BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,792
- 287,994
Misamaha ya kodi na mgawo wa umeme vyakwamisha TRA |
Tuesday, 28 June 2011 20:26 |
Mussa Juma, Arusha Mwananchi MISAMAHA mikubwa ya kodi na mgawo wa umeme unaoendelea nchini, ni miongoni mwa vikwazo vinavyosababisha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kushindwa kukusanya kodi kwa kiwango kikubwa.Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitillya, aliyasema hayo juzi wakati wa kusaini makubaliano ya kusaidiwa na Mamlaka ya Mapato Norway (NRA), kuboresha ukusanyaji mapato. Kitillya alisema bado misamaha ya kodi ambayo inatolewa kwa kampuni na taassisi mbalimbali ni mikubwa, hivyo kuathiri ukusanyaji mapato.Alisema hivi sasa misamaha ya kodi imefikia asilimia 2.5 ya pato la Taifa (GDP), tofauti na nchi za Kenya na Uganda ambako ni asilimia moja ya pato lao. Pia, Kitillya alisema tatizo la mgawo wa umeme na kutokusanywa kodi ipasavyo kwenye kampuni kubwa kama za madini, gesi na mafuta inachangia mapato kuwa kidogo tofauti na nchi nyingine. Alisema kutokana na mazingira hayo, TRA imesaini makubaliano na NRA, ili wafanyakazi wake wajengewe uwezo katika ukusanyaji mapato, hasa ukaguzi na uwazi katika ukusanyaji na ulipaji kodi. "Kama mnavyojua sasa Tanzania tunaelekea kwenye miradi mikubwa ya kuchimba gesi, mafuta na madini, hivyo ni muhimu wafanyakazi wa TRA kuwa na uelewa mkubwa wa kukusanya kodi kwa kampuni kubwa," alsiema Kitillya. Awali, Mkurugenzi wa NRA, Svein Kristensen, alisema inawezekana Tanzania ikakusanya kodi kubwa iwapo wafanyakazi wa TRA na Watanzania watakuwa wazi na kushirikiana. Kristensen alisema Norway yenye watu chini ya milioni tano, imekuwa ikukusanya kiwango kikubwa cha kodi na kimefikia kuchangia asilimia 42.8 ya pato la taifa hilo.Pia, hafla ya kusainiwa makubaliano hayo ilihudhuriwa na Balozi wa Norway nchini, Ingumu Klepsvik. |