Misamaha ya kodi: Chanzo cha kumong'onyoa uzalendo wetu

Kasheshe

JF-Expert Member
Jun 29, 2007
4,694
787
Ndugu zangu,

Kwa mawazo yangu kama kuna kitu kinapunguza sifa/nguvu za mtu kuwa na uzalendo kamili ni huu ugongwa wa msamaha wa kodi.

Kwa maoni yangu wawakilishi wa wananchi ndio watu ambao wanatakiwa wapewe treat ambayo ni sawa kabisa na wananchi wajue machungu na matamu ya wanaowawakilisha.

Kwa muda mrefu sielewi ni kwa nini mwakilishi wa wanachi awe-exempted na kodi ya namna yoyote ile.

Nionavyo mimi exemption ya kodi ni ulaghai wa serikali kudanganya kwamba watu fulani hawalipwi hela nyingi kumbe wanalipwa fedha nyingi.

Lakini muhimu pia ukitaka kila mwananchi apende na kutetea nchi yake wakati wote hakikisha analipa kodi.

Asitokee mwananchi yeyote yule nchini asilipe kodi, alipe kulingana na uwezo wake. hata kama ni sh. tano kwa mwezi lakini aweze kusimama mbele ya raia wenzake na kusema nimelimia sh. tano kwa taifa langu, hivyo na-demand kuletea maji, afya na kadhalika.

Mwisho, ninakerwa na msamaha wa kodi wa namna yeyote ile.
 
Mimi naashangaa hapo nchini kwetu kusikia kitu kinaitwa kusamehe kodi. Hata kule katika dini (mimi si mjuzi wa hayo) nasikia pia watu walikuwa wakilipa kodi. Na kwetu ndio hiyo Zakaat. Sasa hapa leo unasema unamsamehe mtu kodi - vyereje?
 
Sasa mimi raia wa kawaida nitakuwa na hamasa gani kulipa wakati wabunge, mawaziri, majaji wanapeta hawalipi kodi???

Uzalendo wangu utatoka wapi??

Angeaza JK tukajua 2008 amelipa kodi kiasi gani!
 
Misamaha ya kodi ni mwanya mkubwa wa rushwa, futa yote anaetaka kuwekeza alipe kodi, anaetaka kutangaza dini alipe kodi nk nk
 
Misamaha ya kodi nadhani ilikua ni janja ya viongozi wa miaka hiyo ya nyuma. eti wafanyakzi wa serikali,madaktari etc. wanakuwa na exemption kwa sababu gani?????????kodi ni jukumu la kila mwananchi mwenye kipato kiwe kikubwa au kidogo kwani unatakiwa kulipa kadiri ya mapato yako.Hapa ndipo rushwa ilipozaliwa kwa nguvu zote.Watu wote walipe kodi hata kama una nyadhifa ya kufika mbinguni lipa kodi period!!
 
Misamaha ya kodi ni mwanya mkubwa wa rushwa, futa yote anaetaka kuwekeza alipe kodi, anaetaka kutangaza dini alipe kodi nk nk

Tuko pamoja, sioni mantiki ya kusamehe kodi kwa taasisi yoyote na kwa raia yeyote.

Lazima kila mtanzania aweze kusimama mbele ya mwenzake aseme mimi nimechangia nchi yangu kiasi hiki cha kodi.
 
Sasa mimi raia wa kawaida nitakuwa na hamasa gani kulipa wakati wabunge, mawaziri, majaji wanapeta hawalipi kodi???

Uzalendo wangu utatoka wapi??

Angeaza JK tukajua 2008 amelipa kodi kiasi gani!


Mzalendohalisi,

Nakupata, wewe kweli mzalendo halisi!!! very strong point!
 
Tunaomba akina Zitto na Dr. Slaa watueleze kwa nini huwa hawawi wakali kwenye hili?
Na watueleze kweli kuna haja ya kuwa na misamaha ya kodi?

Ni kwa nini? Kusamehe kodi kuna maslahi gani kama sio lugha ya ulaghai tu?
 
This will be the best thing if achieved, as it will be in line with Cannons of taxation 'fairness' - everyone should pay tax.

Nchi za wenzetu hata marais wanatakiwa wafile tax returns and declare income and pay resultant tax na hapo tutpata kuwakamata viongozo amabo awana evade tax kama yalivyotokea UK hivi karibuni (though not directly related with Tax, wao waliwaibia wananchi kwa kudai matumizi yao binafsi)

Watu wote, biashara zote, taasisi zote lazima zilipe kodi ili kuondoa uonevu.

Kama wakitokea wabunge watakaoweza kusubmit hilo suala bungeni na likapitishwa itakuwa ni jambo kuu Tanzania.

Lakini tukumbuke wazi kwamba wabunge wetu wataliona hilo ni jambo gumu kwao (they are selfish) kwani sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004 inasamehe kodi kwa wabunge wote pindi wanapolipwa GRATUITY mwishoni mwa kipindi (5 years). Refer EXEMPT AMOUNTS - paragraph 1 (s) of the Second schedule to the Income Tax Act, 2004.

Vile vile raisi halipi kodi juu ya mshahara wake na marupurupu yote yanayotokana na yeye kuwa raisi!! Refer EXEMPT AMOUNTS - paragraph 1 (a) of the Second schedule to the Income Tax Act, 2004.
 
Lakini tukumbuke wazi kwamba wabunge wetu wataliona hilo ni jambo gumu kwao (they are selfish) kwani sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004 inasamehe kodi kwa wabunge wote pindi wanapolipwa GRATUITY mwishoni mwa kipindi (5 years). Refer EXEMPT AMOUNTS - paragraph 1 (s) of the Second schedule to the Income Tax Act, 2004.

Vile vile raisi halipi kodi juu ya mshahara wake na marupurupu yote yanayotokana na yeye kuwa raisi!! Refer EXEMPT AMOUNTS - paragraph 1 (a) of the Second schedule to the Income Tax Act, 2004.

Tunaelekea kipindi cha uchaguzi hawa wanaojiita wabunge mahiri wa upinzani wakiwabana Spika na Rais... hili linaweza kutendeka.

Kwa nini? Kwa kuwa sheria hiyo ilipitishwa kipindi ambacho wote hawakuwa kwenye vyeo walivyo navyo leo, na kumbuka kwamba wote wanapenda warudi kwenye viti vyao baada ya uchaguzi.

KODI LAZIMA ILIPWE NA KILA RAIA na kiwe kigezo kikubwa cha kupenda Nchi Yetu.

Kodi ni kichocheo kikubwa cha uzalendo wetu na kitafanya raia wote walioko vijini wafuatilia mapato na matumizi ya halmashauri zao.
 
Uzalendo wangu uko pale pale.


Kasheshe,
Kwa mantiki hiyo hizi sifa na nguvu 'kamili' za Uzalendo wangu lazima uwe na, wa-kulipa kodi. Ninakubaliana.
Kwa mantiki hiyo hiyo bila hivyo(kulipa kodi) siwezi kuwa mzalendo 'kamili'?

Hapo juu tunagongana!

Nionavyo mimi exemption ya kodi ni ulaghai wa serikali kudanganya kwamba watu fulani hawalipwi hela nyingi kumbe wanalipwa fedha nyingi.

Na hawa watu ni wananchi hao hao au ni watu fulani tu?
Fafanua...


Lakini muhimu pia ukitaka kila mwananchi apende na kutetea nchi yake wakati wote hakikisha analipa kodi.

Kwa nini nipende Nchi yangu kwa masharti?

Uhakiki gani huu unaozungumzia? Kuhakikisha kuwa tunapata huduma kwa mda mfupi anafanya nani, TRA?

Ala kulli hali, kuna umuhimu wa kufanyia utafiti Misamaha hiyo unayozungumzia hususani umuhimu umekuwa kwa faida ya nani, misamaha hii huwa inakuja na wakati(dynamic) hivyo umuhimu wa kupitia na kufanya uhakiki wa faida zake na huko kumong'onyoa uzalendo wetu lazima ifanywe.

Ndugu yangu, misamaha ya kodi itakuwepo, nafikiri mara nyingi huwa zinachangia pale kunapokuwa kuna kitega uchumi ambao unahitaji nguvu zote za dola,na udundulizaji wa hali ya juu ili kufanikisha azma hizo, za uwekezaji, huwa mara nynigi zinakuwa na faida maradufu na za mda mrefu.

Misamaha itaendelea na Uzalendo wangu utaendelea.

Ahsante
 
Misamaha ya kodi ni mwanya mkubwa wa rushwa, futa yote anaetaka kuwekeza alipe kodi, anaetaka kutangaza dini alipe kodi nk nk
Na hii sio rahisi watu wa kawida kupewa. Wanapewa walewale with access to the big shorts making those decisions. Ninakubaliana kabisa na wewe kuwa hili nalo laweza kuwa mwanya mkubwa wa rushwa. Misamaha yenyewe haiko very clear inatolewaje tolewaje kwa watu wa kawaida
 
Uzalendo wangu uko pale pale.


Kasheshe,
Kwa mantiki hiyo hizi sifa na nguvu 'kamili' za Uzalendo wangu lazima uwe na, wa-kulipa kodi. Ninakubaliana.Kwa mantiki hiyo hiyo bila hivyo(kulipa kodi) siwezi kuwa mzalendo 'kamili'?
Hapo juu tunagongana!

Kama hulipi kodi wewe sio mzalendo kamili wa Taifa letu, na kama unakwepa kodi wewe ni fisadi kwenye Taifa letu.




Na hawa watu ni wananchi hao hao au ni watu fulani tu?
Fafanua...
Misamaha ya kodi mara nyingi imetolea kwa wawakilish, mawaziri, watumishi wa umma etc. Kibaya ni kwamba misamaha hiyo hiyo sio fair mfano na inakelezwa vibaya mfano mtumishi ana msamaha wa kuingiza gari. mwenye kuingiza VX msamaha utakuwa mkubwa kuliko mwenye kuingiza bajaji----> mwishowe ni kama ufisadi fulani hivi.


Kwa nini nipende Nchi yangu kwa masharti?

Well, kama hutoi kodi ni kitu gani kitakufanya uwe na complete ownership of project, fedha za umma, mashirika ya umma etc.


Uhakiki gani huu unaozungumzia? Kuhakikisha kuwa tunapata huduma kwa mda mfupi anafanya nani, TRA?

Swali unapokwenda kwenye hospital ya binafsi ukichajiwa 100,000/- kama huduma unakuwa na nguvu ya kudai huduma bora si ndio? basi ukitoa kodi kwa kadri ulivyojaliwa utakuwa na nguvu hiyo hiyo... hivyo utawala bora utadumishwa.

Ala kulli hali, kuna umuhimu wa kufanyia utafiti Misamaha hiyo unayozungumzia hususani umuhimu umekuwa kwa faida ya nani, misamaha hii huwa inakuja na wakati(dynamic) hivyo umuhimu wa kupitia na kufanya uhakiki wa faida zake na huko kumong'onyoa uzalendo wetu lazima ifanywe.

Ndugu yangu, misamaha ya kodi itakuwepo, nafikiri mara nyingi huwa zinachangia pale kunapokuwa kuna kitega uchumi ambao unahitaji nguvu zote za dola,na udundulizaji wa hali ya juu ili kufanikisha azma hizo, za uwekezaji, huwa mara nynigi zinakuwa na faida maradufu na za mda mrefu.

Misamaha itaendelea na Uzalendo wangu utaendelea.

Ahsante

Hakuna umuhimu wa kufanya utafiti wowote maana hata faida zinazopatikana kwa walengwa zinakuwa hazitendi haki...nakupa mfano... shirika la dini linaloingiza miradi ya bil 5. litakuwa na msamaha mkubwa kuliko zinaloleta bidhaa za million moja. Na mfanyakazi anayeingiza Range Rover atakuwa anapata msamaha mkubwa kuliko anayingiza corola. kwa nini isiwe... posho fulani kwa vyeo fulani mtu aamue mwenyewe anunue gari la gharama kwa uamuzi wake?

In short misahama ya kodi haina faida... raia wote walipe kodi kulingana na uwezo wao and must be well calculated and with no discrimination of any nature. na zisiwe za kuwafaidisha wajanja!
 
Kama hulipi kodi wewe sio mzalendo kamili wa Taifa letu, na kama unakwepa kodi wewe ni fisadi kwenye Taifa letu.







Hakuna umuhimu wa kufanya utafiti wowote maana hata faida zinazopatikana kwa walengwa zinakuwa hazitendi haki...nakupa mfano... shirika la dini linaloingiza miradi ya bil 5. litakuwa na msamaha mkubwa kuliko zinaloleta bidhaa za million moja. Na mfanyakazi anayeingiza Range Rover atakuwa anapata msamaha mkubwa kuliko anayingiza corola. kwa nini isiwe... posho fulani kwa vyeo fulani mtu aamue mwenyewe anunue gari la gharama kwa uamuzi wake?
In short misahama ya kodi haina faida... raia wote walipe kodi kulingana na uwezo wao and must be well calculated and with no discrimination of any nature. na zisiwe za kuwafaidisha wajanja!

Naona utafiti mbadala hapo.
Mie bado Mzalendo.
Ahsante kuelimishana.
 
Back
Top Bottom