Elections 2010 Mipango ya CCM uchaguzi 2010!

tikotiko

Member
Jul 9, 2010
26
0
Wananchi wenzangu, wapiga kura, wapigiwa kura na wapigwa kura 2010. Kuna tetesi zimezagaa kwenye kitaa chetu hapa uswazi, na jamaa wananihakikishia kuwa wamepata nyeti kutoka White House zote mbili (Dodoma na Dar). Hivi ni tetesi tu au ndiyo ukweli? Wanadai hivi:-

  1. Eti CCM wamemnunua ZK na JK yupo tayari kumkabnidhi Wizara moja nyeti sana! Nasikia Chadema wamelitambua hilo na sasa kuna vikao vinaendelea chini kwa chini, ndiyo maana hata masuala ya kutangaza mgombea wao yamekuwa yakisuasua??
  2. Eti, JK tayari ameandaa timu yake ya ushindi, yeye, Shein, Nahodha (kuendelea na wadhifa wake) na Bilal (ingawa hakuwa chaguo lake, JK inasemekana alimuhakikishia Meghji kuwa running mate wake, then baada ya tishio la Bilal kujitoa wakabadili shilingi ghafla)?
  3. Eti kuna mgongano wa mawazo nani aje kumrithi JK 2015? Nasikia kuna kambi inataka kiti kiendelee kuwa bara, na anatajwa Dr Asha Rose Migiro kuwa mrithi wa JK; Wazenji wameapa kutoa mtu roho kwa hilo ndiyo maana JK na timu yake wakamlazimisha Shein aende Zanzibar miaka hii mitano, then 2015 anachukua nchi kama president na Dr Migiro kuwa VP na Bilal anachukua Zanzibar na kustaafia huko (by then atakuwa na 70 yrs…so atastaafu urais wa visiwani akiwa na 75 years na kumrithisha Vuai Nahodha)???.
  4. Eti ni kweli kwamba JK pia amekuwa akihangaika na kutafuta namna ya kumsafisha Lowassa na kumrejesha tena kwenye post kubwa…nasikia wanafikiria awe Foreign Affairs??
  5. Nasikia mojawapo ya ajenda zilizojiri kule Dodoma ni wana-CCM vijana wenye uwezo (wakiwemo mawaziri kadhaa) wameonyesha kukerwa na siasa za CCM kuwaacha wao na kuwajengea mazingira ya ushindi na ulaji wakongwe…hivyo kuwanyima wao nafasi hizo adimu?? Nasikia eti ilifikia baadhi ya mawaziri kuanza kujenga hoja za chini chini kumtisha JK?
  6. Eti ni kweli JK amepanga kumteua mwanawe (RJK) kuwa mbunge wa kuteuliwa kisha 2015 anapoondoka anapata uwaziri kutoka kwa Dr Shein ambaye ni mrithi wake ajaye??
  7. Kuna tetesi pia nimezisikia kwamba mdada Mmoja maarufu aliyechukua fomu kuwania ubunge jijini ametengenezewa mazingira na KIGOGO wa CCM na kwamba anaandaliwa kupata uwaziri ndani ya serikali ijayo?? Inasemekana tayari mbunge maarufu wa jimbo hilo amepigwa mkwara mzito na kuna hatihati akashindwa (kwa mipango) kwenye kura za maoni kama hatajiondoa mwenyewe? Kuna tetesi pia kwamba ameshauriwa akagombee jimbo mojawapo jipya jijini??

Je wenzangu mmezisikia tettesi hizi? Au uzushi tu wa kitaa?

Tikotiko taka tiko
 
Binfasi sijasikia mkuu,

Ila tt kwa CCM hakuna kisichowezekana!!
 
Nakubaliana na Mwanahaki. Lisemwalo huenda likawepo. Kuhusu ZK nareserve comments kwa sasa.
 
Zote ni nyepesi nyepesi tu. Hivi mmeshindwa nini kukitoa madarakani hiki chama?
 
Back
Top Bottom