Kwangu mimi Utamaduni huu wa kuweka haki pembeni (Sheria)na kufarijiana kwa pesa hautatufikisha mbali na zaidi utatuletea yanayoendelea Somalia na kwingineko.Na shawishika kuwa bila kuwaona mbele ya Hakimu/mahakama kundi lote la wale askari waliopo sehemu ya tukio ikiwa pamoja na RPC wa Iringa iko siku! watoto wa Marehemu watatafuta namna mbadala ya kuona haki imetendeka dhidi ya Marehemu Baba yao.
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo Zitto Kabwe Achangia Bima Ya Afya Ya Mjane Wa Mwangosi Na Wanawe Kupitia NSSF
Napata shida sana kuamini haya mambo.Simshambulii Mhe.Zitto na wengineo wengi waliochangishana pesa kwa kumsaidia mjane wa Daudi Mwangosi.
Lakini kwa imani yangu na ufahamu wangu mdogo nilionao, wasamaria wema hawa wangeweza kumtendea haki Marehemu pamoja na Familia yake na kuwapatia faraja Mjane na watoto wake kwa kuanza na jambo hili;
KUSAIDIA KUFUNGUA KESI YA MAUAJI NA MADAI DHIDI YA JESHI LA POLISI NA SERIKALI.
Kwamba wote walioshiriki na kusimamia kifo cha Mwangosi wanafikishwa mbele ya Mahakama na kesi yao kusikilizwa kwa uwazi kama wanavyofanya Mahakama za Kimataifa na hukumu kutolewa.
Kwamba familia inahitaji kuhudumiwa au kulipwa na Serikali baada ya Jeshi la Polisi kuhusika na kifo cha Mzazi huyu ambaye ni tegemeo la familia kwa kila kitu.
Misaada hii itamtoa Mjane wa Mwangosi toka utumwa wa Kilio cha ndani kwa ndani na kumletea faraja ya moyoni kwa kuona watuhumiwa wamefikishwa mahakamani na kuridhika kwake kama mwenendo wa kesi umefuaka sheria.
Lakini pia madai ya fidia italeta uhakika kwa familia kuendesha maisha kadri marehemu alivyokuwa akipigania maendeleo ya kuhudumia familia yake.
Kwa upande mwingine naomba nimkumbushe Mhe.Zito anayedai anaweza kuwa amiri Jeshi Mkuu (Raisi)kwamba kama ni mimi hapa Mtihani mmoja mdogo unaelekea kuufeli.Kama Mbunge aliye na ndoto ya kuwa Raisi,nilitarajia ukipasa Sauti ndani na Nje ya Nchi kuwa RPC wa Iringa aliyekuwepo na kushiriki moja kwa moja na wale askari wote walioshiriki kwenye Kifo cha Daudi wanafikishwa mahakamani ,bila kusahau matukio mingine kama haya.
Na kwamba Michango inayoendeshwa sehemu ya pesa hizi zilifaa zitumike kufungulia Kesi na kutafuta Mawakili watakaosaidia haki kutendeka /ionekane inatendeka.Shughuli hii wewe kama Msomi , Mbunge na mwenye ndoto ya kuwa Raisi na imani unaiweza na ni mtu muafaka kuisimamia kuliko hii ya NSSF kama utaamua kuifanya .
Kwa Mjengwa blog na wanahabari wengineo nawashauri ili kumtendea haki Mwangosi na kama mlivyo andamana jangwani tafuteni namna ya kufungua Kesi ya kweli na ya haki dhidi ya kifo cha Daudi Mwangosi na hii itakuwa zawadi pekee mtakayoweza kumpatia marehemu.(Haki Mbele ya Sheria)
R.I.P- D.Mwangosi
Huu ni mtazamo wangu.
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo Zitto Kabwe Achangia Bima Ya Afya Ya Mjane Wa Mwangosi Na Wanawe Kupitia NSSF
Ari hii ya Watanzania kujitolea kusaidiana kwenye hali kama iliyomkuta mjane wa Daud Mwangosi imedhihirisha umoja na upendo tulionao kama Watanzania, na pia imeonyesha jinsi tunavyoijali amani yetu na hivyo jamii, kupitia michango hii, imeonyesha pia kwa vitendo, dhamira ya kulaani kwao vitendo vya maovu na vinavyotokana na matumizi ya nguvu yasiyo ya lazima kama kile kilichomtokea mwandishi Daud Mwangosi.
Baadhi ya watu maarufu katika jamii waliojitokeza kwa hiyari yao kumchangia mjane wa Daud Mwangosi kupitia mtandao wa kijamii wa Mjengwablog.com ni pamoja na Shy- Rose Bhanji, Ananilea Nkya, John Bukuku ( Mmiliki wa Fullshangwe.blog) na Ndugu Mobhare Matinyi aliyepata kuwa mhariri wa gazeti la Majira.
Lakini kwa imani yangu na ufahamu wangu mdogo nilionao, wasamaria wema hawa wangeweza kumtendea haki Marehemu pamoja na Familia yake na kuwapatia faraja Mjane na watoto wake kwa kuanza na jambo hili;
KUSAIDIA KUFUNGUA KESI YA MAUAJI NA MADAI DHIDI YA JESHI LA POLISI NA SERIKALI.
Kwamba wote walioshiriki na kusimamia kifo cha Mwangosi wanafikishwa mbele ya Mahakama na kesi yao kusikilizwa kwa uwazi kama wanavyofanya Mahakama za Kimataifa na hukumu kutolewa.
Kwamba familia inahitaji kuhudumiwa au kulipwa na Serikali baada ya Jeshi la Polisi kuhusika na kifo cha Mzazi huyu ambaye ni tegemeo la familia kwa kila kitu.
Misaada hii itamtoa Mjane wa Mwangosi toka utumwa wa Kilio cha ndani kwa ndani na kumletea faraja ya moyoni kwa kuona watuhumiwa wamefikishwa mahakamani na kuridhika kwake kama mwenendo wa kesi umefuaka sheria.
Lakini pia madai ya fidia italeta uhakika kwa familia kuendesha maisha kadri marehemu alivyokuwa akipigania maendeleo ya kuhudumia familia yake.
Kwa upande mwingine naomba nimkumbushe Mhe.Zito anayedai anaweza kuwa amiri Jeshi Mkuu (Raisi)kwamba kama ni mimi hapa Mtihani mmoja mdogo unaelekea kuufeli.Kama Mbunge aliye na ndoto ya kuwa Raisi,nilitarajia ukipasa Sauti ndani na Nje ya Nchi kuwa RPC wa Iringa aliyekuwepo na kushiriki moja kwa moja na wale askari wote walioshiriki kwenye Kifo cha Daudi wanafikishwa mahakamani ,bila kusahau matukio mingine kama haya.
Na kwamba Michango inayoendeshwa sehemu ya pesa hizi zilifaa zitumike kufungulia Kesi na kutafuta Mawakili watakaosaidia haki kutendeka /ionekane inatendeka.Shughuli hii wewe kama Msomi , Mbunge na mwenye ndoto ya kuwa Raisi na imani unaiweza na ni mtu muafaka kuisimamia kuliko hii ya NSSF kama utaamua kuifanya .
Kwa Mjengwa blog na wanahabari wengineo nawashauri ili kumtendea haki Mwangosi na kama mlivyo andamana jangwani tafuteni namna ya kufungua Kesi ya kweli na ya haki dhidi ya kifo cha Daudi Mwangosi na hii itakuwa zawadi pekee mtakayoweza kumpatia marehemu.(Haki Mbele ya Sheria)
R.I.P- D.Mwangosi
Huu ni mtazamo wangu.