Kyamkwikwi
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 441
- 146
Ndg Watanzania wenzangu, kwa masikitiko makubwa sana nawasihi tuungane sasa kupinga wizi huu wa pesa na kodi zetu kwa kutumia kisingizio cha mbio za mwenge wa huru.
Nimekuwa nikijaribu kufuatilia kwa makini sana kuhusu mamia ya miradi ambayo huwa inafunguliwa kila kona ya nchi kipindi cha mbio za Mwenge ili kuona jinsi gani inasaidia kuwakwamua wananchi katika lindi hili la umasikini. Kila mwaka huwa tunashuhudia kwenye vyombo vya habari na wengine wetu huwa washiriki kabisa wa matukio mbalimbali ya mbio za mwenge ambapo Wtz wengi huaminishwa kwamba eti mwenge unahamasisha maendeleo na kuibua miradi mipya. Wameenda mbali zaidi na kuongeza uongo mwingine eti kwa kumbiza mwenge umoja na uhuru wa Wtz unadumishwa, eti mwenge huo unachoma maadui, mbona haujawachoma wao ambao ni maadui namba moja wanaoongoza kuiba raslimali za watanzani tena mchana kweupe bila aibu, wangapi tunawajua ni waamishaji wakubwa wa pesa zetu na wezi wakuu wa wanyama bila kutaja madini na maeneo mengine, kwa nini mwenge hauwachomi hawa. Au wakisema maadui wanamaanisha wale wanaopinga wizi na ufisadi wao, wanaowasema na kuwazomea ndio maadui wao, hii inakera sana.
Hebu angalieni picha hizo hapo, hiki ni kibanda cha mabati kilichoitwa mradi wa mashine ya kusaga na kukoboa kama walivyodai wao. Kimefunguliwa tar. 01//10/2010 na kiongozi wa mbio za mwenge, sas hivi ni kichaka na makazi ya mbu na popo. Kibanda hiki kiko mkoa mpya wa Geita tena mjini na sio vijijini, ukitokea barenge njia ya kwenda kwa askofu kabla ya kufika kidaraja cha katundu mkono wa kulia utakiona hiki kibanda cha popo na mijusi kiko kwenye manyasi na bango kubwa mbele likisomeka "ASANTE KIKWETE POSHO MILL, MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA." Hii ni sehemu iliyo wazi kabisa, mkuu wa mkoa wa geita, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, na viongozi wote hupita maeneo haya, lazima wanapaona lakini si wameshakula chao likipanda hata likoza kwani la nini tena....
Kuna bango kwenye jiwe la msingi likinadi ufunguzi wa kibanda hiki cha popo kama mradi uliofunguliwa wakati wa mbio za mwenge 01/10/2010, leo tunamaliza mwaka 2012 na kibanda kiko kichakani na wala sina hakika kama kweli kimeorodheshwa kwenye asset za mkoa au ndo hivyo wameshajilipa kwa kun'goa mashine na kila kitu na kuuza, nani ajuaye....?? Mategemeo yangu yalikuwa kwamba round ya pili ya mwenge ingekuwa kutembelea miradi iliyofunguliwa na kuangalia maendeleo yake lakini badala yake nimesikia na mwaka huu eti wamefungua miradi mipya. Watanzania hivi kweli karne hii ni ya kutenga bajeti ya mabilioni ya pesa eti kuzunguka na mwenge nchi nzima, kwa faida gani hasa..?? Nakubali uanzishwaji wa mwenge wakati huo ulikuwa na mantiki katika kujenga umoja na kuonyesha ishara ya ushindi dhidi ya wakoloni na kuutangaza uhuru wetu. Je, hakuna museums tukaweka mwenge wetu wa uhuru kama kumbukumbu ya kihistoria tukaacha huu ujinga. Kumbuka kuwa hawataki kuuweka mwenge makumbusho kwa sababu ndo njia moja wapo rahisi ya kukomba pesa zisizo ratibiwa, wanakula tu huku wakitangaza miradi hewa bila aibu.
Nawaomba Watanzania kwa umoja wetu sote ebu tulikate hili jinamizi la mbio za mwenge lenye uvundo wa UFISADI uliokubuu. Walimu tunasema pesa ya kuwalipa stahili zao hazipo, madaktari tumewacheka eti wana tamaa japo sisi wananchi ndo tulitakiwa kuyadai yale waliokuwa wakiyalalamikia, shule zimekuwa magofu, dawa tunalishwa feki, hospitali pananuka usiseme, rushwa kila kona ya nchi, maisha kila siku double, ETI TUNAKIMBIZA MWENGE NA KUFUNGUA MIRADI HEWA.....!!!! Kila kukicha Mhesh. Yuko Kwa Obama anaomba asaidiwe net za mbu, SHAME ON HIM....!! Hakika hii laana Chama Cha Mabwepande (CCM) hata mfanyeje haiwabakizi lazima muanguke na kupasuka matumbo tu kabla ya kukanyagwa na kuzikwa, hopeless kabisa
Please let us "SAY NO" ebu tuwe wazalendo na uchungu na pesa zetu - zitutumikie basi, shida na changamoto ziwepo zile ambazo ni za lazima na sio hizi za watu wanaiba halafu kesho wanatutangazia majukwaan sisi masikini, sisi masikini......!!!
Nimekuwa nikijaribu kufuatilia kwa makini sana kuhusu mamia ya miradi ambayo huwa inafunguliwa kila kona ya nchi kipindi cha mbio za Mwenge ili kuona jinsi gani inasaidia kuwakwamua wananchi katika lindi hili la umasikini. Kila mwaka huwa tunashuhudia kwenye vyombo vya habari na wengine wetu huwa washiriki kabisa wa matukio mbalimbali ya mbio za mwenge ambapo Wtz wengi huaminishwa kwamba eti mwenge unahamasisha maendeleo na kuibua miradi mipya. Wameenda mbali zaidi na kuongeza uongo mwingine eti kwa kumbiza mwenge umoja na uhuru wa Wtz unadumishwa, eti mwenge huo unachoma maadui, mbona haujawachoma wao ambao ni maadui namba moja wanaoongoza kuiba raslimali za watanzani tena mchana kweupe bila aibu, wangapi tunawajua ni waamishaji wakubwa wa pesa zetu na wezi wakuu wa wanyama bila kutaja madini na maeneo mengine, kwa nini mwenge hauwachomi hawa. Au wakisema maadui wanamaanisha wale wanaopinga wizi na ufisadi wao, wanaowasema na kuwazomea ndio maadui wao, hii inakera sana.
Hebu angalieni picha hizo hapo, hiki ni kibanda cha mabati kilichoitwa mradi wa mashine ya kusaga na kukoboa kama walivyodai wao. Kimefunguliwa tar. 01//10/2010 na kiongozi wa mbio za mwenge, sas hivi ni kichaka na makazi ya mbu na popo. Kibanda hiki kiko mkoa mpya wa Geita tena mjini na sio vijijini, ukitokea barenge njia ya kwenda kwa askofu kabla ya kufika kidaraja cha katundu mkono wa kulia utakiona hiki kibanda cha popo na mijusi kiko kwenye manyasi na bango kubwa mbele likisomeka "ASANTE KIKWETE POSHO MILL, MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA." Hii ni sehemu iliyo wazi kabisa, mkuu wa mkoa wa geita, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, na viongozi wote hupita maeneo haya, lazima wanapaona lakini si wameshakula chao likipanda hata likoza kwani la nini tena....
Kuna bango kwenye jiwe la msingi likinadi ufunguzi wa kibanda hiki cha popo kama mradi uliofunguliwa wakati wa mbio za mwenge 01/10/2010, leo tunamaliza mwaka 2012 na kibanda kiko kichakani na wala sina hakika kama kweli kimeorodheshwa kwenye asset za mkoa au ndo hivyo wameshajilipa kwa kun'goa mashine na kila kitu na kuuza, nani ajuaye....?? Mategemeo yangu yalikuwa kwamba round ya pili ya mwenge ingekuwa kutembelea miradi iliyofunguliwa na kuangalia maendeleo yake lakini badala yake nimesikia na mwaka huu eti wamefungua miradi mipya. Watanzania hivi kweli karne hii ni ya kutenga bajeti ya mabilioni ya pesa eti kuzunguka na mwenge nchi nzima, kwa faida gani hasa..?? Nakubali uanzishwaji wa mwenge wakati huo ulikuwa na mantiki katika kujenga umoja na kuonyesha ishara ya ushindi dhidi ya wakoloni na kuutangaza uhuru wetu. Je, hakuna museums tukaweka mwenge wetu wa uhuru kama kumbukumbu ya kihistoria tukaacha huu ujinga. Kumbuka kuwa hawataki kuuweka mwenge makumbusho kwa sababu ndo njia moja wapo rahisi ya kukomba pesa zisizo ratibiwa, wanakula tu huku wakitangaza miradi hewa bila aibu.
Nawaomba Watanzania kwa umoja wetu sote ebu tulikate hili jinamizi la mbio za mwenge lenye uvundo wa UFISADI uliokubuu. Walimu tunasema pesa ya kuwalipa stahili zao hazipo, madaktari tumewacheka eti wana tamaa japo sisi wananchi ndo tulitakiwa kuyadai yale waliokuwa wakiyalalamikia, shule zimekuwa magofu, dawa tunalishwa feki, hospitali pananuka usiseme, rushwa kila kona ya nchi, maisha kila siku double, ETI TUNAKIMBIZA MWENGE NA KUFUNGUA MIRADI HEWA.....!!!! Kila kukicha Mhesh. Yuko Kwa Obama anaomba asaidiwe net za mbu, SHAME ON HIM....!! Hakika hii laana Chama Cha Mabwepande (CCM) hata mfanyeje haiwabakizi lazima muanguke na kupasuka matumbo tu kabla ya kukanyagwa na kuzikwa, hopeless kabisa
Please let us "SAY NO" ebu tuwe wazalendo na uchungu na pesa zetu - zitutumikie basi, shida na changamoto ziwepo zile ambazo ni za lazima na sio hizi za watu wanaiba halafu kesho wanatutangazia majukwaan sisi masikini, sisi masikini......!!!
Attachments
-
Asante Kikwete Posho Mill.jpg11.9 KB · Views: 46
-
Asante Kikwete Posho Mill1.jpg9.5 KB · Views: 83
-
Maisha Bora Kwa Kila Mtz.jpg11.4 KB · Views: 84
-
Asante Kikwete Posho Mill2 (2).jpg10.6 KB · Views: 45
-
Asante Kikwete Posho Mill2 (1).jpg13.3 KB · Views: 45
-
Taarifa ya Uzinduzi wa Mashine.jpg11.7 KB · Views: 58
-
Taarifa ya Uzinduzi.jpg17.4 KB · Views: 37