Mimi kama mimi NAIPONGEZA CHADEMA

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Dr Slaa, baada ya kuona kideo yake nimefarijika sana ,na kuona sasa CDM imeanza kupevuka na kuondoa woga ,kwamba inakaribia kuwa ngangari kinoma ,hili kwa sasa sina shaka nalo na ndivyo itakiwavyo.Zile mishe za kusemea bungeni hazina mshiko na zinazimika kama taa ya mshumaa.

Dr Slaa ameweka wazi kuwa usalama wa Taifa uko nyuma ya hujuma wanazozitegemea nakumbuka ni namna gani CUF walivuka stage hii ,kiasi walifika kusema ikianguka sindano ndani ya ikulu basi habari inafika kwenye ofisi za CUF mida hiyohiyo.

Sasa naona Intelijensia za CDM zipo na zinazidi kutupasha ,kuna wakati CUF ilitoboa siri ya hawahawa usalama wa Taifa na habari iilitobolewa kwenye mkutano wa hadhara ,walitajwa washiriki mpaka vespa muda na wakati na yaliyozungumzwa ndani ,ikafika kusemwa kuwa mashushu wa CUF ni hatari na wanatisha kwa jinsi wanavyo pata habari nyeti.

Sina zaidi ni kuwapa hongera viongozi wa CDM kwa kuonyesha moyo wa kishujaa na mnapopata habari kama mlizozitangaza ni bora pia mkazipeleka kwenye balozi za nchi za nje na ofisi ya UN ambazo zipo hapo DSM.

Siasa si ugonvi ni hoja na madongo.
Mimi kama mimi naipongeza Chadema je wewe unangojea nini?
 
Back
Top Bottom