Nimesoma na kushtushwa na habari ambazo zimeendelea kuripotiwa na gazeti la Nipashe, jana na hata leo { 03/08/ 2012} kuwa maeneo ya mpaka wa Tanzania huko mkoani Kagera yamevamiwa na wahamiaji haramu kutoka Nchi za jirani. Wametulia, hawana wasiwasi, wanafanya mambo yao kama vile wako kwao, na wanatii mamlaka ya Nchi wanazotoka!
Cha kushangaza, viongozi husika wanakiri udhaifu, wakiwamo wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama katika maeneo husika. Kwa nini bado wapo katika nafasi hizo?
Hii ni hatari, najiuliza kwa nini tunachezewa kiasi hiki? Viongozi hawaoni? Hili kweli ni jambo la kusubiri mpaka Waziri afanye ziara ndio aelezwe? Inakuwaje tunanunuliwa kwa bei rahisi kiasi hiki?
Napata wasiwasi inawezekana na maeneo mengine ya mipakani nayo yanavamiwa kwa ujinga kama huu na hakuna hatua zinazochuliwa.
Vita ya kumtoa Nduli Idi Amini ilikuwa ya nini kama hatuwezi kulinda mipaka yetu? Maybe alitumia mkakati mbaya, pengine badala ya kuvamia, angekuja na kitu kidogo akatoa rushwa angemegewa pande kubwa tu la ardhi.
Kwa nini Waingereza walipigana vita vya Falklands, maelfu ya km kutoka kwao? Kwa nini hawakuwaachia tu Argentina? Kama walipigana kwa eneo dogo la kisiwa,tena liko mbali, na kuna utata wa umiliki, je ukiwasogelea kwao inakuwaje? Kisiwa cha Migingo je? Mbona hao majirani zetu wanaovamia kwetu walitaka kutwangwana? Ni sisi tu ndio hatujui umihimu wa ardhi?
Viongozi, kaeni chini, chukueni hatua sasa. Mnapuuza viapo vyenu vya kuilinda na kuitetea JMT
Kama huwezi kuwa na viongozi wanaojali hili, ni bora waondoke mapema. Tusimlaumu Chief Mnagungo wa Msovero, kwa upeo na nyakati za kipindi kile:hakujua analolitenda. Wabaya zaidi ni hawa akina Mangungo wa leo, wanouza Nchi, wakijua wanachofanya, kwa vipande thelathini vya fedha!, Huu ni usaliti, na adhabu yao ni mbaya sana. Sitaki kuingia huko kwenye adhabu za wasaliti, lakini ni mbaya. Yaliyompata Yuda, yatufundishe.
Cha kushangaza, viongozi husika wanakiri udhaifu, wakiwamo wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama katika maeneo husika. Kwa nini bado wapo katika nafasi hizo?
Hii ni hatari, najiuliza kwa nini tunachezewa kiasi hiki? Viongozi hawaoni? Hili kweli ni jambo la kusubiri mpaka Waziri afanye ziara ndio aelezwe? Inakuwaje tunanunuliwa kwa bei rahisi kiasi hiki?
Napata wasiwasi inawezekana na maeneo mengine ya mipakani nayo yanavamiwa kwa ujinga kama huu na hakuna hatua zinazochuliwa.
Vita ya kumtoa Nduli Idi Amini ilikuwa ya nini kama hatuwezi kulinda mipaka yetu? Maybe alitumia mkakati mbaya, pengine badala ya kuvamia, angekuja na kitu kidogo akatoa rushwa angemegewa pande kubwa tu la ardhi.
Kwa nini Waingereza walipigana vita vya Falklands, maelfu ya km kutoka kwao? Kwa nini hawakuwaachia tu Argentina? Kama walipigana kwa eneo dogo la kisiwa,tena liko mbali, na kuna utata wa umiliki, je ukiwasogelea kwao inakuwaje? Kisiwa cha Migingo je? Mbona hao majirani zetu wanaovamia kwetu walitaka kutwangwana? Ni sisi tu ndio hatujui umihimu wa ardhi?
Viongozi, kaeni chini, chukueni hatua sasa. Mnapuuza viapo vyenu vya kuilinda na kuitetea JMT
Kama huwezi kuwa na viongozi wanaojali hili, ni bora waondoke mapema. Tusimlaumu Chief Mnagungo wa Msovero, kwa upeo na nyakati za kipindi kile:hakujua analolitenda. Wabaya zaidi ni hawa akina Mangungo wa leo, wanouza Nchi, wakijua wanachofanya, kwa vipande thelathini vya fedha!, Huu ni usaliti, na adhabu yao ni mbaya sana. Sitaki kuingia huko kwenye adhabu za wasaliti, lakini ni mbaya. Yaliyompata Yuda, yatufundishe.