Minister belittles link with JK's son

Mimi naona Mheshimiwa anaikuza ishu! Ile ni kampuni binafsi na it is nobody's business nani wanayemuajiri au kumpa upartner. Pamoja na kusema hivyo ni kuwafanya watanzania wapumbafu kudai kuwa nafasi za wazazi wa huyu kijana na yule dada hazikuingia kwenye mahesabu wakati wa kuwaajiri/kuwafanya partners! Wao kama wafanya biashara wangekuwa wajinga kutokufanya hivyo. Si kila kitu kinategemea performance, ni utaleta nini kwa kampuni. Kama kuwepo kwako kutawafungulia milango kwa nini wasikuajiri hata kama kuna wengine ni vichwa kuliko wewe? Ndiyo biashara, ndiyo ukweli. No shame in it! Sasa kama walitumia kuwepo kwa hao vijana kwa kujifaidisha baadaye, hilo ni suala lingine.
 
1. Mkuu Mugi, karibu tena baada ya kupotea sana na hili jina.

2. Masha, ni my brother in blood, uwaziri wake haumfanyi awe less of a human being, nimeishi naye New York, in the 90s, na nime-share naye apartment kabla ya mimi kuoa, familia yake ni yangu, yangu ni yake, kule Sengerema kwao mimi ni mwenyeji sana, kwa kwenye hili sio kwamba ninaongelea mpita njia, sasa siwezi kumkimbia kwa sababu ni waziri au nimchukie kwa sababu yeye sasa ni waziri na mimi sio, hapana kwenye maisha hivyo, rafiki ni rafiki.

3. Masha, kuzungumzia IMMA, akiwa waziri hilo ameteleza period, angewaachia IMMA wenyewe wajibu, kwenye hilo nimezungumza naye jana ni off the line, lakini haimfanyi awe fisadi au un-qualified kuwa waziri, lakini ni makosa.

4. Mimi sio fisadi na wala sina urafiki na mafisadi, lakini siko hapa kuwahukumu tu viongozi bila ukweli, Masha sio fisadi, amekuwa amekuwa director Oxygen akiwa na miaka 28, ambapo angeweza kufanya mambo mengi ya ajabu kama kweli ni fisadi, Masha sio mmiliki wa IMMA, the matter of fact yeye ni mmoja wa wale waliokuwa chini kwa kipato pale IMMA, kulinganisha na wenziwe, lakini kama kuna wenye ukweli wauweke hapa uchambuliwe, lakini so far sijaona convincing dataz, lakini walionazo waziweke hapa.

Ahsante Mkuu.

Field Marshall. Bravo mkubwa
I think people doesn't condemned Masha as a Fisadi. I said prior that i am still respect his resume. What i don't understand is why did he call the press meeting for something which doesn't affiliated with his job?

Mimi na wewe FM, we love hoja kwa hoja kind of game. Jee won't you rise suspecious about why did he came to public defending Ridhiwaani? He is not working for IMMA, he is not a public speaker for it neither. So, why does he defending him?

Jingine, jee uoni kuna umuhimu wa waandishi kudig more kwamba kulikuwa kuna any relationship prior to job appointment to Ridhiwani?
Mkuu FM our job is to keep public honest, since Hon. Masha get suspecious about the story, then i think we need to push more harder to find out if there is any thing that he don't want the public to know.

We just try to keep the public honest, that is our job.
 
Kwa kweli huo utetezi wake umenishtua. Jamaa inaonekana hakuwa makini kabisa kwa hilo.

Inawezekana pia ni shinikizo. Hilo anajua mwenyewe.

Lakini kwa nafasi aliyo naye kama waziri wa mambo ya ndani ya nchi sikutegemea kabisa maelezo kama hayo. Inaonekana bado hajakomaa na hana chembe uvumilivu.

Hivi hawa watu hawana washauri kweli. Hiyo wizara ni kubwa na nyeti kabisa, natumaini hawa watu wapo, ila kutokana na maslahi binafsi hawa viongozi wanawapuuza.

Haya, tuone kama tutafika.
 
1. Mkuu Mugi, karibu tena baada ya kupotea sana na hili jina.

2. Masha, ni my brother in blood, uwaziri wake haumfanyi awe less of a human being, nimeishi naye New York, in the 90s, na nime-share naye apartment kabla ya mimi kuoa, familia yake ni yangu, yangu ni yake, kule Sengerema kwao mimi ni mwenyeji sana, kwa kwenye hili sio kwamba ninaongelea mpita njia, sasa siwezi kumkimbia kwa sababu ni waziri au nimchukie kwa sababu yeye sasa ni waziri na mimi sio, hapana kwenye maisha hivyo, rafiki ni rafiki.

3. Masha, kuzungumzia IMMA, akiwa waziri hilo ameteleza period, angewaachia IMMA wenyewe wajibu, kwenye hilo nimezungumza naye jana ni off the line, lakini haimfanyi awe fisadi au un-qualified kuwa waziri, lakini ni makosa.

4. Mimi sio fisadi na wala sina urafiki na mafisadi, lakini siko hapa kuwahukumu tu viongozi bila ukweli, Masha sio fisadi, amekuwa amekuwa director Oxygen akiwa na miaka 28, ambapo angeweza kufanya mambo mengi ya ajabu kama kweli ni fisadi, Masha sio mmiliki wa IMMA, the matter of fact yeye ni mmoja wa wale waliokuwa chini kwa kipato pale IMMA, kulinganisha na wenziwe, lakini kama kuna wenye ukweli wauweke hapa uchambuliwe, lakini so far sijaona convincing dataz, lakini walionazo waziweke hapa.

Ahsante Mkuu.



Asante sana ES sasa umejibu kile ambacho huwa nakijua siku zote unapo amua kusimamia issue zako kidete kama hii . Majibu kwa wengi sasa yako nje why unakufa na kumlinda Masha.Ila kuishi naye na kuwa ndugu yako hakuwezi kumfanya asiwe fisadi kuanzia juzi .Maana yuko system na seikali ya kifisadi.Tuendelee .
 
1. Mkuu Mugi, karibu tena baada ya kupotea sana na hili jina.

2. Masha, ni my brother in blood, uwaziri wake haumfanyi awe less of a human being, nimeishi naye New York, in the 90s, na nime-share naye apartment kabla ya mimi kuoa, familia yake ni yangu, yangu ni yake, kule Sengerema kwao mimi ni mwenyeji sana, kwa kwenye hili sio kwamba ninaongelea mpita njia, sasa siwezi kumkimbia kwa sababu ni waziri au nimchukie kwa sababu yeye sasa ni waziri na mimi sio, hapana kwenye maisha hivyo, rafiki ni rafiki.

3. Masha, kuzungumzia IMMA, akiwa waziri hilo ameteleza period, angewaachia IMMA wenyewe wajibu, kwenye hilo nimezungumza naye jana ni off the line, lakini haimfanyi awe fisadi au un-qualified kuwa waziri, lakini ni makosa.

4. Mimi sio fisadi na wala sina urafiki na mafisadi, lakini siko hapa kuwahukumu tu viongozi bila ukweli, Masha sio fisadi, amekuwa amekuwa director Oxygen akiwa na miaka 28, ambapo angeweza kufanya mambo mengi ya ajabu kama kweli ni fisadi, Masha sio mmiliki wa IMMA, the matter of fact yeye ni mmoja wa wale waliokuwa chini kwa kipato pale IMMA, kulinganisha na wenziwe, lakini kama kuna wenye ukweli wauweke hapa uchambuliwe, lakini so far sijaona convincing dataz, lakini walionazo waziweke hapa.

Ahsante Mkuu.

Heshima mbele mkuu! Hapo umekata mzizi wa fitna
 
this guy(Masha)is a joke. According to my knowledge and understanding ya siasa za Bongo, kuchaguliwa kuwa minister si kwamba he has something extra to offer, Karamagi,Mapuri,Meghji etc are the living examples of useless public servants!!

Kuizungumzia IMMA akiwa waziri ni makosa, lakini haimfanyi awe a joke, uwaziri wake umetokana na kushiriki kwenye kundi lililoshinda uchaguzi, lile kundi lingeshindwa asingekuwa waziri.

Tanzania oxygen aliyoiongoza ilikufa kifo kibaya sana!!

Oxygen ilikufa kutokana na makosa ya kukimbilia Stock Exchange bila mipangilio ya kutosha, na Masha hakuwepo alikuwa ameshaondoka tayari, I lost my money too kule exchange.

In conclusion ni kuwa, his position in the government is indeed imekuwa boosted na uhusiano wake na wakuu behind the scene!!Kuendelea kwake kukataa ni kututhibitishia kuwa kuwa ana akili timamu!! Wo would admit this kind of a thing in a million yrs!!

?????????????????????????
 
Mkuu Babah,

Heshima mbele, hii haijakaa sawa, mengine sina uhakika,

1. Masha, alishwahi kuwa Secretary wa Shirika la Oxygen, na baadye akawa director wake, kama kweli ni fisadi basi tungesikia toka akiwa huko ufisadi wake.

2. Amekuwa waziri mdogo wa Nishati, nafikiri hapo ndipo tungemsikia kwenye Richimonduli, lakini Mwakyembe hakumgusa kabisaa meaning kuwa yuko safi.

3. Toka awe waziri kamili wa ndani, hata mwezi hajamaliza, sasa hizi tuhuma zako mkuu mbona nzito sana na hazilingani na Masha kabisaa mkuu.

4. Huko IMMA, ninakubaliana naye kuwa huwa wanaajiri wanafunzi mbali mbali, ninawafahamu wengi waliowahi kuajiriwa hapo ambao baba zao wala sio wakubwa wa nchi.

Ninaomba niseme hivi, Masha ni kijana mdogo sana mwenye shule ya kutosha, na pia ameonyesha uwezo wa kuongoza na ni kichwa pia, maana kijana ana Masters ya sheria ya Georgetown DC, na anayo Bar ya sheria ya New York ambayo hata mtoto wa JFK ilimshinda aliirudia mara tatu lakini huyu kijana Masha aliifanya mara moja tu, hivyo angeweza kubaki huko na kuwa Lawyer mkali na kuishi maisha mazuri kuliko anayoishi sasa, lakini akaamua kurudi nyumbani kulijenga taifa lake,

I mean sina uhakika na base ya mashambulizi yako kwake, lakini nina wasi wasi kuwa humtendei haki kabisa mkuu, I know the kid bro inasikitisha sana kuona kijana mchapa kazi na muadilifu kama huyu, akishambuliwa namna hiii, huku ripoti ya Mwakyembe ikiwashika mpaka katibu wa Nishati, lakini yeye waziri mdogo akiachiwa bila ya kuguswa kabisaa, ninasema mara nyingi kuwa viongozi wazuri na wadilifu tunawafahamu, na mafisadi pia tunawajua, tusiowajua habari zao ziwekwe kwa uwazi na ukweli,

Unless, kuna habari zingine zaidi za ubaya wa Masha, kwa kweli mkuu hizi charges zina walakini mkuu, kulingana na hukumu nzito ulizomhukumu hapo juu, kwamba ati ni mwizi au amepewa kazi kwa kujuana, kwenye hayo naomba kutofautiana na wewe mkuu, Masha ni mbunge wa Nyamagana, uwezo wa uongozi anao maana amekuwa kiongozi akiwa na umri mdogo sana, na hata sasa bado ni kijana mdogo sana, na anaonyesha kuwa atatusadia sana kitaifa na mawazo yake ya kimaendeleo na hasa sera za ki-capitalism, ambazo anaoneakan kuzi-master sana, kwa hiyo mkuu tumpe tu nafasi atuongoze na akosolewe pale akikosea.

Ahsante Mkuu.

Mkuu wewee ni ''Fidelis Masha'' na sio Field Marshal....how can u and ur friend judge BabaH ktk spelingiiiiiiiiiii!!!??Wewe ni mtz au mJK? Nadhani tunahitaji kuwa waangalifu ktk masilahi ya watz yanapopewa wakati wa kuyadiscuss.Hukumtendea haki kila mtz kwa kumkaripia BabaH na sio kudisolve the story na kutoa dukuduku lako huku ukiweka data kama ulivyokuwa unahitaji yeye aweke data!! Nadhani tujitahidi kutokuwa mamluki..Humu wanakuja mpaka watuhumiwa wenyewe kusoma habari hizi na wanakosa la kujitetea,kaka kama huna data kama BabaH tulia kwani habari kaileta yeye !! Masha amefanya na anaendelea kufanya mabaya mengi tu na ndio sababu ana tofauti za kiitikadi na baba yake!! TUWE WATETEZI ZAIDI,HATA KAMA MASHA AMEKUNYANYUA AU ANAKUNYANYUA STAY CALM BEFORE WE GET TO U!
 
Mkuu wewee ni ''Fidelis Masha'' na sio Field Marshal....how can u and ur friend judge BabaH ktk spelingiiiiiiiiiii!!!??Wewe ni mtz au mJK? Nadhani tunahitaji kuwa waangalifu ktk masilahi ya watz yanapopewa wakati wa kuyadiscuss.Hukumtendea haki kila mtz kwa kumkaripia BabaH na sio kudisolve the story na kutoa dukuduku lako huku ukiweka data kama ulivyokuwa unahitaji yeye aweke data!! Nadhani tujitahidi kutokuwa mamluki..Humu wanakuja mpaka watuhumiwa wenyewe kusoma habari hizi na wanakosa la kujitetea,kaka kama huna data kama BabaH tulia kwani habari kaileta yeye !! Masha amefanya na anaendelea kufanya mabaya mengi tu na ndio sababu ana tofauti za kiitikadi na baba yake!! TUWE WATETEZI ZAIDI,HATA KAMA MASHA AMEKUNYANYUA AU ANAKUNYANYUA STAY CALM BEFORE WE GET TO U!

ES amesha sikia na amesha sema wazi kwamba hatetei Nchi tena bali anamtetea Masha mshikaji na ndugu yake Nchi tunaitetea sisi .Hujamwelewa ?kesha sema toka huko nyuma .Turudi kwenye hoja let's not be derailed .
 
Mkuu wewee ni ''Fidelis Masha'' na sio Field Marshal....how can u and ur friend judge BabaH ktk spelingiiiiiiiiiii!!!??Wewe ni mtz au mJK? Nadhani tunahitaji kuwa waangalifu ktk masilahi ya watz yanapopewa wakati wa kuyadiscuss.Hukumtendea haki kila mtz kwa kumkaripia BabaH na sio kudisolve the story na kutoa dukuduku lako huku ukiweka data kama ulivyokuwa unahitaji yeye aweke data!! Nadhani tujitahidi kutokuwa mamluki..Humu wanakuja mpaka watuhumiwa wenyewe kusoma habari hizi na wanakosa la kujitetea,kaka kama huna data kama BabaH tulia kwani habari kaileta yeye !! Masha amefanya na anaendelea kufanya mabaya mengi tu na ndio sababu ana tofauti za kiitikadi na baba yake!! TUWE WATETEZI ZAIDI,HATA KAMA MASHA AMEKUNYANYUA AU ANAKUNYANYUA STAY CALM BEFORE WE GET TO U!

Mkuu Kifo,

Heshima yako mkuu, hakuna aliyemtukana mtoa mada, unless kama wewe ni yeye, Masha kama waziri hawezi kuwa msemaji wa IMMA, otherwise siamini kuwa hoja zako zinatokana na kutonyanyuliwa na viongozi, Masha anafanya mazuri mengi kwa taifa na hasa alipokuwa Nishati, kama una ukweli uweke hapa, in the future weka dataz mkuu sio personal attacks hazina nafasi hapa.
 
Mkuu Babah,

Heshima mbele, hii haijakaa sawa, mengine sina uhakika,

1. Masha, alishwahi kuwa Secretary wa Shirika la Oxygen, na baadye akawa director wake, kama kweli ni fisadi basi tungesikia toka akiwa huko ufisadi wake.

2. Amekuwa waziri mdogo wa Nishati, nafikiri hapo ndipo tungemsikia kwenye Richimonduli, lakini Mwakyembe hakumgusa kabisaa meaning kuwa yuko safi.

........I know the kid bro inasikitisha sana kuona kijana mchapa kazi na muadilifu kama huyu, akishambuliwa namna hiii...........

Ni Zipi Sifa Za Masha??
Field Marshall ES,

Mimi sikubaliani kabisa na wewe jinsi ulivyowatetea vijana Masha na Ridhwani. Ushahidi wa kimazingira upo waziwazi na huu ni muhimu sana katika kutafuta ushahidi halisi wa kumtia mtu korokoroni.

  1. 1. Kusema kuwa Ridhiwani alifanya vema kuliko wanafunsi wengine kuwa ndio kigezo cha kumwajiri ni upuuzi mtupu, kwani Ridhiwani sio sawa na watoto wengine, ana special status kama mtoto wa Raisi mtarajiwa tokea 1995. Kwa hiyo unless watuonyeshe hicho alichofanya cha ziada kuliko wengine otherwise factor kubwa ya ajira yake itaunganishwa zaidi na status yake.
  2. 2. Kwa Masha kupewa uwaziri wowote achilia mbali huo wa mambo ya ndani bila kuangalia jinsi anavyohusiana na JK hapo awali ni kutaka kujidanganya. Wapo watu wengi waliopo bungeni na wenye digrii bora zaidi lakini sio mawaziri. Zaidi ya hayo CV ya kijana Masha ni ndogo sana kwa yeye kupanda hatua haraka haraka hadi waziri wa wizara nyeti kama Mambo ya Ndani.
  3. 3. Zaidi ya hayo, sio yeye tu kutokea IMMA aliyezawadiwa, partner mwenzake Mujulizi, yeye alipewa ujaji wa mahakama kuu. Hii inaonyesha wazi kabisa upendeleo kwa wakurugenzi wa kampuni ya IMMA. Mimi sasa hivi sina imani na kesi yoyote ile itakayopitia kwa Mujulizi, hata kama ni mtaalamu mzuri wa sheria.
  4. 4. Deep Green Finance ilisaidiwa na IMMA kusajiliwa kabla tu ya uchaguzi 2005 na baadaye ikafilisiwa mara tu baada ya JK kuchaguliwa. Kibaya zaidi ni kuwa IMMA hao hao inasemekana ndio walipewa mamlaka ya kuifilisi hiyo Deep Green Finance. Sijui inakuwaje wao wawe wanasheria wao na pia liquidator wao.
  5. 5. Halafu pia kuna kutoeleweka kwa Deep Green Finace kuanzishwa wakati JK alipokuwa anahitaji pesa kwa ajili ya uchguzi, 2005 halafu ikafa mara tu baada ya JK kuwa raisi, 2006, wakati ikiwa mikononi mwa wale aliowazawadia vyeo serikalini.
  6. 6. Kwa Masha kutokutajwa kwenye ripoti ya Richimonduli sio kigezo cha kusema kuwa yeye ni safi, maana hata suala la Richimonduli halijachunguzwa kiundani na kumalizika. Repoti ya Mwakyembe imetengeneza tu misingi wa uchunguzi zaidi.
  7. 7. Ukiangalia hata CV tu ya Masha na kulinganisha na hata ile tu ya msaidizi wake, Balozi Kagasheki, utaona wazi kabisa kuwa kuna upendeleo uliofanyika. Masha hajawahi hata kufanya kazi serikalini kabla ya kuteuliwa uwaziri. Kwa hiyo hata mambo ya civil servant atakuwa anajifunzia ofisini. Hata baadhi ya ajira alizoshika ni questionable e.g. (1997 anaanzisha kampuni yake ya IMMA then wakati huo huo 1997 akapewa TOL, u-Company Secretary na u-Managing Director hapo hapo, what was the plan here, what was going on? From no where to MD??. Ukweli ni kuwa Masha amebebwa kuwa alipo na hii ni kwa vile tu kua kwa JK maslahi binafsi huwa yanazidi utaifa wetu.
  8. 8. Masha pia sio msomi kuliko wengineo waliopo bungeni. Kama elimu ingekuwa ndio kigezo basi akina Mh. Mwakyembe wenye elimu na mzoefu zaidi kuliko Masha wangetakiwa wawe Mawaziri kama tunataka utendaji bora. Alichobahatisha Masha ni kusomea sekondari US baba yake alipokuwa amepewa ulaji huko hivyo akajua kimombo kwa ufasaha, lakini zaidi ya hapo wapo wengi aliomaliza nao UDSM walio na GPA nzuri zaidi kuliko yake, lakini none of them ni mawaziri.
  9. 9. Kwa hiyo hii ina maana kuwa JK na IMMA ni almost parters kwenye mikakati yao before and after uraisi. Unless mtu aamue kwa makusudi mazima kufumbia macho kilichofanyika IMMA, otherwise ni wazi kabisa kuwa kuna special relationship kati ya the Kikwetes na IMMA, i.e.
  • Ridhiwani aajiriwa IMMA ---->
  • IMMA yaunda Deep Green Finace----->
  • Deep Green yalamba Sh8 bilioni ------>
  • JK achaguliwa kwa kishindo huku pesa ikimwagwa kila mahali ----->
  • IMMA Direcotrs wapewa kazi na JK, mmoja waziri mwingine Jaji ------->
  • Deep Green yafunga virago bila kuulizwa pesa za BOT walipozipele
ka pesa za BOT walipozipeleka.

There is definitely more than what eyes can see. Mheshimiwa Masha tunaomba maelezo.
 
Masha hana njaa ya hela kazaliwa kwao zipo, kusema ni kijana mh huo upara je si wautu uzima kweli! huyu ni mkomavu wa uongozi na anastahiki kuwepo alipo. Kwenye vikao vya madiwani hupenda kumwita wakili masha, ni mtu mkweli makini na mahiri.

Ushauri wangu kwake awaachie maPR kujibu hoja uchwara, yeye achape kazi tu, tunajua anakazi kubwa ya kuandaa vitambulisho vya kitaifa.

Sijamsikia Bill Gates akisema ametosheka na pesa, alikadhalika wanaufalme wa Saudia na hata wa Brunei. Masha na familia yake wana kiasi gani kuliko hao ambao kila kukicha wanafanya madudud kuongezea kikubwa zaidi ya walichonacho?
 


Kwanini huyu Waziri aende kufanya press conference ya kumtetea Ridhiwni, wakati kubeana anatafutwa kutolewa roho lakini hajafanya press conference ya kumlinda?.
watu wanatishiwa maisha waziri hazungumzi, leo Ridhiwani kasemwa tu na gazeti, waziri kaja juu na anataka kulifikisha gazeti mahakamani!!!!

Mimi nafikiri kama kweli JF tupo focused, hili ni swali la msingi ambao Masha au surrogates wake ni lazima walijibu. It seems like huyu kijana mwenzetu bado hajaweza ku-internalise vizuri kazi za wizara ya mambo ya ndani au naye ameamua kufanya business as usual, CCM style-ambao cheo ni muhimu kuliko kazi yenyewe inayoambatana na hicho cheo
 
Masha fisadi...i seriously doubt it,did he get the post as fadhila,i seriously think so.
Huko nyuma wakati wa mchakato,kabla ya kupata mgombea urais,mmoja wa wakurugenzi wa IMMA alikuwa akishalewa pale Rose Garden alikuwa mara nyingi akisikika akisema kuwa yeye atakuwa Gavana wa benki kuu na Masha atakuwa waziri wa sheria,haya sio maneno ya mjini,mimi mwenyewe nimeshuhudia hilo.Na kwa bahati mbaya au nzuri,sio yeye aliyepata cheo chochote kati ya viwili walivyopewa wakurugenzi wa IMMA.
 
Mkuu ninajua siku nyingi wewe ni nani, nafikiri umegundua kuwa huwa ninajiepusha na ishu zako, kushikwa mkono? Kwa hiyo wewe shida yako kumbe ni kushikwa mkono?

Eti wewe uliomba kazi IMMA na Ridhiwani? Jamani mambo mengine mumuoogope mungu.

Relation ipi hiyo na wakati nimeshasema wazi uhusiano wangu na waziri, na ninarudia kuwa kosa alilofanya ni kuiongelea IMMA as waziri tu, otherwise sioni ufisadi wake ni nini?

Na kama kweli una dataz na unajua unaousema ni ukweli against Masha, mbona sasa unanianza kuniingia personal mimi badala ya ku-stick na topic yako on Masha? Mimi ninaamini sana kamati ya Mwakyembe, maana imemuondoa mpaka waziri mkuu na mawaziri wawili na bado wengine wanakuja, kama haikumuona waziri mdogo wa nishati Masha, kuwa na makosa siwezi kuja hapa kuyapika, hoja hujibiwa kwa hoja mkuu!
 
Quote: Kubwajinga

Ushahidi wa kimazingira upo waziwazi


Ushahidi wa mazingara unamfanya Masha, awe fisadi kwa hiyo mkuu kelele zote hizi ni ushaidi ma kimazingara?

Maneno uliyosema ni mengi lakini yanaonyesha only one thing kuwa umeenda shule, maana yamepangwa kielimu, lakini hana anything serious zaidi ya msemo wako mwenyewe, yaaani ushaidi wa kimazingira, labda tuendelee kusubiri ushahidi wa kweli utakuja baadaye, so far bado haupo hapa, ila nilichokiona ni ushahidi mwingi wa chuki za binafsi na wivu hauwezi kutusaidia wabongo jamani, tuache hizo.
 
Somo:Unapokuwa mtoto wa Rais kumbe taabu sana hasa katika enzi hizi za "where we talk openly"
 
Ushahidi wa mazingara unamfanya Masha, awe fisadi kwa hiyo mkuu kelele zote hizi ni ushaidi ma kimazingara?

Maneno uliyosema ni mengi lakini yanaonyesha only one thing kuwa umeenda shule, maana yamepangwa kielimu, lakini hana anything serious zaidi ya msemo wako mwenyewe, yaaani ushaidi wa kimazingira, labda tuendelee kusubiri ushahidi wa kweli utakuja baadaye, so far bado haupo hapa, ila nilichokiona ni ushahidi mwingi wa chuki za binafsi na wivu hauwezi kutusaidia wabongo jamani, tuache hizo.

FMES,
Ushahidi uliopo wa kimazingira ni overwhelming. Kama ingekuwa ni kesi mahakamani ungeweza kunapata ushindi bila wasiwasi. La kufahamu hapa ni kuwa, kiongozi sio lazima ahukumiwe mahakamani na tangible evidence ndio uwezo wake kuhudumia jamii ikiwa inamuamini uwe bado intact, bali colaborative evidence ni chumvi tosha ya kumfanya asiaminike na hivyo kutakiwa kuachia ngazi.

Kwa mtirirko wa mambo kati ya Deep Green, ambao tayari inajulikana kuwa ni fisadi, na IMMA ambao baadhi yao walikuwa ni wamiliki wa Deep Green, inawafanya wahusika nao wawe na harufu ya ufisadi kama sio kwamba ni mafisadi tayari, mpaka hapo watakapotoa maelezo ya kueleweka yatakayowasafisha na sio kubrashi tu kama alivyofanya Bw. Masha. Kwetu sisi Masha hana tena sifa za kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani mpaka mambo ya Deep Green yatakaponyooka, just like Lowassa vs Richimonduli.
 
Nina maswali mawili ya ziada kwa wenye details:

1. Kwa wale waliosoma habari iliyo kwenye gazeti la MwanaHalisi, news hiyo ilimtaja Mh. Masha kiasi kwamba akajikuta analazimika kuitisha Press Conference ili kuongelea hilo swala?

2. Kila press conference huwa ina agenda rasmi, je, agenda rasmi ya press conference ya Mh. Waziri ilikuwa ni hiyo news ya MwanaHalisi au alikuwa na mambo mengine na hivyo hilo swala la defence ya Ridhiwan ilikuja kwenye maswala ya nyongeza (mengineyo)?

Kama majibu ya maswali hayo hapo ni NDIYO, basi ninapata walakini mkubwa sana. Kijana anaweza kuwa ameanza kazi ya uwaziri kamili vibaya na hivyo anatakiwa kuwa makini. Tanzania ya leo imeharibika tutamchokonoa hapa mpaka atalipuka na akilipuka atafanya maajabu makubwa zaidi na hivyo kutoa mwanya wa kumuweka kwenye darubini kwa umakini mkubwa zaidi.

Kwa wale walio karibu nae kama Mzee/Komandoo/FMES wanatakiwa wampe ushauri ili asije akajizamisha kwenye matope. Zama hizi ni chafu na hazifai hata kidogo, watu wanawindana usiku na mchana ili kutia mchanga kitumbua. Dirty politics anazifahamu sana na si ajabu alikuwa kwenye mtandao, zama za mtandao zimeisha maana mtandao wenyewe umesambaratika, sasa hivi kila mtu ni adui yako maana hujui atakugeuka saa ngapi!
 
Nina maswali mawili ya ziada kwa wenye details:

1. Kwa wale waliosoma habari iliyo kwenye gazeti la MwanaHalisi, news hiyo ilimtaja Mh. Masha kiasi kwamba akajikuta analazimika kuitisha Press Conference ili kuongelea hilo swala?

2. Kila press conference huwa ina agenda rasmi, je, agenda rasmi ya press conference ya Mh. Waziri ilikuwa ni hiyo news ya MwanaHalisi au alikuwa na mambo mengine na hivyo hilo swala la defence ya Ridhiwan ilikuja kwenye maswala ya nyongeza (mengineyo)?

Kama majibu ya maswali hayo hapo ni NDIYO, basi ninapata walakini mkubwa sana. Kijana anaweza kuwa ameanza kazi ya uwaziri kamili vibaya na hivyo anatakiwa kuwa makini. Tanzania ya leo imeharibika tutamchokonoa hapa mpaka atalipuka na akilipuka atafanya maajabu makubwa zaidi na hivyo kutoa mwanya wa kumuweka kwenye darubini kwa umakini mkubwa zaidi.

Kwa wale walio karibu nae kama Mzee/Komandoo/FMES wanatakiwa wampe ushauri ili asije akajizamisha kwenye matope. Zama hizi ni chafu na hazifai hata kidogo, watu wanawindana usiku na mchana ili kutia mchanga kitumbua. Dirty politics anazifahamu sana na si ajabu alikuwa kwenye mtandao, zama za mtandao zimeisha maana mtandao wenyewe umesambaratika, sasa hivi kila mtu ni adui yako maana hujui atakugeuka saa ngapi!

Keil,

Nina hakika kabisa kuwa maswali muhimu yakiulizwa hapa hii issue itakuwa kubwa. Kuna mambo mawili yanasumbua akili yangu katika hii story. Kuhusika kwa IMMA kwenye utendaji kazi wa Deep Green pamoja na wezi wenzao wa Tangold.

Kuna kitu kinafichwa ambacho tunajaribu kukipata ila so far jamaa wanatuzidi ujanja kwa kusingizia kuwa hili suala ni la usalama wa taifa. Sasa Masha akianza kuita press conference kwenye hili ajue kabisa kuwa anafungua the whole new front.

BTW, nilizani hii topic ilitolewa kwenye siasa as if sio siasa. Naona inazidi kuja hapa na sasa mimi nimekamata pop corn na kama kawaida nasubiria part two ya movie....

tic tak tic tak tic tak tic tak......
 
JK anaweka safu mpya katika utumishi wa umma, ukiangalia karibu wabunge wote wa ccm waliochini ya miaka 45 walioenda shule kidogo wamepata uwaziri mfano ngereja, maige, dr.devid, malima, dr.mwinyi, dr.nchimbi, hawa ghasia, dr.buriani, masha.

mh.Masha kuwa waziri sio issue ya kujadiri ni stahiki yake, dr.matayo david ni mtaalamu wa kilimo na ndiko aliko. Ukitizama vizuri JK amechukua mawaziri wawili kila mkoa, sasa mwanza ukimtoa ngereja, masha na Diallo mbunge gani anafaa kuwa waziri?

Suala la mtoto wa JK nidogo sana kuzungumzwa na waziri wa mambo ya ndani. Hii issue angeweza kuisemea Stella Ndikimi tu, isitoshe huyu kijana ana shahada ya sheria mlitaka akaajiriwe wapi?
 
Back
Top Bottom