Minister belittles link with JK's son

Jamani wadau naomba na mimi niingie jamvini nichangie huu mjadala,japo nawaomba mnielewe sana kwa tafakuri jadidi ya kile nitakachoeleza.
Kwanza kabisa nakuomba mkuu kubwa jinga utoe hiyo picha hapo,yaani picha uloitumia inayomwonesha lowasa hapo kwani true reflection yake inatafsiriwa kama defamation(slander) kwa huyo jamaa,usije ieletea jf matatizo bure.Labda ukitaka kukwepa liability tafuta kikatuni chake lakini sio pseudomatic photo kama hiyo.Anyway huu ni ushauri tu.

Pili,mimi nimebahatika kusoma na huyu bwana Ridhwani high school na pia university kwenye faculty moja huku tukifukuzana madarasa.Kuhusu ufisadi naomba niiri wazi kwamba kwa huyu kijana siujui,ila nachofahamu kwake ni kwamba ni mtu asiye na makuu anayeweza kuinteract na mtu yeyote yule.Hata alipokuwa mkwwa ni watu wachache sana waliojua ni mtoto wa jk waziri wa mambo ya nchi za nje.Tulijua tu kwa kuwa alikuwa anafanana naye na jina la ubini wake.Sote tulikula DH na hakutumia cheo chake.Ila cha ajabu wale waliojua ukweli kuhusu yeye walikuwa wanajitahidi kujipendekeza sana wakati yeye hana mpango.Sawa navyomjua wakati huo labda sio sasa kwani watu wanabadilika.

Kumbuka kuwa hata Mkapa naye alikuwa na sifa karibu hizi zote kabla hajaanza kufanya kazi ikulu.

Vivyo hivyo alipokuja mlimani kitivo cha sheria hakubadilika bado aliendelea kuwa social na mtu asiye mjivuni,kila mtu alimahamu na hadi alipewa ungozi kuwa mwenyekiti wa kitivo cha sheria kwa tiketi ya daruso.Kama kawaida cha ajbu hapa kuna watu walijikomba sana na kujitafutia sifa toka kwake lakini yeye hakujali,akiwamo rais wa daruso wa wakati huo aliyeamua kumpa uwaziri wa mambo ya nchi za nje wa daruso ili afanane na baba yake.Wakina beno malisa wanajua jinsi walivyohusiana na ridhwani.

Kuhusu uwezo wake kimasomo,si kweli kwamba alikuwa na uwezo mkubwa sana kama masha anavyodai.Alikuwa na uwezo wa kawaida tena naweza kusema ni wa chini,kwani supp alikuwa nazo kadhaa hivyo kufanya GPA yake isiwe ya kutisha sana.Hata hivyo kuefli mitihani au kuwa na uwezo fulani ni kitu cha kawaida tu kwa mwanafunzi kwani uwezo wa mtu hautegemei yeye ni mtoto wa nani.Nachojua mimi IMMA huchukua watu cream sana.Tena ukiomba internship pale mnapigwa hadi pepa ikiwa ni pamoja na wao kuomba matokeo toka kitivo cha sheria.Bahati nzuri niliwahi kuwa mjumbe wa bodi ya faculty inayopitisha matokeo hivyo suala la matokeo si geni kwangu.IMMA mara nyingi huchukua watu wenye first class na wakiwakosa sana sana watawachukua wenye upper second ya point 3.7 mwisho.Na wakikosa kabisa huchukua waganda kwani wao kiingereza kinawasaidia kuwaondosha watanzania kwenye kinyang'anyiro.Ridhwani hakuwa na first wala second class upper na wala kiingereza hajui sana tena alikuwa anababaisha tu hadi tunacheka kwenye vikao vya bodi.Hili nalo si tatizo kwani wengi pia hatujui,tunabwabwaja tu,lakini alichukuliwa IMMA.Vigezo walivyomchukulia wao wenyewe wanavijua na havikofixed wanaweza kuvubadili hivyo sitawaingilia sana huko.Sasa kama navyosema aliyejipendekeza hapa huenda ni hao jamaa lakini sio bwana mdogo,kwani wao huenda azma ya baba yake walikuwa wakiijua mapemaaaaaaa.

Hili swali la jinsi alivyoingia IMMA na jinsi alivyowapita wenzie ni kubwa lakini kwangu sio big deal sana hapa.

Kuhusu wanasheria jamaani,hapa mtajadili wee lakini tutajadili kitu ambacho hatukifahamu.Mwanasheria anaruhusiwa kumtetea mtu yeyote hata kama amekiri mbele yake kwamba kweli aliua na hata kama alimwona akiua ili mradi mwanasheria huyo hakuitwa kama shahidi mahakamani.Vilevile hata kama kampuni ni ya kifisadi au vinginevyo,bado ina haki ya kutetewa kisheria na kupata egal services zote,kwani izo huwa ni tuhuma zisizothibitishwa.Na kwa tanzania hatuna sheria inayomkataza wakili kumtetea au kuisajili kampuni yeyote ile,kwani kanuni ya kisheria inayotawala biashara inasema "buyer be ware" caveat emptor hivyo wewe unayeingia makataba na mwizi ndio unatakiwa kuwa makini,kwani kampuni kama richmond inapokuja tanzania,ni vigumu mwanasheria kujua itakuwa ya kitapeli au la,yeye anaisaidia usajili anapokea mkwanja wake basi mkataba na hiyo kampuni inaisha.Ni kazi ya wanasheria wa serikali kuchunguza mtu wanayeingia naye mkataba.

Hakuna makosa kwa wanasheria kutetea wauaji. Wanasheria wanakuwa na matatizo pale ambapo wao wanapokuwa wahusika wa crime (kumbuka wanasheria wa Nixon).

Hivyo basi sheria zinazotawala uwakili tanzania ni moja au mbili tu, ADVOCATES ACT na Tanganyika law society Act.Wanasheria wanabanwa na professional ethics ambazo kwa ufupi zinawakataza wasijitangaze,na ndio maana huoni matangazo yao redioni,au kwenye bill boards,wasiende kusolicit biashra yaani wasijipigie debe ama kupigiwa debe(tauting) wala wasiingie njama na mteja kumdhuru mteja mwingine (champerty) na vilevile kanuni kama vile kuvaa suti,joho kuheshimu mahakama n.k ndizo zinazowabana.Na mwisho na kubwa sana ni rule agaisnt conflict of interests. Kwa mana ya kwamba mwanasheria huwezi kuwatetea wateja wawili wanaopingana,huwezi leo ukaisajili richmond afu kesho ukawa unaishtaki au unahusika katika uchunguzi wake.Wala huwezi kutengeneza mkataba fulani halafu kesho wewe mwenyewe unakuwa wakili wa upande mwingine unaopinga makataba huo huo.Au kama masha huwezi kuwa waziri wa mambo ya ndani halafu idar yako ya polisi inaichunguza deep green ambayo wewe ulihusika kuisajili.Unatakiwa uachie ngazi kumoja ili uruhusu uchunguzi huru kwingine.

Kutokana na mwanga wa maelezo haya,sasa nadhani tunaweza kuona kuna upungufunupi katika sheria za mawakili na maadili yao,suala zima la ridhwani na mambo mengine yanayohusiana na sula hili,maswali maoni welcome

Hapa maswali machache tu yanatakiwa kujibiwa. Ni nini uhusika wa IMMA kwa Tangold na Deep Green? Kwa nini Kikwete hataki uchunguzi huru ufanyike?
 
So far so good. Ila tu tahadhari yetu ileile kwamba hakuna haja ya kuvalisha label; tujenge hoja. Sasa mtu akionekana anamtetea Masha asionekane aliwahi kushikwa mkono na Masha. Vilevile kwa yule anayempiga madongo asionekane anamchukia.

Kilichowazi hapa ni kwamba watu wengi, at least hapa JF, inaonekana wana imani na Masha na wangependa afanye kazi yake vizuri. Nami ni hivyohivyo, nafikiri kwamba katika viongozi tulio nao huyu bwana anaweza kutusaidia. Japokuwa yupo katika mazingira hatari katikati ya jalala la taka, bado ana nafasi ya kuweza kushinda majaribu na kuchapa kazi. Record yake ya huko nyuma ni clean sana: amepata elimu yake katika utaratibu sawia kabisa (sio kama wenzake walioamua kupitia shor cut), he is an intelligent chap, amefanya kazi zikaonekana, hana historia ya kuchipatia mali kwa njia ya mkato. Anachotakiwa sasa awe makini, achape kazi, acheze siasa ya kimaadili-hii itampa heshima sisi ambao tupo the other side of the political spectrum, tutampa heshima kama kiongozi wa nchi. Lakini kama mtindo wenyewe ndio utakuwa huu wa kuwatetea akina Ridhiwani unecessarily and out of context, I see tutakabana mashati.

Hope shule iliyotolewa kwenye hii thread itamfikia mheshimiwa Masha na wanasiasa wengine tunaowategemea katika CCM including Ezekiel Maige.

Kitila,

Najaribu kuamini kuwa Masha ni msafi! kama ni kweli basi aruhusu uchunguzi unaojitegemea wa Deep Green na Tangold ufanyike na wala asije na the old song ya usalama wa taifa hapa.
 
Masha hashabihiani na Lowasa hata chembe, EL kawajibika kwenye uwaziri mkuu. Ubunge wake uko palepale. Kumhusisha masha na wateja wa immma, niufinyu wa fikra,

Mhh kama huu ni ufinyu wa fikra basi naona mwenzangu una yako hapa na hizi name callings. Masha na Lowasa hawana tofauti yoyote ile kutokana na vigezo vyako kuwa kila aliyechaguliwa na wananchi ni mtu safi.

ukitizama profile za partner wake nikweli Masha hakuwa na ubavu na hakustahili kuwa msemaji. Inawezekana ulimi uliteleza tu, ndio kwanza anaanza kuwa mbele ya press. Kwani kampuni ya uwakili inawajibikaje kwa mteja wake?

Haya ya bot ni babies wa balali, mgonja, mramba na megji msitafute wachawi wapya.

Ukisema kuwa Masha hakuwa na ubavu au chochote katika IMMA unaweza kuwa na point. Kama ni kweli kwa nini basi uchunguzi huru usifanyike ili majibu ya Kikwete na Masha wanahusika vipi na Deep Green na Tangold yajibiwe na wao wasafishwe katika hili?
 
Mwafrika nadhani uchunguzi tayari unaendelea, sio DG pekee ni pamoja na makampuni mengine 21 yanayohusika bot na tayari findings zimeanza kutoka ikiwemo kupatikana 50bn na final report itatoka pia, au unamaana wachunguzwe wateja wa immma? kwani imma imekiuka ethics za uwakili? isitoshe sidhani kama nimjumbe nec au cc. Tuwa screen king players.
 
Mwafrika wa Kike Tawile,
NImeipenda sana hii mistari
"Au kama masha huwezi kuwa waziri wa mambo ya ndani halafu idar yako ya polisi inaichunguza deep green ambayo wewe ulihusika kuisajili.Unatakiwa uachie ngazi kumoja ili uruhusu uchunguzi huru kwingine."
 
Mwafrika nadhani uchunguzi tayari unaendelea, sio DG pekee ni pamoja na makampuni mengine 21 yanayohusika bot na tayari findings zimeanza kutoka ikiwemo kupatikana 50bn na final report itatoka pia, au unamaana wachunguzwe wateja wa immma? kwani imma imekiuka ethics za uwakili? isitoshe sidhani kama nimjumbe nec au cc. Tuwa screen king players.

Nadhani unachanganya mambo mawili hapa ambayo Kikwete anajaribu sana kuyaunganisha pamoja. Uchunguzi wa EPA ni tofauti na ule unaohusu Deep Green na Tangold. So far as longer as I know, ule wa Deep Green (ambao uko kwenye dosier ya Dr Slaa) bado haujaanza.

Serikali inajaribu kuufunika na huu wa EPA ili watu wasahau lakini baadhi yetu ambao hatuogopi watu wa usalama wa taifa tumeamua kuwa hii haitapotea kwenye matope hivi hivi/

Bado najiuliza swali kuhusu niliyoka kwenye Bold hapo kuwa IMMA haijakiuka ethics za uwakili. Hili ni sawa na kuuliza kuwa Lowasa alikiuka ethics gani pale aliposaidia serikali kuingia mkataba wa umeme? Kwa analogue yako basi hapo Tanzania hakuna fisadi hata mmoja si ndio?
 
Mwafrika wa Kike Tawile,
NImeipenda sana hii mistari
"Au kama masha huwezi kuwa waziri wa mambo ya ndani halafu idar yako ya polisi inaichunguza deep green ambayo wewe ulihusika kuisajili.Unatakiwa uachie ngazi kumoja ili uruhusu uchunguzi huru kwingine."

Mafuchila, usidhani kama Masha amewekwa kwa bahati mbaya kuwa waziri wa mambo ya ndani. Kuna alot kwenye uteuzi wake hapo na ukiunganisha na uteuzi wa Mujilizi (partner mwingine wa IMMA) kuwa jaji!
 
Mkulu FMES,

Ukimpelekea ujumbe Mhe. Masha kwamba aliteleza, tafadhali mweleze kwamba asilete madharau kwa watz. Siku hizi wana kaakili kiasi cha kutosha, akili zao zimehama hazipo tena visiginoni - kama watawala wengi wa kiafrika wanvyoamini; siku hizi ukiwaeleza jambo wanatafakari. Akisema jambo atafakari kidogo, ndipo asema! After all he is a lawyer by profession. Akumbuke mdomo uliponza kichwa.

Nawasilisha kwako MKUU!

 
Mkulu FMES,

Ukimpelekea ujumbe Mhe. Masha kwamba aliteleza, tafadhali mweleze kwamba asilete madharau kwa watz. Siku hizi wana kaakili kiasi cha kutosha, akili zao zimehama hazipo tena visiginoni - kama watawala wengi wa kiafrika wanvyoamini; siku hizi ukiwaeleza jambo wanatafakari. Akisema jambo atafakari kidogo, ndipo asema! After all he is a lawyer by profession. Akumbuke mdomo uliponza kichwa.

Nawasilisha kwako MKUU!

Na kisha akumbushwe pia kuwa wanaochambua habari zake na za mtoto wa Kikwete kuhusika na kampuni la kifisadi la IMMA sio kwamba wana chuki binafsi na hao wawili bali tu wanataka kujua kuwa Kikwete jr na Masha wanajua nini kuhusu wizi uliofanywa na Deep Green na Tangold kwa usaidizi wa IMMMA.
 
Haya ndiyo yanayokuingiza matatani Mkuu. Name dropping!!! Mtonye kimya kimya bila ya sisi wengine kujua.

Mkuu FM,

Huwa ninakuaminia kuwa ni kichwa, ila ninashangaa wewe kutoa hii kauli, mkuu kinachotufanya JF tuwe tofauti na forum zingine zote duniani, ni wanachama tulioko hapa, kwa kawaida hapa huwezi kumzungumzia kiongozi au mwananchi, halafu ikatokea hakuna asiyemfahamu hapa JF, na watu husema their first hand experience na the subject which makes the topic more interesting kwa wasomaji, na ndio maan huwa sina wasi wasi na kusema anytime ninachokijua first hand na siku zote huwa ninawaomba wengine waige, maana ndio hasa utamu wa mjadala mkuu,

Sasa nashangaa unaanza kunifundisha tabia ya uoga, yaani niogope kusema kwa sababu ya nini mkuu? Kuogopa maneno kutoka kwa nisiowajua na wasionijua ila wananihisi? OOH come on man, yaani wewe unaogopa wananchi wenzio kiasi hicho? Sasa kweli utaweza kumkoma nyani mkuu?

Sasa nisipokuambia nitamtonya utajuaje kuwa zimefika mkuu? Acha uoga mkuu, hapa ni taifa hatuogopi mtu wala watu, hoja hujibiwa kwa hoja, unachaojua unajua, unayemjua unamjua, hakuna anayeweza kuibadili hiyo hata kwa matusi kiasi gani mkuu, kwa hiyo ndio maana siogopi kusema mkuu, samahani kama imekukwaza kuwa nitamfikishia ujumbe, lakini hapa JF ni kawaida hiyo, acha uoga mkuu simamia taifa na unaowafahamu hapa bila kuogopa watu usiowajua na wasiokujua mkuu. Hebu pitia threads humu JF utaona watu wakikata ishus kwa kutumia first hand experience, majuzi tu Mkulu Mtanzania, alitupa elimu kuhusu siasa za Mbeya, anazozijua first hand hakuna ubishi wala hoja, Kiula alitajwa hapa, mkulu Kitla akatupa first hand anavyomjua toka jimbo lake kuwa ni bomu la kutupwa boom hakuna ubishi, ndio utamu wa mjadala mkuu, usiogope watu hapa, hakuuwi mtu, hapa ni hoja tu mkuu, kama una access na kiongozi sema mkuu unaweza kuwasaidia wengi hapa, kuliko kuogopa.

My point ilikuwa ni kuweka wazi kuwa Masha ni binadamu kama wewe na mimi, zile enzi za viongozi wetu kuwa kama alliens, kina Kingunge hakuna anayewajua au aliyesoma nao, wala kuishi nao na anayeweza kuwaongelea personal ziliisha, siku hizi viongozi ni sisi mkuu, yaani walalahoi, leo uko hapa kesho waziri, hakuna noma.

Ahsante mkuu.
 
Mkuu FM,

Huwa ninakuaminia kuwa ni kichwa, ila ninashangaa wewe kutoa hii kauli, mkuu kinachotufanya JF tuwe tofauti na forum zingine zote duniani, ni wanachama tulioko hapa, kwa kawaida hapa huwezi kumzungumzia kiongozi au mwananchi, halafu ikatokea hakuna asiyemfahamu hapa JF, na watu husema their first hand experience na the subject which makes the topic more interesting kwa wasomaji, na ndio maan huwa sina wasi wasi na kusema anytime ninachokijua first hand na siku zote huwa ninawaomba wengine waige, maana ndio hasa utamu wa mjadala mkuu,

Sasa nashangaa unaanza kunifundisha tabia ya uoga, yaani niogope kusema kwa sababu ya nini mkuu? Kuogopa maneno kutoka kwa nisiowajua na wasionijua ila wananihisi? OOH come on man, yaani wewe unaogopa wananchi wenzio kiasi hicho? Sasa kweli utaweza kumkoma nyani mkuu?

Sasa nisipokuambia nitamtonya utajuaje kuwa zimefika mkuu? Acha uoga mkuu, hapa ni taifa hatuogopi mtu wala watu, hoja hujibiw akwa hoja, uchaojua unajua, unayemjua unamjua, hakuna anayeweza kuibadili hiyo hata kwa matusi kisasi gani mkuu, kwa hiyo ndio maana siogopi kusema mkuu, samahani kama imekukwaza kuwa nitamfikishia ujumbe, lakini hapa JF ni kawaida hiyo, acha uoga mkuu simamia taifa na unaowafahamu hapa bila kuogopa watu usiowajua na wasiokujua mkuu.

Ahsante mkuu.



Mkuu Es duh!!! Mkuu naona this time watu wamehama kwa Mzee Malecela wamekukamata pengine . Ama kweli mwenye chake . Tuendelee ila ukweli ni kwamba watu wanataka viongozi safi . Jana umemtetea kazuka kwenda kufanya maajabu .Je tuseme alichanganyikiwa ? Na kama alichanganyikiwa kwa lipi na sababu ipi ? Kijana wa JK anaweza kuja hapa na huwa anakuja hapa mbona asiseme? Ila ana dharau kama za Baba yake .Aliwadharau wapiga kura wa kule Mwanza kwa kusema Mbunge alite foji vyeti yeye aendelee tu maana makelele ya mpangaji yaani wananchi na mwenye nyumba ni CCM na kesi ikafutwa ndiyo wanayo tuletea hapa mkuu.
 
Huyu Masha kama ni safi basi aruhusu uchunguzi huru wa kampuni ya IMMA na uhusika wake na Deep Green na Tangold. Kama atajaribu kushitaki gazeti la mwanahalisi basi ajue kuwa kutakuwa na jehanam hapo bongo.

Masha kama unajipenda kisiasa achana na gazeti la mwanahalisi kwani labda unaweza kuimaliza hii issue ya Deep Green kwa visingizio vya kuwa ni ya usalama wa taifa kama ambavyo mmekuwa mnafanya. Hili la kulishtaki gazeti la mwanahalisi naona mnakosea na mnataka kuanzisha vita nchini.
 
Huyu Masha kama ni safi basi aruhusu uchunguzi huru wa kampuni ya IMMA na uhusika wake na Deep Green na Tangold. Kama atajaribu kushitaki gazeti la mwanahalisi basi ajue kuwa kutakuwa na jehanam hapo bongo.

Masha kama unajipenda kisiasa achana na gazeti la mwanahalisi kwani labda unaweza kuimaliza hii issue ya Deep Green kwa visingizio vya kuwa ni ya usalama wa taifa kama ambavyo mmekuwa mnafanya. Hili la kulishtaki gazeti la mwanahalisi naona mnakosea na mnataka kuanzisha vita nchini.

Masha hawezi kwenda mahakaman yale ni manen ya jana kwenye Press .Masha ni mtoto wa mjini na hawezi kuwa na kiburi kuwazidi akina Chenge na kundi lao ambao wamenywea.Mzimu huu wa deepgreen ni mkubwa utawabana wote .Alijisemea tu si unajua serikali ya JK maneno majukwaani lakini kama kweli ni safi mwache aende aone ushahidi wa nguvu kama hawawezi kuadhirika . Masha hawezi kwenda kokote .
 
Malecela, has nothing to do na ishu hapa mkuu, here you are nilifikiri umekuja na mapya mkuu, vipi tena mzee si alishastaafu au naye ni IMMA? Sasa naona mkuu umeamua kuiharibu hii topic, kama unataka kuongelea Malecela, si ipo kule uliiianzisha wewe mwenyewe mkuu au? Ya maleecela huwa ni ya kwako lakini hayanisumbui mkuu.

Sijashikwa popote mkuu, mimi ni ex baharia sihitaji ufisadi, nina mali zangu za kunitosha nilizochuma baharini, ingawa ni ndogo, sina shida ya kuwa fisadi au kushirikiana na mafisadi, ili nipewe ufisadi, never mkuu.

Ridhiwani, kwangu ni bwana mdogo sana, ninajua kuwa ni clean kid lakini siwezi kumtetea sana maana viwanja vyangu ni tofauti kabisaa na vyake, kuhusu yeye kuja hapa mimi hilo sielewi maana sipo hapa kumzungumzia au kumtetea, mimi kwenye hii topic ninamtetea Masha, tena on a serious note, kwa sababu he is a friend.

Lakini so far sijaona strong evidence za kuwahukumu wote Masha na Ridhiwani. naomba ku-retire sasa kwa amani wakuu.

Anyways, nimesema ya kutosha naona it is about time nii-retire.
 
Masha hawezi kwenda mahakaman yale ni manen ya jana kwenye Press .Masha ni mtoto wa mjini na hawezi kuwa na kiburi kuwazidi akina Chenge na kundi lao ambao wamenywea.Mzimu huu wa deepgreen ni mkubwa utawabana wote .Alijisemea tu si unajua serikali ya JK maneno majukwaani lakini kama kweli ni safi mwache aende aone ushahidi wa nguvu kama hawawezi kuadhirika . Masha hawezi kwenda kokote .

Inaonekana kabisa kuwa si yeye wala IMMA wenye uwezo wa kwenda mahakani kwenye hili. Kwa nini basi wanapiga kelele na kumtisha Kubenea wa watu. Hii issue ya Deep Green tutaishikia bango na mpaka kitu kifanyike na wala wasidhani kuwa tutasahau. Hata kama miaka kumi au 20 itapita lakini siku moja tutapata nafasi yetu na wote waliohusika wao au watoto wao lazima wafikishwe kwenye sheria.

Masha na Kikwete mnaweza kuwa mnashinda kwa sasa kwa kuzuia uchunguzi wa Deep Green na Tangold lakini kumbukeni kuwa katika hili kuna watu hatutasahau na record zinatunzwa (kwa hiyo hata msidhani kuwa kutuma usalama wa taifa marekani au kupanga njama za "kudhibiti wakorofi" kama mwafrika wa kike zitasaidia).

Masha I double dare you au IMMA kwenda mahakani na kulishtaki gazeti la mwanahalisi.
 
Malecela, has nothing to do na ishu hapa mkuu, here you are nilifikiri umekuja na mapya mkuu, vipi tena mzee si alishastaafu au naye ni IMMA? Sasa naona mkuu umeamua kuiharibu hii topic, kama unataka kuongelea Malecela, si ipo kule uliiianzisha wewe mwenyewe mkuu au? Ya maleecela huwa ni ya kwako lakini hayanisumbui mkuu.

Sijashikwa popote mkuu, mimi ni ex baharia sihitaji ufisadi, nina mali zangu za kunitosha nilizochuma baharini, ingawa ni ndogo, sina shida ya kuwa fisadi au kushirikiana na mafisadi, ili nipewe ufisadi, never mkuu.

Ridhiwani, kwangu ni bwana mdogo sana, ninajua kuwa ni clean kid lakini siwezi kumtetea sana maana viwanja vyangu ni tofauti kabisaa na vyake, kuhusu yeye kuja hapa mimi hilo sielewi maana sipo hapa kumzungumzia au kumtetea, mimi kwenye hii topic ninamtetea Masha, tena on a serious note, kwa sababu he is a friend.

Lakini so far sijaona strong evidence za kuwahukumu wote Masha na Ridhiwani. naomba ku-retire sasa kwa amani wakuu.

Anyways, nimesema ya kutosha naona it is about time nii-retire.

Mkuu ni muhimu uwe unaprovide back-stoping kama hivi, usiweke kalamu chini mkuu, so far mjadala umenoga kwa vile tunapata kusikia kutoka pande zote za shilingi, sasa uki-retire na wewe una first hand experience, ndo tuseme utakuwa umekubali 'uoga uliofundishwa' hapo juu mkuu? Hapa ni kumkoma nyani, wengine tunafatilia kwa karibu, hatuandiki kwa sababu hatuna facts na hili mkuu, ndo unaona tunakula low profile, ila tunafollow up mkuu, so unless una dharura, hapa uwepo wako mkuu ni muhimu and appreciated!
 
Mkuu ni muhimu uwe unaprovide back-stoping kama hivi, usiweke kalamu chini mkuu, so far mjadala umenoga kwa vile tunapata kusikia kutoka pande zote za shilingi, sasa uki-retire na wewe una first hand experience, ndo tuseme utakuwa umekubali 'uoga uliofundishwa' hapo juu mkuu? Hapa ni kumkoma nyani, wengine tunafatilia kwa karibu, hatuandiki kwa sababu hatuna facts na hili mkuu, ndo unaona tunakula low profile, ila tunafollow up mkuu, so unless una dharura, hapa uwepo wako mkuu ni muhimu and appreciated!

NT,

Sidhani kama Mkulu FMES amegive up. The guy ana historia ya kusimamia anachoamini no matter what. Inabidi watu wamzoee FMES maana yeye akijua kitu huwa anatetea kwa nguvu zote na sio kwa sababu anapata kitu. Kuna thread ya kumpondoa Mbowe ilianzishwa hapa na FMES alisimama Kidete kumtetea Mbowe na akasema kila anachojua (na sidhani kuwa alipewa chochote na Mbowe).

Nadhani FMES atarudi tu hapa kuendelea na thread ila!
 
Malecela, has nothing to do na ishu hapa mkuu, here you are nilifikiri umekuja na mapya mkuu, vipi tena mzee si alishastaafu au naye ni IMMA? Sasa naona mkuu umeamua kuiharibu hii topic, kama unataka kuongelea Malecela, si ipo kule uliiianzisha wewe mwenyewe mkuu au? Ya maleecela huwa ni ya kwako lakini hayanisumbui mkuu.

Sijashikwa popote mkuu, mimi ni ex baharia sihitaji ufisadi, nina mali zangu za kunitosha nilizochuma baharini, ingawa ni ndogo, sina shida ya kuwa fisadi au kushirikiana na mafisadi, ili nipewe ufisadi, never mkuu.

Ridhiwani, kwangu ni bwana mdogo sana, ninajua kuwa ni clean kid lakini siwezi kumtetea sana maana viwanja vyangu ni tofauti kabisaa na vyake, kuhusu yeye kuja hapa mimi hilo sielewi maana sipo hapa kumzungumzia au kumtetea, mimi kwenye hii topic ninamtetea Masha, tena on a serious note, kwa sababu he is a friend.

Lakini so far sijaona strong evidence za kuwahukumu wote Masha na Ridhiwani. naomba ku-retire sasa kwa amani wakuu.

Anyways, nimesema ya kutosha naona it is about time nii-retire.

Mkuu naweka rekofi streiti kabisa kwamba kwa hili ngoma imepata mpigaji na si kwa ubaya .Nikakukumbusha jinsi unavyo simamia hoja na hasa zikiwa zinakugusa wewe ama washikaji zako .Nikatoa mfano wa Malecela ambaye miaka yote unasimama kidete kwake , then Kilango na leo Masha .Mbowe hajawahi kutetewa na ES .Mbowe amepondwa na ES miaka yote kias wanajuana namekuwa pamoja ila sasa mmoja yuko NY na mwingine Tanzania .Nadhani sasa umenielewa why I mentioned neno la Mwenyekiti mstaafu maana hana qualifications za kuwa waziri Mkuu mstaafu kwa kuwa hakumaliza miaka 5 kwa mujibu wa Sheria na aliye yasema haya ni mwanasheria wa Zenji .

Juu ya Masha na kijana mdogo wewe huwezi kuona kwa kuwa umesema yote unayo yajua juu yake lakini umeona yeye kakurupuka akidhani anazima issue kumbe kaweka mafuta sasa kwenda kwenye press na kusema mambo mengi.Hapo ndipo JF huwa wanataka kuendelea nakujau kulikoni.Kasema anafungua kesi sote tunangoja tuone amempeleka Kubenea huko Mahakamani aone nondo.Naanza kuingia wasi wasi juu ya vitisho juu ya Kubenea sasa na yeye ndiye waziri wa dhamani ya ulinzi kweli Kubenea atasalimika ? Maana ukisha kaa genge la wezi na kula nao hata kama hukuwa mwizi lazima hisia na wizi na matendo yataanza kukuingia .Masha kesha onja utamu .
 
Naona hii topic imeanza kuyumba kidogo... basi ni hivi.

. Lau Masha, Mujuluzi, Ishengoma, Magai... wajanja wa mjini. Kwanza wanafahamiana na JK long time. Ilikupata vi consultancy vya serikali firm nyingi huwaweka watoto wakubwa... Pale mkono yuko mtoto wa maghembe,step daughter wa Malecela, Rex walikua na mtoto wa Kimei, wengine wanakamata watoto wa Majaji n.k. Ndio bongo ilivyo. Yule JKjr ni mtu mmoja ambae yuko very weak kielimu, hajui hata kuongea in an articulate way. He really is nothing special kama mwanasheria au mwanafunzi. Jamaa walimrecruit zamani wakijua baba yake atakua Rais. Anaendesha BMW X5, which costs on average 60-70 million(used tena) (anatabia yakujifanya anaongea na simu all the time akiwa kwenye gari... which is funny)Ameanzaje kazi na kupata hela yakununua ile gari in one year??? Nnamfahamu jamaa mwengine yuko pale kama advocate.. JOse... hana hata prado....yuko senior kuliko huyo dogo. Jamaa hajui chochote kuhusu deep green, hilo dili la watu wazima wameshirikiana na IMMMA partners,kulicheza. mimi ni lawyer, yule dogo sio partner wala nini... tena aliletwa hk UK traineeship na partner firm moja inaitwa DLA Piper Rudnick Gray Cary UK LLP.

Wamempa x5,atese, wao wawena skio la mzee. maisha yanaendelea.
Watuwengi wasiokuwa na access yakirahisi ma muungwana wanawatumia watoto na watu wengine wakaribu kumpelekea proposals za madili,lakini in this case hawa jamaa wajanja wanajiwekea uhakika na rafiki yao aliye juu sana asije akawasahau.swala zima ndio hilo.Huyu sidhani kama anahusika na deep green,and even if he did, basi ni very initial stage.. lakini i doubt it.

http://www.immma.co.tz/index.html
 
Mkuu ustaafu ni marupu rupu sio maneno matupu, hata Maalim Seif ni mstaafu mkuu, huyo AG wa ZNZB haelewi anachosema, ninajibu kwa kuwa Mheshimiwa Mwafrika Wa Kike, ameniomba, yeyote aliyewahi kuwa waziri mkuu hupewa hata kama amefukuzwa, ,ni bunge tu linaweza kuamua tofauti.

Location yangu haijawahi kuhusika na mawazo yangu, ninajua ulipo lakini siwezi kusema hapa maana ni against the rules.

Hii hoja ni Masha na Ridhiwani, ukitaka mengine yafungulie topic,

naona umeanza kubadili majina yako mkuu, see yah!
 
Back
Top Bottom