VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kwanza wafanyakazi wa UDSM wameanza kupokea mishahara ya mwezi uliopita tangu jana tarehe 4/10/2012 saa sita mchana. Wameanza wafanyakazi wenye akaunti katika benki ya Makabwela yaani 'National Microfinance Bank-NMB'.
Katika mishahara hiyo, wapo watumishi waliopata ongezeko la mishahara. Wapo pia pia wasiopata ongezeko.Hawa wamepata mshahara wao wa kawaida kabla ya ongezeko. Vilevile wapo walioshushwa mishahara.
Hakuna sababu zilizotolewa na Serikali wala Chuo. Nyaraka za mishahara zinaonesha hivyo. Taarifa zinaonesha kuwa Utawala wa UDSM umeziba pengo la walishushwa mshahara ili kuzuia mgomo wa wafanyakazi wa aina hiyo.
Hali ni tete. Lolote laweza kutokea pale...
Katika mishahara hiyo, wapo watumishi waliopata ongezeko la mishahara. Wapo pia pia wasiopata ongezeko.Hawa wamepata mshahara wao wa kawaida kabla ya ongezeko. Vilevile wapo walioshushwa mishahara.
Hakuna sababu zilizotolewa na Serikali wala Chuo. Nyaraka za mishahara zinaonesha hivyo. Taarifa zinaonesha kuwa Utawala wa UDSM umeziba pengo la walishushwa mshahara ili kuzuia mgomo wa wafanyakazi wa aina hiyo.
Hali ni tete. Lolote laweza kutokea pale...