Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 44
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania (HESLB), itafanya mabadiliko makubwa ya utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu nchini kwa mwaka ujao wa fedha kama hatua mojawapo ya kupunguza matatizo yaliyokuwa yakiikumba bodi hiyo katika utendaji kazi wake.
Uamuzi huo wa Bodi ulitangazwa jana jijini hapa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Nicholaus Mbwanji wakati alipozungumza na waandishi wa habari. Nia yetu kama Bodi ni kufungua ukurasa mpya wa utendaji wetu na zaidi kuweka utaratibu wa utoaji mikopo na vigezo vyake na pia kuishauri serikali katika utoaji mikopo na urejeshaji wake, alisema Profesa Mbwanji.
Alisema chini ya mabadiliko hayo, kuanzia mwaka ujao wa fedha maombi yote ya mikopo yatakuwa yakijadiliwa na kupitishwa na kamati za elimu katika ngazi ya kijiji, kata ama tarafa na baadaye kupitishwa kwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya husika. Alisema lengo likiwa ni kuwabaini zaidi ni wanafunzi gani walio na uwezo na ambao hawana uwezo ili wakati wa utoaji wa mikopo iwe ni rahisi kwa Bodi kuyashughulikia maombi yao.
Lengo la mabadiliko haya ni kuzuia udanganyifu na kuwasilishwa kwa taarifa zisizo sahihi kwetu na maombi ambayo hayakupitishwa katika kamati hizo hayatapokelewa na Bodi, alisisitiza na kuongeza kuwa katika mwaka ujao wa fedha, Bodi pia itaendelea kutumia vigezo sita katika kutambua uwezo wa kiuchumi kwa waombaji wa mikopo inayotolewa na bodi yake.
Kwa mujibu wake, vigezo hivyo ni historia ya elimu ya mwombaji ili kumbaini mwombaji anayeghushi nyaraka za kujiunga na chuo; kiwango cha elimu ya wazazi wake; shughuli zake za kiuchumi; mali za mwombaji na za wazazi wake; hifadhi yake ya maisha na hali yake ya kijamii kwa ujumla.
Kuhusu sifa kwa wale wanaopatiwa mikopo, alisema sifa za ufaulu kwa viwango vya daraja la kwanza na la pili havitatumika tena kuanzia mwaka ujao wa fedha na badala yake, Bodi itazingatia udahili unaofanywa na vyuo vya elimu ya juu nchini. Nawaomba Watanzania watambue kuwa katika kuzingatia mpango huu, wanafunzi watakaopata udahili katika kozi za sayansi kwa mwaka 2009/10 watapewa mikopo yao kwa asilimia mia, hii imetokana na kubainika kuwa wanafunzi wa sayansi wanaonufaika na mikopo hiyo imekuwa ni pungufu ya asilimia 35 tu, hali hii sio nzuri kwa taifa letu, aliongeza.
Chanzo: Habari Leo
Maswali ya kujiuliza:
Kwa kuwa haya ndio mambo ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele na wanavyuo, wazazi, DARUSO, TSNP, TAHLISO, CHADEMA nk; je ni kwamba serikali imesikiliza kilio cha umma au ni kwa sababu uchaguzi wa 2010 umekaribia?
Kwa kuwa utaratibu huu unakuja baadaye, si ishara ya kwamba wanafunzi wa sasa walikuwa na hoja, kwa nini mpango huu usihusu pia wanafunzi ambao mwaka huu wameshindwa kuendelea na masomo yao kutokana na masharti yale ya mwanzo?
Palikuwa na haya gani kutumia nguvu ya dola kama madai haya ya wanafunzi yalikuwa ni ya kweli?
Je, ilikuwa sahihi kufanya udahili upya kwa wanafunzi? Kwanini udahili mpya haukufuata utaratibu huu?
Zaidi ya wanafunzi 2000 walishindwa kujaza fomu kwa hiyo serikali imetangaza kuwa wamejifukuzisha fomu. Je, fomu zilikuwa zinapatikana vijijini waliporudishwa baada ya chuo kufungwa? Je, masharti na muda wa kupata fomu hizo viliruhusu wote kupata? Kwanini bodi isitangaze utaratibu wa kuwawezesha hao pia kusoma?
Asha
Uamuzi huo wa Bodi ulitangazwa jana jijini hapa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Nicholaus Mbwanji wakati alipozungumza na waandishi wa habari. Nia yetu kama Bodi ni kufungua ukurasa mpya wa utendaji wetu na zaidi kuweka utaratibu wa utoaji mikopo na vigezo vyake na pia kuishauri serikali katika utoaji mikopo na urejeshaji wake, alisema Profesa Mbwanji.
Alisema chini ya mabadiliko hayo, kuanzia mwaka ujao wa fedha maombi yote ya mikopo yatakuwa yakijadiliwa na kupitishwa na kamati za elimu katika ngazi ya kijiji, kata ama tarafa na baadaye kupitishwa kwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya husika. Alisema lengo likiwa ni kuwabaini zaidi ni wanafunzi gani walio na uwezo na ambao hawana uwezo ili wakati wa utoaji wa mikopo iwe ni rahisi kwa Bodi kuyashughulikia maombi yao.
Lengo la mabadiliko haya ni kuzuia udanganyifu na kuwasilishwa kwa taarifa zisizo sahihi kwetu na maombi ambayo hayakupitishwa katika kamati hizo hayatapokelewa na Bodi, alisisitiza na kuongeza kuwa katika mwaka ujao wa fedha, Bodi pia itaendelea kutumia vigezo sita katika kutambua uwezo wa kiuchumi kwa waombaji wa mikopo inayotolewa na bodi yake.
Kwa mujibu wake, vigezo hivyo ni historia ya elimu ya mwombaji ili kumbaini mwombaji anayeghushi nyaraka za kujiunga na chuo; kiwango cha elimu ya wazazi wake; shughuli zake za kiuchumi; mali za mwombaji na za wazazi wake; hifadhi yake ya maisha na hali yake ya kijamii kwa ujumla.
Kuhusu sifa kwa wale wanaopatiwa mikopo, alisema sifa za ufaulu kwa viwango vya daraja la kwanza na la pili havitatumika tena kuanzia mwaka ujao wa fedha na badala yake, Bodi itazingatia udahili unaofanywa na vyuo vya elimu ya juu nchini. Nawaomba Watanzania watambue kuwa katika kuzingatia mpango huu, wanafunzi watakaopata udahili katika kozi za sayansi kwa mwaka 2009/10 watapewa mikopo yao kwa asilimia mia, hii imetokana na kubainika kuwa wanafunzi wa sayansi wanaonufaika na mikopo hiyo imekuwa ni pungufu ya asilimia 35 tu, hali hii sio nzuri kwa taifa letu, aliongeza.
Chanzo: Habari Leo
Maswali ya kujiuliza:
Kwa kuwa haya ndio mambo ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele na wanavyuo, wazazi, DARUSO, TSNP, TAHLISO, CHADEMA nk; je ni kwamba serikali imesikiliza kilio cha umma au ni kwa sababu uchaguzi wa 2010 umekaribia?
Kwa kuwa utaratibu huu unakuja baadaye, si ishara ya kwamba wanafunzi wa sasa walikuwa na hoja, kwa nini mpango huu usihusu pia wanafunzi ambao mwaka huu wameshindwa kuendelea na masomo yao kutokana na masharti yale ya mwanzo?
Palikuwa na haya gani kutumia nguvu ya dola kama madai haya ya wanafunzi yalikuwa ni ya kweli?
Je, ilikuwa sahihi kufanya udahili upya kwa wanafunzi? Kwanini udahili mpya haukufuata utaratibu huu?
Zaidi ya wanafunzi 2000 walishindwa kujaza fomu kwa hiyo serikali imetangaza kuwa wamejifukuzisha fomu. Je, fomu zilikuwa zinapatikana vijijini waliporudishwa baada ya chuo kufungwa? Je, masharti na muda wa kupata fomu hizo viliruhusu wote kupata? Kwanini bodi isitangaze utaratibu wa kuwawezesha hao pia kusoma?
Asha