Misaada; Mjane wa Daudi Mwangosi

Mp Kalix2

JF-Expert Member
Oct 4, 2010
5,940
3,041
Kwangu mimi Utamaduni huu wa kuweka haki pembeni (Sheria)na kufarijiana kwa pesa hautatufikisha mbali na zaidi utatuletea yanayoendelea Somalia na kwingineko.Na shawishika kuwa bila kuwaona mbele ya Hakimu/mahakama kundi lote la wale askari waliopo sehemu ya tukio ikiwa pamoja na RPC wa Iringa iko siku! watoto wa Marehemu watatafuta namna mbadala ya kuona haki imetendeka dhidi ya Marehemu Baba yao.

Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo Zitto Kabwe Achangia Bima Ya Afya Ya Mjane Wa Mwangosi Na Wanawe Kupitia NSSF

Ari hii ya Watanzania kujitolea kusaidiana kwenye hali kama iliyomkuta mjane wa Daud Mwangosi imedhihirisha umoja na upendo tulionao kama Watanzania, na pia imeonyesha jinsi tunavyoijali amani yetu na hivyo jamii, kupitia michango hii, imeonyesha pia kwa vitendo, dhamira ya kulaani kwao vitendo vya maovu na vinavyotokana na matumizi ya nguvu yasiyo ya lazima kama kile kilichomtokea mwandishi Daud Mwangosi.

Baadhi ya watu maarufu katika jamii waliojitokeza kwa hiyari yao kumchangia mjane wa Daud Mwangosi kupitia mtandao wa kijamii wa Mjengwablog.com ni pamoja na Shy- Rose Bhanji, Ananilea Nkya, John Bukuku ( Mmiliki wa Fullshangwe.blog) na Ndugu Mobhare Matinyi aliyepata kuwa mhariri wa gazeti la Majira.

Napata shida sana kuamini haya mambo.Simshambulii Mhe.Zitto na wengineo wengi waliochangishana pesa kwa kumsaidia mjane wa Daudi Mwangosi.

Lakini kwa imani yangu na ufahamu wangu mdogo nilionao, wasamaria wema hawa wangeweza kumtendea haki Marehemu pamoja na Familia yake na kuwapatia faraja Mjane na watoto wake kwa kuanza na jambo hili;

KUSAIDIA KUFUNGUA KESI YA MAUAJI NA MADAI DHIDI YA JESHI LA POLISI NA SERIKALI.

Kwamba wote walioshiriki na kusimamia kifo cha Mwangosi wanafikishwa mbele ya Mahakama na kesi yao kusikilizwa kwa uwazi kama wanavyofanya Mahakama za Kimataifa na hukumu kutolewa.

Kwamba familia inahitaji kuhudumiwa au kulipwa na Serikali baada ya Jeshi la Polisi kuhusika na kifo cha Mzazi huyu ambaye ni tegemeo la familia kwa kila kitu.

Misaada hii itamtoa Mjane wa Mwangosi toka utumwa wa Kilio cha ndani kwa ndani na kumletea faraja ya moyoni kwa kuona watuhumiwa wamefikishwa mahakamani na kuridhika kwake kama mwenendo wa kesi umefuaka sheria.

Lakini pia madai ya fidia italeta uhakika kwa familia kuendesha maisha kadri marehemu alivyokuwa akipigania maendeleo ya kuhudumia familia yake.

Kwa upande mwingine naomba nimkumbushe Mhe.Zito anayedai anaweza kuwa amiri Jeshi Mkuu (Raisi)kwamba kama ni mimi hapa Mtihani mmoja mdogo unaelekea kuufeli.Kama Mbunge aliye na ndoto ya kuwa Raisi,nilitarajia ukipasa Sauti ndani na Nje ya Nchi kuwa RPC wa Iringa aliyekuwepo na kushiriki moja kwa moja na wale askari wote walioshiriki kwenye Kifo cha Daudi wanafikishwa mahakamani ,bila kusahau matukio mingine kama haya.

Na kwamba Michango inayoendeshwa sehemu ya pesa hizi zilifaa zitumike kufungulia Kesi na kutafuta Mawakili watakaosaidia haki kutendeka /ionekane inatendeka.Shughuli hii wewe kama Msomi , Mbunge na mwenye ndoto ya kuwa Raisi na imani unaiweza na ni mtu muafaka kuisimamia kuliko hii ya NSSF kama utaamua kuifanya .

Kwa Mjengwa blog na wanahabari wengineo nawashauri ili kumtendea haki Mwangosi na kama mlivyo andamana jangwani tafuteni namna ya kufungua Kesi ya kweli na ya haki dhidi ya kifo cha Daudi Mwangosi na hii itakuwa zawadi pekee mtakayoweza kumpatia marehemu.(Haki Mbele ya Sheria)

R.I.P- D.Mwangosi
Huu ni mtazamo wangu.
 
THE COMMISSION FOR HUMAN RIGHTS AND GOOD GOVERNANCE

ACT, 2001

15.-(l) The Commission shall have power to investigate any human rights abuses or mal-administration -
(a) on As own initiative; or
(b) on receipt of a complaint or allegation under this Act by -
(i) an aggrieved person acting in such persons own interest;
(ii) an association acting in the interests Of its members;
(iii) a person acting in the interest of a group or class of persons.
(2) After conducting an investigation- under was Act, the Commission
shall have power to-
(a) where appropriate, promote negotiation and compromise between
the parties concerned; or
(b) causing the complaint and the findings of the Commission to be reported to the appropriate authority or person having control over the person m respect of whose act or conduct an investigation has been carried out by the Commissioner; or
(c) recommending to the, relevant person or authority such measures,or requiring that authority to take such measures, as will provide an effective settlement, remedy or redress.

(3) Notwithstanding the provisions of subsection 2 of this section,for the purposes of performing its functions under the Constitution and this Act, the Commission may bring an action before any court and may seek any remedy which may be available from that court.



Bado na amini kuliko kuchangishana kugenga minara na kuisaidia familia ya Marehemu.D.Mwangosi na hasa Watoto wake waliokuwa wakimtegemea kuona anawawezesha kuwa na Maisha Bora kuna haja ya kufungua Kesi Dhidi ya Polisi/Serikali na kudai Fidia kwa mtindo kama huu;

JK AWAACHIA HURU POLISI WALIOMUUA JENERALI KOMBE ...


Madai ya familia
Baada ya polisi hao kupatikana na kuhukumiwa adhabu ya kifo kwa kile Jaji Buxton Chipeta alichosema: “Uzembe wa hali ya juu”, mjane wa Kombe, Roselyne Kombe alifungua kesi ya madai dhidi ya Serikali.

Mjane huyo na watoto wa marehemu, walifungua kesi Mahakama Kuu wakiidai Serikali fidia ya Sh690 milioni kwa msingi kuwa kifo cha Kombe kiliifanya miradi iliyoanzishwa na marehemu kupoteza mwelekeo na kufa.

Oktoba 4, 2001, Jaji Lawrence Mchome ambaye sasa amestaafu, aliiona Serikali kuwa inawajibika kuilipa familia hiyo fidia kutokana na vitendo vya watumishi wake hao wawili lakini ikaiamuru ilipe fidia ya Sh300 milioni.

Hata hivyo, Serikali haikuridhika na hukumu hiyo na ilikata rufaa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ambayo kimsingi nayo iliafiki Serikali kulipa fidia isipokuwa ilipunguza kiwango cha fidia hadi kufikia Sh200 milioni.



Ni mwaka moja umepita!

Haya ni baadhi ya mambo unashindwa kuamini !
Je mpaka leo ni kiasi gani imepatikana na imefanya nini?
Kweli hii ni aibu kwa jamii inayolilia haki kutendeka!






Kamuhanda aondolewa Iringa - Kitaifa - mwananchi.co.tz
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Senso nafasi ya Kamuhanda, ambaye hivi karibuni alipandishwa cheo na kuwa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), inachukuliwa na Kamishna
UTPC YAPINGA MAOMBI YA CHADEMA KUTAKA KUIHUSISHA ... /Chadema yadaiwa kumtumia Mwangosi kisiasa
 
Kwangu mimi Utamaduni huu wa kuweka haki pembeni (Sheria)na kufarijiana kwa pesa hautatufikisha mbali na zaidi utatuletea yanayoendelea Somalia na kwingineko.Na shawishika kuwa bila kuwaona mbele ya Hakimu/mahakama kundi lote la wale askari waliopo sehemu ya tukio ikiwa pamoja na RPC wa Iringa iko siku! watoto wa Marehemu watatafuta namna mbadala ya kuona haki imetendeka dhidi ya Marehemu Baba yao.




Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo Zitto Kabwe Achangia Bima Ya Afya Ya Mjane Wa Mwangosi Na Wanawe Kupitia NSSF










Napata shida sana kuamini haya mambo.Simshambulii Mhe.Zitto na wengineo wengi waliochangishana pesa kwa kumsaidia mjane wa Daudi Mwangosi.
Lakini kwa imani yangu na ufahamu wangu mdogo nilionao, wasamaria wema hawa wangeweza kumtendea haki Marehemu pamoja na Familia yake na kuwapatia faraja Mjane na watoto wake kwa kuanza na jambo hili;


KUSAIDIA KUFUNGUA KESI YA MAUAJI NA MADAI DHIDI YA JESHI LA POLISI NA SERIKALI.



Kwamba wote walioshiriki na kusimamia kifo cha Mwangosi wanafikishwa mbele ya Mahakama na kesi yao kusikilizwa kwa uwazi kama wanavyofanya Mahakama za Kimataifa na hukumu kutolewa.
Kwamba familia inahitaji kuhudumiwa au kulipwa na Serikali baada ya Jeshi la Polisi kuhusika na kifo cha Mzazi huyu ambaye ni tegemeo la familia kwa kila kitu.
Misaada hii itamtoa Mjane wa Mwangosi toka utumwa wa Kilio cha ndani kwa ndani na kumletea faraja ya moyoni kwa kuona watuhumiwa wamefikishwa mahakamani na kuridhika kwake kama mwenendo wa kesi umefuaka sheria.



Lakini pia madai ya fidia italeta uhakika kwa familia kuendesha maisha kadri marehemu alivyokuwa akipigania maendeleo ya kuhudumia familia yake.

Kwa upande mwingine naomba nimkumbushe Mhe.Zito anayedai anaweza kuwa amiri Jeshi Mkuu (Raisi)kwamba kama ni mimi hapa Mtihani mmoja mdogo unaelekea kuufeli.Kama Mbunge aliye na ndoto ya kuwa Raisi,nilitarajia ukipasa Sauti ndani na Nje ya Nchi kuwa RPC wa Iringa aliyekuwepo na kushiriki moja kwa moja na wale askari wote walioshiriki kwenye Kifo cha Daudi wanafikishwa mahakamani ,bila kusahau matukio mingine kama haya.



Na kwamba Michango inayoendeshwa sehemu ya pesa hizi zilifaa zitumike kufungulia Kesi na kutafuta Mawakili watakaosaidia haki kutendeka /ionekane inatendeka.Shughuli hii wewe kama Msomi , Mbunge na mwenye ndoto ya kuwa Raisi na imani unaiweza na ni mtu muafaka kuisimamia kuliko hii ya NSSF kama utaamua kuifanya .



Kwa Mjengwa blog na wanahabari wengineo nawashauri ili kumtendea haki Mwangosi na kama mlivyo andamana jangwani tafuteni namna ya kufungua Kesi ya kweli na ya haki dhidi ya kifo cha Daudi Mwangosi na hii itakuwa zawadi pekee mtakayoweza kumpatia marehemu.(Haki Mbele ya Sheria)



R.I.P- D.Mwangosi
Huu ni mtazamo wangu.

Mchango mzuri makini. tatizo nnaloliona ni utayari na uthubutu wa kutekeleza hili suala.
 
Back
Top Bottom