Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,570
Mazishi ya Tanzania top most celeb, Stephen Kanumba, yamegharimu Shilingi za Kitanzania, Milioni 60 kasoro 2!.
Kwa mujibu wa taarifa ya M/Kiti wa kamati ya mazishi, Mtitu, gharama halisi za mazishi hayo ni Shilingi milioni 58!.
Kusema ukweli, hizi sii fedha nyingi ukilinganisha na mambo makubwa yaliyofanyika, lakini pia kwa nchi masikini kama Tanzania, na hali halisi ya maisha ya baba yake mzazi Kanumba, Mzee Charles Kanumba anayoishi pale kijijini TBC ilipomtembelea, fedha hizi sii fedha ndogo!.
Natamani kamati itoe mchanganua wa matumizi hayo ili kuondoa dhana kufa kufaana, tusije kuta service providers za huduma zote pale msibani, ni hao hao wasanii wenyewe, na sio tuu wame imflate gharama halisi ili kuvuta cha juu, bali wanaweza kabisa kuwa wamefanya usanii mpaka kwenye msiba wa msanii mwenzao kwa kujilipa wenyewe fedha pesa ndefu na kutuletea hesabu za kisanii pia!.
Usikute hata zile suti nyeusi, hesabu ni mumo humo!.
Usikute hata yale matangazo live hesabu ni mumo humo!
Usikute zile fulani tuliombiwa zinagawiwa bure lakini watu tukauziwa, hesabu ni mumo humo!.
Usikute ile line up ndefu ya wasanii ambao wange perform nao hesabu ni mumo humo! etc, etc!
Hatuna tatizo na huduma zozote kulipiwa malipo halali kwa huduma iliyotakiwa, ila tuna tatizo kama huduma hizo zilitolewa at inflated rates, ikiwemo watu baki kuvaa suti msiba wa Kanumba ili hali kuna uwezekano mkubwa Baba mzazi alipata homa ya ghafla kwa kuogopa atavaa nini mbele ya kadamnasi ya watu kwenye msiba wa mwanae!
Ukiondoa hayo, kamati hiyo inastahili kupewa sifa kwa kufanikisha mazishi ya huyu Tz. No. 1 Celeb, Stephen Kanumba "The Great", ambayo yamechukua nafasi ya pili kwa umaarufu ukiondoa msiba wa Baba wa Taifa.
Wito: Kuvunjwa kwa Kamati kusiwe ndio mwisho wa usaidizi wao kwa mpendwa wao, wajipange kusaidiana na wazazi kuanzisha "Kanumba The Great Memorial Foundation" ili fedha zinazotokana na kazi zake, ziingie kwenye hiyo foundation ili angalau wazazi wa Kanumba wote wawili, waishi maisha yanayo reflect hazina ya utajiri mtoto wao aliyoiacha humu duniani, vinginevyo ni ma distributor (wadosi) ndio watakaofaidika na jasho la Kanumba, huku Mzee Charles Kanumba akiendelea kuishi maisha ya mwanakijiji wa kawaida wa Tanzania kule kijijini!.
Hongereni Kamati!
Rip SK The Great!.
Pasco!.
Kwa mujibu wa taarifa ya M/Kiti wa kamati ya mazishi, Mtitu, gharama halisi za mazishi hayo ni Shilingi milioni 58!.
Kusema ukweli, hizi sii fedha nyingi ukilinganisha na mambo makubwa yaliyofanyika, lakini pia kwa nchi masikini kama Tanzania, na hali halisi ya maisha ya baba yake mzazi Kanumba, Mzee Charles Kanumba anayoishi pale kijijini TBC ilipomtembelea, fedha hizi sii fedha ndogo!.
Natamani kamati itoe mchanganua wa matumizi hayo ili kuondoa dhana kufa kufaana, tusije kuta service providers za huduma zote pale msibani, ni hao hao wasanii wenyewe, na sio tuu wame imflate gharama halisi ili kuvuta cha juu, bali wanaweza kabisa kuwa wamefanya usanii mpaka kwenye msiba wa msanii mwenzao kwa kujilipa wenyewe fedha pesa ndefu na kutuletea hesabu za kisanii pia!.
Usikute hata zile suti nyeusi, hesabu ni mumo humo!.
Usikute hata yale matangazo live hesabu ni mumo humo!
Usikute zile fulani tuliombiwa zinagawiwa bure lakini watu tukauziwa, hesabu ni mumo humo!.
Usikute ile line up ndefu ya wasanii ambao wange perform nao hesabu ni mumo humo! etc, etc!
Hatuna tatizo na huduma zozote kulipiwa malipo halali kwa huduma iliyotakiwa, ila tuna tatizo kama huduma hizo zilitolewa at inflated rates, ikiwemo watu baki kuvaa suti msiba wa Kanumba ili hali kuna uwezekano mkubwa Baba mzazi alipata homa ya ghafla kwa kuogopa atavaa nini mbele ya kadamnasi ya watu kwenye msiba wa mwanae!
Ukiondoa hayo, kamati hiyo inastahili kupewa sifa kwa kufanikisha mazishi ya huyu Tz. No. 1 Celeb, Stephen Kanumba "The Great", ambayo yamechukua nafasi ya pili kwa umaarufu ukiondoa msiba wa Baba wa Taifa.
Wito: Kuvunjwa kwa Kamati kusiwe ndio mwisho wa usaidizi wao kwa mpendwa wao, wajipange kusaidiana na wazazi kuanzisha "Kanumba The Great Memorial Foundation" ili fedha zinazotokana na kazi zake, ziingie kwenye hiyo foundation ili angalau wazazi wa Kanumba wote wawili, waishi maisha yanayo reflect hazina ya utajiri mtoto wao aliyoiacha humu duniani, vinginevyo ni ma distributor (wadosi) ndio watakaofaidika na jasho la Kanumba, huku Mzee Charles Kanumba akiendelea kuishi maisha ya mwanakijiji wa kawaida wa Tanzania kule kijijini!.
Hongereni Kamati!
Rip SK The Great!.
Pasco!.