Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Dua anashauri kwamba serikali ingenunua dhahabu yote na tanzanite yote kwa kipindi cha miaka 3, ili tujue kiasi halisi. Kwa mwaka, Tanzania inauza nje dhahabu ya $700 milioni na tanzanite ya $400 milioni. Serikali yetu haina uwezo wa kununua madini ya $1,100 milioni kwa mwaka na ikabaki na fedha za matumizi muhimu. Kwa miaka 3, tungehitaji $3,300 milioni. Hii ni zaidi ya fedha zote za kigeni tulizo nazo.

Namshukuru Mwagenzi kwa upambanuzi wake wa kina kuhusu vigezo vinavyohatarisha amani ya nchi. Kwa maoni yangu, wizi wa kura na rushwa katika chaguzi zetu ni kigezo kinachoweza kuleta uchafuzi Tanzania mapema kuliko vigezo vingine vyote. A time will come when the opposition parties will choose to fight fire with fire. Kwa sasa, CCM inatumia nguvu za Jeshi, Usalama wa Taifa na Polisi kuhakikisha "wanashinda" karibu kila uchaguzi.

Jasusi,

Laiti tungekuwa na bunge lenye demokrasia ya kweli. Ungepita mswada wa kutaka kusiweko na kampuni ya nje yenye zaidi ya 40% ya hisa kwenye kuchimba madini. Naamini wabunge karibu wote wangeunga mkono mswada kama huo. Kinachokwamisha ni kukosekana demokrasia.

Tuko katika kipindi cha unyonyaji wa kutisha. Ni unyonyaji unaofanywa na makampuni ya madini, kwa makubaliano na serikali yetu. Kwa vile makubaliano yenyewe si ya haki, hairuhusiwi wananchi kuyajua. Hata wawakilishi wa wananchi, yaani wabunge, hawana haki kuyafahamu hayo makubaliano.

Historia inaonyesha kwamba makundi yanoyoweza kuokoa nchi iliyo katika lindi la ukandamizaji kama wa kwetu, ni wafanyakazi na wanafunzi. Laiti wanafunzi wetu wangetambua kwamba maisha ni zaidi ya mikopo yao! Inaelekea wafanyakazi wa Tanzania hawajui kwamba hali yao ya umasikini wa kutisha sio matakwa ya Mungu. Ni hali inayotokana na unyonyaji wa ajabu, na uongozi mbaya unaosimamiwa na CCM.

Augustine Moshi
 
Dua anashauri kwamba serikali ingenunua dhahabu yote na tanzanite yote kwa kipindi cha miaka 3, ili tujue kiasi halisi. Kwa mwaka, Tanzania inauza nje dhahabu ya $700 milioni na tanzanite ya $400 milioni. Serikali yetu haina uwezo wa kununua madini ya $1,100 milioni kwa mwaka na ikabaki na fedha za matumizi muhimu. Kwa miaka 3, tungehitaji $3,300 milioni. Hii ni zaidi ya fedha zote za kigeni tulizo nazo.

Kwani hayo madini yanayochimbwa na kuuzwa sasa hivi yalikuwa yanachangia uchumi miaka kumi iliyopita? Hii ni kuonyesha kwamba tunaibiwa, kama hatuwezi kusitisha kuuza madini ambayo ni ya kwetu basi nani anafaidi? Tunapositisha sio kwamba tunaacha kuchimba tunahodhi bidhaa adimu ambayo kila kukicha inapanda bei. Tanzania tuamke na kuwafurumusha hawa wezi walioingia kwa speed kali.

Nchi nyingi wanahodhi gold bars na kuuza wanapoona bei ni nzuri. sisi tumejaliwa na Tanzanite na madini mengine kem kem. Hata kama Serikali haiwezi kununua kama unavyosema tunaweza kujikopesha mali yetu. (Mbona USA, UK wanajikopesha makaratasi yao).
 
Hata kama Serikali haiwezi kununua kama unavyosema tunaweza kujikopesha mali yetu. (Mbona USA, UK wanajikopesha makaratasi yao).

"Mali yetu"? You cannot eat your cake and have it. Ukishauza madini yako hayabaki kuwa YAKO tena. Gesi ya Songo Songo na machimbo ya dhahabu tuliyowapa watu ili watupe 3% kila mwaka si vyetu tena! Hatuwezi kukopa kwani wenye mali hawatakubali. Na hatuwezi kuwashtaki mahali popote ila Uingereza (mahakama zetu haziruhusiwi kuzungumzia mikataba kati ya serikali yetu na hao wenye mali).

Ni kosa walilonalo Watanzania wengi, la kudhani vitu tulivyouza bado ni vyetu.

Augustine Moshi
 
"Mali yetu"? You cannot eat your cake and have it. Ukishauza madini yako hayabaki kuwa YAKO tena. Gesi ya Songo Songo na machimbo ya dhahabu tuliyowapa watu ili watupe 3% kila mwaka si vyetu tena! Hatuwezi kukopa kwani wenye mali hawatakubali. Na hatuwezi kuwashtaki mahali popote ila Uingereza (mahakama zetu haziruhusiwi kuzungumzia mikataba kati ya serikali yetu na hao wenye mali).

Ni kosa walilonalo Watanzania wengi, la kudhani vitu tulivyouza bado ni vyetu.

Augustine Moshi

Hawajauza kama vile unavyotaka tuamini ndio maana kuna hizo percentage na kwenye law kuna kitu kinaitwa unfair contract ni Jukumu la waliopewa dhamana kuhakikisha wananchi wanafaidi na rasilimali zao. haiwezi kuchukua hata miaka mitano tutaanza kushuhudia yale yanayotokea Nigeria delta. Natumaini vile vile umesikia habari ya Uranium kuweko kwa wingi kusini mwa Tanzania hivyo hii serikali sijui itatupeleka wapi kwa mtindo huu waliouendekeza wa kuneemesha wageni.
 
New hope for uranium wealth in Dar
By WILFRED EDWIN
Special Correspondent

Tanzania is set to experience a flurry of activities in its mining industry as recent explorations have identified uranium rich sandstone formations in the country.

Two foreign exploring companies — Uranium Resources Plc, a uranium mining company focusing on Southern Africa, and Australia-based Western Metals Ltd — said last week that “recent exploration results have been highly encouraging and indicate the economic potential of the region.”

The companies, currently undertaking a joint venture, Mtonya Uranium project in the country, said they had entered “a very exciting phase of exploration” for the mineral, whose world demand is outstripping supply. The initial reconnaissance drilling at the Mtonya Uranium project has identified uranium hosted in sandstone units similar to those found at neighbouring Malawi’s Kayelekera uranium project.

Western Metals is listed on the Australian Stock Exchange, while Uranium Resources Plc is listed on the London Alternative Investment Market (AIM). The joint venture says the initial first pass-drilling programme has “achieved its aim of identifying significant subsurface uranium mineralisation in the Mtonya JV licence areas.”

James Pratt, an official of Uranium Resources, told The EastAfrican from the United Kingdom last week: “The joint venture is now positioned to progress its exploration activities aggressively over the remainder of 2007 and beyond.” Drilling will recommence in August with a view to further testing the anomalies and following up the initial results, and apart from the drilling, an extensive trenching, sampling and mapping programme will be undertaken.

According to Mr Pratt, uranium operations are complicated as safety and environmental precautions are involved, and as such, commissioning of the mines could take up to five years if all goes well. He said the project has already consumed about $1 million. Dr Peter Kafumu, the Commissioner for Minerals at the Ministry for Energy and Minerals, confirmed last week that the companies have been granted uranium exploration licences and are currently engaged in uranium exploration.

Industrial sources say the present world demand for uranium is outstripping supply and about a third of annual demand for uranium is being met by declining inventories and Russia’s highly enriched uranium weapons decommissioning. The Sydney-based Resource Capital Research sees a bullish outlook for the uranium market and has predicted that the uranium price will reach $125/lb this year and may escalate to $140/lb by September 2008.

The major application of uranium in the military sector is in making high profile weapons, whereas its main civilian use is to fuel commercial nuclear power plants. Experts say by the time it is completely fissioned, one kilogramme of uranium can theoretically produce about 20 trillion joules of energy, or as much electricity as 1,500 tonnes of coal.

Currently, 17 per cent of world electricity is generated through uranium, but still its demand is hardly met by the supply. Global electricity demand is growing rapidly. Even with effective energy efficiency programmes in developed countries, the International Energy Agency (IEA) expects global electricity consumption to double by 2030.

If indeed the uranium exploration develops into “full commodity availability,” it will definitely become one of Tanzania’s more important foreign exchange earners, analysts predict. This prediction is bolstered by the fact that there has been little exploration for 25 years and no new mines built outside Canada for the past 20 years, and that there is not enough uranium capacity to satisfy existing plants — crucially, new uranium deposits need to be put into production now.

Experts say despite the favourable geology for uranium deposits and several known occurrences, the average historical expenditure on uranium exploration in Tanzania has been $4 per square km, compared with $16 per square km in the West Africa and $224 per square km in the United States.

They say Tanzania has also favourable regulatory and stable political conditions for exploration, as evidenced by the boom in its gold mining sector in the past 10 years as well as the strong investment in nickel, platinum and coal exploration.

Western Metals has an agreement with Uranium Resources plc including the Mtonya Project in Tanzania where it predicts it can earn 60 per cent profits by spending $4 million. It also has a 42.5 per cent interest in an additional 10,413 sq km of tenements in Tanzania, bringing the license area to 13,851 sq km with a further 211 sq km under a 45 per cent joint venture.

George Bauk, Western Metal managing director, and Willie Rowe of Gryphon Management Australia said in an update announcement posted at the company’s website that the results of the reconnaissance are considered encouraging, and that “Western Metals is entering a very exciting phase of exploration in Tanzania.”

“Several anomalous areas identified will require further detailed exploration during the second half of 2007 including drilling and detailed airborne radiometric surveys. Assay results of samples and details of sites visited will be released when they are received.”

Uranium Resources has primarily concentrated on expanding and developing its portfolio of uranium licences in the highly prospective Karoo Basin in the Southern Tanzania where it currently has a land package in excess of 7,600 sq km.

Tutaona mengi kwenye hii mikataba
 
Wazungu wa madini ‘waingia mitini’

na Christopher Nyenyembe, Mbeya

WAZUNGU waliovamia Kijiji cha Matebete-Madunguru, Wilaya ya Mbarali na kuharibu mazingira kwa madai ya kusaka madini, wametimka nchini na kuacha madeni makubwa kwa wamiliki wa mitambo walikokodi.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa baada ya kutimka kwa Wazungu hao, kazi waliyokuwa wanaifanya sasa inafanywa na wamiliki wa mitambo hiyo ambao nao walikuwa wakifanya uchimbaji huo kinyume cha sheria, hali iliyosababisha wapigwe marufuku kuendelea na uchimbaji na kutakiwa kufukia mashimo yote.

Amri ya wachimbaji hao haramu kupigwa marufuku ilitolewa mwishoni mwa wiki na Ofisa Madini Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Alex Magayane, baada ya kubaini mtu aliyekuwa na kibali kutokea jijini Mwanza, Ahmed Mselemu, hana kampuni bali ni mchimbaji binafsi ambaye hakuwa na leseni ya uchimbaji na alishirikiana na Yusuph Sapi Mkwawa, kuwaleta Wazungu hao kwenye eneo hilo.

Inadaiwa kuwa Wazungu hao waliingia nchini kutoka Marekani na kwenda katika eneo hilo wakiongozwa na ramani waliyopewa kutoka nchini Ujerumani, inayoonyesha maeneo ambayo viliachwa vito vya thamani na wakoloni wa Kijerumani wakati walipokimbia baada ya kushindwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.

Inadaiwa kuwa Wazungu watatu wakiongozwa na mwenzao, Mike Martin ambaye ni Mmarekani, mwaka jana walifika katika Kijiji cha Matebete, kinachomilikiwa kihalali na wafugaji kutoka kabila la Wamasai na kukodi mitambo ya kuchimbia vito hivyo kutoka kwenye kampuni moja ya malumalu jijini Mbeya.

Habari zaidi zinadai kuwa kazi ya uchimbaji huo usiokuwa halali ilikuwa ikifanywa kwa kutumia vibali vidogo vya utafiti walivyopewa na Idara ya Madini mkoani hapa na hawakuwa na leseni yoyote inayowaruhusu kuchimba madini.

Walipewa vibali hivyo kwa madai kuwa walikuwa wakisaka madini aina ya dhahabu.

Katika mazingira hayo na ujanja, waliweza kuwarubuni viongozi wa Kijiji cha Matebete na kuingia porini walikoanza kuchimba mashimo makubwa na kukata miti ovyo wakisaka vito vya thamani vilivyoachwa na Wajerumani huku wenyeji wakijua kuwa wanachotafuta ni madini.

Inadaiwa kutoka kwenye vyanzo vya habari kuwa baada ya Wazungu hao kuishiwa fedha walizokuwa wakitumiwa na wenzao kutoka Ulaya, waliamua kutimka huku wakiacha madeni makubwa ya mitambo na kuikabidhi kazi hiyo kwa Watanzania wenye asili ya Kiasia na Mtanzania mwenye asili ya Kiarabu, ambao bado wanaendelea kusaka vito hivyo.

Tanzania Daima ilipofuatilia kwa undani ilibaini kuwa kampuni hiyo ya Kitanzania inayojihusisha na shughuli nyingine, iliweza kufanya kazi hiyo baada ya kupata kibali cha utafiti mdogo cha sh 20,000 kwa mwaka mzima ili kuendelea na uchimbaji huo kinyume cha sheria za madini kwa kumtumia Mselemu.

Pia inadaiwa kuwa Watanzania hao wenye asili ya Kiasia (majina tunayo), walichukua jukumu hilo la kuendelea kusaka vito hivyo vilivyoachwa na Wajerumani baada ya kutolipwa na Wazungu hao kiasi kikubwa cha fedha walizokodishia mitambo, wakiwa na ramani iliyochorwa enzi za ukoloni, ikionyesha kuna mali nyingi zilizokuwa zimefichwa katika maeneo hayo.

Mbali ya kuanza kuifanya kazi hiyo kwa kutumia mgongo wa Mtanzania huyo mwenye asili ya Kiarabu, hawakutaka wajulikane katika uchimbaji huo huku kibali walichonacho walichokata Machi 20 mwaka huu kikiwa hakiwaruhusu kuchimba madini isipokuwa kimetolewa kwa ajili ya utafiti mdogo wa madini.

Alipohojiwa, Mselemu alikiri kukata kibali hicho kwa mgongo wa Watanzania hao wenye asili ya Kiasia, huku akiendelea na kazi hiyo akijifanya kuwa ndiye aliyekodisha mitambo na kumiliki kibali cha uchimbaji.

Alisema mara baada ya Wazungu hao kutimka, ndipo alipoitwa na Waasia hao na kupewa kazi ya kusimamia uchimbaji huo wa kusaka vito vya thamani bila serikali kujulishwa kazi inayoendelea kwenye pori hilo.

Mkwawa naye alikiri kufika na Wazungu hao kwenye kijiji hicho na kudai kuwa mara walipoishiwa fedha waliamua kuondoka, huku Martin akiwa amerejea Ulaya kumuuguza mkewe ambaye alidai kuwa amepooza.

Kufuatia utata huo uliojitokeza katika uingiaji na kuanza kuchimba mashimo, Ofisa Madini Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Magayane, akiwa ameongozana na gazeti hili, alifika katika eneo hilo umbali wa kilometa saba kutoka kwenye barabara kuu ya Tanzania-Zambia na kushuhudia uharibifu huo.
 
The Kiwira coal power project saga: Mkapa, Yona broke the law

-Various sections of Leadership Code of Ethics Act quoted

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam


FORMER president Benjamin Mkapa and senior minister Daniel Yona are now understood to have acted illegally in the privatisation and takeover of the Kiwira Coal Mine in Mbeya Region, by failing to disclose their personal vested interests in the matter and using information obtained while executing public office duties for their own personal gain.

According to the Public Leadership Code of Ethics Act of 1995, a copy of which has been availed to THISDAY, a public leader shall be considered to have breached the Act if he or she acquires any significant financial advantage, or assists another person to acquire such gain, by ’’improperly using or benefiting from information which is obtained in the course of his/her official duties and which is not generally available to the public.’’

With full access to all confidential information regarding the state-owned coal mine and its operations by virtue of their powerful positions in government, Mr Mkapa and Yona founded Tanpower Resources Company Limited in December 2004, when one was sitting president of the United Republic and the other served as minister for energy and minerals respectively.

Just a few months later, in mid-2005, the company that was apparently the brainchild of Mr Mkapa, Yona and some of their immediate family members took over control of the Kiwira Coal Mine.

Stated objectives of Tanpower Resources include ’’to carry on the business of miners of coal and iron; to process such coal and iron and generally treat, prepare, render marketable, sell and dispose of such coal and iron or by-products resulting therein in their raw or manufactured state.’’

The company was also licensed to ’’deal with coal mining in order to generate electricity for consumption and sale; to generate power generators, transmitters and general distributors; and to provide power and general projects management, project appraisers and consultants.’’

The first listed directors of Tanpower Resources were named as the then first lady Mrs Anna Mkapa; the then minister for energy and minerals Daniel Yona; Nicholas Mkapa (the president and Mrs Mkapa’s son); Joseph Mbuna (Nicholas Mkapa’s father-in-law); and one Evans Mapundi.

Mrs Mkapa sat on the board as a representative of ANBEM Limited; Yona from DEVCONSULT Ltd; Mkapa junior from Fosnik Enterprises; Mbuna from Choice Enterprises; and Mapundi representing yet another company, Universal Technologies Limited, in which he shares ownership with one Wilfred Malekia.

Both Mr Mkapa and Yona as president and energy/minerals minister respectively - were deeply and directly involved in the privatisation of the Kiwira Coal Mine, and were privileged with full access to all confidential information regarding its assets, operations and business potential.

They are understood to have engineered the acquisition by Tanpower Resources of 70 per cent shares in the Kiwira Coal Mine, as part and parcel of the ’fast-track’ privatisation process. This was later increased to 85 per cent, with the remaining, token 15 per cent shares being retained by the government of the day.

However, states that a public leader shall be considered to have breached the law if he knowingly acquires any significant financial advantage or assists in the acquisition of any such advantage by another person by the following manner:

Apart from improper use of, and benefit from, information obtained in the course of carrying out official duties and which is not generally available to the public, Section 12 (1) of the Public Leadership Code of Ethics Act also states other ways in which a public leader will be considered to have breached the law, including:

’’By directly or indirectly converting government property for personal or any other unauthorised use, for the purposes of reaping private economic benefit.’’

Furthermore, section 13 (1) of the same legislation also states that ’’a public leader shall not speak in the Cabinet, National Assembly, in a local government council or a committee thereof, or in or at any other official forum or part of it, on any matter in which he has a direct pecuniary (financial) interest unless he has disclosed the nature of that interest to the Cabinet, the Assembly, the council, committee or such other forum or part of it.’’

Section 13 (2) of the same law states that ’’the separately owned assets of the spouse or minor children of a public leader shall be deemed to constitute an interest for disclosure by him.’’

And section 14 (1) requires that ’’where a public leader has an interest in a contract that is made, or is supposed to be made by the government, and has not made a sufficient declaration under subsection (4) in relation to the contract, the public leader shall as soon as practicable make a declaration of his interest in relation to the contract, specifying the nature and extent of his interest.’’

Section 14 (3) states that ’’the interest of the spouse or spouses, or of the children of a public leader in relation to the government contract, shall be deemed to be the interest of the public leader.’’

Under this law, a public leader has an interest in a government contract ’’if he will derive any material benefit, whether direct or indirect, from the contract; or if one party to the contract is a firm or body corporate and he has a material interest, whether direct or indirect, in the firm or body corporate.’’

It has been established that very few government functionaries were even aware of the real people behind Tanpower Resources when it took over control of the hitherto state-owned Kiwira Coal Mine, and that the company and its operations were from the outset shrouded in heavy secrecy.

Tanpower Resources is currently the majority shareholder in the renamed Kiwira Coal and Power Limited company which in March 2006 entered into a controversial, $271.8m (approx. 340bn/-) contract with the state-run Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) for the supply of 200 megawatts of electricity to the national power grid.

It has also emerged that with Tanpower Resources at the helm, Kiwira Coal and Power Limited was also given control of a separate, additional area with lucrative coal deposits that was formerly owned by the government. Our sources say the Kabulo Coal Prospect, also in Mbeya Region where the Kiwira mine is located, was wrestled away from the control of the State Mining Corporation (STAMICO) - a government-run agency - and handed on a ’silver platter’ to Kiwira Coal and Power Ltd.

Previous studies commissioned by the government itself have shown that the Kabulo area, which lies within the East African Rift Valley system in south-western Tanzania, has proven reserves of up to 14 million tonnes of coal.

Before being sidelined, STAMICO had been actively promoting the Kabulo area with the intention of attracting a strategic investor to develop a coal-fired power station.
 
Makampuni ya madini yaihujumu serikali

Na Ramadhan Semtawa

WAKATI wananchi wakilalamikia serikali kutokana na kutoa misamaha mingi ya kodi kwa wawekezaji, imebainika kwamba baadhi makampuni ya madini na ujenzi wa barabara yaliyopewa misamaha ya kodi kuagiza mafuta kutoka nje, yanauza bidhaa hizo mitaani.

Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi unaonyesha kuwa baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hayo ambayo majina yake tunayo wamekuwa wakiuza mafuta hayo kwa wamiliki wa vituo vya mafuta kwa bei ya chini.

Inaelezwa kwamba makampuni hayo yamekuwa yakiagiza mafuta mengi zaidi ya matumizi yao na yanayobaki kuyauza mitaani kwa wafanyabiashara na kujipatia mamilioni ya fedha.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa wizi huo umekuwa ukifanywa kwa ushirikiano na baadhi ya wafanyakazi wa serikali ambao huidhinisha makampuni hayo kuagiza mafuta mengi zaidi ya matumizi yake ya kawaida.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, amekiri kuwapo hujuma hiyo na kusema kuwa tayari serikali ilikwishakamata baadhi ya wajanja hao na kuwachukulia hatua.

Mgonja alisema serikali ilikamata watu hao maeneo ya Chalinze baada ya kubainika kuidanganya serikali. Alisema kwamba inaendelea na msako na kwamba watakaobanika watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Hata hivyo, Mgonja hakuwa tayari kueleza majina ya makampuni yaliyokamatwa yakitaka kuhujumu uchumi na hatua zilizochukuliwa.

"Ni kweli kabisa, kuna watu wanatumia mwanya wa msamaha wa kodi kufanyabiashara, tunalijua hilo, lakini tukimkamata mtu huwa hatuna utani," alisema Mgonja na kuongeza:,

"Tulishakamata baadhi maeneo ya Chalinze na tumewachukulia hatua, unajua tatizo la wafanyabiashara wao wanaangalia faida tu, lakini tutawashughulikia," alionya.

Uchunguzi umebaini kwamba wajanja hao huwauzia mafuta hayo baadhi ya wamiliki wa vituo vya mafuta vilivyopo kando kando ya barabara kuu ya kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani.

Serikali hutoa msamaha wa kodi za mafuta kwa zaidi ya lita 100,000 kwa mwezi kwa makapuni ya madini nchini.

Ingawa serikali imeweka mita za mafuta katika bandari za Dar es Salaam na Tanga kwa lengo la kudhibiti ukwepaji wa kulipa kodi, hivi sasa mwanya wa msamaha wa kodi ndio unatumiwa zaidi na wafanyabiashara hao.
 
Kwani kesi ya Dr Judithi Mhina iliishia wapi.Huu ni mtandao ambao unasimamiwa na viongozi wakubwa ktk serikali,na unafanywa na makampuni makubwa ya mafuta ya wafanyabiashara maarufu ambao wapo Dar,Morogoro,Moshi,Arusha na Tanga.
 
Washitakiwe wachukuliwa sheria. Whoever breaks the law should face the music.
 
...very interesting...sasa This Day wangeeleza basi adhabu inayoambatana na kukiukwa kwa sheria hizo. labda wataeleza kwenye toleo lijalo.

...hivi Mkapa hayuko IMMUNE na mashtaka yoyote yale wakati akiwa Raisi, au wakati akitekeleza majukumu yake kama Raisi?
 
Mimi ningekuwa Rais wa Tanzania, inapokuja kwenye kusaini mikataba ya madini ambayo imelalamikiwa sana na wananchi wangu kwamba haina maslahi na Watanzania na ni mikataba ya mabilioni ya pesa basi nitahakikisha naipitia na kujua details zote za mikataba hiyo kabla ya kutoa go ahead.

'Si lazima JK ataarifiwe inaposainiwa mikataba'

Shadrack Sagati
HabariLeo;
August 21, 2007


OFISI ya Rais Ikulu imesema Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi hakuwa analazimika kumuarifu Rais Jakaya Kikwete wakati wa kusaini mkataba wa uwekezaji wa mradi wa dhahabu wa Buzwagi jijini London, Uingereza.

Kitengo cha Habari cha Ikulu kimeliambia gazeti hili kuwa Rais aliarifiwa juu ya mazungumzo ya mkataba wa uwekezaji ambayo yalikuwa yanafanywa kati ya Serikali na wawekezaji wa kigeni.

Karamagi alisaini mkataba huo Februari mwaka huu wakati akiwa amefuatana na Rais Kikwete kwenye ziara ya kikazi katika nchi za Ulaya na Scandinavia.

Rais kabla ya ziara ya nchi za Scandinavia, alianzia Uingereza.

Katika msafara huo Rais alifuatana na wafanyabiashara, waandishi wa habari na maofisa wengine wa serikali.

Mwandishi wa Habari wa Rais, Premmy Kibanga alisema Waziri ana mamlaka ya kutia saini mikataba inayohusiana na sekta yake kwa sababu ameteuliwa na Rais kumsaidia kazi katika sekta hiyo.

“Rais anawaamini watendaji wake na amewapa dhamana ya kuwakilisha nchi katika masuala mbalimbali,” alisema Kibanga na kumtetea Karamagi kuwa waziri huyo alifuata taratibu zote kabla ya mkataba huo kutiwa saini.

Alisema alichofanya Karamagi kuweka saini mkataba wa uchimbaji wa madini wa Buzwagi bila kumuarifu Rais ni sahihi kwa vile hatua za majadiliano juu ya mkataba huo zilikuwa zinafahamika ndani ya Serikali na Rais alikuwa anaarifiwa.

Ikulu iliongeza kuwa hata Mwanasheria Mkuu wa Serikali naye alihusishwa katika majadilianao hayo na hata kwenda kusainiwa nje ya nchi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ilishirikishwa kikamilifu.

“Kwa hiyo siyo lazima waziri akitaka kusaini mkataba amuarifu Rais, cha msingi ni wakati wa majadilino na hatua inayofikiwa kabla ya kusainiwa,” alisema Premmy na kuongeza kuwa alichofanya Karamagi ni kuhitimisha kitendo ambacho tayari kilikuwa kinafahamika ndani ya serikali.

Mwandishi wa Rais alisema kwa kuwa hatua zote za awali zilijulikana na Rais akawa anafahamu, hakukuwa na tatizo kwa Karamagi kusaini mkataba huo bila kumjulisha Rais Kikwete.

Juzi Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), aliwaambia wananchi waliojitokeza kumpokea kuwa hata Rais Kikwete hakuwa na taarifa kwamba Karamagi alisaini mkataba kuhusu uwekezaji katika mgodi wa dhahabu wa Buzwagi ingawa wote walikuwa kwenye ziara.

Zitto alisema mkataba huo ulisainiwa katika Hoteli ya Churchill wakati Rais Kikwete aliyekuwa katika ziara hiyo hana taarifa, jambo ambalo mbunge huyo alidai ndiyo hoja yake kubwa ya kuweka saini kwa kificho.

Buzwagi ni mgodi nne kumilikiwa na kampuni ya kigeni ya Barrick Gold Corporation ya Canada kati ya migodi saba
ya dhahabu iliyoko nchini.

Kampuni hiyo inamiliki migodi katika nchi za Marekani, Canada, Australia, Peru, Chile, Argentina na Tanzania.

Kutokana na utata huo, Zitto aliwasilisha hoja binasfi bungeni kutaka kuundwe kwa Kamati teule ya Bunge kuchunguza utata ambao umegubika utiaji saini wa mkataba huo.

Hata hivyo, wabunge walikataa hoja yake badala yake Bunge likamwona alimsingizia Karamagi uongo kuwa waziri huyo alilidanganya Bunge wakati alipokuwa anajibu hoja za wabunge baada ya kuwasilisha makadirio ya matumizi na mapato ya Wizara ya Nishati na Madini.
 
yeye kutaarifiwa hakuna tatizo lakini mko kwenye msafara mmoja, na Waziri wako anaenda hotelini kutia sahihi mkataba ambao utajenga mgodi wa dola milioni 400, hauambiwi unasema ilikuwa sawa? Hivi ni nani huyo anayewakurupusha kujibu? Sasa leo Rais kakataliwa na wananchi kuingia Buzwagi.. wataeleza na hilo ni sawa? Haya ndiyo naita majibu ya kihuni!
 
yeye kutaarifiwa hakuna tatizo lakini mko kwenye msafara mmoja,

..hilo tayari tatizo!


na Waziri wako anaenda hotelini kutia sahihi mkataba ambao utajenga mgodi wa dola milioni 400, hauambiwi unasema ilikuwa sawa?

..hili nalo tatizo!

Hivi ni nani huyo anayewakurupusha kujibu?

..keshajibu,hakutaarifiwa! hilo ndo swali tulikuwa tukijiuliza!


Sasa leo Rais kakataliwa na wananchi kuingia Buzwagi..

..hili haliwezi tokea,si tanzania hii!

wataeleza na hilo ni sawa?

..unafikiri ikiwa hivyo atakuwepo wa kueleza tena!


Haya ndiyo naita majibu ya
kihuni!

..bora hata lingekuwa la kihuni!kukaa kimya kungesaidia zaidi!

..ka nasikia kizunguzungu!
 
Hata kwenye mikutano ya cabinet? Sasa inakuwaje rais aseme serikali imesimamisha zoezi la kusaini mikataba mipya hadi review ya ile ya zamani ikamilike wakati waziri wake akeindelea na zoezi la kusaini mikataba mipya?
 
mwenzenu nafikiri Karamagi alipitiwa tu, sasa kwa vile hatuna utamaduni wa kuomba msamaha na kukubali kukosea ndio imebidi agangamale hivyo hivyo, kwani nani kati yetu hakosei? tuachane na mambo haya na tusonge mbele.

asanteni
 
Ama kweli nchi yetu imeingiliwa na hawa vilaza!...
Inakuwaje majadiliano kati ya serikali na wawekeshaji yawe muhimu sana kumtaarifu rais wa nchi lakini inapofikia makubaliano ya majadilaino hayo isiwe muhimu?... Jamani hivi kweli hawa viongozi wetu wanafikir sisi ni wajinga kisi hicho!. Kulikuwa na umuhimu gani kumjulisha toka mwanzo!...
Wabunge wasifahamu lolote na hata mbunge mwakilishi wa Buzzwagi hana taarifa zozote za uwekeshaji huo leo iwe ni swala la kuaminiana kati ya rais na Karamagi!..

Labda hawa viongozi wanafikiria kuwa wananchi hawafahamu mikataba ya ukubwa wake, huu sii mkataba wa biashara kati ya mtu na mtu ama kampuni na kampuni bali ni Mkataba wa serikali iweje kujulishwa rais isiwe muhimu?.
Hivi kweli Waziri anaweza kuweka mkataba wowote ule unahusu maslahi ya nchi bila rais kufahamu! acha kutoa ruksa ya Go ahead!..basi kesho kesho kutwa tutakuja kuta tumeuzwa hata raia, maanake ni maamuzi ya Waziri
Tumeambiwa sheria ya madini bado ilikuwa ikipitiwa na kufanyiwa marekebisho na SHERIA ya madini hata siku moja mtunzi wa sheria hawezi kuwa waziri bali BUNGE, isipokuwa sera ya chama CCM ktk madini ndiyo inaweza badilishwa na chama.

Ama kweli tunazidi kuibiwa, hata madai yao kuwa mwanasheria mkuu alishirikishwa hii haina umuhimu kabisa kwani mwanasheria anatakiwa kuwepo pindi mkataba unapo wekwa sahihi. Na mashahidi wa upande wa serikali yetu ktk mkataba huo ni akina nani?.
 
Mkandara upo Ok
Hili la waziri kusaini mkataba wa madini au natural resources nyingine bila Rais kuwa na taharifa au kutoa baraka zake haliingii hakilini.Ni kawaida ndani ya serikali zetu mambo "yakimbumbuluka" kuwatupia mizigo mawaziri. Tunaweza kurejea issue ya RICHMOND walimtosa Msabaha kama ni muhusika number moja wakati aliyelazimisha mradi Lowasa hakuguswa. Pili tunaweza kurejea Waziri Danieli Yona kusukumiziwa mpira ndiye aliyeingia mikataba mobovu ya madini na kumuacha Mkapa kama mtu safi. Matokea yake leo tunawekewa wazi na THISDAY Jinsi gani Mkapa alihusika.

Hoja yangu ni kwamba Kikwete anahusika kwa asilimia kubwa na hili dili wanaosema hausiki sio wakweli.Kama haitoshi Deo Mwanyika (Afisa uhusiono wa Bariki) ameshakiri mkataba umesainiwa UK na ni Hotelini(chungulikia Mwananchi online)Sasa Kikwete anasubili ushahidi gani tena hili kumkiki out Karamaji.Hii ni kashfa kwa Bunge na nchi kwa ujumla.
 
mwenzenu nafikiri Karamagi alipitiwa tu, sasa kwa vile hatuna utamaduni wa kuomba msamaha na kukubali kukosea ndio imebidi agangamale hivyo hivyo, kwani nani kati yetu hakosei? tuachane na mambo haya na tusonge mbele.

asanteni

Dada yangu,two wrongs do not make a right.Kwa vile kati yetu hakuna ambaye hakosei haimaanishi basi mtu akikosea kama tulivyokosea sie basi anakuwa sahihi.Na unaposema tuachane na mambo haya na tusonge mbele,una ushauri wowote tusonge mbele kuelekea wapi?Tusipoangalia pale tulipojikwaa kuna mwamana gani kuwa huko mbele tunakosonga hatutotumbukia shimoni kabisa?

A practical example,suppose ungekuwa unaibiwa mumeo (just like wananchi wanavyoibiwa rasilimali zao) ungebaki na msimamo huohuo kwamba hakuna mtu asiyekosea,na kujishauri kuwa usonge mbele AU ungetaka kieleweke kwanza kabla ya kuamua kusamehe na kusahau?
 
Back
Top Bottom