Mila gandamizi dhidi ya wanawake wa Kichagga

Shelute Mamu

Member
Mar 17, 2009
37
1
Inasikitisha kuona kuwa mpaka leo hii kabila la Kichagga linawakandamiza wanawake katika familia zao. Wiki iliyopita nilishuhudia familia moja ikimfukuza dada yao ambaye hakubahatika kuolewa na kulazimika kuendelea kukaa kwenye mji wa wazazi wake. Lakini kaka zake kwa kushirikiana pamoja walimlazimisha kuondoka pale nyumbani pasipo kujali atakwenda kuishi wapi? na kwa nani! Si huyu tu bali wako wengine ambao wamefukuzwa nyumbani kwa kisingizio kwamba hawajaolewa na pale siyo kwao. Wanawake wasioolewa wanaitwa (WALIFU) kwa kichagga cha SIHA.

Lakini kinachosikitisha zaidi Wazee na Jamii ya SIHA inakubaliana na jambo hili. Nafikiri sasa umefika wakati kwa jamii kuondoa hii mila potofu ya unyanyasaji wa jinsi hii. Naamini ndani ya Jamii Forum kuna Waandishi, Wanasheria naomba wasaidie suala hili.
 
Inasikitisha kuona kuwa mpaka leo hii kabila la Kichagga linawakandamiza wanawake katika familia zao. Wiki iliyopita nilishuhudia familia moja ikimfukuza dada yao ambaye hakubahatika kuolewa na kulazimika kuendelea kukaa kwenye mji wa wazazi wake. Lakini kaka zake kwa kushirikiana pamoja walimlazimisha kuondoka pale nyumbani pasipo kujali atakwenda kuishi wapi? na kwa nani! Si huyu tu bali wako wengine ambao wamefukuzwa nyumbani kwa kisingizio kwamba hawajaolewa na pale siyo kwao. Wanawake wasioolewa wanaitwa (WALIFU) kwa kichagga cha SIHA.

Lakini kinachosikitisha zaidi Wazee na Jamii ya SIHA inakubaliana na jambo hili. Nafikiri sasa umefika wakati kwa jamii kuondoa hii mila potofu ya unyanyasaji wa jinsi hii. Naamini ndani ya Jamii Forum kuna Waandishi, Wanasheria naomba wasaidie suala hili.

Hizo ni baadhi ya mila potofu zinazopigwa vita. Hao waliomfukuza ni wahalifu kama wahalifu wengine, na tabia hii imekuwa sugu kwa badhi ya maeneo ya mkoa wa kilimanjaro, cha msingi huyo dada ni kupeleka suala hili kwenye serikali ya kijiji kwa kuanzia na kama ataona hana msaada wowote, kabla ya kukimbilia mahakamani kudai haki yake, amuone mkuu wa wilaya na kumweleza hayo yaliyomkuta, maagizo ya mkuu wa wilaya kwa watendaji wa kata yanaweza kumsaidia kuokoa muda. aidha ajaribu kuwasiliana na taasisi kama TAWLA au WILAC naamini atapata msaada wa kisheria ili safari yake ya kwenda mahakamani iwe ya kishindo.
 
Nakushukuru sana kwa ushauri wako, isipokuwa hao Serikali ya kijiji eneo hilo ni hao hao wanaounga mkono ukandamizaji huo.
 
Back
Top Bottom