Mikoa iliyoendelea Tanzania-Wanamageuzi

unaweza kuniambia chadema imeleta maendeleo gani kilimanjaro? Anza na kwa chair wao kule jimbo la hai
 
unaweza kuniambia chadema imeleta maendeleo gani kilimanjaro? Anza na kwa chair wao kule jimbo la hai
mfano igunga ndo dira ccmagamba.uwongo mbele ukwel nyuma,itoke ccmagamba madarakan waje waume wa kazi
 
Ni aibu kutoa data za namana hii, unaposema maendeleo unamaanisha nini? kwa kuangalia nini? je maendeleo ni kujenga barara?ni kuzoa taka kama ilivyo hapa Moshi? ni kwa nini hayo maendeleo yamekuja? je miaka ya 1940 KILIMANJARO ilikua sawa na mkoa gani? na kwa ninini? hebu tengeneza hoja usitengeneze kioja
 
Moja ya tatizo linaloikabili CDM ni kuwa na washabiki/wafuasi wasio wazalendo.
Wako tayari kuisifia hata kwenye mambo yasiyo na mashiko. Kwa mwendo huu watakuwa kama magamba tu.
 
Kiukweli kusema tu mkichagua wapinzani ghafla mikoa inaendelea nadhani sio sahh sana..Labda kama mtoa hoja alitaka kusemea Uelewa wa wananchi wa mikoa fulani...hapo anaweza kuwa sahihi
Uelewa mkubwa wa wananchi juu ya mambo mbalimbali unachangia Maendeleo kwa maana Watu wakiwa waelewa ni rahisi pia kuzitumia fursa zilizopo mkoani mwao..Kitu ambacho pia kinachangia kuuchangamsha mkoa husika katika mambo ya kuchagua viongozi..manake ili uchaguliwe inabidi uwe umejipanga sawasawa.
Tofauti na mikoa mingine ambako hakuna mwamko wa Kielimu na hivyo kupelekea wananchi wa huko kurubunika kwa vitu vidogovidogo kama vile tshirt, skafu na hata khanga!!
 
Nimefikiri sana na kugundua kua mikoa yote iliyopiga hatua hapo Tanzania,ni mikoa ya mageuzi na ambayo hukubali sera na sio chama.Mfano Mbeya, Kilimanjaro,Bukoba,Mwanza,Shinyanga,Iringa,Arusha,Kigoma inakuja kwa kasi,DSM kwa sasa,n.k.Lakini mikoa ambayo imeendelea kuikumbatia CCM kwa asilimia kubwa wako nyuma kimaendeleo kuliko mikoa tajwa hapo juu.Wakati umefika sasa kwa mikoa iliyo nyuma kujivua GAMBA na kusema CCM basi.Zaidi ya miaka 50 llakini umeme wa shida,maji safi shida,Reli iliyojengwa na mkolo ni hiyo hiyo na inakufa.

Mkuu in reality hakuna penye afadhali hapa TZ; kila sehemu ni shida na tabu kwenda mbele. Labda mwenzetu ungetufafanulia maana ya maendeleo kwa mtazamo wako.
Lakini kama unamaanisha maendeleo in the sense of human development, kila mahala TZ ni hoehae!!
 
Jamani huyu mtoa maada nadhani hayuko makini kabisa na yawezeka hajui kinachoendelea nchini mfano ametaja Bukoba sijui anamanisha mkoa au wilaya(majimbo) mawili ambayo ni vijijini na mjini na yote yako chini ya ccm na hakuna maendeleo kule hawa watu wepesi wakudanganywa na ccm.
Rejeo bajeti ya mwaka 2011 to 2012 ilionesha kuwa mikoa kumi ambayo hiko nyuma nani maskini saana ukiwemo mkoa wa Kagera-Bukoba.
Huu ni mkoa ambao kwa mali hautafautiani na Kirimanjaro,Mbeya na Morogoro lakini huko nyuma saana watu wengi maskini,ajira hamna,elimu imeshuka,bei ya bidhaa hiko juu etc
Kagera ni moja ya mikoa kumi maskini Tanzania.
 
Back
Top Bottom