeni kupisha muafaka!

Sheria zipo, ni kipi kigumu kuzitumia katika kutafuta ukweli?

Chelewa chelewa inayoendelea inaweza kuchukuliwa kama kununua muda
Ukweli upo na unachotakiwa ni kuwekwa wazi.

Kura zipo, hakuna msimamizi wa jimbo aliyelalamika na wamesaini matokeo.

Leo ZEC ndio wanaolalamika na si wasimimizi wa chaguzi katika majimbo na vituo.

Ni NEC hao hao wanaotaka uchaguzi ufutwe tena kwa kutumia kauli ya mtu mmoja

Tujiulize, hivi sheria za nchi zimewekewa akina nani?

Endapo hatuheshimu sheria zetu wenyewe nani aje kutusaidia kwa hilo?

Je tunataka commonwealth warudi tena kuweka viongozi mezani!

Hii ni aibu, na miaka 50 ya uhuru, lazima tujiulize kama kweli tupo njia sahihi

Tusemezane
 

HOJA ZA UCHAGUZI ZNZ ZIMEANZAKUPOTEZWA
SASA NI ENDAPO UCHAGUZI UTARUDIWA AU LA!
Mtakumbuka mabandiko yaliyopita kuhusu uongo unavyogeuzwa kuwa ukweli na ukwelii kuwauongo. Hayo ndiyo yanayotokea sasa
Wiki hii kuna mvutano kati ya CUF na CCM iliyohusu kauli za kurudia uchaguzi. CCM wanasema hayondiyo makubaliano , CUF wakisema hakuna kitu kama hicho.
Kwa hisani ya IPP media http://www.ippmedia.com/?l=86548
Ukiisoma taarifa hiyo kwa umakini , makamu wa pili wa Rais wa ZNZ anakanusha kutoakauli ya kurudia uchaguzi , kwakauli kuwa CCM ?ZNZ wamekubali uchaguzi urudiwe kama ilivyoamukiwa na TUME yauchaguzi ZNZ (ZEC)
Mwisho wa habari hiyo, gazetilimeandika hivi ?? Chimbuko la mazungumzo hayo ni mgombea wa urais kwa tiketi yaCuf, Maalim Seif Sharif Hamad kupinga uamuzi wa Tume wa kufuta matokeo yauchaguzi mkuu kwa madai ulikuwa huru na wa haki na yeye ndiyo mshindi wauchaguzi huo??
TUZIANGALIE KAULI HIZOMBILI KWA UNDANI
Kwanza, Makamu wa Rais wa ZNZ haijulikani aliongeakwa nafasi gani katika CCM
Je aliwakilisha kamati inayohudhiria mazungumzo? Je aliongea kama kiongozi wa chama ? Nakwanini kauli isitolewe na CCM makao makuu?
Pili, Makamu wa pili wa Rais anazungumzia kurudiwa uchaguzi. Kwanini haelezi uchaguzi unarudiwa kwa malalamiko ya nani. CCM haikuwahi kulalamika katika majimbo na ilitia saini. Mlalamikaji wa suala hili ni ZEC. Iweje CCM iwe mlalamikaji sasa na kupora kauli ya ZEC!
Tatu, Makamu wa Rais anasemauchaguzi urudiwe kama ilivyoagiza ZEC nakutangazwa na gazeti la serikali. ZEC haikuwahi kutangaza kurudiwa uchaguzi. Aliyetangaza ni mwenyekiti wa ZEC akiwamwenyewe. Leo kwanini ZEC iwe mtu mmojana si kamisheni ya Wajumbe. Makamuaeleze ZEC ipi iliyotangaza marudio
Nne, gazeti limeandika chimbuko la tatizo nimgombea wa CUF kupinga maamuzi ya tume (mwandishi akimaanisha ya kurudiauchaguzi)
Ukifuatilia kwa umakini suala zima limeshahamishwa kutoka chanzo chake na limefikia hatua nyingine ya endapo uchaguzi urudiwe au la!
Inaendelea


 
HOJA YA KURUDIA UCHAGUZI


KWANINI CCM WANATAKA MARUDIO

Tumeona hapo juu ,hoja kubwa iliyoko mezani ni kurudiwa uchaguzi.

Hakuna anayeeleza kwa kina na mantiki kwanini uchaguzi urudiwe. CCM wamekazania uchaguzi urudiwe

Msuluhishi aliyetumwa naye amekaririwa akisema uchaguzi urudiwe.


Aliyekuwa Rais waMuungano hakutoa msimamo kama Rais au mwenyekiti.

Kurudiwa kwa uchaguzi bila sababu za kwanini urudiwe zimelenga katika mambo kadhaa

Kwanza, uchaguzi wabara umekwisha na mshindi katangazwa iwe kwa mtazamo wa aina yoyote, halali augoli la mkono.

Kilichopo ni ukweli kuwa ametangazwa Rais


Kumalizika uchaguzi bara uliokuwa na hali mbaya kwa CCM, kunatoa nafasi kwa kwendakushughulikia mambo ya Zanzibar.

Pengine mambo yasingalikuwa yalivyo kama uchaguzi-Bara ungekuwa ‘laini' kama ulivyozoeleka

Kurudiwa kutamaanisha, nguvu zote za CCM za kichama au nyingine zitatumika katika kuhakikisha ushindi.

Endapo CCM imeweza kushawisha ‘Tume' kufuta uchaguzi bila sababu , nini kitashindikana?


Pili, wafuasi wa CUF wanaamini kwa dhati kabisa walifanyakila liwezekanalo kuziba mianya

Kurudia uchaguzi kutwakatisha tamaa na political base itasambaratika.


Kutaondoa Imani ya wananchi kuhusu umuhimu wa kura zao na kutopiga kura

CCM wana advantage na kila sababu za kidemokrasia, kidola aukichama kushinda marudio hata kama yatasimamiwa na viumbe kutoka sayari nyingine

Mgogoro umalizwe kwa njia za sheria ili Taifa lisongembele.

Viongozi wenye dhamana wakubali kuwa dhamana zao zinatoka kwa wananchi na si wao kudhamini wananchi


Tatizo la ZNZ linagusa bara kama tunavyosema mara nyingi sana.

Kuchelewa kutangazwa kwa baraza la mawaziri kunaweza kuwa na sababu za mgogoro wa ZNZ


Kikao cha wakuu wa EAC kilichokuwa kifanyike Nov 30 siku yaEAC kimeahirishwa kwasababu Tanzania imeomba hivyo kwavile bado haijakamilisha safu ya serikali

Yote hayo yaliangaliwa kwa mtazamo mpana yanaishia au kuanzia visiwani

Tusemezane
 
MSIBA WAUKAWA ?GEITA

TUKIO LAKUSHANGAZA NA KUSIKITISHA

Tunaendelea na tathmini kutoka kila kona tuki donoa donoa matukio yanayoambatana na uchaguzi.
Tukio kubwa wiki hii ni kifo cha mwanachama wa CDM au UKAWA, aliyeuawa katika mazingira tatanishi sana


Kifo chake kinazua utata pale mazishi yake yalipogeuka kuwa suala la dola dhidi ya vyamavya siasa.
Ni tukio linaloeleza hali ya kisiasa ilivyokuwa nailivyo katika taifa


Taarfa zilizopo Mawazo(RI) kauawa katika mikutano na wanaosaidikiwa wa chama kimoja cha siasa nchini.

Tatizo lilizuka palipotokea mtafaruku kati ya waombolezaji waliosafirisha mwili wa marehemu hadi Bugando Hospitali.
Ina taarifiwa mlinzi wa usalama kujeruhiwa na baadhi ya watukuwekwa mahabusu


Mazishi ya Mawazo yalizongwa na sintofahamu zinazotia shaka.

Polisi walizuia mikusanyiko yote kwasababu mbali mbali.

Kwanza, kama walivyonukuliwa viongozi wa UKAWA mazishini, polisi walizuia kwasababu mbili.
Kwamba, Marehemu mawazo alikuwa wa Geita na heshima zifanyike huko.

Pili , kulikuwa na kipindu pindu na mikusanyiko haikuruhusiwa


Mahakama iliamua shughuli za kutoa heshima ziendelee Mwanza kama ilivyoombwa na viongozi wa UKAWA

Hapa kuna maswali ya kujiuliza

Mosi,kwanini Polisi walitumia nguvu kukabiliana na waombokezaji badala ya kutumia nguvu hizo kuwafikisha wahusika mbele ya sheria?

Pili, kuna sheria gani ya nchi inayokataza watu kutoa heshima zao katika eneo Fulani?

Mbona leo watu wanatoa heshima Dar es Slaamu ili hali marehemu ni wa mikoani?

Marehemu Regia Mtema(RIP) alikuwa mkazi wa Dar?

Marehemu Sumari alikuwa mkazi wa Dar? Orodhani ndefu .

Tunaweza kusema hakuna sheria ya namna hiyo


Tatu,lini jeshi la Polisi limekuwa wasimamizi wa afya nchini?

Tangazo la magonjwa hutolewa na taasisi husika na jeshi husimamia tu utekelezaji.

Kilichotokea Mwanzani jeshi ''kujivika joho' la kusimamia sekta ya afya nchini


Kitendo cha jeshi la Polisi kubwagwa Mahakamani, na kitendo chaUKAWA kutoa heshima zao pasi na fujo au vurugu, kimeliabisha jeshi la Polisi.

Wao wakiwa wasimamizi wa sheria hawakupaswa kushindwa mahakamani, hawakupaswa kuingia katika malumbano yanayoelekea kuwa ya kisiasa na hawakupaswa kukataza Raai kutumia haki zao za kikatiba kukusanyika tena katika tendo la kibinadamu


Hili jambo limeacha ukakasi mkubwa na kuondoa shaka iliyokuwa inasemwa kuhusu jeshi la Polisi kutumiwa aukutumika nje ya taratibu zake kama mahakama ilivyoonyesha kwa suala la mawazo

Wakati taifalikiwa katika mgawanyiko kamatulioushuhudia bungeni na kwingineko,jeshi la Polisi linapaswa kuwa kiungo kizuri na si sehemu ya tatizo.

Yaliyokea Mwanza yanaeleza hali ilivyokuwa wakati wa uchaguzi na pengine ilivyo sasa nchini


Inatia shaka kuwa, marufuku ya kuzuia mikutano ya kisiasa nchini yana namna nyuma yake.

Pengine ni wakati wa kujiangalia kama taifa, haya yanatusaidia kujenga umoja au yanazidi kutuvuruga tukiwa tayari tumegawanyika kiasi hiki?


Tusemezane
 
Nguruvi3,

Sasa hivi tutaona vituko vingi vya ukosefu wa Busara kutoka kwa watendaji wengi sana wa Serikali. Hii ni kwa makusudi ili kuchochea na kuamsha fujo na kudhoofisha amani.

Hapakuwa na busara yeyote ya RC na RPC Mwanza.

Na doa hili linatupiwa Serikali kwa makusudi ya watu wachache ambao hawataki kukubali kuwa Upinzani umekuwa Tanzania na hata dhamana ya kuongoza nchi inategemeana muafaka na kuheshimiana na si ubabe wa chama tawala.
 
Nguruvi3,

Sasa hivi tutaona vituko vingi vya ukosefu wa Busara kutoka kwa watendaji wengi sana wa Serikali. Hii ni kwa makusudi ili kuchochea na kuamsha fujo na kudhoofisha amani.

Hapakuwa na busara yeyote ya RC na RPC Mwanza.

Na doa hili linatupiwa Serikali kwa makusudi ya watu wachache ambao hawataki kukubali kuwa Upinzani umekuwa Tanzania na hata dhamana ya kuongoza nchi inategemeana muafaka na kuheshimiana na si ubabe wa chama tawala.
Hapa kuna mjadala kidogo.

Tumesema mara nyingi sana kuwa Taifa limegawanyika na kuna hali isiyo ya kawaida miongoni mwetu.

Yote yanaanzia katika kampeni hadi uchaguzi.

Ganzi kubwa zaidi ni jinsi tume ilivyoendesha uchaguzi na jinsi mshindi alivyopataikana. Zile hisia kuwa hakuna haki zikazidi kupaliliwa

Haina maana nani kashinda nani kashindwa, hata hivyo watu wakiwemo walioshinda waliona tatizo latika zoezi zima
Kwa ujumla uchaguzi uliofanyika kwa wengine tuliona tatizo na wala si kitu kigeni

Ikafuata marufuku ya mikutano, pengine wahusika wakijua namna hali ilivyo.

Kumalizika kwa uchaguzi si kumalizika kwa siasa,kufuta mikutano inajenga hisia lipo lisilotakiwa kuzungumzwa

Ikifauta kifo cha mwanasiasa kwa kupigwa kule Geita. Mlolongo uliofuata unasikitisha. Ni kama hakukuwa na tukio

Mazishi yakaleta mzozo, polisi wakizuia watu kufanya mazishi kwasababu eti mtu alifia Geita hairuhusiwi kuomboleza Mwanza. Na kwamba, kuna kipindu pindu, Polisi walichukua majukumu ya wizara na idara nyingine

Mahakamani wakshindwa, mazishi yakafanyika bila tatizo, ikieleza zaidi juu ya marufuku ya mikutano iliyotolewa mwanzoni

Tukasikia DC akiweka watu rumande kwa kuchelewa eneo la mikutano. Wahusika hawakufikishwa mahakamani.

Hiyo ilikuwa ukiukwaji wa haki za binadamu na matumizi mabaya ya madaraka. Wahusika serikalini wamekaa kimya

Tukasikia kuna maeneo likizo zimefutwa bila dharura bali utashi wa watu na nguvu za kimadaraka. Hakuna anayeona tatizo

Haya yote ukichanganya na 'makovu' ya uchaguzi, tatizo linaonekana

Hatuwezi kufanikiwa kama taifa kama hatupo pamoja na wamoja.

Kuna maisha baada ya uchaguzi, lakini uchaguzi usitugawe kiasi kinachoonekana.

Uongozi uliopo unatakiwa kuwa na maridhiano ya kitaifa kujenga umoja kwanza kama Taifa tulilozoea
 
NINI KIMEBADILIKAKABLA NA BAADA YA ``UCHAGUZI``

Turudie kusisitiza maoni yetu , uchaguzi hauwezi kufanyiwa tathmini kwakuangalia matokeo.

Tulisema muundo wa tume ya uchaguzi na tuliyo yaona,tathmini yoyote kuhusu mataokeo itakuwa ubabaishaji na siuhalisia.

Tuna hoji, uchaguzi ulikuwa huru na haki, Je, ulikuwa na credibility na integrity inayoweza kufanyiwa tathmini


Hata hivyo, yapo yaliyojitokeza na kubadilisha hali ya kisiasa siku zaleo na usoni. Hayo tunaweza kuayazungumza

Kwanza, tumeona ule mwiko wa viongozi kuhama ukivunjwa.
Mawaziri wakuu wa, mawaziri, mawaziri wastaafu nawatu wenye heshima katika chama tawala kuhama.


Matukio hayo yamefungungua ukurusa mpya wa siasa za nchi yetu. Kwamba, upinzani si uhalifu kama wananchi walivyoaminishwa.
Na kwamba, kuhama chama cha siasa si dhambi kama ilivyoshadidiwa


Siku zijazo kuhama chama kimoja kwenda kingine itakuwa jambo la kawaida.
Hili limewafungua wananchi Kamba walizokuwa nazo, kwamba, kuhama upinzani kwenda CCM ni dhambi au kinyume chake


Pili, hali hiyo itaweka nidhamu katika vyama vya siasa. Vyama vitaelewa wanachama wasiporidhika wana uwezo wa kuhama na kuendelea na maisha ya kisiasa bila tatizo

Tatu, kupungua kwa viburi vya kisiasa

Inaendelea…….
 
Kupungua kwa viburi
Mfano mzuri ni wa chama tawala kilichoamua kufanya mambo kwa mazoea tu.

Tumeshuhudia mambo kama katiba na miswada ya kipuuzi ikipitishwa pasi kujali wananchi wanamaoni gani


Kampeni za uchaguzi za CCM zilikiacha chama pembeni na kumweka mgombea wake kama chama.
Ilikuwa dhambi kubwa kutamka chagua CCM. Zomea zomeaza wenye sare za CCM zilifikia kiwango cha polisi kuingilia kati


Mawaziri wamepoteza nafasi zao wakiwemo waandamizi. Tena yupo waziri mwandamizi aliyebwagwa na binti mchanga kisiasa

Waziri huyo mwandamizi alikuwa kinara katika kutekeleza kiburi cha chama tawala kulazimisha miswada na sera zisizo na maana

Somo kubwa ni kuwa hakuna mwenye immunity katika community au society`kwa sasa.
Atakayendeleza ubabe atapigwa chini na wananchi kwa ujumla wao


Nne, CCM na bunge lao wajiangalie . Uwepo wao wenye shaka kutokana na uchaguzi unaangaliwa kwa hisia na hasira kutoka sehemu kubwa ya jamii. Ubabe wa kupitisha miswada na sheria kwa wingi kutakimaliza chama katika muda mfupi sana.

Kuna uwezekano kuelekea uchaguzi mwingine CCM ikawa na wakati mgumu kuliko waliopambana nao
wakisaidiwa vyombo dola

Tano, Uchaguzi umeonyesha kuwa sera za wapinzani zinaweza kutekelezeka wakifanya kazi pamoja na chama tawala.

Hoja za ukubwa wabaraza la mwaziri, uzembe, wizi na ubadhirifu zilikuwa za wapinzani na sasa zinafanyiwa kazi na Rais aliyetoka CCM


Sita wapinzani wanasimama wapi


Inaendelea……..
 

Iaendelea
Sita
Kumekuwepo nahoja kuwa wapinzani hawana hoja baada ya Rais kuchukua `hatua` za kukabiliana na uzembe na ufisadi.

Wenye hoja hii wanasahau kuwa hoja nyingi zinazofanyiwa kazi ni matokeo ya kelele zawapinzani.

Lakini pia wanasahau kuwa hoja za wapinzani si kukabaliana na `hatua zadharura`bali kujenga muundo wa kudumu(sustainable)

Kufanyiwa kazi hoja za wapinzani kunapeleka ujumbe kwa umma kuwa , wapinzani wana maono zaidi ya chama tawala.
Na kwamba madai yao ni ya msingi isipokuwa hayasiklizwi nawahusika


Hili linatoa msukumo kwa wapinzani kuendelea kupiga kelele si za hatua za reja rejabali kubadili mfumo mzima.

Kubadili mfumo kunahitaji marekebisho makubwa ya mfumo kupitia katiba.
Tunasema katiba kwasababu ndiyo chimbuko la sheria na miundo mingine inayoendesha taifa


Kinachoendelea sasa hivi si marekebisho ya mfumo, ni kazi za zimamoto.

Mfano, kumuondoa kamishna wa TRA hakujatoa ufumbuzi wa tatizo.
Je,kamishna alikuwa huru kutekeleza majukumu yake bila kuingiliwa.

Je, vyombo vingine vilikuwa huru kukabiliana na uhalifu hata vilipotaarifa.

Je, mtandao mzima wa uhalifuumejulikana chanzo chake ni udhaifu wa eneo gani


Maeneo ya kuzungumzia kutokana na kushindwa kwa sera zaCCM ni mengi.
Kwa mfano, nini itakuwasera ya kilimo, ufundi, teknolojia , makazi, umiliki wa ardhi, elimu na afya , maliasili, madinin.k.


Hivyo, hoja zipo nyingi sana inategemea jinsi gani wapinzani watajipanga na kuzianisha

Itakuwa ni ujinga kwa Watanzania kushangilia majukumu na si kuhoji sera za mambo yanayofanyika


Saba, serikali ya CCM chini imeingia ikiwa na changamoto kubwa ya tatizo la Zanzibar.
Ingawa linapewa kisogo,tatizo lililopo mbeleni ni kubwa sana kiasi cha kutishia muungano


Kuchelewa kutangazwa kwa baraza la mawaziri inaweza kuwa sehemu ya tatizo. Mbele yasafari , nguvu za Rais wa JMT zitapungua kutokana na jinsi serikali ya muungano inavyojiweka mbali na tatizo

Rais mstaafu alionja joto ya tatizo la muungano. Alielewa hali kule ZNZ kama ilivyokuwa bara haikuwa nzuri kwa CCM.
Kwa visiwani `udhibiti`ulishindikana kwa vile nguvu kubwa ilibidi kuelekeza bara

Matokeo yalionyesha hali visiwani kutokuwa nzuri. Ilibidi aondoke mapema akijua mzigo wa safari hii ni mzito.
Si suala la kutafuta suluhu bali ``kuhofia kifo cha muungano ``mikononi`


Changamoto nyingine ni namna ya kutekeleza majukumu kwa nguvu inayoonekana kwa kutumia mfumo uliochakaa.

Yapo maswali,nini kianze kwanza, kubadili mfumo ufuate utekelezaji au hapa kazi tu katika mfumo uliochakaa! Tutajadili zaidi


Tusemezane




.
 
Nguruvi3,

Kwa hali iliyopo na tunayoyaona, Upinzani hoja waliyonayo moja na inawabidi waifanyie kazi kwa nguvu zote ni kulilia kwa machozi ya damu kuundwa kwa mfumo imara wa Kiserikali utakaohakikisha kuwa mihimili yote minne (ongezea vyombo vya habari) vya Serikali vinafanya kazi zao kwa uhuru, umakini na uadilifu.

Tayari kwa kuangalia kesi za TRA, TPA, Muhimbili, TRL na hata Tanesco, ni wazi kuan madhaifu makubwa ya kimfumo na utendaji ambayo yameishia kutegema mtu mmoja mmoja (in this case, nchi nzima inamtegemea Magufuli na CCM bila haya ya udhaifu wa awamu ya nne, inajitapa kwa nguvu kuwa Magufuli anatekeleza Ilani ya CCM.

Kero, matatizo, vilio na shida wananchi walizotolea kauli miaka nenda kuhusu rushwa, uwajibikaji, uadilifu, maji safi, afya bora, elimu, ajira, miundombinu na mambo mengine ni orodha ndefu ya wananchi kila kata, tarafa, mtaa, wilaya, mkoa na Taifa ambayo vyama vya siasa vimeziita ni ilani.

Tuna bahati ya mtende kuwa Magufuli anaelekea hana simile na ubabaishaji na hii ni fursa muhimu kwa Upinzani kusukuma hoja ya kuundwa upya kwa katiba, kupitiwa upya kwa sheria na miiko ya viongozi, kupitia sheria zinazozuia haki, kandamizi na onevu, kutoa uhuru kamili kwa vyombo vya dola kufanya kazi bila kuingiliwa na wanasiasa na hata kuvunja kabisa mazoea na mfumo unaoruhusu chama chenye wabunge wengi au chama tawala kujifanyia mambo hasa kwa watendaji wakuu na wanasiasa wake wanaojiamulia mambo.

Ni aibu sana kuona jinsi gani kwa muda mfupi ukereketwa wa Magufuli unaelekea kuamsha watendaji wa serikali na hata hatua za maana kubana matumizi, kuongeza mapato na kuwajibisha watu ghafla yanatokea. Magufuli anajaribu kuturusisha katika namba sufuri (0) katika mstari wa namba maana tulitumbukia katika upande wa hasi wa mstari wa namba kwa miaka 15!

Ukweli ni kuwa Magufuli kama Magufuli na si CCM, amejaa uthubutu kufanya lile lililosahihi kwa Watanzania. Na changamoto kubwa kadhaa za kufanya kwa umakini lakini pia kwa uharaka: Suala la uchaguzi wa Zanzibar, Katiba mpya ya wananchi, Tume huru ya Uchaguzi-mgombea huru, sheria za uchaguzi na muda wa kampeni na uchaguzi, daftari la wapiga kura, Msajili wa vyama, Tume ya maadili, Civil servant contracts na vyombo huru, makini na imara vya sheria na dola.

Kama upinzani unataka kubakia relevant, ni lazima vita (war) iongeze wigo wake na si kulilia mapigano (battle) ya October 25.

There is a big prize ahead and the only way to win it is to fight and defend rights of citizens which will ensure transparent government, that is efficient, accountable and fair, it carries laws and rules that are not partisan or oppressive, the law and order execute their work in fairness and just, a people's constitution and a meaningful resolution to empower equally both parts of the Union including revision of articles of Union and structure of union.

That is the prized war that Opposition need to spearhead and not the small battles of personality contests or petty rhetoric of nani katimiza ilani ya kukusanya mapato na kudhibiti rushwa na ufisadi!
 
Mkuu Rv Kishoka
Mwanzo wa bandiko tulisema , agenda ya wapinzani ni mabadiliko ya mfumo.


Hii ni kwasababu kuu mbili

Moja, kuwezesha uwepo wa uwanja sawa wa siasa.Tunajua yaliyotokea wakati wa uchaguzi na kila mmoja anajua hilo

Tunajua nini kinaendelea ZNZ na sote tunashuhudia

Bila kurekebisha mfumo, upinzani utajihakikishia nafasi ya kudumu katika upinzani.

Kazi haitakuwa rahisi, lakini ni rahisi sana wakati huu umma ukiwa na dukuduku cha mazingaombwe yaliyofanyika


Pili,kubadili mfumo kutawezesha hoja za wapinzani kuwa na maana.

Tumeona ‘jeshi la mtu' mmoja kwakutumia nguvu-sheria zinavyoleta matatizo


Wengi hawaoni kama ni tatizo, lakini ni tatizo kubwa. Kumekuwa na utekalezaji wa mambo kwa kutumia mtu na hofu.

Maana yake ni kuwa mtu huyo asipokuwepo kwa sababu yoyote ile, tunarudi square one


Lakini pia tunaona jinsi ambavyo kukosekana kwa mfumo mahususi wa utawala unavyoweza kumwakwaza mheshimiwa

Kwa mfano,mh anateua watu kushika nyadhifa kubwa na leo tunajua watu hao wapo katika kashfa kama tunazoziona za bandari.

Hapa kunakujiuliza, hapakazi inakuwaje?


Tunasikia tetesi kamati kuu imeanza kutoa makucha dhidi yake. atawezaje kutekeleza azma zake njema katika mazingira kama hayo

Tunashuhudia wakuu wa wilaya wakitumia mahubusu bila sababu za msingi. Wakuu wa mikoa wakizuia likizo nakila aina ya mkanganyiko.

Kibaya zaidi, huwezi kuamini watu wameteuliwa kwa nyadhifa mbali mbali siku chache kabla ya Mh mstaafu hajaondoka.

Hii maana yake ni kuwa mfumo unauruhusu watu kupeana zawadi za nyadhifa.Ni kama tulivyoona vyeo vikitolewa kama zawadi au fadhila


Ukiangalia orodha ya watendaji alioachiwa na mh mstaafu, wengi ni ima watoto, vijana au watu waliosaidia kampeni n.k.

Hii maana yake, hatuna vetting system kama alivyowahi kusema mh Mkapa.
Kwamba mfumo wetu unaruhusu mtu na si mfumo mzima kuwa sustainable.


Sustainability inawezekana pale tu tutakapokuwa na system inayofanya kazi yenyewe ikijiangalia ‘checks and balances'
 
Nguruvi3,

Kwa hali iliyopo na tunayoyaona, Upinzani hoja waliyonayo moja na inawabidi waifanyie kazi kwa nguvu zote ni kulilia kwa machozi ya damu kuundwa kwa mfumo imara wa Kiserikali utakaohakikisha kuwa mihimili yote minne (ongezea vyombo vya habari) vya Serikali vinafanya kazi zao kwa uhuru, umakini na uadilifu.

Tayari kwa kuangalia kesi za TRA, TPA, Muhimbili, TRL na hata Tanesco, ni wazi kuan madhaifu makubwa ya kimfumo na utendaji ambayo yameishia kutegema mtu mmoja mmoja (in this case, nchi nzima inamtegemea Magufuli na CCM bila haya ya udhaifu wa awamu ya nne, inajitapa kwa nguvu kuwa Magufuli anatekeleza Ilani ya CCM.

Kero, matatizo, vilio na shida wananchi walizotolea kauli miaka nenda kuhusu rushwa, uwajibikaji, uadilifu, maji safi, afya bora, elimu, ajira, miundombinu na mambo mengine ni orodha ndefu ya wananchi kila kata, tarafa, mtaa, wilaya, mkoa na Taifa ambayo vyama vya siasa vimeziita ni ilani.

Tuna bahati ya mtende kuwa Magufuli anaelekea hana simile na ubabaishaji na hii ni fursa muhimu kwa Upinzani kusukuma hoja ya kuundwa upya kwa katiba, kupitiwa upya kwa sheria na miiko ya viongozi, kupitia sheria zinazozuia haki, kandamizi na onevu, kutoa uhuru kamili kwa vyombo vya dola kufanya kazi bila kuingiliwa na wanasiasa na hata kuvunja kabisa mazoea na mfumo unaoruhusu chama chenye wabunge wengi au chama tawala kujifanyia mambo hasa kwa watendaji wakuu na wanasiasa wake wanaojiamulia mambo.

Ni aibu sana kuona jinsi gani kwa muda mfupi ukereketwa wa Magufuli unaelekea kuamsha watendaji wa serikali na hata hatua za maana kubana matumizi, kuongeza mapato na kuwajibisha watu ghafla yanatokea. Magufuli anajaribu kuturusisha katika namba sufuri (0) katika mstari wa namba maana tulitumbukia katika upande wa hasi wa mstari wa namba kwa miaka 15!

Ukweli ni kuwa Magufuli kama Magufuli na si CCM, amejaa uthubutu kufanya lile lililosahihi kwa Watanzania. Na changamoto kubwa kadhaa za kufanya kwa umakini lakini pia kwa uharaka: Suala la uchaguzi wa Zanzibar, Katiba mpya ya wananchi, Tume huru ya Uchaguzi-mgombea huru, sheria za uchaguzi na muda wa kampeni na uchaguzi, daftari la wapiga kura, Msajili wa vyama, Tume ya maadili, Civil servant contracts na vyombo huru, makini na imara vya sheria na dola.

Kama upinzani unataka kubakia relevant, ni lazima vita (war) iongeze wigo wake na si kulilia mapigano (battle) ya October 25.

There is a big prize ahead and the only way to win it is to fight and defend rights of citizens which will ensure transparent government, that is efficient, accountable and fair, it carries laws and rules that are not partisan or oppressive, the law and order execute their work in fairness and just, a people's constitution and a meaningful resolution to empower equally both parts of the Union including revision of articles of Union and structure of union.

That is the prized war that Opposition need to spearhead and not the small battles of personality contests or petty rhetoric of nani katimiza ilani ya kukusanya mapato na kudhibiti rushwa na ufisadi!

Mkuu,

Mimi naomba niulize jambo moja ambalo naona linamezwa sana na hizi nyimbo za mfumo mfumo. Hivi kwa hizi kesi zinazoendelea mfano TRA na TPA, tatizo ni kuwa hakuna mfumo ambao kama ungefuatwa yaliyotokea yasinge tokea au tatizo ni kuwa watu waliokuwa ndani ya huo walikuwa wako so corrupted kiasi walijiamulia kwa utashi wao na uroho wao kutofuata mfumo uliopo na kufanya wanavyotaka?

I am of the opinion ya kuwa na mfumo mzuri peke yake sio suluhisho, unahitaji pia kuwa na watu wawajibikaji na ambao wanaamini katika huo mfumo. Kinachotoke sasa hivi ndani ya mfumo uliopo ni kuwa amepatikana mtu muajibikaji hicho peke yake ndio kilichobadilika. Organs zote zilizotakiwa kuhakikisha kuwa mfumo unafanya kazi nazo zilijihusisha katika katika kuhakikisha kuwa huo mfumo haufanyi kazi!! Kuna a human and moral aspect hapa ambayo watu wengi wanaoimba wimbo wa mfumo mfumo mfumo nadhani wanaikosa. Kama taifa, at a human level corruption ilitutawala, head to toes!

Iko katika nature ya watu kufight mifumo inayowekwa na kutafuta loop holes. Na huwezi kuwa na mfumo ambao ni fool proof, hakuna hicho kitu katika reality, unacho hitaji ni kuwa na watu ambao wanaamini na wana uzalendo wa kuhakikisha mifumo iliyopo inafanya kazi kwa ajili yetu sote. Na hiyo behaviour ya either kukubali corruption au kukataa ina flow downward toka kwa wale wenye madaraka kwenda mpaka kwa wale makabwela wa manzese.

Niseme wazi, nakubali argument ya kuwa tunahitaji kuimarisha mifumo yetu ili iweze kusimama yenyewe..Lakini kama taifa pia tuna hitaji zaidi a wake up call in what we believe to be right and wrong at a morality level. Ukiwa na sheria nzuri ambayo hakuna anaetaka kuifuata na wale wanaotakiwa kuhakikisha watu wanaifata nao hawataki kuifuata, hata hiyo sheria iwe nzuri kiasi gani haiwezi kufanya gani.


Nimepingana na Nguruvi katika uzi mwingine kule kwenye jukwaa la siasa, kwa sababu opinion zake nimeona zimekaa kilawama zaidi, bado yuko kwenye uchaguzi, anataka achorewe picha lakini anapinga jitihada za kuichora hiyo picha ila some how anataka hiyo picha out of thin air itokee.

Hata kuelekea kwenye kubadili huo mfumo ni lazima kuwe na sehemu ya kuanzia, lazima kuna critical institutions za kuanza nazo. Alipo anza huyu jamaa kila mtu amepaona na ntafurahi zaidi the next guy atakae zungumzia mfumo asiseme tu tunahitaji mfumo ubadilike, aseme ubadilike vipi au tuanzie wapi katika kufanya hayo mabadiliko na Je tuache jitihada zote zinazofanyika sasa hivi mpaka tukipata mfumo mpya ndio tuendelee?

There is a difference between having critical negative opinion and having a purely negative attitude. Kadri hii thread inavyoenda i see more of the later from Nguruvi, i might be wrong and i hope i am.

#CHANGETANZANIA
 
Mkuu GalaxyS3

Umetoa hoja nyingi , naomba nizipitie katika mabandiko tofauti

Hoja ya kwanza, kwamba nipo katika uchaguzi na napinga 'ramani' na nataka ichorwe out of thin air nikiwa na lawama

Nakuhakikishia kuwa uchaguzi kwa upande wangu uliisha kabla ya kuanza.
Matokeo yaklikuwepo kabla ya mtu mwingine hajaona.
Nilisema uchaguzi si sanduku la kura ni zaidi ya hapo. Niliandika kwa undani kwanini CCM 'itashinda'

Pili, nahitaji kuona ramani halisi katika blue print, si ramani katika karatasi ya kufungia sigara.
Kinachoendelea si ramani ni mhemuko tu ambao nimesema wazi ATAFELI

Kufanikiwa kwa Rais ni kufanikiwa kwa nchi na kufeli kwake ni kufeli kwa nchi.

Sisi tunaosema ukweli tunamsaidia sana kuona picha kwa ukubwa wake, kuliko wanaomtia matumaini feki kwa kushangilia bila kuona umbali mrefu

Tatizo si nia wala maadili ya kiroho ya watu. Nchi za wenzetu masuala ya kiroho yapo katika nyumba za ibada.
Nchi zao zinaongozwa na sheria kuhakikisha maadili yanafuatwa kisheria na si kumsingizia mungu.

Hakuna nchi iliyo perfect , hata hivyo suala si perfection bali striving for excellence

Nikuonyeshe tatizo la mfumo na jinsi linavyoanza kumkwaza mheshimiwa

1. Suala la Muhimbili :

Kumuondoa mkurugenzi kwasababu MRI hazikufanya kazi miezi zaidi ya 3 si suluhu.
Hakuna ushahidi kama mkurugenzi alizembea kutoomba pesa.

Hakuna ushahidi kama pesa zilitoka akazitumia tofauti
kwa maoni yetu at least, kama upo ushahidi hilo ni suala lingine

Kuna ushahidi kuwa pesa hazikuwepo. Siku alipomteua mkurgenzi mpya aliagiza pesa zitolewe haraka siku hiyo.

Maana yake ni kuwa somewhere somewhat kuna uzembe. Je, uzembe ni wa mkurugenzi peke yake?

Kama aliomba pesa hazina na hakupewa angefanya nini zaidi?
Na kama kuna uzembe hazina, mbona hatua hazikuchuliwa dhidi ya wazembea?

Kama mfumo ungekuwa sahihi, tungekuwa na majibu bila kupepesa.

Kila mmoja angetoka na kuweka wazi wapi tatizo lilipo

Inawezekana pesa zilitumika kununua magari kwa mamia ya jeshi la Polisi. Je, hilo ni tatizo la mkurugenzi?

Iweje mabailioni yatumike kununua magari na zisiwepo pesa za MRI? Je, ni tatizo la mkurugenzi kutoa vipaumbele

Lakini pia, iweje tatizo liwe la mkurugenzi na si katibu mkuu au waziri au uongozi wa juu wa nchi.

Ilikuwaje utawala uliopita haukuona tatizo. Maana yake ni rahisi, mambo yanaamuliwa na watu na si mfumo.

Mkurugenzi ni mtu aliyewajibika kwasababu ya mazingira tu. Kwa undani zaidi mfumo mzima ulifeli

Ilikuwaj bunge la katiba lilitumia mabailioni katika shughuli zake, wakati huo huo zikizkosekana bilioni 2 au 3 za kufanyia marekebisho ya MRI.

Ni mfumo gani ulioruhusu kiasi kikubwa kutumika katika allowance na si MRI ya wananchi

Utaona hadi hapo suala si mtu bali system nzima ilifeli

Huu ni mfano wa kwanza, inafuata mingine
 
Last edited by a moderator:
Mfano wa 2

TRA: Kamisha anateuliwa na Rais, Bodi inateuliwa na Rais. Baadhi ya watendaji wanateuliwa na bodi

Kwa maana nyingine, vyombo hivyo havina uwiano wa uwajibikaji. Kamishana anaweza kukaidi hoja za bodi, na bodi wanaweza kukaidi hoja za kamishana na watendaji wanaweza kukaidi hoja za kamishna
Mfumo huu unawezaje kuhakikisha kuwa kila kitu kipo sawa?

Kamishna kaondolewa kwa makontena yasiyolipiwa kodi. Je, kuna mizigo mingapi imepita kwa misamaha bila sababu za msingi? Nani anatoa misamaha hiyo? Kamishna anaidhinisha,lakini nguvu zake zipo wapi ikiwa anawajibika kwa watu wengine? Nguvu za bodi zipo wapi ikiwa hawana uwezo wa kumwajibisha kamishna?

Tuna uhakika gani kulikuwa na uzembe wa kamishna? Amekiri kuwa na majina na hakuyafanyia kazi hadi wakati 'anafumaniwa' je kwanini hakuyafanyia kazi?

Je, kama kuna vimemo vya kutoa misamaha kutoka juu au vimemo vingine yeye angefanya nini!
System haimuruhusu na analipa gharama za system , lakin, je,ni ukweli kuwa yeye ndiyo tatizo?

Kamishna kaondolewa, vipi kuhusu bodi nzima kama anavyouliza The Boss kila mara. Hapa huoni kuna tatizo mkuu!

TPA: Kumekuwepo na malumbano ya muda mrefu kuanzia kwa mawaziri wawili waliopita kuhusu utandaji wa bodi
Leo imevunjwa kwa uzembe. Je, ni uzembe wa bodi au ni uzembe wa system iliyowaweka?

Kulikuwa na vetting ya kutosha kuhusu wajumbe au ilikuwa 'technical know who'

Tunaona wajumbe wa bodi baadhi wamepewa nyadhifa kubwa kitaifa. Ilikuwaje wazembe wale wale wapewe fursa za kuongoza Taifa ikiwa wamefeli kuongoza taasisi?

Nani aliyefeli hapa mjumbe aluyeula au waliomteua bila kuangalia background yake.

Hata kama walijua background, aliwezaje kupenya hadi katika ngazi tunazoziona?

Jibu ni rahisi, system imefeli na si mtu au watu. System ilifeli kuanzia utawala uliopita hadi uliopo

Je, suala ni kuweka viraka au kufumua mfumo mzima ili kuhakikisha kila mtu anawajibika na mauza uza yanajulikana mara yanapoanza kujitokeza! Hatujui kwa miaka mingi ya nyuma kiasi gani kimepotea, sasa iweje tudhani viraka vinaweza kutusaidia. Akija mh mwingine naye atakuja na yake kwavile system inategemea watu na si yenyewe

Natoa mfano mmoja , India iliwahi kudumu miezi 3 bila waziri mkuu, UK ikadumu wiki 3 bila PM. Na katika wakati huo hakuna kilichokwenda kombo kwasababu system ilikuwa inafanya kazi yenyewe.
Viongozi wanaongoza tu na si kuwa system wao kama wao

Tutaendelea na hoja zingine, mifano miwili inatosha kukueleza kwanini tunazungumzia system na si reja reja
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,

Mimi naomba niulize jambo moja ambalo naona linamezwa sana na hizi nyimbo za mfumo mfumo. Hivi kwa hizi kesi zinazoendelea mfano TRA na TPA, tatizo ni kuwa hakuna mfumo ambao kama ungefuatwa yaliyotokea yasinge tokea au tatizo ni kuwa watu waliokuwa ndani ya huo walikuwa wako so corrupted kiasi walijiamulia kwa utashi wao na uroho wao kutofuata mfumo uliopo na kufanya wanavyotaka?
Mtu akiwa corrupt hawezi kufuata mfumo. Hatutegemei kipya kutoka kwake isipokuwa corruption. Tunachoweza kufanya ni kuzuia corruption isitokee, na ikitokea iwe rahisi kubaini wahusika wote na ushirika wao, na kisha kuwachukulia hatua

Kinachofanyika sasa hivi ni kuchukua hatua. Je hatua za kuzuia zilikuwepo? Wahusika wote wanajulikana?

Mdororo wa uchumi ulipotokea, Marekani walitafuta chanzo, wakabaini wahusika na kisha kuwachukulia hatu
Halafu wakakaa chini na kuweka taratibu zitakazo zuia insittution za fedha kuzembea na kusababisha madhara

Tunaona mfumo chakavu usioendana na mazingira ya sasa. Mfumo uliochakaa kama ilivyochakaa katiba yetu

Tungekuwa na mfumo thabiti haya yasingetokea au yangetokea na kubainika mapema tena na watu wa chini si Rais
 
Mkuu,
I am of the opinion ya kuwa na mfumo mzuri peke yake sio suluhisho, unahitaji pia kuwa na watu wawajibikaji na ambao wanaamini katika huo mfumo. Kinachotoke sasa hivi ndani ya mfumo uliopo ni kuwa amepatikana mtu muajibikaji hicho peke yake ndio kilichobadilika. Organs zote zilizotakiwa kuhakikisha kuwa mfumo unafanya kazi nazo zilijihusisha katika katika kuhakikisha kuwa huo mfumo haufanyi kazi!! Kuna a human and moral aspect hapa ambayo watu wengi wanaoimba wimbo wa mfumo mfumo mfumo nadhani wanaikosa. Kama taifa, at a human level corruption ilitutawala, head to toes
Unapopata mtu mwajibikaji katika mazingira yasiyoruhusu kuwajibika ni kutia maji kwenye pakacha

Warioba kasema , jitihada zake zilishindwa kwasababu ya kukosekana kwa maadili ya viongozi n.k.
Akasema lazima turudi katika miiko na maadili ili tuweze kufanikiwa.

Akasisitiza kuwa maadili na miiko lazima iwe sehemu ya katiba ya nchi

Maana yake, ni lazima vitu hivyo viwe katika sheria za nchi. Ingawa vinaonekana vya kiroho zaidi, ni muhimu vikalindwa na sheria kuliko ilivyo sasa.

Nikuulize bwana GalaxyS3, tunasikia viongozi wanataja mali. Lini umesikia wakitueleza mali walizo nazo baada ya kustaafu

Hapa ni kwasababu, wao walijifanya na maadili na miiko, hakuna sheria inayowalazimu kutaja mali zao wakimaliza

Wameweka system hata ukitaka kujua wana nini ni ngumu. Hawa ndio walinzi wa'human and moral issues' Unazosema

Human and moral issues haziwezi kufanya kazi peke yake. Huko kwenye masinagogi, misikiti na makanisa tumeona serious violation of ethics and high libertine. Na wao wameweka taratibu zao za viongozi

Leo unataka wanasiasa ambayo basically ni morally corrupt wawe huru ku exercise moral issue, itawezekana wapi

Uzalendo unaousema upo, kinachoharibu uzalendo ni wale waliopewa dhamana.

Hivi ukisikia kuna watu wamelamba bilioni 80 za kodi kwa kukwepa, wakati mwenye cheki ya milioni 1 kwa mwezi analambwa kodi kisa tu ni mfanyakazi, uzalendo utoke wapi. Tuweni wakweli

Hoja hapa ni kuwa lazima tuwe na mfumo unatazama kila mmoja katika kuwajibika.

Hatuwezi kumsingizia mungu kwamba ni masuala ya kiroho tukijua wezi wanatumia mwanya wa mfumo dhaifu kutuumiza

Fikiria hivi, wezi waliiba huko nyuma wakiwa maafisa waandamizi. Wametumia pesa hizo na wamerudi bungeni

Hakuna aliyewazuia ndani ya chama au nje ya chama. Wanajua udhaifu wa mfumo na wanautumia vema sana

Wanagawana pesa kwenye magunia na hatuwezi kuwashtaki kwasababu wanajua udhaifu wa mfumo wetu

Viongozi wanatumia mfumo dhaifu kuunda tume za kipuuzi ambazo hazina majibu kwasababu wanajua udhaifu wa mfumo

Kwa miaka 10 nchi imeundiwa tume kwa makumi kama si mamia.
Viongozi wametumia mfumo dhaifu kuficha na kuwahifadhi watu wao

GalaxyS3, nikuulize ile tume iliyoundwa na IGP, Mwanasheria mkuu na mkuu wa Pccb unajua matokeo yake?
Hakuna anayejua, kilichotokea ilikuwa kupunguza hasira za walipa kodi

Na ukitaka kujua tuna mfumo hovyo, jiulize, hivi kazi ya Polisi ni nini ikiwa kila tukio linaundiwa tume?

Jibu lake ni rahisi, ili kukwepa mfumo lazima zitumike tume kuficha uovu

Tukiendelea na muundo huo tutafeli kama Taifa, na dalili za kufeli zimeanza ingawa wengi hawaoni
 
Back
Top Bottom