Miradi Mikubwa Iliyokamilishwa chini ya Uongozi wa Nyerere

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,037
23,827
Viongozi wa mwanzo wa Taifa la Tanzania kote Tanganyika na Zanzibar hawawezi kupuuzwa kuwa hawakuwa na moyo wa dhati kuanzisha miradi mikubwa iliyo na nia thabiti ya kunufaisha Watanzania.

Kwa leo mimi naanza na mradi wa reli ya TAZARA ambayo Mwalimu Nyerere na Abdulrahman Babu walipitia mitihani migumu ya 'nchi rafiki kama USA, RUSSIA, CANADA, IMF' kukataa kutoa msaada kwa ujenzi wa reli hiyo.

Lakini kutokana na mikakati na ufahamu mkubwa wa viongozi wetu, Mwl. Nyerere na waziri wake Abdulrahman Babu pamoja na Rais wa Zambia Kenneth Kaunda waliweza kuishawishi China ya Mao Dze Tung na Chou En Lai kufadhili ujenzi wa mradi huo mkubwa kabisa wa kihistoria.

Miradi mingine mikubwa iliyotekelezwa ni ya mabwawa ya nishati ya umeme n.k ambavyo mpaka leo tunavitumia. 'Sijui' viongozi wa sasa ni miradi gani mikubwa ya kutambulika iliyotekelezwa kuanzia mwaka 2000 itakumbukwa miaka 40 ijayo, yaani mwaka 2050?!

London School of Economics wanachambua ushirikiano wa China na nchi kama Tanzania na Zambia kipindi cha 'Cold War' Video clip http://www.youtube.com/watch?v=Z0IZV4cplDM&feature=related hii inatupatia historia ktk dakika 3:59 za changamoto kutoka kona mbalimbali za ulimwengu kujaribu kuhujumu mradi huo wa TAZARA hata kabla haujaanza ikiwemo South Africa chini ya utawala wa kibaguzi (apartheid).
 
That was then this is now.

Walifanya mambo yaliyondani ya wajibu wao kama viongozi hawastahili sifa hata kidogo.
Dr akiingia Surgery room na kufanya upasuaji hapati sifa ya ziada kwani hiyo ndiyo kazi yake.
Rais akianzisha mradi wa kitaifa wa kujenga barbara reli au sibitali sioni sababu ya kumjazia misifa kwani hiyo ndiyo kazi yake.

Viongozi tulionao sasa tofauti na wale wa zamani ni kwamba hawafanyi hata yale yanayoangukia katika utendaji wa kawaida.
Yale yanayoangukia katika utendaji wa kawaida ngazi ya juu kaa miradi mikubwa ya kitaifa ndo hasa yanayo kuwa chanzo cha ugomvi wetu na wao.
Miradi mikubwa ya kitaifa imejaa wizi na umalaya.Bado sioni haja ya kumpa kiongozi yeyote extra credit ntaendelea kuzishikilia na ikibidi nitazitumia kuwatimua ikulu waende hukohuko kwa Mabasha wao wakapashwe zaidi.
 

:coffee:

Kwa leo naomba NIJADILI kwanza MCHANGO WANGU KWENYE MIRADI YA TAIFA then labda hapo kesho nitachangia mchango wa hawa viongozi wa sasa kwenye miradi

Nimechangia asilimia kubwa ya miradi inayoendelea pamoja na kujaza matumbo ya mafisadi wasiokemewa na mkuu wa nchi, kupitia kodi ninayokatwa kila mwezi kwenye mshahara wangu wa mwezi
 
Ujenzi wa viwanda vingi nchi hii ulifanyika kipindi cha Mwalimu. mfano viwanda vya kahawa, pamba, korosho, nguo nk
 
Check bob mara zote anatumia, hazalish.

Lkn tuzingatie pia sera za kimataifa zinavoinfluence maendleo ya nchi zetu maskini. Km wa West walivopinga Reli, ndo yanaendlea. Badala ya kuweka mikakati aka MIKUKUTA na mifumo endelevu ya kiuchumi na huduma za jamii..tunasambaza consumerboz-vyandarua, vyakula vya misada na kondom. Hawa jamaa hawasapoti kuwekeza ktk viwanda wala mifumo ya kuuondoa umaskin. Km unauelewa MKUKUTA-MKUZA unanipata.

Km umezoea mipasho, maneno machaf na siasa za Sintofahamu... C u kwny topic km "Zuma na JK unawafananishaje"? Hahaha!
 
Ujenzi wa viwanda vingi nchi hii ulifanyika kipindi cha Mwalimu. mfano viwanda vya kahawa, pamba, korosho, nguo nk


Mwalimu alifanya mengi sana kwa Tanzania ukilinganisha na Marais wote waliomfuatia.
 
Miradi mikubwa ya awamu zilizofuata baada ya Mwl ni:
Ubinafsishaji wa mashirika ya umma,
Miradi ya Uchimbaji Madini,
Miradi kama RICHMOND/DOWANS,
Mradi wa Kusafirisha maji toka ziwa Victoria hadi Shinyanga etc.
 
Mradi mkubwa zaidi wa Mwalimu ulikuwa ni kuijenga TANZANIA na WATANZANIA. Mradi ambao sasa, kuliko wakati mwingine wowote unabomolewa kwa kasi ya ajabu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom