TWIZAMALLYA
JF-Expert Member
- Oct 1, 2011
- 397
- 81
Nimesikia uchambuzi wa magazeti asubuhi ya leo kupitia MAGIC FM,gazeti la uhuru wameandika kuwa Milya alikuwa ni mzigo kwa ccm na kwamba alikuwa ni mmoja wa magamba yaliyokuwa yanategemewa kujivua.Kama Milya alikuwa ni mtu wa karibu sana na Mheshimiwa Lowasa mpaka akawa anajulikana kama mtu wa Lowasa na hapa CCm wanadiriki kusema waziwazi kuwa Milya alikuwa ni mmoja wa magamba yaliyokuwa yanategemewa kujivua,je hii kauli inamaanisha nini kwa Mheshimiwa Lowasa?.Je ni kweli kuwa Lowasa Ni Gamba ndani ya CCM?.