Mimi na CUF Dam dam: Rais Karume

Junius

JF-Expert Member
Mar 11, 2009
3,181
139
ZANZIBAR haiwezi kujengwa bila ya kuwepo umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi na ushiriki wa viongozi wa Chama Cha CUF katika shughuli za miradi ya maendeleo ni mafanikio ya umoja huo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Amani Abeid Karume aliyasema hayo katika ufunguzi wa skuli mpya ya Mjini Kiuyu Shehia ya Kiuyu Minungwini katika Mkoa wa Kaskazini Pemba ambapo viongozi mbalimbali wa chama na serikali walihudhuria wakiwemo viongozi wa chama cha CUF.

Katika hotuba yake aliyoitoa katika sherehe hiyo, Rais Karume alisema kuwa yeye mwenye binafsi amefarajika kuona ushiriki wa viongozi wa Chama Cha CUF katika sherehe hizo na kusisitiza kuwa huo ndio umoja na mshikamano ambao unajenga amani, utulivu na upendo na kuahidi kuusimamia.

Alisema kuwa Wazanzibari wote ni wamoja hivyo kuna kila sababu ya kuishi kwa upendo na maelewano hatua ambayo itaipeleka mbali Zanzbar katika kuimarisha uchumi wake na miradi yake ya maendeleo sanjari na uimarishaji wa amani na utulivu.

“Sisi Wazanzibari wote ni wamoja na wala wasitokee watu wakatudanganya tukajigawa na ili uwe Mzanzibari ni lazima utokee Unguja ama Pemba na hata ingekuwa si wamoja kwani ingekuwa vibaya kuungana, mbona leo Ulaya wameungana na kuunda (EU) ambapo ni nchi nyingi na watu wake ni wengi na wanaongea lugha tofauti”,alisisitiza Rais Karume...

Source: Zanzibar yetu web blog
 
woe to the presidental post aspirants...Msakatonge na wenzako mpo?
 
hawa wanasiasa wa visiwani nuru imewaangazia......... wanushinda uroho wa madaraka na tamaa ya kuhodhi vyeo....... wanaanza kuwa tayari kshirikiana na kuongoza kwa pamoja.... hongereni sana.........kwa ujasiri wa kuwapuuza akina JK, wangewapotezea muda wenu tu na siasa za kukumbatia ufisadi wakati huko kwenu hakuna hata cha kufisidi.............
 
Ni mtazamo finyu nani ameshindwa?? CCM au CUF usilete dharau kaka bali imetumika hekima baada ya kuona zanzibar inateketea

Pole sana mdonoaji kama nimekukwaza, nafikiri ( na huu ni mtazamo tu) umeshindwa kuufikiri huu msemo kwa mapana zaidi, ukitaka niseme nani mshindi kati ya CUF na CCM, well wote ni washindwa na mshindi hapa ni WAZZNZIBAR! naamini bado unakumbuka asili ya mgogoro wa zanzibar ilikuwa ni kutokubaliana kwa vyama hivyo viwili Zanzibar, na hasa chanzo cha lkutokubaliana ni kila chama kuangalia maslahi yake zaidi kuliko maslahi ya zanzibar. So hoja yangu ni kuwa mvutano ulikuwa kati ya maslahi ya wanasiasa na maslahi ya wazanzibar, sasa baada ya wanasiasa (CUF na CCM) kuona kuwa Maslahi yao hayawezi shinda maslahi ya WAZANZIBAR ndio hapo walipoona kumbe masikio hayawezi shinda kichwa, ni bora waungane kuangalia maslahi ya wazanzibar na ndio maana nikasema "kama huwezi washinda ungana nao" I was just thinking aloud!
 
Back
Top Bottom