Misingi ya ukristo au uislamu wetu, na wale waliouleta(waarabu na wazungu) kipi cha muhimu?

QALQAL MARTIN

Member
Jan 13, 2011
14
3
WANA JF NAPENDA TUJADILI MADA HUSIKA ILI NAMI NIPATE UELEWA ZAIDI.
Kila kukicha huwa haikosekani thread za udini kwa upeo wangu mdogo nafikiri tunachanganya mambo mawili 'misingi za dini na wale waliotuletea hizo dini'...wale waliotuletea dini wametimiza kazi yao ya kuhubiri misingi kuu ya husika husika.kwa lengo moja tu ya uhakika wa kuishi baada ya kifo. kazi ya kuiendeleza imani ya dini husika ktk ardhi ya AFRIKA ni ya WAAFRIKA wenyewe, kazi iliyobaki ni kulinda misingi ya dini na si kufungamana na wale walioleta dini, wao wanaweza kuzivuruga lakini ss tutawarekebisha. mfano dini flani huko ulaya waliruhusu askofu kuwa shoga lakini dini hiyo hiyo huku Afrika walisema si sawa, kwanini? walikataa si kwasababu ya kulinda misingi ya dini husika.
Tunakosea wapi?
1.tunakosea kuacha kazi ya kuendeleza dini kwa wale wale, kiasi cha kuwaogopa kama Mungu na kuwaogopa kuliko misingi ya dini.
2.tunatoa mapenzi yetu kwa wale waliotuletea hizo dini,kiasi cha kuwapeda hata wanapokosea na kuwatetea.
3.kazi ya kujenga makanisa na misikiti ni yetu na si yao, kazi yao wameimaliza.
Hayo matatu hayamanishi hatunaushirika na wliotuletea dini, ila lazima tuelewe na kutenganisha 'misingi ya dini na waliotuletea dini' ....
naomba kuwasilisha.....
 
Back
Top Bottom