Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Napenda kukiri wazi kwamba nina tabia ya ajabu sana katika mahusiano yangu na mama Ngina. Sijui niite ni ila mbaya au ni udhaifu au ujinga.
Katika maisha yangu na mke wangu tangu tuoane, nimekuwa nikifanya mambo kinyume na matarajio yake, pale anapotarajia jibu la hapana huwa ninasema ndiyo, na pale anapotarajia jibu la ndiyo mimi nasema hapana.
Kwa mfano, mke wangu anaweza kuniomba tufuatane kwenye mwaliko wa sherehe fulani ambayo amealikwa, mimi naweza kukataa kuandamana naye nikidai nina kazi nyingi za kufanya hapo nyumbani, anaweza kunibembeleza, na mimi nikakataa katakata, lakini akishajiandaa na kutaka kutoka namuomba anisubiri tuandamane. Wakati akiwa ameshikwa na butwaa, mimi nabadilisha nguo haraka haraka na kuongozana naye.
Mfano mwingine, inatokea tunataka kufanya jambo fulani, yeye anaweza kuja na maoni yake mazuri tu, na akayajengea hoja mpaka nikaelewa, lakini kutokana na kupenda kwangu kutofautiana naye, naweza kupinga wazo lake na kujenga nadharia yangu ya kufikirika na kwa sababu hapendi kubishana na mimi anakubali wazo langu. Lakini wakati wa utekelezaji, nafuata ushauri wake kama alivyotaka, basi huwa anabaki ananishangaa.
Amekuwa hanielewi na anawaeleza hata rafiki zake kuwa mimi ni mtu nisiyeeleweka kabisa, lakini ndio keshanizoea mumewe kimeo..................!
Katika maisha yangu na mke wangu tangu tuoane, nimekuwa nikifanya mambo kinyume na matarajio yake, pale anapotarajia jibu la hapana huwa ninasema ndiyo, na pale anapotarajia jibu la ndiyo mimi nasema hapana.
Kwa mfano, mke wangu anaweza kuniomba tufuatane kwenye mwaliko wa sherehe fulani ambayo amealikwa, mimi naweza kukataa kuandamana naye nikidai nina kazi nyingi za kufanya hapo nyumbani, anaweza kunibembeleza, na mimi nikakataa katakata, lakini akishajiandaa na kutaka kutoka namuomba anisubiri tuandamane. Wakati akiwa ameshikwa na butwaa, mimi nabadilisha nguo haraka haraka na kuongozana naye.
Mfano mwingine, inatokea tunataka kufanya jambo fulani, yeye anaweza kuja na maoni yake mazuri tu, na akayajengea hoja mpaka nikaelewa, lakini kutokana na kupenda kwangu kutofautiana naye, naweza kupinga wazo lake na kujenga nadharia yangu ya kufikirika na kwa sababu hapendi kubishana na mimi anakubali wazo langu. Lakini wakati wa utekelezaji, nafuata ushauri wake kama alivyotaka, basi huwa anabaki ananishangaa.
Amekuwa hanielewi na anawaeleza hata rafiki zake kuwa mimi ni mtu nisiyeeleweka kabisa, lakini ndio keshanizoea mumewe kimeo..................!