Milion 3 biashara gani naweza kufanya?

Biashara ya duka la Dawa Baridi inalipa sana kama utapata mtalaam wa kukushauri, ingawa kwa sasa naona sheria zimekuwa ngumu but unaweza ukaanza kujua procedures lakini naona inalipa ..... ntawailiana na jamaa yangu mmoja ni mfamasia wa mkoa fulani anipe vigezo then ntakuwasilisha hapa jamvini lakini hii ni hadi kesho!!
 
hivi kwa joto la dar, ng'ombe wa maziwa ni biashara inalipa au ni ile kujisikia tu kuwa nimefuga ng'ombe wa maziwa? maana ngombe wa maziwa kwa ukweli wanastawi sana maeneo ya baridi.

Mkuu ng'ombe wa maziwa wanalipa sana hapa dar kuliko unavyodhania. can u belive wahindi wanafuga ng'ombe wa maziwa posta na kariakoo tena magorofani?.

Mama derek kwa songea sina uzoefu nako sana ila nasikia pande hizo mbuzi katoliki wanalipa, mafuso yanakuja huko kusomba kwa wingi,
pia boda boda zinalipa sana mikoani sijui hesabu yenu huko ni ngapi
 
Mama D Kuna P3 kwenye biashara yeyote tarajiwa ili ufanikiwe!
P1 Product;
Bidhaa gani unataka kuuza! mf huwezi ukaanzisha biashara ya kuuza kiti moto kati ya jamii ya kiislamu au biashara ya kuuza magari kati ya maskini...
P2 Place
chagua eneo muafaka kwa biashara husika usihamehame wala kubadilibadili aina ya biashara, pia uwepo kwenye biashara siku na wakati wote ili wateja wawe na uhakika wa kupata huduma....
P3 Publicity
Matangazo kwamba una bidhaa gani na iko wapi ni muhimu sana sana. Weka bango wafahamishe jamii wewe binafsi au kwa njia yeyote Unauza nini
NB Jumla ya pesa ya mauzo uelewe kwamba sio FAIDA Uelewe ukifuga ng'ombe aidha upate maziwa ukose nyama au upate nyama ukose maziwa huwezi ukapata nyama wakati huo maziwa!
Haiwezekani!
 
Biashara ya duka la Dawa Baridi inalipa sana kama utapata mtalaam wa kukushauri, ingawa kwa sasa naona sheria zimekuwa ngumu but unaweza ukaanza kujua procedures lakini naona inalipa ..... ntawailiana na jamaa yangu mmoja ni mfamasia wa mkoa fulani anipe vigezo then ntakuwasilisha hapa jamvini lakini hii ni hadi kesho!!

nashkuru sana baba ubaya kwa ushirikiano wako.nasubir ayo majibu io kesho.thanx again
 
Mkuu ng'ombe wa maziwa wanalipa sana hapa dar kuliko unavyodhania. can u belive wahindi wanafuga ng'ombe wa maziwa posta na kariakoo tena magorofani?.

Mama derek kwa songea sina uzoefu nako sana ila nasikia pande hizo mbuzi katoliki wanalipa, mafuso yanakuja huko kusomba kwa wingi,
pia boda boda zinalipa sana mikoani sijui hesabu yenu huko ni ngapi
yeah uku mbuzi katoliki ni wengi kilo ni 3500 tu.i think ata hii ni biashara nzur ila inahitaji space ya kutosha.
Kwa bodaboda hesabu yao ni 7000 kwa cku ila inabd kupata mtu mwaminifu sn,weng wao huwa hawalet hela cku zote,sbb kibao kila cku
 
Mama D Kuna P3 kwenye biashara yeyote tarajiwa ili ufanikiwe!
P1 Product;
Bidhaa gani unataka kuuza! mf huwezi ukaanzisha biashara ya kuuza kiti moto kati ya jamii ya kiislamu au biashara ya kuuza magari kati ya maskini...
P2 Place
chagua eneo muafaka kwa biashara husika usihamehame wala kubadilibadili aina ya biashara, pia uwepo kwenye biashara siku na wakati wote ili wateja wawe na uhakika wa kupata huduma....
P3 Publicity
Matangazo kwamba una bidhaa gani na iko wapi ni muhimu sana sana. Weka bango wafahamishe jamii wewe binafsi au kwa njia yeyote Unauza nini
NB Jumla ya pesa ya mauzo uelewe kwamba sio FAIDA Uelewe ukifuga ng'ombe aidha upate maziwa ukose nyama au upate nyama ukose maziwa huwezi ukapata nyama wakati huo maziwa!
Haiwezekani!

thanx alot kwa mawazo yako ntayafanyia kazi mgeni
 
yeah uku mbuzi katoliki ni wengi kilo ni 3500 tu.i think ata hii ni biashara nzur ila inahitaji space ya kutosha.
Kwa bodaboda hesabu yao ni 7000 kwa cku ila inabd kupata mtu mwaminifu sn,weng wao huwa hawalet hela cku zote,sbb kibao kila cku

mama derick ...watu wengi wanakua sio waaminifu pale wanapokua na wasiwasi na future yao kwani hofu ni kwamba unaweza kubadili mawazo...lakini unapokua na mkataba na mtu wa boda boda na kum guarantee piki piki itakua yake baada ya muda fulani kama mkuu mdizi alivyo tuambia kwenye post yake ya biahara ya boda boda basi ataitunza piki piki na hesabu ataleta...angalizo...nunua boda boda mpya...ukizingatia sasa hivi inakuja sheria ngumu sana ya TBS kuhusu Piki piki...ukiwahi ukafanya vizuri ni watu wachache wata monopolize hii biashara kwani mtaani hakutakua na mapiki piki mengi hovyo hovyo yasiyo na viwango kama ilivyo sasa..unaweza weka kijana mmoja kama moderator wa biashara... na biashara ikamlipa yeye kwa kufuatilia malipo...wape a/c no. yako hivyo kila jumamosi warudishe piki piki... halafu wakileta bank slip ya hesabu ndio unamrudishia piki piki
 
Mama Derick..... Swali lako linakuwa gumu in so far watu hatujui market ya hapo ulipo....., kuna mtu kasema duka la madawa (je hapo ulipo yapo mangapi, je suppliers watakuwa wapi, je competition ni kubwa au watu wanapendelea miti shamba kuliko hizo dawa?) hapo meaning yangu ni kwamba inategemea na soko...., mfano biashara ya kiti moto huenda ikawa nzuri Dar na isilipe Dubai..., au huwezi ukafanya biashara ya kuuza Ice kwa eskimos...,

Kwahiyo kila biashara inalipa kama kuna soko, unasource ya product nzuri, na unaweza ukauza sawa au chini ya competition na bado ukapata faida, kwahiyo cha maana angalia kitu ambacho hakipo hapo... (if there is a need, then there is an opportunity)..., kuna mtu kasema matunda na mboga mboga, kama hapo hazipo angalia kama unaweza ukazipata nje ya mkoa na kuzileta hapo ulipo ili uuze. Je kuna biashara yoyote hapo ambayo mtu anafanya lakini wewe unaweza kuifanya bora...., (mfano saloon ya kusuka au kinyozi, unaweza ukawa unaleta products chache kutoka dar, ukipata msusi mzuri watu watakuja), au unaweza ukawa mfugaji..,

Je una skills zozote, mfano mapishi (unaweza ukapika keki) na kuzisambaza kwenye maduka na kuuzia watu. In short hapa utaona biashara yoyote unaweza ukafanya, na kufanikiwa kwako sio kwa sababu fulani na yeye amefanikiwa ni management yako, anything you do can work better or worse kutokana na commitment sio sababu biashara fulani ni nzuri na nyingine ni mbaya.

Kwahiyo Information is the key..... Unajua ni wapi unaweza ukapata products kwa bei rahisi ambazo zina soko hapo kwako
Au una skills zozote mfano kusuka au kupika? au unaweza kupata msusi au kinyozi mzuri ukamuajiri kwenye saloon
Au je una good people skills na marafiki ambao unaweza ukawauzia bidhaa (mfano nguo na urembo) ambavyo unaweza kuagiza kutoka dar
Au ukizunguka mjini biashara gani unayoiona unadhani unaweza ukaifanya bora zaidi kuliko inavyofanywa sasa hivi
Je sehemu ulipo kuna shida ya bidhaa gani au watu huwa wanasumbuka sana kutafuta bidhaa gani

The list is endless..

By the way kuna jamaa yangu ni Wakala wa MPESA ni biashara yenye faida ndogo sana lakini its all about volume..., je kuna mawakala wa hii kitu huko, na je kuna customers wengi wa kutosha, nadhani alianza na mtaji wa 3 m na yeye am not sure lakini faida ni ndogo but he seems happy with it
 
mama derick... je songea juices za concentrates kama zinazokua packed kwenye cups kama za METL zinapatikana.... kuna machine ndogo (semi automatic sealing machine) yaku seal juice kwenye cups kama hizo za METL ....zinapatikana china kwa bei ndogo sana...halafu utanunua juice concentrates with different flavour from anywhere pamoja na cups and seal film zitatoka china... ukapack na ku seal na kuuza katika mji mzima wa songea... ukaipa brand name ya derick juices.... budget yako ni nzuri kwa mradi huu... ni PM nikutumie more details pamoja na photos na machine particulars uamue kusuka au kunyoa bure kabisa


cups.jpg


something like this
 
Mama Derik, kule Njombe maeneo ya Chaugingi kuna kiwanda kimoja cha kanisa karibu na ofisi za halmashauri ya mji wa Njombe. Wanatengeneza chupa za plastic na wanauza maji swafi ya kunywa kwenye chupa za plastic.
Ushauri wangu kama mdau alivyodokeza hapo juu nunu kifaa cha kufungia chupa za plastic na kisha wasiliana na wakala wa juice uwe unajaza kwenye chupa za plasic na kuweka brand name ya biashara yako. Usisahau kupitia kwa idara ya afya wa mji ili wahakiki ubora wa bidfhaa yako.
Mwanzo mgumu lakini subira yavuta kheri, kwa mtai wako ukiwa mstahimilivu utafika mbali. Njombe na Songea si mbali.
Kumbuka biashara si kuiga ya fulani, hapa wadau wametoa mapendekezo mazuri, buni yako ili uwe na soko zuri, na wengine watakapofunguka akili kuiga we utakuwa umeshafika mbali na kuteka soko tayari.
Ishaallah
 
Mama Derick..... Swali lako linakuwa gumu in so far watu hatujui market ya hapo ulipo....., kuna mtu kasema duka la madawa (je hapo ulipo yapo mangapi, je suppliers watakuwa wapi, je competition ni kubwa au watu wanapendelea miti shamba kuliko hizo dawa?) hapo meaning yangu ni kwamba inategemea na soko...., mfano biashara ya kiti moto huenda ikawa nzuri Dar na isilipe Dubai..., au huwezi ukafanya biashara ya kuuza Ice kwa eskimos...,

Kwahiyo kila biashara inalipa kama kuna soko, unasource ya product nzuri, na unaweza ukauza sawa au chini ya competition na bado ukapata faida, kwahiyo cha maana angalia kitu ambacho hakipo hapo... (if there is a need, then there is an opportunity)..., kuna mtu kasema matunda na mboga mboga, kama hapo hazipo angalia kama unaweza ukazipata nje ya mkoa na kuzileta hapo ulipo ili uuze. Je kuna biashara yoyote hapo ambayo mtu anafanya lakini wewe unaweza kuifanya bora...., (mfano saloon ya kusuka au kinyozi, unaweza ukawa unaleta products chache kutoka dar, ukipata msusi mzuri watu watakuja), au unaweza ukawa mfugaji..,

Je una skills zozote, mfano mapishi (unaweza ukapika keki) na kuzisambaza kwenye maduka na kuuzia watu. In short hapa utaona biashara yoyote unaweza ukafanya, na kufanikiwa kwako sio kwa sababu fulani na yeye amefanikiwa ni management yako, anything you do can work better or worse kutokana na commitment sio sababu biashara fulani ni nzuri na nyingine ni mbaya.

Kwahiyo Information is the key..... Unajua ni wapi unaweza ukapata products kwa bei rahisi ambazo zina soko hapo kwako
Au una skills zozote mfano kusuka au kupika? au unaweza kupata msusi au kinyozi mzuri ukamuajiri kwenye saloon
Au je una good people skills na marafiki ambao unaweza ukawauzia bidhaa (mfano nguo na urembo) ambavyo unaweza kuagiza kutoka dar
Au ukizunguka mjini biashara gani unayoiona unadhani unaweza ukaifanya bora zaidi kuliko inavyofanywa sasa hivi
Je sehemu ulipo kuna shida ya bidhaa gani au watu huwa wanasumbuka sana kutafuta bidhaa gani

The list is endless..

By the way kuna jamaa yangu ni Wakala wa MPESA ni biashara yenye faida ndogo sana lakini its all about volume..., je kuna mawakala wa hii kitu huko, na je kuna customers wengi wa kutosha, nadhani alianza na mtaji wa 3 m na yeye am not sure lakini faida ni ndogo but he seems happy with it

nashkuru sana voice of reason.ama kwa hakika am hap with u all wana jf kwa moyo wenu wa ukarimu.em ngoja nijaribu biashara aliyosema LAT ya kupack juice,huku hamna io kitu kbs
 
mama derick... je songea juices za concentrates kama zinazokua packed kwenye cups kama za METL zinapatikana.... kuna machine ndogo (semi automatic sealing machine) yaku seal juice kwenye cups kama hizo za METL ....zinapatikana china kwa bei ndogo sana...halafu utanunua juice concentrates with different flavour from anywhere pamoja na cups and seal film zitatoka china... ukapack na ku seal na kuuza katika mji mzima wa songea... ukaipa brand name ya derick juices.... budget yako ni nzuri kwa mradi huu... ni PM nikutumie more details pamoja na photos na machine particulars uamue kusuka au kunyoa bure kabisa


View attachment 21901


something like this

thanx LAT ngoja nku pm unipe detailz.thanx alot
 
Mama Derik, kule Njombe maeneo ya Chaugingi kuna kiwanda kimoja cha kanisa karibu na ofisi za halmashauri ya mji wa Njombe. Wanatengeneza chupa za plastic na wanauza maji swafi ya kunywa kwenye chupa za plastic.
Ushauri wangu kama mdau alivyodokeza hapo juu nunu kifaa cha kufungia chupa za plastic na kisha wasiliana na wakala wa juice uwe unajaza kwenye chupa za plasic na kuweka brand name ya biashara yako. Usisahau kupitia kwa idara ya afya wa mji ili wahakiki ubora wa bidfhaa yako.
Mwanzo mgumu lakini subira yavuta kheri, kwa mtai wako ukiwa mstahimilivu utafika mbali. Njombe na Songea si mbali.
Kumbuka biashara si kuiga ya fulani, hapa wadau wametoa mapendekezo mazuri, buni yako ili uwe na soko zuri, na wengine watakapofunguka akili kuiga we utakuwa umeshafika mbali na kuteka soko tayari.
Ishaallah

nashkuru sana candid jmn kwa mchango wako wa mawazo bure kbs.Mungu awabarik jmn.je unaweza ukawa unajua chupa moja wanauza bei gani ndugu yangu?
 
We zinywe pombe tu, make hizo huwezi kufanya chochote. ukilazimisha kufanya biashara yoyote haziwezi kutoka make ni kidogo sana
Nyange we vipi? Mama Derick baadhi ya watu watakukatisha tamaa lakini usitishike kwani inawezekana, muhimu ni kuweka nia , kisha ni kuangalia kuna opportunity gani kama alivyokushauri Prime Dynamics, msingi wako kweli ni mdogo kwa hivo ni muhimu katika chochote kile utakachofanya inabidi uwajibike wewe mwenyewe (Front line)
Kama walivokueleza waliotangulia kuna watu walianzia biashara na hela ndogo zaidi ya hapo, mfano biashara ya mama ntilie haihitaji msingi mkubwa, kwa uzoefu wangu kwa kiasi kama cha kwako ni bora ujishughulishe na biashara inayohusiana na chakula, (ufugaji kuku, ngombe wa maziwa, bekari, mama ntilie, mazao etc.) biashara ya chakula always ina high demands, muhimu ni kuangalia competition na uboreshe huduma iwe juu zaidi ya wengine.
Nikupe mifano miwili.
1. Nimeona mara nyingi naenda bar mida ya usiku unaagiza mbuzi unaambiwa imekwisha, kuku imekwisha muhudumu anakwambia labda tumebaki na ndizi tu! Kwa hio hapo kuna marketing opportunity, kama utanunua deep freezer unaenda kwa wafugaji vijiji vya karibu ( kufuata unafuu) unanunua kuku, kitimoto ama mbuzi mfano kwa kuanzia kuku 100 kilo 50 mbuzi na 50 kitimoto kwa wiki, unachinja unawahifadhi kwenye Freezer yako, weka contact zako kwenye mabaa wakihitaji emergency unawaletea fasta fasta nadhani kwa siku unaweza kuuza kuku kama 10 kirahisi kabisa, hapo vifaa vinavohitajika ni Freezer, bodaboda 1 na kama hela inaruhusu jenereta yenye nguvu ya kuendesha hio freezer, kwa vile umeme wetu wa mgao ili biashara yako isioze kwa kukikosekana umeme, na hapa kwa hii jenereta ndio utapiga bao sana, na hii bodaboda nyakati za mchana unaweza kuipigia kazi ya abiria vilevile.
Nafasi na biashara za kufanya hata kwa kima ulichonacho ni nyingi, wewe kwa kuanza angalia mazingira yaliyokuzunguka, jee kuna usumbufu gani unaweza kuupatia suluhisho kwa kiwango cha fedha uliyonayo? Ama huduma gani ya kijamii ambayo unaona imezorota na unaweza kuiboresha?
2. Nimeona wafanyakazi wakisumbuka kufuata lunch umbali wa maili nzima na wakifika mkahawani waanze kupanga ques by the time wamepata oda yao na lunch break imeisha! ( jee wazo la kuchukua tenda ya kuhudumia lunch boxes maofisini?) kama utaweza kuanza kuwa-convince hata wafanyakazi 10 na kuingia dili na mwenye mkahawa unaleta lunch boxes on time ofisini na kutoza hela ndogo si ajabu baada ya mwezi unaweza kujikuta una wateja kama 100.
The opportunities is endless, just kaa kitako, fikiria kero, angalia uwezo wako, unaweza kuboresha ama kuondoa hio kero? unaweza fanyia kazi hio issue na kama huwezi fikiria tena kitu kingine mpaka utakapopata kile kilicho kwenye uwezo wako.
Mfano:Mimi binafsi sipendi kunununua bidhaa nikafungiwa na gazeti, kama ningalikuwa naishi hapa ningeanza na kuangalia uwezekano kwa kutengeneza cheap environmental friendly paper caring bags.
 
Mama Derik, ukitaka kupata maelezo zaidi wasiliana nami kwa email hii: sndoyela@yahoo.com
Nitakupa maelekezo namna ya kuwapata hao na huenda kwa maelekezo wana wawakilishi wao hap hapo Songea. Mimi niko mbali sana na huko na pengine nje ya nchi, ila nafahamu vema shughuli zao hapo.
Unaweza nipa email nikupe maelekezo zaidi.
Penye nia pana njia. Na njia ya kujikomboa kiuchumi ni kujiamini. Ukijifungia ndani hakuna atakayejua ugonjwa wako, lakini ukitoka nje wengi watakuona na wenye huruma watakusaidia kufika hospitalini.
 
Back
Top Bottom