Wana JF kwa kuzingatia yanayojiri kuhusu mipaka ya ziwa Nyasa kwamba wao wanadai kumiliki 100% ya ziwa naomba kwa wale wenye taarifa watupatie mipaka ya ziwa Tanganyika/Victoria. Katika maziwa hayo mipaka ipo wapi au tunamiliki wa % ngapi na hiyo mipaka iliwekwa kwenye mikataba ipi? Isijekuwa tunadanganyika na elimu ya geographia kuwa maziwa haya yapo Tanzania maana hata ziwa nyasa tulifundishwa lipo Tanzania kumbe ni ziwa la mgogoro tokea enzi ya Mwalimu.