Mitandao isitumike kumchafua Rais

Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.

Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-

1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.

Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.


Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.

Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012
Kweli kabisa. Uhuru wa mmoja huishia unapoanzia wa mwenzake. Mitandao ni chombo bora na muhimu kabisa katika kuijenga jamii na kukosoa masuala yanayoenda arijojo, lakini si lazima watu kutumia lugha chafu ili kuwasilisha jumbe mbalimbali. Binafsi siipendi kabisa CCM na hata JK mwenyewe lakini namheshimu kama Rais aliye madarakani na naamini anapokosolewa hufanyika hivyo kwa maslahi ya nchi zaidi kuliko binafsi. Hivi karibuni nilichangia thread moja iliyokuwa ikimsifu kwa kutumia busara kufanya uamuzi wa kuurejesha muswaada wa mabadiliko ya Katiba Bungeni na nilisema waziwazi kwamba mara nyingi Kikwete anapotoshwa na wapambe wanaomzunguuka na ambao hufanya hivyo kwa maslahi yao zaidi kuliko ya taifa. Mimi naamini mtandao kama wa JF ni chombo chenye faida pande zote mbili yaani kwa serikali inayotuongoza kupima mwonekano wake kwa umma na kwetu tunaoongozwa kujadili na kutoa mapendekezo na hata kupumua hasira zetu; lakini bado nasisitiza bila kutumia lugha za matusi. Ni kwa mantiki hii naungana kikamilifu na Mhariri wa Tanzania Daima kuwasihi wanamitandao ya jamii kuepuka lugha za matusi dhidi ya kiongozi wetu mkuu licha ya mapungufu yake.
 
JamiiForums is a 'User Generated Content' site

Hutaki unaacha.

Mitandao isitumike kumchafua Rais


Tanzania Daima. 15 Feb, 2012

HIVI karibuni, Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (Necta), lilitangaza matokeo ya kidato cha nne yaliyofanyika nchini mwaka 2011.

Na miongoni mwa wahitimu waliofanya mtihani huo ni mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, aliyemaliza katika moja ya shule za sekondari jijini Dar es Salaam.

Kwa bahati mbaya sana, matokeo ya mtoto huyo hayakuwa mazuri licha ya shule yake kufanya vizuri kitaifa katika mitihani hiyo na kuwa moja ya shule kumi bora.

Hoja yetu si kurejea matokeo hayo, bali tungependa kukemea matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii hasa wakati wa kujadili masuala kadhaa na hata mengine ambayo kimsingi ni ya kibinafsi lakini yanahusishwa moja kwa moja na maslahi kwa umma.

Tunasema hivyo kutokana na baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao hiyo, kuchukulia matokeo mabaya ya mtoto wa Rais kama suala la kitaifa lenye kuhusishwa na uongozi wa baba yake, na hivyo kumshambulia kiongozi huyo bila sababu ya msingi.

Kwanza, lazima tutambue kuwa kufanya vibaya katika mitihani ni jmabo la bahati mbaya ambalo kimsingi linamuumiza mtahiniwa na vile vile wazazi au walezi wake, lakini tunapaswa kuelewa kuwa mtoto wa Rais ameshindwa kama walivyoshindwa wanafunzi wengine pasipo kujali amesoma shule gani au mzazi ana wadhifa gani.

Pili, tunapaswa kulichukulia jambo hili kama funzo na changamoto kwa elimu yetu, kwani ni watoto wachache sana wa viongozi wetu wakuu wanasoma shule za hapa Tanzania, na kwa ubabaishaji uliyopo kwenye usimamizi wa mitihani bado Rais angeweza kutumia nguvu yake kuhakikisha mwanaye anapendelewa lakini haikuwa hivyo.

Ni vyema wakati wa kujadili na kuchangia maoni hasa kuwahusu watawala wetu, tukazingatia majukumu na wajibu wa msingi tunaowapa viongozi ili watekeleze, na hivyo tunapaswa kuwahukumu kwa kuzingatia mipaka hiyo si kuingilia hata mambo yao binafsi na familia zao.

Mtoto wa Rais kushindwa mtihani si jambo la kutufanya tumtukane baba yake, yeye si malaika kwani huo ndiyo uwezo aliopewa na Mungu na walimu wake wakaongezea ujuzi wao.

Kama hoja ni kwamba kila anayeshindwa mtihani wazazi wake wasakamwe kwa matusi, basi hebu tuwatazame kwanza wa kwetu.

Tunaamini umefika wakati kwa wale wamiliki wa mitandao hiyo kuwa makini na hoja zinazoletwa hewani kujadiliwa na kujifanyia uhakiki kabla ya kuzichapisha, vnginevyo tutajikuta tumegeuka taifa linalovunja haki za msingi za binadamu kwa kuingilia masuala binafsi ya watu wengine.

Kama hoja ni kufeli kwa mtoto wa Rais, basi kafeli kama wale wa kwetu ambao tunawasomesha kwenye shule duni au zile za mamilioni lakini mwisho wa siku hawafaulu, sasa iweje tumwandame kiongozi wetu kwa suala lisilohusiana na kazi tuliyompa?

Tundhani kwa hili Rais alipaswa kusifiwa kuwa si mbinafsi kwa kuwa hakumpeleka mtoto wake kusoma Ulaya kama ambavyo viongozi wengi wa nchi hii wafanyavyo hata kwa watoto wao wasiokuwa na uwezo kimasomo.
 
Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.

Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-

1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.

Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.


Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao..
Anachafuliwa, kwani lini alishakuwa msafi??? Ni maajabu kama unaweza kumchafua mtu ambaye ni mchafu tayari!
 
Nani kakwambia mimi ni muajiriwa serikalini? Unadhan madaraka ya Rais ni sawa na ya mwalimu?

Kama si mwajiriwa wa Serikali, ujue kuwa hata barabara unazopita na shule ulizosoma kijijini kwenu ni hela zetu pia. Mimi nililinganisha ajira serikalini kwamba yeyote na ajira ya namna hiyo anatumia pesa zetu kwa kuwa analipwa mshahara... sikumaanisha kufananisha ukubwa wa vipato na nafasi.
 
Kikombe cha baba watoto wanakinywa na kikombe cha watoto baba anakinywa vile vile!, ndivyo ilivyokua kwa Sadam Hussein, kwa Gadaffi n.k! Mbona mazuri ya wazazi wanajivunia?, iweje mabaya wasijutie?. Mi nadhani mjadala haukutosha kabisa, ilitakiwa tujadili kwa undani kilichofanya afeli sio kukimbilia kusema bahati mbaya!, kama ni kampeni za uchaguzi uliopita tujue kabisa make familia yote ilihamia kwenye kampeni. HALAFU TUNASUBILI BABA YAKE ATAMUENDELEZAJE ILI NA WANGINE WOOOTE WALIOFELI WADAI HAKI HIYO, eee, ndio!, kikwete si ndio baba yao wote?
 
Kama si mwajiriwa wa Serikali, ujue kuwa hata barabara unazopita na shule ulizosoma kijijini kwenu ni hela zetu pia. Mimi nililinganisha ajira serikalini kwamba yeyote na ajira ya namna hiyo anatumia pesa zetu kwa kuwa analipwa mshahara... sikumaanisha kufananisha ukubwa wa vipato na nafasi.

I DONT KNOW WHAT YOU KEEP BETWEEN YOUR EARS!......mimi nalipa PAYE karibu Tshs 2.4m, VAT karibu Ths 1m kwa mwezi sasa kwa nini barabara zisijengwe?
 
watoto/watahiniwa walioandika bongo fleva, matusi, kuchora wachezaji ndio walipaswa kupewa mjadala zaidi kuliko mtoto wa Rais.
 
Tujadili matokeo ya jumla. Mtoto wa mkulima na maskini akipata matokeo hayo ndio mwisho wa maisha yake lakini sio mtoto wa Rais ambaye bado ana fursa nyingi za kusonga mbele. Tulijadili taifa sio mtu mmoja mmoja.
 
Wewe na hilo gazeti lako ulilotolea sourse ndo munalenga kumchafua Baba Mwanaasha, hili jambo lilikuwa lishaisha hata hapa jamvini jana na juzi hakukua na thread mpya ilohusu mada yako naona Gazeti lako na wewe mumeamua kuuza kwa kumchafua mkuu wa kaya kwa kuendeleza mjadala.Samahani napita tu naelekea Arumeru Mashariki kurudisha fomu
Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.

Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-

1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.

Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.


Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.

Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012

Mitandao isitumike kumchafua Rais


Tanzania Daima. 15 Feb, 2012

HIVI karibuni, Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (Necta), lilitangaza matokeo ya kidato cha nne yaliyofanyika nchini mwaka 2011.

Na miongoni mwa wahitimu waliofanya mtihani huo ni mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, aliyemaliza katika moja ya shule za sekondari jijini Dar es Salaam.

Kwa bahati mbaya sana, matokeo ya mtoto huyo hayakuwa mazuri licha ya shule yake kufanya vizuri kitaifa katika mitihani hiyo na kuwa moja ya shule kumi bora.

Hoja yetu si kurejea matokeo hayo, bali tungependa kukemea matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii hasa wakati wa kujadili masuala kadhaa na hata mengine ambayo kimsingi ni ya kibinafsi lakini yanahusishwa moja kwa moja na maslahi kwa umma.

Tunasema hivyo kutokana na baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao hiyo, kuchukulia matokeo mabaya ya mtoto wa Rais kama suala la kitaifa lenye kuhusishwa na uongozi wa baba yake, na hivyo kumshambulia kiongozi huyo bila sababu ya msingi.

Kwanza, lazima tutambue kuwa kufanya vibaya katika mitihani ni jmabo la bahati mbaya ambalo kimsingi linamuumiza mtahiniwa na vile vile wazazi au walezi wake, lakini tunapaswa kuelewa kuwa mtoto wa Rais ameshindwa kama walivyoshindwa wanafunzi wengine pasipo kujali amesoma shule gani au mzazi ana wadhifa gani.

Pili, tunapaswa kulichukulia jambo hili kama funzo na changamoto kwa elimu yetu, kwani ni watoto wachache sana wa viongozi wetu wakuu wanasoma shule za hapa Tanzania, na kwa ubabaishaji uliyopo kwenye usimamizi wa mitihani bado Rais angeweza kutumia nguvu yake kuhakikisha mwanaye anapendelewa lakini haikuwa hivyo.

Ni vyema wakati wa kujadili na kuchangia maoni hasa kuwahusu watawala wetu, tukazingatia majukumu na wajibu wa msingi tunaowapa viongozi ili watekeleze, na hivyo tunapaswa kuwahukumu kwa kuzingatia mipaka hiyo si kuingilia hata mambo yao binafsi na familia zao.

Mtoto wa Rais kushindwa mtihani si jambo la kutufanya tumtukane baba yake, yeye si malaika kwani huo ndiyo uwezo aliopewa na Mungu na walimu wake wakaongezea ujuzi wao.

Kama hoja ni kwamba kila anayeshindwa mtihani wazazi wake wasakamwe kwa matusi, basi hebu tuwatazame kwanza wa kwetu.

Tunaamini umefika wakati kwa wale wamiliki wa mitandao hiyo kuwa makini na hoja zinazoletwa hewani kujadiliwa na kujifanyia uhakiki kabla ya kuzichapisha, vnginevyo tutajikuta tumegeuka taifa linalovunja haki za msingi za binadamu kwa kuingilia masuala binafsi ya watu wengine.

Kama hoja ni kufeli kwa mtoto wa Rais, basi kafeli kama wale wa kwetu ambao tunawasomesha kwenye shule duni au zile za mamilioni lakini mwisho wa siku hawafaulu, sasa iweje tumwandame kiongozi wetu kwa suala lisilohusiana na kazi tuliyompa?

Tundhani kwa hili Rais alipaswa kusifiwa kuwa si mbinafsi kwa kuwa hakumpeleka mtoto wake kusoma Ulaya kama ambavyo viongozi wengi wa nchi hii wafanyavyo hata kwa watoto wao wasiokuwa na uwezo kimasomo
.
 
Ubaya au uzuri aliandika waraka huu hajajitaja jina.....au mhariri ndio kaandika tahariri?? basi ni kilaza wahedi
 
kwani ukisema hili ni embe wakati ni embe kweli kuna makosa kisheria?
 
Utetezi wako ni mzuri tu........niambie kwa high standards za FEZA GIRLS huyu alifikaje Form IV?.....una hakika gani baba yake hakujaribu kuratibu majibu yake wakati anadaiwa kuratibu kura za watanzania 2010?.....na ni nani kasema kufeli kwake mtihani ndio kafeli maisha?

mkuu wangu nakubaliana nawe kwamba hiyo ni shule ambayo kwa mtoto hasiye na uwezo wa kutosha kiakili darasani ktk mazingira ya kawaida hawezi kufika kidato cha nne,angekwisha rudishwa nyumbani lakini hakuna mwenye ushahidi kujua kama huyu mtoto alikua hapati alama za kutosha huko nyuma.
 
hao tanzania daima wanatafuta umaarufu tu kupitia mgongo wa nyumba mbona kuna mambo kibao tu jamii ina discuss tena hoja za msing wanapotezea wasiturudishe nyuma sie tupo mbele km 200000 'nyuma yao
 
Utetezi wako ni mzuri tu........niambie kwa high standards za FEZA GIRLS huyu alifikaje Form IV?.....una hakika gani baba yake hakujaribu kuratibu majibu yake wakati anadaiwa kuratibu kura za watanzania 2010?.....na ni nani kasema kufeli kwake mtihani ndio kafeli maisha?

Mhh hapo panaitaji tafakari
 

Attachments

  • Mawazo.jpg
    Mawazo.jpg
    8.8 KB · Views: 176
Pili, tunapaswa kulichukulia jambo hili kama funzo na changamoto kwa elimu yetu, kwani ni watoto wachache sana wa viongozi wetu wakuu wanasoma shule za hapa Tanzania, na kwa ubabaishaji uliyopo kwenye usimamizi wa mitihani bado Rais angeweza kutumia nguvu yake kuhakikisha mwanaye anapendelewa lakini haikuwa hivyo.[/COLOR][/B].

huyu Mwandishi Kihelehele kumbe anajua kuwa watoto wa Viongozi hawasomi katika Shule za hapa nchini????

Mbona hajasema na sababu inayofanya wasisome hapa nchini; Si wanaogopa shule walizozianzisha wenyewe kwa sababu hazina vifaa na walimu wa kutosha. Pia hata hao walimu wachache waliopo hawafundishi kwa moyo mkunjufu kwa sababu wanadhurumiwa haki zao ikiwa ni pamoja na mishahara midogo.

Kwa nini watoto wa viongozi wasisome hapa katika shule za KATA zilizotapakaa kila kona ya nchi yetu na kuzinduliwa kwa mbwembwe nyingi!!!!!!

Sisi hatuna nia ya kumtukana mtu bali kutoa fundisho kuwa watoto wa kitanzania wanafeli kutokana na mazingira duni ya shule zetu. Hii ni changamoto hata kwa Mh. Raisi ili aboreshe shule zetu walalahoi.

Tena ni heri mtoto huyu amesoma yule ya FEZA,

Mtoto wa mlalahoi Mtanzania = anayesoma katika shule za kata, tena anaamka alfajili saa10, ili kuwahi kupigania daladala, hana hata pesa ya kununua mhogo au maji, kurudi anachelewa kufika home kutokana na adha ya daladala. na elimu anayopata ni duni kutokana na shule kukosa vifaa vya kufundishia.

Mtoto wa kiongozi = anakwenda shule na gari nzuri, ana pesa ya kutosha matumizi, anarudishwa na gari

Hili ni fundisho kwa viongozi wetu.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom