jamiif
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 2,413
- 990
mi nina mashaka hapo..inawezekana ulikuwa unevaa nusu uchi halafu unajiona mkali maana hata hapa dar mdada aliyevee nusu uchi ndio husikia manenokama hayo, na aliyevaa kwa heshima wala hakuna ishu hizo....kwanza hakuna hata mtu mmoja anayependa kula chakula kilichoachwa wazi, kwani pale ni mainzi tiu yanachezea na kusepa, watu makini wanapenda vyakula vilivyofunikwa...akili kichwani......shauri yako dada dunia mapito jiangalie!
Leo jumapili ilikuwa nzuri sana. Nikiwa boad nimejikongoja na kuamua ninyoshe miguu mitaa
ya Sakina hapa A-Town. Yaliyo nikuta huko imenipa picha na negative yake kuwa ukitaka kujua
jinsi gani upo hot and SEXY, ukitaka kujua kama umependeza au umechekesha siku hiyo pita mitaa
ya uswahilini. Utapenda! Huitaji kioo. Kumbe ni kupita tu uswazi ukutane na vijana kibao wasiogopa
kumsifia mwanamke mzuri kama mimi. Ndio narudi sasa nikaona why nisishee na wana MMU, hizi
habari zilizonitasabamisha jioni nzima, zikanifanya niliporudi nivue nguo niende kwenye kioo
nikajiangalie upya. Nafikiria kutoa shoo ya kuonesha mwili wangu; inaweza nilipa sana kama
kuna PR mzuri hapa mmu nafasi iko wazi. Hio imekuja leo hii mimi Erotica
nilivopita nimepata hizi comments.
Kwa vijana wa vijiweni-Duh wakubwa wanafaidi. Huyu ukiwa nae pressure tu hizo za
kujitakia-vijana wengine kijiweni. maradhi hayo-wazee kibarazani. Kwa mtindo huu Ukimwi
hautaisha babake-dereva taxi. Dada kweli wewe ni mzurii ngoja nikatafute pesa nitajirike
nitakutafuta-mbeba tenga kichwani. Shemeji leo kaka kakuachia utembee kwa miguu?
Mamaaa!-haka katoto naona ndio kame balehe. Weweeeee!-kijiwe kingine.
Hao hata kwetu wapo hao! Dada mambo? Uongo kazi umependeza! Na miruzi.
Ilifika time nikawa natabasamu hata sikumbuki mengine.
Mwaaaaah! I feel SEXY! :A S-heart-2: