Mombo Wetu
JF-Expert Member
- Aug 5, 2008
- 377
- 36
Ni mwaka mwingine tena unakaribia kuanza, mwaka (2011) ambao Tanzania itasherehekea miaka yake 50 tangu kuwepo kwenye ramani ya dunia. Kama taifa ni nini tunatafakari wakati huu?
Je kama taifa nini ilikuwa misingi yetu wakati tukianza?
Najiuliza hiyo misingi bado ipo au imeharibika na je ikiharibika mwenye haki atafanya nini?
Hupendi rushwa lakini hupati huduma bila kutoa rushwa
Hupendi nepotism (Undungu?) lakini nafasi za ajira chache, ushindani ni mkubwa na wewe hunachakuwapa wanao
Hupendi udini lakini wewe unadini yako na unaipenda kwa moyo moja kuliko huyo Mungu unayemwamini ambaye ameumba vyote.
Hupendi umaskini lakini fursa hazipatikani za kuondokana na umaskini bila kufanya ufisadi
Unapenda kutumikia wenzako kwa moyo wako wote lakini malipo hayatoshelezi mahitaji ya familia
Umwanafunzi mtiifu na mwenye kupenda shule lakini hakuna waalimu wala miundo mbinu ya kusoma
Unakipaji cha uongozi na unajiamini lakini uongozi haupatikani bila kuwa na kianzio...(Chapa), pia uwe mwanachama wa chama fulani hatakama huamini wanachokiamini etc etc
Lakini je tulianzaje? Misingi yetu ilikuaje? Hizo changamoto hazikuwepo wakati tunaanza?
Ndipo nikaamua kurudi katika imani maana kimwili sikupata swali litakalo jumuisha yote nitakayo kuyauliza....Imani yangu inaniuliza swali, Misingi ikiharibika mwenye haki atafanya nini?
Je misingi ni katiba; kama ndivyo hii ya sasa mbona inaamini katika ujamaa; je tu wajamaa? Na kujitegemea mbona tu tegemezi? Je misingi ni ipi?
Wanazuoni wanadai kuwa (kama tutakubaliana) misingi ambayo inaweza kuijenga jamii iliyostaarabika na yenye tija basi lazima kuwe na high "SOCIAL CAPITAL" (Nisaidieni kiswahili chake = Uaminifu?)
Kwakifupi ni kuwa uaminifu/social capital humfanya mfanya biashara akafanya biashara bila matumizi makubwa ya nguvu za sheria; mwalimu akafundisha kwa moyo bila usimamizi wa ziada; dakatari akatibu kwa kutumia nguvu zake zote akili yake yote na moyo wake wote kuokoa maisha ya mgonjwa; mbunge akawasaidia wapiga kura wake kama vile aisaidiavyo familia yake pale nyumbani kwa mke/mume na watoto wake; mwananchi akafuata sheria bila kujali uwepo wa polisi au mahakama na magereza na kila mmoja akawajibika kwa hiari huku akimfikiria mwingine bila kutumia nguvu zozote isipokuwa kulingana na makubaliano ya pamoja kama vile Katiba etc etc
Ni vipi basi tunaweza kujenga social capital?
Niwatakie heri ya mwaka ujao wana JF huku tukisaidiana kujibu hili swali tuweze kulisaidia taifa letu kuendelea kuwepo katika ramani ya dunia.
Je kama taifa nini ilikuwa misingi yetu wakati tukianza?
Najiuliza hiyo misingi bado ipo au imeharibika na je ikiharibika mwenye haki atafanya nini?
Hupendi rushwa lakini hupati huduma bila kutoa rushwa
Hupendi nepotism (Undungu?) lakini nafasi za ajira chache, ushindani ni mkubwa na wewe hunachakuwapa wanao
Hupendi udini lakini wewe unadini yako na unaipenda kwa moyo moja kuliko huyo Mungu unayemwamini ambaye ameumba vyote.
Hupendi umaskini lakini fursa hazipatikani za kuondokana na umaskini bila kufanya ufisadi
Unapenda kutumikia wenzako kwa moyo wako wote lakini malipo hayatoshelezi mahitaji ya familia
Umwanafunzi mtiifu na mwenye kupenda shule lakini hakuna waalimu wala miundo mbinu ya kusoma
Unakipaji cha uongozi na unajiamini lakini uongozi haupatikani bila kuwa na kianzio...(Chapa), pia uwe mwanachama wa chama fulani hatakama huamini wanachokiamini etc etc
Lakini je tulianzaje? Misingi yetu ilikuaje? Hizo changamoto hazikuwepo wakati tunaanza?
Ndipo nikaamua kurudi katika imani maana kimwili sikupata swali litakalo jumuisha yote nitakayo kuyauliza....Imani yangu inaniuliza swali, Misingi ikiharibika mwenye haki atafanya nini?
Je misingi ni katiba; kama ndivyo hii ya sasa mbona inaamini katika ujamaa; je tu wajamaa? Na kujitegemea mbona tu tegemezi? Je misingi ni ipi?
Wanazuoni wanadai kuwa (kama tutakubaliana) misingi ambayo inaweza kuijenga jamii iliyostaarabika na yenye tija basi lazima kuwe na high "SOCIAL CAPITAL" (Nisaidieni kiswahili chake = Uaminifu?)
Kwakifupi ni kuwa uaminifu/social capital humfanya mfanya biashara akafanya biashara bila matumizi makubwa ya nguvu za sheria; mwalimu akafundisha kwa moyo bila usimamizi wa ziada; dakatari akatibu kwa kutumia nguvu zake zote akili yake yote na moyo wake wote kuokoa maisha ya mgonjwa; mbunge akawasaidia wapiga kura wake kama vile aisaidiavyo familia yake pale nyumbani kwa mke/mume na watoto wake; mwananchi akafuata sheria bila kujali uwepo wa polisi au mahakama na magereza na kila mmoja akawajibika kwa hiari huku akimfikiria mwingine bila kutumia nguvu zozote isipokuwa kulingana na makubaliano ya pamoja kama vile Katiba etc etc
Ni vipi basi tunaweza kujenga social capital?
Niwatakie heri ya mwaka ujao wana JF huku tukisaidiana kujibu hili swali tuweze kulisaidia taifa letu kuendelea kuwepo katika ramani ya dunia.